Jumuiya ya wakurugenzi wa serikali za Mitaa wapatao 60 Kutoka Uganda wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa kampuni ya MAXCOM Africa mapema leo walipokuwa wametembelea Ofisi za Maxmalipo Kujifunza ni jinsi Gani kampuni hii Imeweza kugundua teknolojia inayosaidia kudhibiti makusanyo kwenye vyanzo mbalimbali vya mapato katika Halmashauri za miji na majiji Nchini Tanzania. |
MATUKIO BUNGENI DODOMA
Wabunge wakiingia bungeni mjini Dodoma.PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG
Wabunge wakijadiliana jambo ndani bunge
Wabunge wakipata habari kupitia kwenye simu bungeni
Mbunge wa Jimbo la Momba, David Silinde akichangia hoja bungeni
Mbunge wa Jimbo la Mkuranga, Abdallah Ulega akichangia hoja
Majadilianao yakiendelea
Wabunge, Prosper Mbene, Dk.Mary Mwanjelwa na Allan Kiula wakiingia bungeni
Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu akijibu maswali bungeni
Mbunge wa Viti Maalum, Mariam Kisanga akiuliza swali
Waziri wa Viwanda na Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage akijibu maswali
Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Huruma ya Dodoma wakitambulishwa bungeni
Wabunge wakijadiliana jambo ndani bunge
Wabunge wakipata habari kupitia kwenye simu bungeni
Mbunge wa Jimbo la Momba, David Silinde akichangia hoja bungeni
Mbunge wa Jimbo la Mkuranga, Abdallah Ulega akichangia hoja
Majadilianao yakiendelea
Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu akijibu maswali bungeni
Mbunge wa Viti Maalum, Mariam Kisanga akiuliza swali
Waziri wa Viwanda na Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage akijibu maswali
Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Huruma ya Dodoma wakitambulishwa bungeni
MKUU WA WILAYA YA TEMEKE, SOPHIA MJEMA AZINDUA MICHUANO YA UMISETA UWANJA WA UHURU JIJINI DAR ES SALAAM LEO
Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Sophia Mjema ambaye alikuwa mgeni rasmi wa uzinduzi wa Michuano ya Shule za Sekondari Nchini (UMESETA), akipiga dana dana wakati wa uzinduzi huo uliofanyika Uwanja wa Uhuru Dar es Salaam leo.
Wanafunzi wa shule za sekondari za mkoa wa Dar es Salaam wakiwa kwenye uzinduzi huo.
Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Sophia Mjema (kushoto), akikabidhi vifaa vya michezo kwa Shule ya Sekondari ya Azania vilivyotolewa na Kampuni ya Coca Cola. Kulia Ofisa kutoka kampuni ya Coca Cola wadhamini wakubwa wa michuano hiyo kwa mwaka 2016.
DC Mjema akisalimiana na mwamuzi wa mchezo kati ya timu ya Sekondari ya Tirav ya Yombo na Makongo uliopigwa katika Uwanja wa Uhuru Dar es Salaam. Makongo ilishinda mabao 2-1.
DC Mjema akiwasalimia wachezaji wa timu ya Tirav.
DC Mjema akisalimiana na wachezaji wa timu ya Makongo Sekondari.
Mkuu wa Wilaya Sophia Mjema (kulia), akitoa nasaha zake kwa wachezaji hao kabla ya kuanza kucheza.
DC Mjema hapa akiwa katika picha ya pamoja na wachezaji wa timu ya sekondari ya Tirav na viongozi mbalimbali.
DC Mjema hapa akiwa katika picha ya pamoja na wachezaji wa timu ya sekondari ya Makongo na viongozi mbalimbali.
Hapa akiwa katika picha ya pamoja na waamuzi wa mchezo huo na viongozi mbalimbali.
Hapa mtanange ukiendelea.
Golikipa wa timu ya Tirav, Abdul Badi akiokoa moja ya hatari katika lango lake.
Wachezaji wa timu ya Makongo wakishangilia baada ya kupata bao lao la kwanza.
Na Dotto Mwaibale
MKUU wa Wilaya ya Temeke Sophia Mjema amezindua michuano ya Shule za Sekondari Nchini (UMESETA) katika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam huku akisisitiza kuwa yataendelea kuwaibua wachezaji wengi chipukizi.
Akizungumza katika uzinduzi huo Mjema aliishukuru kampuni ya Cocacola kwa kudhamini mashindano hayo huku akiyaomba makampuni na wadau wengine kujitokeza kudhamini michezo mbalimbali.
Mashindano hayo yatashirikisha timu zaidi ya 40 katika mchezo wa mpira wa kikapu kwa vijana wa Shule za Sekondari kutoka mikoa mbalimbali hapa nchini huku ikishirikiana na waandaaji wa michuano ya michezo ya Shule za Sekondari UMISETA katika kuhakikisha wanapata wachezaji wenye elimu kutoka mikoa yote hapa nchini.
Akizungumzia mashindano hayo Meneja wa Biashara wa Coca Cola Maurice Njowoka alisema wameamua kuongeza mchezo ili kupanua wigo wa mashindano hayo hapa nchini.
Aidha alisema lengo la kuungana na waandaaji hao, badala ya Shirikisho la soka Tanzania (TFF) pekee ni kutaka kupata wachezaji sahihi, kutoka mikoa yote, na ambao wako katika mashule ya Sekondari.
"Hii itatusaidia kupata wachezaji sahihi wenye elimu na ambao kweli wanasoma shule za sekondari,"alisema Njowoka.
Alisema tofauti na mwaka jana, tuliwatumia TFF pekee jambo ambalo tulipata wachezaji lakini katika mazingira magumu zaidi.
Alisema michuano ya mwaka huu wanaimani watapata wachezaji kiurahisi kwa sababu UMISETA ina rekodi ya wanafuzni wanaosoma katika shule za sekondari.
Njowoka alisema kwa kuanzia jijini Dar es Salaam, wametoa jezi na vifaa kwa shule za Sekondari zilizohudhuria katika mashindano hayo.
Alisema baada ya Dar es Salaam, wanaelekea Mwanza, Mbeya, Arusha na Moshi kwa ajili ya kuzindua rasmi michezo hiyo ambayo shule zinaanza kufanya mazoezi kwa ajili ya kujiandaa.
Alisema katika udhamini wao watatumia kinywaji cha Coca Cola kwa upande wa soka, wakati Kikapu watatumia Sprite, lengo ni kufanikisha michuano hiyo safari hii kutokana na kuongeza idadi ya mchezo.
RAIS DKT. MAGUFULI AFANYA MAZUNGUMZO NA MABALOZI WATATU KUTOKA NCHI MBALIMBALI IKULU JIJINI DAR ES SALAAM LEO.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
akisalimiana Balozi wa Vatican hapa nchini anayemaliza muda wake
Francisco Montecillo Ikulu jijini Dar es Salaam. Balozi huyo wa Vatican
alifika Ikulu kwa ajili ya kuagana na Rais Dkt. Magufuli mara baada ya
kumaliza muda wake ya Ubalozi nchini.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza
na mgeni wake Balozi wa Vatican hapa nchini anayemaliza muda wake
nchini Francisco Montecillo
ais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na
Balozi wa Vatican hapa nchini anayemaliza muda wake Francisco
Montecillo Ikulu jijini Dar es Salaam.
Balozi
wa Algeria hapa nchini Belabed Saada akikabidhi ujumbe uliotoka kwa
Rais wa Algeria kuja kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.
John Pombe Magufuli Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
akisalimiana na Balozi wa Canada hapa nchini Alexandre Leveque Ikulu
jijini Dar es Salaam. Balozi huyo wa Canada alifika Ikulu na ujumbe wake kwa ajili ya kufanya mazungumzo na Rais Dkt. Magufuli
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa
katika picha na Balozi wa Canada hapa nchini Alexandre Leveque wapili
kutoka kulia pamoja na waakilishi wengine wa Serikali pamoja na Ubalozi
wa Canada.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Balozi wa Canada hapa nchini
Alexandre Leveque mara baada ya kumaliza mazungumzo yao Ikulu jijini Dar es
Salaam.
PICHA NA IKULU
MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA AFUNGUA MKUTANO WA NANE WENYE LENGO LA KUDHIBITI SILAHA HARAMU KWA NCHI WANACHAMA MAZIWA MAKUU
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan,
akifungua mkutano wa nane kwa Mawaziri wa Nchi Wanachama wa Taasisi
inayopambana na tatizo la Silaha Haramu. Mkutano huo wa siku moja
unajadili kuhusu kudhibiti matumizi ya Silaha ndogo ndogo katika Nchi za
Maziwa Makuu na pembe ya Afrika umefanyika leo April 22,2016 katika
ukumbi wa Hoteli ya Naura Spring Mkoani Arusha.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan,
akisalimiana na Baadhi ya Mawaziri wa Nchi Wanachama wa Taasisi
inayopambana na tatizo la Silaha Haramu baada ya kufungua Mkutano wa
siku moja unajadili kuhusu kudhibiti matumizi ya Silaha ndogo ndogo
katika Nchi za Maziwa Makuu na pembe ya Afrika umefanyika leo April
22,2016 katika ukumbi wa Hoteli ya Naura Spring Mkoani Arusha.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan,
akiwa katika picha ya pamoja na Mawaziri wa Nchi Wanachama wa Taasisi
inayopambana na tatizo la Silaha Haramu baada ya kufungua Mkutano wa
siku moja unajadili kuhusu kudhibiti matumizi ya Silaha ndogo ndogo
katika Nchi za Maziwa Makuu na pembe ya Afrika umefanyika leo April
22,2016 katika ukumbi wa Hoteli ya Naura Spring Mkoani Arusha.
(Picha na OMR)
Rais wa Zanzibar Dk.SHEIN AZUNGUMZA NA UONGOZI WA ZATUC
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein
alipokuwa akizungumza na Uongozi wa Shirikisho la Vyama Huru vya
Wafanyakazi Zanzibar (ZATUC) ulipofika Ikulu Mjini Zanzibar Ukiongozwa
na Waziri wa Kazi,Uwezeshaji,Wazee,Vijana,Wanawake na Watoto
Mhe,Moudline Castico (wa pili kulia),
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein
alipokuwa akizungumza na Uongozi wa Shirikisho la Vyama Huru vya
Wafanyakazi Zanzibar (ZATUC) ulipofika Ikulu Mjini Zanzibar Ukiongozwa
na Waziri wa Kazi,Uwezeshaji,Wazee,Vijana,Wanawake na Watoto
Mhe,Moudline Castico (wa pili kulia),
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein
akiwa katika picha ya pamoja na Uongozi wa Shirikisho la Vyama Huru vya
Wafanyakazi Zanzibar (ZATUC) baada ya mazungumzo ulipofika Ikulu Mjini
Zanzibar Ukiongozwa na Waziri wa Kazi,Uwezeshaji,Wazee,Vijana,Wanawake
na Watoto Mhe,Moudline Castico (wa pili kulia),
[Picha na Ikulu.]
JAJI MKUU AWATAKA WATUMISHI WA MAHAKAMA MKOA WA MBEYA KUFANYA KAZI YA UTOAJI HAKI KWA UADILIFU.
JAJIMkuu
wa Tanzania, Mohamed Chande Othman, amefanya ziara ya kikazi ya
kutembelea na kukagua shughuli za Mahakama katika Kanda ya Mbeya.
Jaji Mkuu wa Tanzania, Mohamed
Chande Othman akiweka sahihi katika kitabu cha wageni mara baada ya
kuwasili katika Mahakama ya Wilaya ya Mbozi mkoani Mbeya.
Ziara
ya Mhe. Jaji Mkuu katika kanda hii imelenga kujionea hali ya utendaji
kazi wa Mahakama katika mkoa huo ikiwa ni pamoja na kuwakumbusha
Watumishi wa Mahakama kufanya kazi kwa ufanisi na weledi ili kuboresha
huduma ya utoaji haki nchini.
Katika
ziara yake Mhe. Jaji Mkuu aliambatana na Maafisa na Watendaji kadhaa wa
Mahakama kutoka Makao makuu ili kujionea hali ya utendaji kazi ikiwa ni
pamoja na kubainisha na kufanyia kazi changamoto ambazo watumishi
wanakumbana nazo katika utendaji kazi wa kila siku.
Jaji Mkuu wa Tanzania, Mohamed
Chande Othman, (katikati) akipata taarifa fupi ya utendaji kazi wa
Mahakama Kanda ya Mbeya kutoka kwa Mhe. Noel. P. Chocha, Jaji Mfawidhi
Kanda ya Mbeya (aliyesimama), mara baada ya kuwasili katika kikao
kilichohusisha Mahakimu Wakazi Wafawidhi,Watendaji, Maafisa Utumishi na
Maafisa Tawala wa Kanda ya Mbeya.
Mhe.
Mohamed Chande Othman, Jaji Mkuu wa Tanzania ambaye alipata nafasi ya
kukagua na kuongea na Watumishi wa ngazi mbalimbali za Mahakama katika
mkoa huo.
Katika
kikao alichofanya na Watumishi wa Mahakama mkoani humo ikiwa ni pamoja
na Wahe. Majaji na Mahakimu, Mhe. Jaji Mkuu alisisitiza mara zote juu ya
utendaji kazi kwa kujituma ili kubadili taswira ya Mahakama kwa
wananchi ambao ndio wadau muhimu wa Mahakama.
Akiongea
na Watumishi wa Mahakama wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Jaji Mkuu alieleza
kufurahishwa na kasi ya usikilizaji na umalizwaji wa mashauri katika
Mahakama za Mwanzo mkoani humo.
Jaji Mkuu wa Tanzania, Mohamed
Chande Othman akizungumza na Mahakimu Wakazi Wafawidhi,Watendaji,
Maafisa Utumishi na Maafisa Tawala wa Kanda ya Mbeya alipokutana nao na
kuwaasa kuendelea kutenda Haki kwa wakati ili kuweza kupunguza na
kumaliza mashauri yanayowasilishwa mahakamani.
Awali;
katika taarifa yake kwa Mhe. Jaji Mkuu, Mhe. Noel Chocha, Jaji
Mfawidhi, Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya, alimtaarifu Mhe. Jaji Mkuu juu ya
mkakati waliojiwekea wa kumaliza mashauri ya aina yoyote kwa kipindi
kisichozidi miezi sita.
Aidha
Mhe. Jaji Mkuu alitumia ziara hiyo ya kikazi kuwaeleza Watumishi juu ya
mikakati ambayo Mahakama imejiwekea katika kuhakikisha kuwa huduma ya
utoaji haki inaboreshwa nchini.
“Kwa
hivi sasa Mahakama ya Tanzania imejiwekea mikakati/vipaumbele ambavyo
vinalenga kuboresha huduma ya utoaji haki nchini, na malengo haya
inabidi yafanyiwe kazi na kila mmoja wetu kwa maana ya kila Mtumishi na
mdau wa Mahakama awajibike katika kufikia malengo yetu ya kuboresha
huduma ya utoaji haki nchini.” Alisema, Mhe. Jaji Mkuu.
Uimarishaji
wa ukusanyaji wa takwimu; hili pia ni eneo ambalo limewekwa kama
kipaumbele katika maboresho Mahakamani, Mhe. Jaji Mkuu alisema Mahakama
pia imejipanga vyema kuhakikisha inakuwa na takwimu sahihi za kesi
mbalimbali zilizopo katika Mahakama mbalimbali nchini ili kuangalia ni
sehemu ipi inayohitaji nguvu zaidi katika kushughulikia mashauri/kesi za
muda mrefu.
Uboreshaji
wa Miundombinu: miundombinu hii ni pamoja na majengo ya Mahakama,
vitendea kazi n.k, Mhe. Jaji Mkuu alisema pia katika kuboresha huduma
zake Mahakama imejipanga katika kuboresha miundombinu yake ikiwa ni
pamoja na kujenga majengo ya Mahakama na kukarabati majengo
yaliyochakaa.
“Tatizo
kubwa ambalo Mahakama inakabiliana nalo ni uchakavu wa miundombinu
yake, kwa hili tuko mbioni kuhakikisha Mahakama inakuwa na miundombinu
bora zaidi, tumejipanga kuboresha ikiwa ni pamoja na kujenga Mahakama
Kuu katika mikoa yote ambao haina majengo, taratibu zinaendelea na kwa
mwaka huu tumepanga kuanza ujenzi wa Mahakama Kuu katika mikoa ya Kigoma
na Musoma/Mara.
Uboreshaji
wa hali ya Wafanyakazi wa Mahakama; Hili pia ni moja kati ya eneo
ambalo limepewa kipaumbele katika maboresho yanayoendelea kufanyika
ndani ya Mahakama; Mhe. Jaji Mkuu aliwaeleza Watumishi wa Mahakama Mbeya
kuwa uboreshaji huu unaangalia upatikanaji wa stahili za Watumishi kwa
wakati ikiwa ni pamoja na nauli za likizo, madeni mbalimbali, uboreshaji
wa mishahara ya watumishi suala ambalo linaendelea kufanyiwa kazi.
Aidha
Mhe. Jaji Mkuu aliongeza kuwa suala Maadili na nidhamu pia limewekewa
kipaumbele, alisema kuwa kuna baadhi ya Watumishi wa Mahakama hawana
nidhamu na maadili katika utendaji kazi, hali hii imesababisha kuwa
Mahakama nzima kutupiwa lawana juu ya utendaji kazi wake.
“kuna
baadhi ya Watumishi ya watumishi wa Mahakama hawana maadili na nidhamu
hali hii inachafua taswira nzima ya Mahakama, lazima tuongeze uadilifu,
Watanzania wanataka Watumishi wanaotoa haki, wanaoaminika ili kila
mwananchi aridhike,” alisema.
Naibu
Msajili, Mahakimu Wakazi Wafawidhi,Watendaji, Maafisa Utumishi na
Maafisa Tawala wa Kanda ya Mbeya waliokutana na kuzungumza na Jaji Mkuu
wa Tanzania kuhusu utendaji kazi Mahakama kwa Kanda ya Mbeya.
MUOGELEAJI WA TANZANIA HILAL HILAL ATWAA MEDALI YA SHABA DUBAI.
Kikosi cha
timu ya Taifa ya Tanzania kinanchoshiriki katika mashindano ya Cana
Kanda ya nne. kutoka kulia ni Amani Doggart, Catherine Mason, Hilal
Hilal na Smriti Gokarn.
Na Mwandishi wetu
Muogeleaji
wa Tanzania, Hilal Hilal ametwaa medali ya Shaba katika mashindano ya
kuogea ya Cana Kanda ya Nne yanayoendelea nchini Mauritius.
Hilal
ambaye ni nahodha wa timu ya Taifa katika mchezo huo, amemaliza katika
nafasi ya tatu katika staili ya butterfly kwa kutumia muda wa sekunde
26.70 katika mashindano hayo magumu yaliyoshirikisha nchi za Uganda,
Kenya, Rwanda Burundi, Djibouti, Eritrea, Ethiopia, Somalia, Sudani
Kusini na Sudan.
Nafasi
ya kwanza ilichukuliwa na muogeleaji kutoka Zambia, Ralph Goveia
aliyetumia muda wa 25.11 na kupata medali ya dhahabu huku Tom Donker
wa Zambia pia akimaliza katika nafasi ya pili kwa kutumia muda wa 25.66
na kupata medali ya fedha.
Hilal
pia alishiriki katika mashindano ya mita 50 ya staili ya backstroke na
kumaliza katika nafasi ya saba kati ya waogeleaji 13 kwa waogeleaji
wenye umri zaidi ya miaka 17. Hilal alitumia muda wa 29.91 katika
mashindano hayo ambapo Mzambia Tom Donker alishinda medali ya dhahabu
kwa kutumia muda wa sekunde 27.40.
Mbali
ya Hilal, muogeleaji mwingine wa Tanzania Catherine Mason alimaliza
katika nafasi ya nne katika mashindano ya mita 50 butterfly kwa kutumia
muda wa 31.89 kwa wasichana wenye umri wa zaidi ya miaka 17. Catherine
pia alimaliza katika nafasi ya nne katika mashindano ya mita 50 ya
staili ya backstroke kwa kutumia muda wa 34.13.
Pia
muogeleaji wa klabu maarufu ya Dar Swim Club (DSC) , Smriti Gokarn
alishika nafasi ya 14 kati ya waogeaji 18 katika mashindano ya mita 200
ya backstroke kwa kutumia muda wa 3.21.30.
Muogeleaji
huyo pia alishika nafasi ya tisa kwa kumia muda wa 2.31.31 katika
mashindano ya freestyle mita 200 na katika mita 50 butterfly alimaliza
katika nafasi ya 11 kwa kutumia muda wa 34.28. Pia alimaliza katika
nafasi ya 11 katika mita 50 kwa upande wa staili ya backstroke kwa
kutumia muda wa 36.43.
Naye
Amani Doggart alianza kwa kushika nafasi ya 14 katika staili ya
butterfly kwa kutumia muda wa 38.54 na baadaye kumaliza wa Saba katika
staili ya backstroke kwa kutumia muda wa 37.41 katika mashindano ya
mita 50.
Subscribe to:
Posts (Atom)