TASWIRA : KAMATI KUU YA CHADEMA ILIVYOKUTANA DAR

July 21, 2014


Mwenyekiti wa Taifa wa Chadema,Freeman Mbowe akizungumza  kwenye  mkutano wa kamati kuu ya CHADEMA uliofanyika Dar es Salaam
Katibu Mkuu wa Chadema,Dk Willbroad Slaa(kulia)na Mkurugenzi wa Fedha,Antony Komu
Mbunge wa Ubungo,John Mnyika(kulia)akiteta jambo Antony Komu

TANESCO KUWABANA WAWEKEZAJI WABABAISHAJI

July 21, 2014
NA MWANDISHI WETU,TANGA.
WIZARA ya Nishati na Madini imesema itahakikisha haitoi mwanya kwa wawezezaji wababaishaji wanaotaka kuwekeza kwenye nishati ya umeme na kuwaingiza Watanzania kwenye mgawo wa umeme bila sababu.
Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Eliakimu Maswi, alitoa kauli hiyo wakati wa mkutano mkuu wa viongozi wa chama cha wafanyakazi, TUICO matawi ya Shirika la Umeme (Tanesco) na viongozi wa wizara.
Alisema asilimia 24 ya Watanzania zaidi ya milion 44 ndio waliounganishwa na huduma ya umeme katika maeneo mbalimbali vijijini na mijini.
Maswi alisema kiwango hicho kinaonyesha kwamba kuna watanzania wengi wanaotumia mkaa na kuharibu mazingira nchini.
Kwa sababu hiyo idadi serikali kupitia sekta ndogo ya nishati ya umeme inadhaniria kuongeza idadi ya watumiaji wa umeme hadi kufikia asilimia 50 ifikapo mwaka 2025.
Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco, Mhandisi Felichesmi Mramba, alisema shirika hilo limeanza kufanya vizuri huku akisema ifikapo mwaka 2033 asilimia 75 ya Watanzania watanufaika na huduma hiyo.
Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Luteni mstaafu Chiku Gallawa, alisema mkoa huo umedhamiria kuinua pato la mtu mmoja mmoja, hivyo anaamini kwamba kupitia umeme Watanzania wengi watanufaika na huduma bora za shirika hilo
Chanzo;Tanzania Daima

RAIS KIKWETE AZINDUA KITUO CHA AFYA CHA GEREZA LA KITAI MBINGA

July 21, 2014

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akikata utepe kufungua rasmi kituo cha afya katika Gereza la Kitai wilayani Mbinga jana.Kushoto ni Mkuu wa Gereza hilo Alexander Richard Nyefwe.Kituo hicho kitatoa huduma kwa askari magereza,wafungwa na vijiji jirani. Picha na Freddy Maro.

*MREMBO BORA WA KANDA YA MASHARIKI KUPATIKANA AGOSTI 8 MJINI MOROGORO

July 21, 2014

Baadhi ya warembo washiriki wa shindano la Miss Kanda Mashariki wakiwa katika pozi,wakati wa mazoezi yao ya maandalizi.
Na Mwandishi Wetu
Mashindano ya kumsaka mrembo kanda ya Mashariki ( Redds Miss Eastern Zone 2014) yatafanyika siku ya sikukuu ya Nanenane kwanue ukumbi wa  Nashera Hotel, mkoani Morogoro.
Mashindano hayo yatashirikisha jumla ya warembo  14 kutoka mikoa minne ambayo ni Pwani, Lindi, Mtwara na mwenyeji, Mkoa wa Morogoro chini ya udhamini wa Zanzi Cream Liquer, Pepsi, Usambara Safari Lodge, Kitwe General Traders, Starwing Lodge, Nashera Hotel, CXC Africa, Sykes Travel, Sasa Saloon, Grand Villa Hotel, Shabibi Line na Clouds FM.
Mratibu wa masindano hayo, Alex Nikitas aliwataja warembo watakaoshindana siku hiyo kuwa ni Lucy Julius Diu, Prisca  Mengi, Tarchisia Noback Mtui na Angel  Shio ambao wanatoka Morogoro.
Warembo wengine ni Elizabeth Tarimo, Lilian  Andrew na Leila  Abdul  Ally ambao wanatoka mkoa wa Lindi ambapo kutoka Mtwara ni  Nidah Fred Katunzi, Lightness  Mziray na Nelabo Emmanuel.
Pia warembo kutoka Pwani ni Khadija Ramadhan Sihaba, Irene Rajabu Soka, Mary  Mpelo na Arafa Shaban. Nikitas alisema kuwa warembo hao watakuwa kambini kuanzia Julai 29 kwenye hotel ya Usambara Safari Lodge chini ya Miss Kanda ya mashariki mwaka jana, Diana Laizer.

RAIS KIKWETE AKAGUA KILIMO CHA KAHAWA MBINGA LEO.

July 21, 2014


RC na RAS nchini kujengewa uwezo na kuhuisha uhai wa utekelezaji wa majukumu yao.

RC na RAS nchini kujengewa uwezo na kuhuisha uhai wa utekelezaji wa majukumu yao.

July 21, 2014

01 
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ally Idd akifungua mafunzo ya Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala Mikoa nchini leo jijini Dar es salaam.
02 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Hawa Ghasia akimpongeza Mgeni Rasmi Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ally Idd na mara baada ya kufungua mkutano wa mafunzo ya Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala Mikoa nchini leo jijini Dar es salaam.
03 
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ally Idd akitete jambo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Hawa Ghasia wakati wa mkutano wa mafunzo ya Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala Mikoa nchini leo jijini Dar es salaam.
0405 
Baadhi ya washiriki wa mkutano wa mafunzo ya Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala Mikoa nchini leo jijini Dar es salaam.
(Picha zote na Eleuteri Mangi-Maelezo)
Eleuteri Mangi-MAELEZO
21/07/2014
Viongozi wa Wakuu wa Mikoa nchini wameaswa kufahamiana  kama viongozi ili kubadilishana uzoefu wa kujenga mtandao wa mawasiliano na mahusiano kwa ajili ya kupashana habari na kushauriana.
Kauli hiyo imetolewa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ally Idd wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya Wakuu wa Mikoa (RC) na Makatibu Tawala Mikoa (RAS) nchini leo jijini Dar es salaam.
“Jengeni mshikamano wa mahusiano katika utendaji kazi wenu mkiimarisha maelewano miongoni mwenu mtarahisisha utendaji na kuepuka migogoro isiyo ya lazima” alisema Balozi Seif.
Balozi Seif aliendelea kusema, “Tumieni nafasi hii kufahamiana muweze kujenga mtandao wa mahusiano, mawasiliano mkiimarisha mashirikiano ili kuleta maendeleo katika maeneo yenu ya kazi kwa manufaa ya wananchi”.
Balozi Seif alisema kuwa kila kazi inachangamoto zake, katika kutekeleza majukumu yao vizuri na kubainisha kuwa viongozi hawa baadhi yao wamekuwa na misuguano ya hapa na pale ambayo husababishwa na mawasiliano yasiyoridhisha.
Balozi Seif alisisitiza kuwa dawa ya misuguano hiyo itapatikana kupitia mafunzo hayo ya siku tatu ambapo viongozi hao watakumbushwa mengi waliyoyasahau, watapata mengi ya kujifunza, kujikumbusha na kujinoa ili kuhuisha uhai wa utekelezaji wa majukumu yao ambao utaleta mshikamano na umoja miogoni mwa watendaji hao.
Naye Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Hawa Ghasia alipokuwa akimkaribisha Mgeni Rasmi alisema kuwa mafunzo hayo yataimarisha mahusiano na mawasiliano ya viongozi hao katika kutekeleza majukumu yao ili yapate tija iliyokusudiwa.
Waziri Ghasia amewaasa viongozi hao kuwa wasipofanya kazi kama timu hawawezi kupata tija katika maeneo yao ya kazi hasa katika kuwaletea maendeleo wananchi wanaowaongoza na nchi  kwa ujumla.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Wakuu wa Mikoa ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro akimshukuru  na kumhakikishia Mgeni Rasmi Balozi Seif kuwa wanamatumaini makubwa kuimarisha mahusiano kati yao vilevile na wanasiasa wote na kuahidi kuwa watatoa huduma bora zaidi.    
 Aidha, mikoa ya Lindi, Mtwara na Ruvuma viongozi wao hawatashiriki mkutano huo kwa kuwa kwa sasa wapo kwenye ratiba ya ziara ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete katika mikoa hiyo.
Wakuu wa mikoa hiyo waunganishwa kupata mfunzo kama hayo na Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala wa mikoa ya Zanzibar ambayo itapangwa kufanyika hapo baadaye ambapo Serkali ya Mapinduzi imeahidi kushirikiana na Tasisi ya Uongozi kutoa mafunzo hayo.
Mafunzo hayo yameandaliwa na Taasisi  ya Uongozi kwa lengo la kuwawezesha viongozi hao kufahamu kwa kina umuhimu wa mawasiliano bora baina ya viongozi wa kisiasa na watendaji Wakuu wa ngazi ya Mkoa ili kuimarisha utoaji bora wa huduma  kwa wananchi.
MAKAMU MKUU WA MUHAS AONGOZA KUAAGA MWILI WA PROFESA MBWAMBO

MAKAMU MKUU WA MUHAS AONGOZA KUAAGA MWILI WA PROFESA MBWAMBO

July 21, 2014

1 (3) 
Makamu Mkuu wa Chuo  Kikuu  cha Afya  na  Sayansi Shirikishi Muhimbili, (MUHAS) Profesa  Ephata  Kaaya akiuaga mwili wa  Mhadhiri wa wa chuo hicho , marehemu,  Profesa  Zakaria Mbwambo , ambaye ni mume wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Afrika Mashariki, Bi .  Joyce Mapunjo  leo kwenye viwanja vya chuo hicho jijini Dar es Salaam.
1b 
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afrika Mashariki, Bi.  Joyce Mapunjo  akifarijiwa na baadhi  ya waambolezaji  leo, wakati wa kuuaga mwili wa marehemu  mumewe  Profesa  Zakaria Mbwambo, ambaye alikuwa ni Mhadhiri  wa  Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili, (MUHAS) kwenye viwanja vya chuo hicho  jijini Dar es Salaam.
2 (3)4 (2) 
Baadhi ya maprofesa wa Chuo  Kikuu  cha Afya  na  Sayansi Shirikishi Muhimbili, (MUHAS), wakitoa  heshima za mwisho kwa mwili wa Profesa  mwenzao ,  marehemu,  Profesa  Zakaria Mbwambo , ambaye ni mume wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Afrika Mashariki, Bi .  Joyce Mapunjo  leo kwenye viwanja vya chuo hicho jijini Dar es Salaam.
6 
Baadhi ya waombezaji  waiombeleza
8 
Baadhi ya maprofesa wa Chuo  Kikuu  cha Afya  na  Sayansi Shirikishi Muhimbili, (MUHAS), wakiwa katika  hali ya huzuni wakati  wa kuuaga mwili wa Profesa  mwenzao ,  marehemu, Profesa  Zakaria Mbwambo , ambaye ni mume wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Afrika Mashariki, Bi . Joyce Mapunjo  leo kwenye  viwanja vya chuo hicho jijini Dar es Salaam.
Picha zote na Magreth Kinabo – Maelezo
MAUAJI YA VIKONGWE YASHIKA KASI MLELE- KATAVI

MAUAJI YA VIKONGWE YASHIKA KASI MLELE- KATAVI

July 21, 2014

??????????????????????????????? 
Madiwani wakifuatilia kwa umakini wakati mwenzao akichangia hoja katika kikao hicho
(Picha zote na Kibada Kibada –Mlele Katavi)
Na Kibada Kibada –Mlele Katavi.
Wimbi la mauaji kwa watu wenye umri kuanzia  miaka 60 na kuendelea  Wilayani Mlele Mkoani Katavi linaonekana kushika kasi na kutishia hali ya ulinzi na usalama kama hatua za makusudi hazitachukuliwa.
Hii ni kwa Mujibu wa Taarifa ya Hali ya ulinzi na Usalama Wilayani humo  iliyotolewa na Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai wa wilaya hiyo , Zabron Ibeganisa kwenye Mkutano Mkuu wa Baraza la Madiwani uliokuwa ukipokea taarifa ya utekelezaji wa shughuli mbalimbali zilizotekelezwa kwa kipindi cha mwaka  wa 2013/2014.