FRED SWAGG AACHIA ‘NIMEWAKA’ MTANDAONI

FRED SWAGG AACHIA ‘NIMEWAKA’ MTANDAONI

November 03, 2015
IMG-20151102-WA0031
Na Modewjiblog, team
Mwanamuziki anayekuja kwa kasi katika tasnia ya muziki Bongo, Fredrick Kalala ama jina la usanii akijulikana zaidi, Fred Swagg ameachia wimbo mpya mtandaoni ‘NIMEWAKA’ au ‘Nimelewa’.
Akizungumza na Modewjiblog kwa njia ya simu kutoka jijini Mwanza, Fred Swagg mkali wa vibao vya Maandishi alichowashirikisha Younf Killer na Kad Go. Ameeleza kuwa katika wimbo wake huo mpya wa Nimewaka, upo katika mahadhi ya rap, ni maalum kwa watu wa rika zote hasa sehemu za starehe ikiwemo Club.
“Wimbo huu mpya wa Nimewaka ni wa ku-Party’ ndani yake kuna komediani ikielezea watu wanavyotumia pesa na kulewa pombe za aina mbalimbali.. hivyo fans wakae mkao wa kula kuanzia sasa itakuwa mtandaoni ikiwemo mkito.com “ ameleza Fred Swagg.
Fred Swagg anabainisha video ya wimbo huo zinatarajia kuanza muda wowote kuanzia mwezi ujao huku kwa sasa akiendelea na promo za nyimbo zake zingine zinazofanya vyema kwenye vituo vya radio mbalimbali za ndani na nje wimbo wa ‘Kikomo’ aliomshirikisha Msanii, Da Prince na wimbo wa Maandishi aliowashirikisha Young Killer na Kad-Go.
-- Zainul A. Mzige, Operation Manager, MO BLOG, www.modewjiblog.com +255714940992.
TWIGA YAENDELEA KUJIFUA KUWAVAA MALAWI

TWIGA YAENDELEA KUJIFUA KUWAVAA MALAWI

November 03, 2015
Timu ya Taifa ya Wanawake ‘Twiga Stars’ inayonolewa na kocha mkuu Rogasian Kaijage imendelea na mazoezi kujiandaa na mchezo wa kirafiki dhidi ya Timu ya Taifa ya Wanawake ya Malawi utakaochezwa Novemba 07, mwaka huu jijini Dar es salaam katika uwanja wa Azam Chamazi.
Twiga Stars iliingia kambini Oktoba 29, katika hosteli za Shirikisho zilizopo Karume, ina kikosi cha wachezaji 22 wanaofanya mazoezi asubuhi na jioni katika uwanja wa Karume.
Mchezo dhidi ya Malawi ni mchezo wa kirafiki wa kimataifa, ambao kocha Kaijage atautumia kuangalia maendeleo ya wachezaji wake kwa ajili ya maandalizi ya micheo ya kimataifa.
Wachezaji waliopo kambini ni Asha Rashid, Estha Chaburuma, Fatuma Bushiri, Fatuma Omari, Mwajuma Abdallah, Mwanahamis Omar, Fatuma Khatibu, Amina Ally, Fatuma Issa, Belina Julius, Happines Hezron na Donizia Daniel.
Wengine ni Maimuma Hamisi, Stumai Abdallah, Anna Hebron, Anastazia Anthony, Shelder Boniface, Wema Richard, Tumaini Michael, Jane Cloudy, Saada Ramadhani na Sofia Mwasikili.

PUMZIKA WA AMANI MAREHEMU ANNETH CHRISTIAN KAJURA

November 03, 2015
Mume wa marehemu akitoa heshima za mwisho kwa aliyekuwa mke wake Anneth Christian mwishoni mwa wiki iliyopita nyumbani kwa marehemu Mbezi Beach - SalaSala Jijini Dar es Salaam na baadae maziko yalifanyika Makaburi ya Kondo - Bahari Beach.
 Mmoja ya wanandugu akitoa heshima ya mwisho.
 Mume wa marehemu Anneth Christian akiweka mchanga katika kaburi la mke wake katika Makaburi ya Kondo - Bahari Beach.
 Mama wa marehemu akitoa heshima za mwisho kwa aliyekuwa mwanae Anneth Christian mwishoni mwa wiki iliyopita nyumbani kwa marehemu Mbezi Beach - SalaSala Jijini Dar es Salaam na baadae maziko yalifanyika Makaburi ya Kondo - Bahari Beach.
 Mume wa marehemu akiweka shahada la ua katika kaburi la mke wake katika Makaburi ya Kondo - Bahari Beach.
 Mtoto wa marehemu akiweka mchanga katika kaburi la mama yake.
 Mama wa marehem akiweka mchanga katika kaburi la mwanae.
 Wanafamilia wakiweka maua katika kaburi la Anneth Christian.
Mwili wa Marehemu Anneth Christian ukiingizwa nyumbani kwake Mbezi Beach - SalaSala Jijini Dar es Salaam na baadae maziko yalifanyika Makaburi ya Kondo - Bahari Beach.
 Waombolezaji.
-- ---- Cathbert Angelo Kajuna, Founder and Mananging Director Kajunason Blog, P.O Box 6482, Dar es Salaam. Tel: +255 787 999 774 Alt: +255 765 253 445 www.kajunason.blogspot.com "Everything is Possible Through Peace & Stability''