March 11, 2014

WACHIMBAJI WA MADINI WAWILI WAFARIKI DUNIA NA WATATU KUJERUHIWA BAADA YA KUPONDWA NA UDONGO

Watu wawili wamekufa na watatu kuokolewa katika machimbo ya wachimbaji wadogowadogo mchanga yaliyoko katika kijiji cha Mponvu wilayani Geita baada ya  kufukiwa na udongo ndani ya shimo.

Tukio hilo limetokea Machi 9 mwaka huu majira saa 6 usiku ambapo watu watano walipanda katika mlima wa Samina na kuanza kuchimba mara ghafla udongo uliporomoka na kuwaponda waliokuwemo ndani ya shimo hilo.
March 11, 2014
Release No. 042

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Machi 11, 2014



22 KUSHIRIKI SEMINA YA WAAMUZI DAR

Waamuzi na waamuzi wasaidizi 22 wameteuliwa kushiriki semina na mtihani wa utimamu wa mwili kwa robo ya kwanza ya mwaka huu itakayofanyika jijini Dar es Salaam kuanzia Machi 14 hadi 16.

Semina hiyo inashirikisha waamuzi wote wenye beji za Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) na wale wa ngazi ya juu (elite) kutoka Tanzania Bara za Zanzibar.

Waamuzi hao ni Charles Simon (Dodoma), Dalila Jafari (Zanzibar), Ferdinand Chacha (Mwanza), Hamis Chang’walu (Dar es Salaam), Helen Mduma (Dar es Salaam), Israel Mujuni (Dar es Salaam), Issa Vuai (Zanzibar), Janeth Balama (Iringa), Jesse Erasmo (Morogoro), John Kanyenye (Mbeya) na Jonesia Rukyaa (Bukoba).

Viwavijeshi vyavamia mashamba Kilindi

March 11, 2014
Wadudu  waharibifu wa mazao aina ya viwavijeshi wamevamia mashamba ya wakulima wa vijiji mbalimbali vilivyopo Kata nane za wilayani ya Kilindi na kuharibu mahindi.
Uharibifu wa wadudu hao umezua hofu ya kuibuka kwa baa la njaa wilayani hapa.

Wakizungumza katika mahojiano na NIPASHE kwenye Kijiji cha Msente, kilicho Kata ya Mswaki, wilayani Kilindi wakati walipokuwa wakikabidhiwa vyeti vya kuzaliwa vilivyoratibiwa na shirika la World Vision Tanzania, baadhi ya wakulima walisema hatua hiyo imewaathiri kwa kuwa wanakabiliwa na uhaba wa chakula.

MAJAMBAZI YAUA KIBORILONI-MOSHI-MKOANI KILIMANJARO

March 11, 2014
Majambazi wavamia duka la jumla na kumuua mfanyabiashara maarufu mkoani Kilimanjaro ameuawa kwa kumpiga risasi mbili Kichwani na tumboni kabla ya kutoweka kusikojulikana.

Tukio hilo lilitokea jana majira ya saa 2:15 usiku katika maeneo ya Mnazi kata ya Kiboriloni, wilaya ya moshi, mkoani hapa ambapo watu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi wakiwa na silaha inayosadikiwa kuwa ni SMG/SAR walimvamia na kumpiga risasi mfanyabiashara, Respiki Eustarck Shirima.

kwa mujibu wa taarifa zilizothibitisha na Kamanda wa polisi mkoani hapo, Robert Boaz, tukio hilo lilitokea juzi machi 10 mwaka huu na kuongeza kwamba majambazi hao walimpiga risasi mbili kabkla ya kutoweka kusikojulikana.

Boaz amesema mpaka sasa haijafahamika kama kuna mali zilizo chukuliwa na majambazi hao na kwamba uchunguzi unaendela ili kubaini chanzo cha mauaji hayo na kuongeza kuwa Jeshi lake limeanza msako mkali kuwasaka majambazi hao.
March 11, 2014

Ridhwani achukua fomu za Ubunge Chalinze

 Mgombea Ubunge wa Jimbo la Chalinze kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi Ridhwan Kikwete akionesha fomu aliyochukua ya kugombea ubunge jimbo la hilo kulia kwake ni Katibu wa CCM wa Wilaya ya Bagamoyo, Kongo Kamate na Mbunge wa viti maalum wa jimbo la Chalinze Subira Mgalu.
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Chalinze kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Ridhwan Kikwete akijaza fomu ya kugombea jimbo hilo.
March 11, 2014

UZUSHI MITANDAO YA KIJAMIII NCHINI WAMKERA EDWARD LOWASSA

Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa amekerwa na tabia ya baadhi ya watu wanaosambaza uzushi katika mitandao ya kijamii kwa kutumia jina lake.
Lowassa alisema kuna watu wanaoendeleza kusambasa picha ya noti ya Sh500 yenye picha yake huku wakiongeza maneno mabaya juu yake.
March 11, 2014

*BADO KUNA TATIZO LA UPUNGUVU WA MAJAJI- JAJI RUTAKANGWA

DSC_0003
Mgeni rasmi Jaji wa Mahakama ya Rufani, Edward Rutakangwa (katikati) akiwasili kufungua rasmi mafunzo ya siku nne juu ya sheria za kimataifa za kazi kwa majaji na wasajili wa mahakama nchini yalioandaliwa na Shirika la Kazi Duniani mjini Bagamoyo. Kulia ni Mkurugenzi wa Shirika la Kimataifa la kazi duniani kwenye nchi nne Tanzania, Kenya, Rwanda na Uganda, Alexio Musindo.
***********************************************
Na Damas Makangale, Bagamoyo
JAJI wa Mahakama ya Rufani, Tanzania, Edward Rutakangwa amesema bado kuna upungufu mkubwa wa majaji katika mahakama za Tanzania kiasi cha kusababisha mrundikano wa kesi katika mahakama hapa nchini. MOblog inaripoti.
Akifungua rasmi mafunzo ya siku nne kwa majaji, wasajili na wasajili wasaidizi wa Mahakama ya Kazi, Jaji Rutakangwa amesema kwamba pamoja na Mheshimiwa wa Rais kuteua majaji bado kuna upungufu mkubwa wa majaji nchini.
March 11, 2014

SHEREHE ZA WANAWAKE ZAFANA DAR

mamaaaa shuguli mwenyewe
Shamim akiongea jambo
Mgeni rasmi  wa shughuli ,
mke wa makamo wa Rais wa jamhuri wa Muungano
 wa Tanzania
Mama Asha Bilali

wadada walivinyuka