NHC yaelezea namna ilivyosaidia vijana kupitia mradi wa ufyatuaji wa matofali na ujenzi wa nyumba za gharama nafuu

October 17, 2014

 Meneja wa Mkoa wa Tabora Bw. Erasto Chilambo,  akimpa maelezo ya ujenzi wa nyumba za gharama nafuu Mkuu wa Mawasiliano na Huduma kwa Jamii Bi Susan Omari alipotembelea mradi huo ulioko eneo la Isikizya Wilayani Uyui jana. (Picha kwa hisani ya Kitengo cha Mawasiliano ya Umma na Huduma kwa Jamii cha Shirika la Nyumba la Taifa)
 Mwonekanao wa nyumba za gharama nafuu zilizojengwa na NHC eneo la Isikizya Mkoani Tabora.
 Meneja wa Mkoa wa Tabora Bw. Erasto Chilambo akiendelea kutoa maelezo ya mradi kwa Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Huduma kwa Jamii, Bi Susan Omari
 Nyumba 38 zilizojengwa karibu kabisa na Makao Makuu ya Wilaya ya Uyui eneo la Isikizya. Nyumba zingine 12 zimejengwa upande wa pili wa barabara eneo la Isikizya.
 Mkuu wa Kitengo cha Huduma kwa Jamii wa NHC, Bi Susan Omari akitoa maelekezo kwa Meneja wa Mkoa wa Tabora Bw. Chilambo
 Msimamizi wa mradi wa NHC isikizya Bw. Tokimu Mondo akitoa maelezo ya utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa nyumba za gharama nafuu eneo la Isikizya jana.
 Sehemu ya nyumba zilizojengwa katika mradi wa nyumba za gharama nafuu eneo la Isikizya Wilayani Uyui zinavyoonekana.

KIKAO CHA HALMASHAURI KUU YA CCM CHAENDELEA MJINI DODOMA LEO

October 17, 2014
 MKURUGENZI MKAZI WA UNESCO AMTEMBELEA MKUU WA MKOA WA DODOMA LEO

MKURUGENZI MKAZI WA UNESCO AMTEMBELEA MKUU WA MKOA WA DODOMA LEO

October 17, 2014

DSC_0206
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues (katikati) akiongoza na Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Jaji Francis Mtungi (kulia) baada ya kuwasili ofisini kwa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Rehema Nchimbi. Kushoto ni Afisa Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) Bw. Al Amin Yusuph.
DSC_0209
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Rehema Nchimbi akimkaribisha ofisini kwake Mkurugenzi Mkazi wa UNESCO Tanzania, Zulmira Rodrigues alipomtembelea na kufanya naye mazungumzo. Kushoto ni Msajili wa Vyama vya Siasa nchini. Jaji Francis Mtungi na kushoto ni Afisa Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) Bw. Al Amin Yusuph na Nyuma kabisa ni Msajili Msaidizi kutoka Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Sisty Leonard Nyahoza.
DSC_0232
Mkurugenzi Mkazi wa UNESCO Tanzania, Zulmira Rodrigues akisaini kitabu cha wageni ofisini kwa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dkt. Rehema Nchimbi alipomtembelea leo na kufanya nae mazungumzo juu masuala mbalimbali ya maendeleo likiwemo suala la elimu na changamoto zake katika mkoa wa Dodoma.
DSC_0237
Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Jaji Francis Mtungi (wa pili kulia) akibadilishana mawazo na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Rehema Nchimbi (kushoto), Mkurugenzi Mkazi wa UNESCO Tanzania, Zulmira Rodrigues (wa pili kushoto) pamoja na Afisa Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) Bw. Al Amin Yusuph, Msajili Msaidizi kutoka Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Sisty Leonard Nyahoza walipomtembelea Mkuu huyo wa mkoa ofisini kwake leo.
DSC_0248
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues (wa pili kushoto) akitoa maelezo ya kazi mbalimbali zinazofanywa na shirika lake ikiwemo Mradi wa Micro Science Kits (MSKs) ulioendeshwa kwa miaka minne wa kusaidia ufundishaji wa masomo ya sayansi kwa kufanikisha majaribio ya maabara uliokuwa ukifadhiliwa na Shirika lake na kuendeshwa na Wizara ya Elimu nchini katika shule 180 zilizopo katika wilaya 34 ambao umemalizika hivi karibuni kwa mafanikio makubwa.
DSC_0280
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Rehema Nchimbi katika picha ya pamoja na ugeni huo ofisini kwake mjini Dodoma leo.
DSC_0330
Mkurugenzi Mkazi wa UNESCO Tanzania, Zulmira Rodrigues akisisitiza jambo kwa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Rehema Nchimbi alipokuwa akigana nae mara baada ya mazungumzo ofisini kwake mjini Dodoma.

KLABU YA MICHEZO YA UTUMISHI I YAKABIDHI VIKOMBE VYA SHIMIWI KWA WAZIRI MH.KOMBANI

October 17, 2014


Naibu Katibu Mkuu Utumishi Bw. HAB Mkwizu (kushoto) akimkaribisha Waziri wa Utumishi Mh.Celina O. Kombani (Mb) (katikati) kuzungumza na watumishi katika hafla fupi ya kuzipongeza timu za Utumishi zilizoshinda kwa kishindo katika Michezo ya SHIMIWI 2014.Kulia ni Mwenyekiti wa Michezo Utumishi Bw.Lumuli Mtaki.
Mshindi wa kwanza wa mbio za baiskeli kwa wanaume kutoka Utumishi Bw.Hassan Ligoneko akimkabidhi kombe Waziri wa Utumishi Mh.Celina O. Kombani (Mb) wakati wa hafla fupi ya kuzipongeza timu za Utumishi iliyofanyika ukumbi wa Utumishi.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais,Menejimenti ya Utumishi wa Umma Mh.Celina O. Kombani (Mb) akitoa mkono wa pongezi kwa Timu ya mpira wa pete ya Utumishi katika hafla fupi iliyofanyika ofisini kwake.
Kapteni wa timu ya mpira wa pete ya Utumishi Elizabeth Fusi (kushoto) akimkabidhi kombe la mshindi wa kwanza mpira wa pete Waziri wa Utumishi Mh.Celina O. Kombani (Mb) (katikati) katika hafla fupi ya kuzipongeza timu za Utumishi zilizoshinda michezo ya SHIMIWI, iliyofanyika ukumbi wa Utumishi. Wengine wanaoshuhudia ni Naibu Katibu Mkuu Utumishi Bw. HAB Mkwizu (kushoto) na Mwenyekiti wa Michezo wa Utumishi Bw.Lumuli Mtaki.(kulia).
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais,Menejimenti ya Utumishi wa Umma Mh.Celina O. Kombani akitoa mkono wa pongezi kwa timu ya kamba ya Utumishi katika hafla fupi ya kuzipongeza timu za Utumishi zilizoshinda michezo ya SHIMIWI, iliyofanyika ukumbi wa Utumishi.
Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma Mh.Celina O. Kombani (Mb) akizungumza na watumishi wa Ofisi ya Rais-Utumishi (hawapo pichani) katika hafla fupi ya kuzipongeza timu zilizoshinda mashindano ya SHIMIWI yaliyomalizika mjini Morogoro hivi karibuni. Kulia ni Mwenyekiti wa Michezo wa Utumishi Bw.Lumuli Mtaki.
Baadhi ya watumishi wakimsikiliza Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma Mh.Celina O. Kombani (Mb) (hayupo pichani) wakati wa hafla fupi ya kuzipongeza timu za Utumishi zilizoshinda michezo ya SHIMIWI katika ukumbi wa Utumishi.

MPANGO WA UCHANGIAJI WA HIARI WA PSPF NI MKOMBOZI

October 17, 2014

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Ikulu Bw. Peter Ilomo amewashauri watanzania kujiunga na Mpango wa Uchangiaji wa Hiari wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF ili kujiongezea kipato na hatimaye kuishi ya staha.


Bw. Ilomo alisema hayo Mjini Bagamoyo wakati wa semina iliyoandaliwa na Mfuko wa Pensheni wa PSPF kwa ajili ya Maafisa Rasilimali Watu kutoka wakala mbalimbali za Serikali

Kutokana na mabadiliko kwenye sekta ya hifadhi ya jamii, PSPF ilianzisha Mpango wa Uchangiaji wa Hiari maarufu kama PSS ili kuweza kuwahudumia Watanzania wote ambao wanahitaji huduma za hifadhi ya jamii ambao walikosa fursa hiyo huko nyuma.

“Mpango huu ni mkombozi kwani unazidi kukuongezea kipato na kukufanya uishi maisha yenye staha sasa na hata wakati wa ustaafu wako. Mpango huu pia unatoa ruksa kwa mtu asiye raia wa Tanzania lakini anafanyakazi hapa nchini kihalali kuwa mwanachama” alisema Bw. Ilomo.

Akizungumzia juu ya ujio ya kanuni moja ya ukokotoaji wa mafao, Bw. Ilomo alisema, “Kuwepo kwa kanuni moja ya ukokotoaji mafao ni changamoto kwa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii, kwa kuwa kigezo kikubwa cha kuvutia wanachama kitakuwa ni ubora katika huduma na mafao ya muda mfupi. Hivyo, nawaagiza watendaji wote wa PSPF kuhakikisha mnatumia vyema fursa hii kutoa elimu sahihi kwa watendaji hawa muhimu katika utumishi wa umma hapa nchini”.

Kutokana na Wizara ya Kazi na Ajira kutangaza kuwa Mifuko yote ya Hifadhi ya itakuwa ikitoa mafao yanayolingana, alisema wanachama wa PSPF waliokuwepo hadi tarehe 30/6/2014 watalipwa kwa utaratibu wa zamani na wote walioajiriwa kuanzia Julai 1, 2014 watalipwa mafao yao kwa mujibu wa kanuni mpya.

Katibu Mkuu huyo kutoka ofisi ya Rais aliipongeza PSPF kwa kuandaa semina hiyo na kuongeza, “ Semina hizi ni muhimu kwani zinatoa fursa ya kuonana na wadau na kutoa ufafanuzi juu ya masuala mbalimbali kwa manufaa ya Mfuko na wanachama wake”.

Awali akizungumza katika semina hiyo Mkurugenzi Mkuu wa PSPF Bw. Adam Mayingu aliwahakikishia washiriki wote wa semina hiyo kwamba PSPF itahakikisha inafikia dira yeke ambayo ni kuwa mtoa huduma bora wa hifadhi ya jamii nchini, na kufanyakazi kwa mujibu wa dhima ya Mfuko ambayo ni kutoa huduma zenye ushindani katika sekta ya Hifadhi ya Jamii kwa wateja wake kwa kutumia watumishi wenye ari ya kazi na teknolojia inayofaa.

Katika kuhakikisha inafikia dira yake na kuishi dhima yake, Bw. Mayingu aliahidi kwamba PSPF itaendelea kutekeleza majukumu yetu ya utendaji wa kila siku ikiongozwa na uwajibikaji, wajibu, muitikio, nidhamu, juhudi, uwazi na unyenyekevu kwa wote.
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Adam Mayingu, akizunfumza wakati wa semina ya siku moja iliyoandaliwa na Mfuko huo kwa maafisa rasilimali watu kutoka wakala za serikali iliyofanyika mjini Bagamoyo mkoa wa Pwani Alhamisi Oktoba 16, 2014.
Katibu Mkuu Ikulu,Peter Ilomo akitoa hotuba ya ufunguzi wa Semina ya siku moja iliyoandaliwa na Mfuko wa Pensheni wa PSPF, kwa maafisa rasilimali watu huko Bagamoyo mkoani Pwani, Alhamisi Oktoba 16, 2014. Warsha hiyo ililenga kuwapatia elimu waajiri kuhusu huduma mbalimbali zitolewazo na Mfuko huo kwa wanachama wake.
Mmoja wa washiriki wa semina hiyo, akizungumza.
Washiriki wa semina wakifuatilia kwa makini mada zilizokuwa zikitolewa na wataalam wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, kuhusu huduma mbalimbali zitolewazo na Mfuko huo kwa wanachama wake, Semina hiyo ilifanyika mjini Bagamoyo Alhamisi Oktoba 16, 2014.
Katibu Mkuu Ikulu, Peter Ilomo, (Kulia), akiongozana na Mkurugenzi wa Uwekezaji wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Gabriel Silayo, wakati wa mapumziko ya chai baada ya kufungua semina ya siku moja iliyoandaliwa na Mfuko huo kwa maafisa rtasilimali watu huko Bagamoyo mkoani Pwani, Alhamisi Oktoba 16, 2014.

MISA TANZANIA YAKUTANA NA MAAFISA HABARI KUJADILI CHANGAMOTO ZA UTOAJI TAARIFA

October 17, 2014

Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya vyombo vya habari Kusini mwa Afrika(MISATAN) Bwana Andrew Marawiti  akizungumza jambo wakati akifungua kongamano na maafisa habari wa taasisi za serikali zilizofanyika jana jijini Dar es Salaam.

Na Mwandishi wetu
Maafisa habari mbalimbali kutoka wizara na mihimili tofauti ya nchi, jana walikutana katika hoteli ya JB Belmont hapa Dar es Salaam kujadili changamoto wanazo kumbana nazo wakati kwa kutoa taarifa kwa wananchi.
Kongamano hilo linafuatia matokeo ya utafiti wa upatikanaji taarifa kwenye taasisi za umma uliofanywa na Taasisi ya Vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika (MISA) nakuzinduliwa rasmi siku ya tarehe 28 Septemba, ambayo pia ni Siku ya Kimataifa ya Haki ya Kupata Taarifa.

Miongoni mwa taasisi zilizoshiriki katika kongamano hilo ni Bunge, Mahakama, Wizara ya Katiba na Sheria, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Wizara ya Nishati na Madini, Idara ya Habari Maelezo, Mamlaka ya Taifa ya Vitambulisho (NIDA) na Idara ya Taifa ya Takwimu. Wizara za Afya na Mambo ya Nje hazikuweza kuwakilishwa licha ya kupata mwaliko. 
 Mwanasheria kutoka Taasisi Kitaifa ya Msaada wa Kisheria (National Organization of Legal Assistance-nola)  Bwana James Malenga akisisitiza jambo alipokuwa anawasilisha mada yake kwenye kongamano hilo la maafisa habari wa taasisi za kiserikali lililoandaliwa na Misa-Tanzania.
Afisa Habari na Utafiti wa Misa-TanzaniaBwana Sengiyumva Gasirigwa akitoa ufafanuzi kwenye mada aliyokuwa anaiwasilisha kwenye kongamano la maafisa habari wa taasisi za kiserikali(hawapo picha)  
Mfanyakazi wa  Misa-TanzaniaBwana Idrisa Abdallah akizungumzia adha anazozipata anapokuwa anakwenda taasisi na idara mbalimbali za serikali kupeleka barua ama maombi ya taarifa.
Afisa habari wa Mahakama Bi. Mary C. Gwera akizungumza  jinsi ofisi yake ilivyopokea Tuzo ya Kufuli na ambavyo imekuwa chachu ya mabadiliko katika kutoa taarifa kwa umma.
Afisa Mwandamizi wa habari kutoka Idara ya Habari Maelezo Bwana Abraham Nyantori akielezea changamoto za utoaji taarifa katika taasisi na idara za serikali.



 Maafisa habari wakifuatilia kwa umakini mada ya Umuhimu wa Kutoa/Kupata Taarifa serikalini kutoka kwa mwanasheria wa kujitegemea Bwana James Marenga.
Kaimu Mkurugenzi wa Misa-Tanzania Bwana Andrew Marawiti  akitoa shukrani wa wageni waliofika kwenye kongamano hilo.
TAARIFA MPYA KUHUSU ASKARI WALIOFUKUZWA KAZI

TAARIFA MPYA KUHUSU ASKARI WALIOFUKUZWA KAZI

October 17, 2014

BAADA ya kuvuja kwa picha katika mitandao ya kijamii wiki iliyopita, iliyowaonesha askari wawili wa usalama barabarani wakiwa ‘kimahaba niue’ ndani ya sare za kazi na kusababisha kupoteza ajira zao kutokana na kukiuka maadili, siri zaidi nzito zimezidi kuvuja kuhusiana na ishu hiyo na Amani limemuibua afande wa kike baada ya kumsaka sana.

Askari aliyefukuzwa kazi kutokana na kosa la ukiukaji wa maadili, Veronica Mdeme. Kwa mujibu wa vyanzo makini kutoka wilayani Misenyi mkoani Kagera, askari wa kike aliyeonekana kwenye picha hiyo chafu, WP. 8898 Veronica Mdeme, inadaiwa kuwa alipata uhamisho kutoka polisi mkoani humo na kupelekwa katika wilaya mpya ya Misenyi mwaka 2011 ambako mwaka mmoja baadaye, ndipo akapigwa picha hiyo iliyoleta gumzo kubwa ndani na nje ya Bongo.
Ilidaiwa kwamba, picha hiyo ilipigwa katika barabara ya lami iendayo Mutukura, umbali wa Kilomita 50 kutoka Misenyi na kwamba askari hao walikuwa katika Kituo cha Polisi cha Kyaka.
Nguzo ya umeme inayoonekana nyuma yao, ni zile zinazopeleka umeme nchini Uganda kutoka Bwawa la Umeme la Mtera, Tanzania.

*PRESIDENT KIKWETE MEETS UN SPECIAL ENVOY ON GREAT LAKES IN DODOMA TODAY

October 17, 2014


 President Drk Jakaya Mrisho Kikwete welcomes UN Special Envoy fir the Great Lakes Region H.E Mr Said Djinnit at Dodoma State lodge this evening. The Two leaders then held talks concerning the current situation in the Great Lakes Region.
H.E Mr. Said Djinnit, is an Algerian diplomat. He was appointed as a UN Special Envoy for the Great Lakes Region on 17th July, 2014 succeeding Mrs. Mary Robinson who was appointed as a UN Special Envoy for Climate Change.
President DR.Jakaya Mrisho Kikwete poses for a photo with the UN Special Envoy for Great Lakes Region Mr.Said Djinnit (left) together with Mr. Alvaro Rodrigues who Resident Coordinator for the UN System in Tanzania(right) at Dodoma State lodge this evening.
Photos by Freddy Maro

SHIRIKISHO LA SOKA NCHINI TFF LASHAURIWA KUHUSU UFADHILI LIGI DARAJA LA KWANZA NCHINI.

October 17, 2014
SHIRIKISHO la soka nchini (TFF) limeshauriwa kuangalia namna ya kuzitafutia ufadhili timu zinazoshiriki michuano ya Ligi daraja la kwanza nchini ili kuweza kuongeza ushindani na ladha ya mashindano hayo kama ilivyokuwa kwa ligi kuu soka Tanzania.
Hatua hiyo inatokana na timu nyingi zinazoshiriki ligi hiyo kutokuwa na uwezo wa kutosha jambo ambalo linapunguza ushindani na kuzifanya timu zinazojiweza kucheza vema na kuweza kufikia malengo waliojiwekea.
Hayo yalisemwa hivi karibuni na Kocha Mkuu wa timu ya African Lyon Charles Ottieno mara baada ya kumalizika kwa mechi yao dhidi ya African Sports ambapo timu hiyo ilikubali kichapo cha bao 1-0,mchezo uliochezwa kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani mjini hapa.
Katika mchezo huo bao la African Sports liliwekwa wavuni na Hassani Materema kunako dakika ya 10 baada ya kumalizia kazi nzuri iliyokuwa imefanywa na Ayoub Masoud ambapo bao hilo lilidumu mpaka timu zote zinakwenda mapumziko.
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi ambapo kila timu iliingia uwanjani hapo ikiwa na lengo la kutaka kupanda ushindi ambapo African Lyon walionekana kubadilika na kuanza kulisakama lango la wapinzani wao bila mafanikio ya aina yoyote yale.
Naye kwa upande wake,Kocha wa African Sports,Ally Maliki alisema wanamshukuru mungu kwa kupata pointi tatu muhimu kwenye mechi hiyo na kuhaidi kujipanga vema ili kufanya vizuri kwenye michezo yao iliyosalia lengo likiwa kuipandisha timu hiyo kucheza Ligi kuu msimu ujao.
Kwenye mechi hiyo kikosi cha African Sports kiliwakilishwa na Yusuph Yusuph,Ayoub Masoud,Issa Shabani,Juma Shemvuni,Mwaita Ngereza,Hussein Issa,Evarigestus Munjwahuka,Daudi Milandu,Hassani Materema,Ally Ramadhani na James Mendy.
Kwa upande wa African Lyon wao waliwakilishwa na Abubakari Hashim,Omari Kindamba,Kassim Simbaulanga,Baraka Jaffari,Yusuph Mlipili,Hamadi Manzi,Miraji Athuman,John Simbeta,Omary Ramadhani,Kashakala Ndere na Abdallah Mguihi.

SARE YA LIPULI YAIPASUA KICHWA AFRICAN SPORTS

October 17, 2014


KIKOSI CHA TIMU YA AFRICAN SPORTS .
Kitendo cha timu ya African Sports “Wanakimanumanu” kuruhusu sare na timu ya Lipuli ya Iringa kwenye mechi ya Ligi daraja la kwanza uliochezwa jana kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani jambo hilo limewaumiza viongozi wa timu hiyo na kuifikia hatua ya kuwaweka kitimito wachezaji wao.
Kitimoto cha wachezaji hao waliwekwa mara baada ya kumalizika mechi hiyo kwenye uwanja wa huo ambapo wachezaji wote walikalishwa na viongozi wao na kupewa mawaida ya kuhakikisha hawaruhusu sare nyengine mechi inayofuata.
Mechi hiyo ilimalizika kwa timu zote kutoka sare ya kufungana bao 1-1 ndani ya dakika tisini za mchezo huo ambapo African Sports ndio walikuwa wakwanza kupata bao lao kupitia Ally Ramadhani dakika ya 44 kwa njia ya penati iliyotokana na mchezaji wa timu hiyo Hassani Materema kufanyiwa madhambi na Stone Peter wa Lipuli eneo la hatari na mwamuzi wa mechi hiyo Klina Kabala kutoka Dar kuamuru ipigwe penati.
KIKOSI CHA LIPULI FC YA IRINGA.

Bao hilo lilidumu mpaka timu zote zikienda mapumziko ambapo kipindi cha pili kilianza kwa kasi ambapo kila timu iliingia uwanjani hapo ikiwa na hari mpya baada ya kufanya mabadiliko kwa baadhi ya wachezaji
wao.
Lipuli FC ndio walikuwa wa kwanza kuweza kufanya mabadilio ambapo walimtoa Keneth Kipanga na kumuingia Lawama Onole wakati African Sports iliwatoa Hussein Issa na Evarigestus Munjwahuki ambao nafasi zao zilichukuliwa na Maulidi Abbasi na James Mendy.

Akizungumza mara baada ya kumalizika mechi hiyo,Kocha wa African Sports,Ally Manyani alisema kuwa kubwa lililopo mbele yake ni kuhakikisha wanayafanyia kazi mapungufu yaliyojitokeza kwenye mechi hiyo ili waweze kupata ushindi.

Aidha aliwataka wadau wa soka kuendelea kuisapoti timu hiyo ili iweza kutimiza malengo yao waliojiwekea ya kuhakikisha wanapata nafasi ya kucheza ligi daraja la kwanza msimu ujao.