WACHIMBAJI WA MADINI WAWILI WAFARIKI DUNIA NA WATATU KUJERUHIWA BAADA YA KUPONDWA NA UDONGO
Watu wawili
wamekufa na watatu kuokolewa katika machimbo ya wachimbaji wadogowadogo mchanga yaliyoko katika kijiji cha Mponvu
wilayani Geita baada ya kufukiwa na udongo ndani ya shimo.
Tukio
hilo limetokea Machi 9 mwaka huu majira saa 6 usiku ambapo watu
watano walipanda katika mlima wa Samina na kuanza kuchimba mara ghafla
udongo uliporomoka na
kuwaponda waliokuwemo ndani ya shimo hilo.