Waziri wa Kilimo,Maliasili Mifugo
na Uvuvi Hamad Rashid kushoto akibadilishana mawazo na Waziri wa Fedha
na Mipango Dk,Khalid salum Mohammed katika baraza la Wawakilishi
Zanzibar.PICHA NA YUSSUF SIMAI/MAELEZO ZANZIBAR
Waziri wa Habari Utalii Utamaduni
na Michezo Rashid Ali Juma akibadilishana mawazo na Muakilishi wa Jimbo
la Kikwajuni Nassor Salim Ali katika baraza la Wawakilishi Zanzibar.
-Makamo wa Pili wa Rais wa
Zanzibar Balozi Seif Ali Idi akitoa hotuba ya Ufungaji wa Baraza la
Wawakilishi ilioambatana na uchambuzi wa masuala mbalimbali
yaliojadiliwa katika baraza hilo Mbweni Zanzibar.
-Makamo wa Pili wa Rais wa
Zanzibar Balozi Seif Ali Idi akitoa hotuba ya Ufungaji wa Baraza la
Wawakilishi ilioambatana na uchambuzi wa masuala mbalimbali
yaliojadiliwa katika baraza hilo Mbweni Zanzibar.
……………………………………………………………
Na Faki Mjaka-Maelezo Zanzibar
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
imewataka Wananchi ambao wanadai kuchukuliwa maeneo yao kufuatia zoezi
la kuzuia Mchanga wawasilishe Vielelezo vyao katika Taasisi husika ili
kufanyiwa kazi kwa mujibu wa sheria na taratibu za nchi.Hayo yamesemwa
na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi katika hotuba
yake ya kuahirisha kikao cha Tisa cha Baraza la Wawakilishi mbweni nje
kidogo ya mji wa Zanzibar.
Amesema hatua iliyochukuliwa
ilikuwa na lengo la kuweka utaratibu mzuri wa matumizi bora ya Mchanga
ambao kadri unavyotumika unaendelea kumalizika.Balozi amesema Serikali
imeandaa utaratibu ambao kama utafuatwa vyema utaweza kuinusuru Zanzibar
na uhaba wa mchanga kwa vizazi vya sasa na baadae.