MAKAMU WA PILI WA RAIS ZANZIBAR BALOZI SEIF ALI IDI AFUNGA KIKAO CHA BARAZA LA WAWAKILISHI

MAKAMU WA PILI WA RAIS ZANZIBAR BALOZI SEIF ALI IDI AFUNGA KIKAO CHA BARAZA LA WAWAKILISHI

June 23, 2017
bas1
Waziri wa Kilimo,Maliasili Mifugo na Uvuvi Hamad Rashid kushoto akibadilishana mawazo na Waziri wa Fedha  na Mipango Dk,Khalid salum Mohammed  katika baraza la Wawakilishi Zanzibar.PICHA NA YUSSUF SIMAI/MAELEZO ZANZIBAR
bas2
Waziri wa Habari Utalii Utamaduni na Michezo Rashid Ali Juma akibadilishana mawazo na Muakilishi wa Jimbo la Kikwajuni Nassor Salim Ali katika baraza la Wawakilishi Zanzibar.
bas3
-Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Idi akitoa hotuba ya Ufungaji wa Baraza la Wawakilishi ilioambatana na uchambuzi wa masuala mbalimbali yaliojadiliwa katika baraza hilo Mbweni Zanzibar.
bas4
-Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Idi akitoa hotuba ya Ufungaji wa Baraza la Wawakilishi ilioambatana na uchambuzi wa masuala mbalimbali yaliojadiliwa katika baraza hilo Mbweni Zanzibar.
……………………………………………………………
Na Faki Mjaka-Maelezo Zanzibar
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imewataka Wananchi ambao wanadai kuchukuliwa maeneo yao kufuatia zoezi la kuzuia Mchanga wawasilishe Vielelezo vyao katika Taasisi husika ili kufanyiwa kazi kwa mujibu wa sheria na taratibu za nchi.Hayo yamesemwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi katika hotuba yake ya kuahirisha kikao cha Tisa cha Baraza la Wawakilishi mbweni nje kidogo ya mji wa Zanzibar.
Amesema hatua iliyochukuliwa ilikuwa na lengo la kuweka utaratibu mzuri wa matumizi bora ya Mchanga ambao kadri unavyotumika unaendelea kumalizika.Balozi amesema Serikali imeandaa utaratibu ambao kama utafuatwa vyema utaweza kuinusuru Zanzibar na uhaba wa mchanga kwa vizazi vya sasa na baadae.
WAZIRI MWAKYEMBE AMKABIDHI KAMUSI KUU YA KISWAHILI WAZIRI SIMBACHAWENE LEO MJINI DODOMA

WAZIRI MWAKYEMBE AMKABIDHI KAMUSI KUU YA KISWAHILI WAZIRI SIMBACHAWENE LEO MJINI DODOMA

June 23, 2017
simv1
Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Dk.Harrison Mwakyembe akitia saini kitabu cha wageni baada ya kuwasili katika Ofisi za TAMISEMI mjini Dodoma.Kulia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI Mhe.George Simbachawene.
Picha zote na Daudi Manongi,MAELEZO,DODOMA.
simv3
Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Dk Harrison Mwakyembe akimkabidhi Kamusi kuu ya Kiswahili  Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI Mhe.George Simbachawene leo Mjini Dodoma.

BALOZI ADADI AWAFUTURISHA WAKAZI WA JIMBO LAKE

June 23, 2017
Mbunge wa Jimbo la Muheza(CCM) Balozi Adadi Rajabu akizungumza na wananchi wa Jimbo hilo mara wakati wa futari iliyoandiandaa nyumbani kwake kwa wananchi
Mbunge wa Jimbo la Muheza(CCM) Balozi Adadi Rajabu kushoto katikati ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Muheza wakiwa na wageni waalikwa wakipiga dua
Mkuu wa wilaya ya Muheza,Hajat,Mhandisi Mwanasha Tumbo akizungumza wakati wa futari hiyo
Wageni waalikuwa wakipata futari hiyo ambayo iliandaliwa na Mbunge wa Jimbo la Muheza,Balozi Adadi Rajabu nyumbani kwake
 Wageni waalikuwa wakipata futari hiyo ambayo iliandaliwa na Mbunge wa Jimbo la Muheza,Balozi Adadi Rajabu nyumbani kwake
 MNEC wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Mkinga,Mwasingo naye akipata futari hiyo



Mbunge wa Jimbo la Muheza(CCM) Balozi Adadi Rajabu akiwa na wananchi wa Jimbo lake wakipata futari
 Mwandishi wa AZAM TV mkoani Tang,Mariam Shedafa kulia na Anna Peter wakipata futari 
 Mkuu wa wilaya ya Muheza,Hajat,Mhandisi Mwanasha Tumbo kushoto mwenye kikombe cha chai akipata futari na wageni wengine.
 Katiby Tawala wa wilaya ya Muheza (DAS) Desderia Haulekulia akipata futari na wageni wengine waalikuwa nyumbani kwa Mbunge wa Jimbo la Muheza,Balozi Adadi Rajabu

Mbunge wa Jimbo la Muheza Mkoani Tanga,Balozi Adadi Rajabu akiagana na wananchi waliofika kupata futari nyumbani kwake

WAHAMIAJI HARAMU 45 WAKAMATWA WILAYANI MKINGA.

June 23, 2017
IDARA ya Uhamiaji Mkoani Tanga imewakamata wahamiaji haramu 45 kutoka nchini Ethiopia katika Kijiji cha Horohoro wilayani Mkinga mkoani Tanga kwa kosa la kuingia nchini kinyume cha sheria wakiwa shambani kwa wananchi wanakula mahindi kabla ya kutiwa nguvuni.
Licha ya kukamatwa kwa wahamiaji haramu hao lakini pia idara hiyo inamshikilia raia mmoja kutoka nchini Kenya ambaye ndio alikuwa akiwaongoza wahamiaji haramu hapa.

Akizungumza na waandishi wa habari,Afisa Uhamiaji Mkoa wa Tanga, Crispin Ngonyani alisema wahamiaji haramu hao walikamatwa June 18 mwaka huu katika kijiji hicho baada kupata taarifa kutoka kwa wasamaria wema  wa eneo hilo.

Alisema wahamiaji haramu hao walikamatwa wakiwa porini katika jiji hicho wakati wakisafiri kuelekea nchini Afrika Kusini ambapo waligunduliwa na wananchi baada ya kufika mashambani mwao wakawakuta wanakula mahindi ndio walipotoa taarifa kwa askari wa Polisi wa Horohoro na hivyo wakaenda kuwakamata.

Aliwataja wahamiaji haramu hao kuwa ni Melesa Manesha, Asaf
Erisid,Ashnif Agide,Mulugeta Menano,Demek Sorebeto,Samal
Latbo,Temesgen Tefera,Tememi Juheri,Mubarc Lamago,Temesa
Kibemo,Haftamu Tumiso,Teshum Assfe,Yohanness Ayano na Daniel Abbate.

Aidha Ofisa Uhamiaji huyo aliwataka wengine walio kamatwa kuwa ni Kibmam Abab,Temesgzeen Ayele,Akilu Abraham,Pxirose Makore,Munyasha Lombaso,Berekei Cezenzeni ,Detebo Erikato, Ayele Kebamo,Tamrat Mamo.

Wengine waliokamatwa kuwa ni Saniel Wolde,Tomiot Deto Gem,Abeje Alemeyo, Ashenaf Waje,Tariko Dutamo,Birhanu Atso,Tesefaye Dena,Tekel Abush,Tesyfe Landu na Abdi Hassani.

Kwa mujibu wa ofisa uhamiaji huyo aliwataja wengine kuwa ni Daafa Daimo,Getahun Zeleke,Yonas Liliso, Amanei Ashebo, Xesabo Womago,Isagay Tikie Mubarik Analo,Begaye Ganorem,Dawit Teso,Teshele Kemiso,Samweli Hyle na Tamasgen Sorsa.

Alisema wahamiaji haramu hao wamefikishwa mahakamani jana kujibu tuhuma zinazowakabili akiwemo msindikizaji  Mongela Kidhome ambaye ni Mkenya na mkazi wa mpakani mwa Kenya na Tanzania Horohoro.

Hata hivyo aliwataka mawakala wa wahamiaji haramu kuacha mara moja vitendo vya kuwaingiza nchini kwani watakaobainika watafikishwa kwenye vyombo vya kisheria kujibu tuhuma zinazowakabili.

DC TEMEKE MHE FELIX LYAVIVA AWAAGIZA WAKURUGENZI JIJINI DAR ES SALAAM KUANZISHA DAFTARI LA WAKAZI KILA MTAA

June 23, 2017
MKUU wa Wilaya ya Temeke jijini Dar es salaam Mhe Felix Lyaviva akizungumza wakati wa semina ya mamlaka ya Mawasiliano Tanzania kuhusu hali ya sekta ya mawasiliano na utangazaji nchini
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Mhandisi James Mitayakingi Kilaba akitoa maelezo kuhusu semina ya mamlaka ya Mawasiliano Tanzania kuhusu hali ya sekta ya mawasiliano na utangazaji nchini
Baadhi ya washiriki wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Temeke jijini Dar es salaam Mhe Felix Lyaviva akizungumza wakati wa ufunguzi wa semina ya mamlaka ya Mawasiliano Tanzania kuhusu hali ya sekta ya mawasiliano na utangazaji nchini
Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo akifatilia kwa makini semina ya mamlaka ya Mawasiliano Tanzania kuhusu hali ya sekta ya mawasiliano na utangazaji nchini
Mrakibu msaididzi wa Polisi Makao Makuu kitengo cha Makosa ya mitandao Joshua Mwangasa Akielezea takwimu na jinsi ya kudhibiti makosa ya mitandao ya kijamii nchini.
Meya wa Manispaa ya Ubungo Ndg Boniface Jacobo (Kulia) akifatilia kwa makini semina ya mamlaka ya Mawasiliano Tanzania kuhusu hali ya sekta ya mawasiliano na utangazaji nchini
Katibu Tawala wa Manispaa ya Kinondoni Bi Gift Msuya akifatilia kwa makini semina ya mamlaka ya Mawasiliano Tanzania kuhusu hali ya sekta ya mawasiliano na utangazaji nchini
Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo akifatilia kwa makini semina ya mamlaka ya Mawasiliano Tanzania kuhusu hali ya sekta ya mawasiliano na utangazaji nchini
Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar es salaam Bi Theresia Mbando akifatilia kwa makini semina ya mamlaka ya Mawasiliano Tanzania kuhusu hali ya sekta ya mawasiliano na utangazaji nchini
Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es salaam Mhe Isaya Mwita akitoa mtazamo wake wakati wa semina ya mamlaka ya Mawasiliano Tanzania kuhusu hali ya sekta ya mawasiliano na utangazaji nchini

Na Mathias Canal, Dar es salaam

MKUU wa Wilaya ya Temeke jijini Dar es salaam Mhe Felix Lyaviva amewaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri za Manispaa za Kigamboni, Ilala, Temeke, Kinondoni na Ubungo kuanzisha daftari la wakazi katika kila Mtaa katika Jiji la dar es salaam.

KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YA WILAYA YA KILWA YAFANYA ZIARA KATIKA KISIWA CHA SONGO SONGO

June 23, 2017
 Meneja Mradi wa kuchakata na kusafirisha Gesi katika Kisiwa cha Songo Songo, Andrew Hooper (kulia) kutoka Kampuni ya Pan African Energy akitoa maelezo mbele ya Kamati ya Ulinzi na Usalama inayoongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Kilwa, Christopher Ngubiagai (Wapili kushoto) walipotembelea mitambo ya Gesi Songas iliyopo katika kisiwa hicho juzi. 
MATUKIO KATIKA PICHA: YALIYOJIRI KATIKA KIKAO CHA 54, MKUTANO WA SABA BUNGE LA 11 MJINI DODOMA LEO JUNI 23, 2017.

MATUKIO KATIKA PICHA: YALIYOJIRI KATIKA KIKAO CHA 54, MKUTANO WA SABA BUNGE LA 11 MJINI DODOMA LEO JUNI 23, 2017.

June 23, 2017
PIC 1 Mhe.Zungu
Mwenyekiti wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Azzan Zungu  akiongoza    kikao cha hamsini na nne cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Juni 23, 2017.
PIC 2 Mhe.Kijaji
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe.Dk Ashatu Kijaji  akijibu maswali mbalimbali ya wabunge katika kikao cha hamsini na nne cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Juni 23, 2017.
PIC 3 Mhe Manyanya
Naibu Waziri wa Elimu ,Sayansi na Teknolojia Mhe.Eng Stella Manyanya akijibu maswali mbalimbali ya wabunge  katika kikao cha hamsini na nne  cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Juni 23, 2017.
PIC 4 Mhe.Mwigulu
Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe.Mwigulu Nchemba akijibu maswali mbalimbali ya wabunge katika kikao cha hamsini na nne cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Juni 23, 2017.
PIC 5 Mhe.Mhagama na Kijaji
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Bunge,Kazi,Vijana ,Ajira na watu wenye Ulemavu Mhe.Jenista Mhagama  akijadili jambo na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe.Dk Ashatu Kijaji  katika kikao cha hamsini na nne cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Juni 23, 2017.
PIC 6 Mhe Maghembe na Rita Mlaki
Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe.Prof Jumanne Maghembe akiteta jambo na Mbunge wa Viti Maalum Bi Martha Mlata   katika kikao cha hamsini na nne cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Juni 22, 2017.
PIC 7 Mhe.Lukuvi na Kessy
Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe.William Lukuvi  wakifuatilia jambo na Mbunge wa Nkasi kaskazini Mhe.Ally Kessy  katika kikao cha hamsini na nne cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Juni 23, 2017.
PIC 8 Mhe.Kamwelwe na Nsanzugwako
Naibu Waziri Wizara ya Maji na Umwagiliaji Mhe.Isack Kamwelwe  akimskiliza Mbunge wa Kasulu Mjini Mhe.Daniel Nsanzugwako  katika kikao cha hamsini na nne  cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Juni 23, 2017.
Picha Zote na Daudi Manongi- Dodoma MAELEZO, DODOMA

RAIS MAGUFULI ATOA MSAADA WA VITANDA,MAGODORO NA MASHUKA KATIKA HOSPITALI YA LEVOLOSI

June 23, 2017
 Mbunge wa viti maalumu ccm Mkoa wa Arusha  Catherine Magige akitoa nasaha mara tu baada ya kukabidhi msaada huo wa vitanda,magodoro na mashuka yaliyotolewa na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania
 Picha ikionyesha  wa kwanza kulia Mbunge wa viti maalum(CCM)Catherine Magige akikabidhi kwa niaba ya Rais  John Magufuli    msaada wa magodoro 25,mashuka 25 pamoja na vitanda  25 katika  kituo cha afya cha Levolosi  ,ambapo msaada wa vitu hivi umetolewa na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ikiwa ni moja wapo ya ahadi zake alizozitoa katika kipindi cha kampeni  ,katikati ni Mganga  mkuu wa kituo cha Afya cha Levolosi  Feksi Edward ,wa kwanza kushoto ni Mganga mkuu wa Halmashauri ya jiji la Arusha Saimoni Chacha (picha na Woinde Shizza,Arusha)
 Katibu wa UWT mkoa wa Arusha Fatuma Hassan akiwasalimia wananchi wakati wa hafla hiyo
 Mkuu  wa wilaya ya Arusha  Gabriel Fabian Daqarro akiongea na wananchi  wa jiji la Arusha


 Baadhi ya manesi na madaktari wa jiji la Arusha wakiwa wamelibeba moja ya godoro mara baada ya kukabidhiwa hii leo
   Mkurugenzi wa Jiji la Arusha Mh: Athuman Kihamia akitoa neno la shukrani kwa niaba ya jiji  mara baada ya kupokea msaada huo na kuhadi kuvitunza vifaa hivyo walivyokabidhiwa
 Mbunge wa viti maalumu Catherine Magige akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wananchi wa jiji la Arusha mara baada ya kukabidhi vifaa hivyo

Baadhi ya madaktari na manesi wakiwa wanashuhudia makabidhiano ya msaada huo wa vitanda ,mashuka na magodoro (habari picha na Woinde Shizza,Arusha)