FAIDA NA HASARA ZA AKILI MNEMBA KUJADILIWA KWA UPANA MAADHIMISHO YA UHURU WA VYOMBO VYA HABARI DUNIANI.

May 02, 2024

 Na Janeth Raphael -MichuziTv -Dodoma


Katika kuelekea kilele cha Siku ya Uhuru wa vyombo vya Habari ambayo huadhimishwa May 3 kila mwaka Duniani suala la akili mnemba limeendelea kujadiliwa kwa upana kwa faida na hasara zake ambapo moja ya faida zake imeelezwa kuwa ni kuleta utambuzi wa mbolea gani inaweza kufaa katika eneo lipi hapa Nchini ili badala ya kuwa mbolea aina moja hivyo itaweza kutambua na kuwa nambolea tofauti tofauti.

Hayo yamesemwa na Mbunge wa viti Maalum wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwanzilishi wa NGO's ya Omuka Hub Neema Lugangira katika moja ya mijadala iliyokuwa ikiendelea katika shamla shamla za kuelekea Maadhimisho ya siku ya uhuru wa vyombo vya habari Duniani inayofanyika Jijini Dodoma.

"Tunapoongelea akili mnemba kuna faida nyingi sana hakuna ambaye anaweza kupinga kwamba ina faida sana, tukichukulia mfano katika Sekta ya kilimo kwa kutumia akili mnemba tunaweza tukatambua labda ni mbolea gani ainaweza kufaa eneo gani la nchi ili badala ya kununua aina moja ya mbolea ambazo tunanunua kulingana na maeneo husikahiyi ni moja ya faida. Lakini hata katika Sekta ya Afya kuna faida zake,hata kwa wanafunzi kufanya tafita zao"

Sambamba na hayo pia Neema amaeleza Changamoto za hiyo akili mnemba kuwa ni pamoja na utoaji wa taarifa zisizo sahihi yaani upotoshaji wa Taarifa na kutoa mfano kilichotokea kwa Raisi wa Zambia mwaka ambapo clip ilisambaa ikisema kuwa Raisi huyo hatagombea tena Uraisi na vyombo vya habari vikaamini hivyo mpaka pale Ofisi ya Raisi ilipokanusha kuwa clip hiyo haina ukweli.

"Lakini pia kila lililo jema lina upande wake mwingine akili mnemba inachangamoto zake nyingi sana na changamoto hizi zisipotiliwa mkazo au maanani hata zile faida zitakuwa hazina maana".

"Katika changamoto zilizopo moja ni upotoshaji wa wa taarifa,Mfano mwaka jana Raisi wa Zambia ilitoka Video Clip yake ikisema kuwa yeye hatogombea tena Uraisi ilikuwa video ambayo ukiitizama unaona yeye kasema,ikaoneshwa kila mahali na hata vyombo vikubwa wakaichukua na kuiweka, lakini baadae Ofisi ya Raisi waksema si kweli na kuwa imetengenezwa sasa fikiria taharuki iliyokuwa imetokea hapo".

Pia amezungumzia masuala ya ukatili kwa wanawake na akili mnemba hasa katika kipindi hiki tunachoelekea katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa na Hata Uchaguzi Mkuu wa 2025 kuwa waathirika wakubwa watakuwa ni Wanawake katika Siasa.


"Na hivi tunavyoelekea kwenye Uchaguzi nadhani kuna umuhimu mkubwa sana wa Wanahabari kabla ya habari kutoka,kuichapisha na kuisambaza kuhakikisha kwamba hii habari ni kwelie. Kwasababu inaweza kuzua taharuki kubwa sana".

"Lakini ukija katika eneo lingine ni kwenye ukatili wa kijinsia wa wanawake hasa linapokuja suala la matumizi ya teknolojia kwa bahati mbaya sana kati ya waathirika wakubwa ni sisi wanawake katika Siasa,kwani sisi soye sauti zetu zinajulikana video clip zetu zipo kwahiyo mtu anaweza akachukua maneno utafikiri wewe ndo umeyasema kumbe hujawahi kusema. Lakini mbaya zaidi uanweza ukatengenezewa kitu cha ajabu kwamba uko na mtu fulani na mkifanya jambo fulani na Uchaguzi ndo katikati umewaka moto,sasa kwa jambo hilo kwenye Uchaguzi itakuwaje,kwahiyo kunwa mambo lazima kayaangalia mapema".

Naye Harold Sungusia wakati akichangia Mada hiyo ya matumizi ya akili mnemba amesema kuwa katika changamoto hizo tusikate tamaa kwani anaamini pamoja na changamoto kuonekana kuwa nyingi lakini tukijipanga tunaweza fanya vizuri katika eneo hilo.

"Kitu ambacho nilikuwa najaribu kupendekeza kwenye hizi changamoto ni tusikate tamaa,lakini naamini kwamba tukijipanga vizuri bado tukafanya vizuri,kwasbabu tayari tunao Watanzania wanaofanya vizuri.Mfano kwenye Sekta ya afya,Sekta imetoa muongozo wa matumizi ya akili mnemba katika sekta afya Nchini na Imeonesha kusapoti vijana na vikundi mbalimbali kubadili matuzimi mabaya ya akili bandia na kuwa matumizi mazuri".

Kwa upande wake Nuzulack Dausen ambaye ni Mtendaji Mkuu Nukta Afrika amesema kuwa akili mnemba katika sekta ya habari inatumika katika uchakataji wa habari yani kuanzia kukusanya habari hizo,tofauti na zamani kulikuwa hakuna hiko kitu.

"Kwenye sekta hii ya habari akili mnemba inatumika katika mfumo wa uchakataji wa habari kwamba kuanzia kukusanya habari,zamani tulikuwa tulitumia maiki na kwenda kuchakata Radioni lakini saizi tunaweza kutumia akili mnemba kufanya hicho kitu".





WAZIRI BASHE ABAINISHA MIKAKATI YA SERIKALI KUONGEZA UZALISHAJI ZAO LA MKONGE

May 02, 2024

 Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe amebainisha mikakati ya serikali katika kuongeza uzalishaji wa zao la Mkonge kutoka tani 56,732.69 mwaka 2023/2024 hadi tani 80,000 mwaka 2024/2025.


Akiwasilisha Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha ya Wizara ya Kilimo kwa Mwaka 2024/2025, Mhe. Bashe amesema Wizara yake kupitia Bodi ya Mkonge Tanzania (TSB) lengo hilo litafikiwa kwa kununua zana za kilimo kwa ajili ya kuwezesha uendelezaji wa mashamba makubwa ya pamoja na kununua mashine ya kuchakata mkonge (korona).

“Pamoja na mambo mengine, tutaendeleza miundombinu ya kituo cha uchakataji cha Handeni, kukarabati miundombinu ya shamba la Kibaranga na kuwezesha umiliki wa ardhi ya kilimo yenye ukubwa wa hekta 6,000 kwa ajili ya kuanzisha mashamba makubwa ya pamoja katika mikoa ya Tanga, Singida na Morogoro.

“Aidha, Bodi itaratibu usambazaji wa miche ya Mkonge milioni tatu katika maeneo ya uzalishaji na kupitia TARI itatoa mafunzo kuhusu uzalishaji wa Mkonge na fursa zitokanazo na zao hilo kwa wadau 100,000 na maafisa ugani 500,” amesema Mhe. Bashe.

Mhe. Bashe amesema katika kuongeza matumizi ya mmea wa Mkonge, Bodi kwa kushirikiana na Chuo cha Sayansi na Teknolojia cha Nelson Mandela (NM-AIST), itajenga kituo cha uzalishaji wa Inzi chuma (black soldier flies) kwa kutumia mabaki ya Mkonge (Sisal waste) ili kutengeneza protini kwa matumizi ya binadamu na mifugo (wanyama, ndege na samaki).

“Pia, Bodi itawezesha utafiti wa zao la Mkonge utakaofanywa na watafiti kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), TARI-Mlingano, Chuo cha Sayansi na Teknolojia cha Nelson Mandela (NM-AIST) kwa kushirikiana na Kampuni ya Carbonovia UK ya Oxford Uingereza kuhusu uwezekano wa kuzalisha protini kutokana na hewa ukaa (Carbon dioxide) kutoka kwenye mabaki ya Mkonge.

“Aidha, Bodi kwa kushirikiana na Jeshi la Magereza na Chuo cha Mafunzo Zanzibar itaanzisha na kuimarisha utaalamu wa uzalishaji wa bidhaa za mikono za Mkonge ili kutengeneza ajira kwa vijana na wanawake,” amesema Mhe. Bashe.

SERIKALI YATOA NENO KUHUSU UTOAJI WA MIKOPO YA KIDIGITALI PAMOJA NA MIKOPO YENYE RIBA KUBWA

May 02, 2024

 

Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu (Mb) akijibu swali, bungeni jijini Dodoma la Mbunge wa Viti Maalumu Mhe. Shally Raymond aliyetaka kufahamu ni lini kampuni za simu zitalazimishwa kutoa elimu kwa wananchi kabla ya kutoa mikopo, kwa kuwa kampuni za simu ndizo zinazoongoza kutoa mikopo kwa haraka bila kujaza fomu au chochote ambapo vijana na wajasiriamali wengi wakiwemo wakina mama huvutiwa nayo.

(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Fedha - Dodoma)

Na. Joseph Mahumi, WF, Dodoma.


SERIKALI imesema inafuatilia kwa karibu mwenendo wa utoaji wa mikopo kwa njia ya kidigitali iliyoidhinishwa na kwamba itakapobainika kuwa kuna ukiukwaji wa matakwa ya leseni ya utoaji wa mikopo hiyo hatua stahiki zitachukuliwa ikiwa ni pamoja na kuwafutia leseni watoa huduma husika. 

Hayo yameelezwa bungeni jijini Dodoma na Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu (Mb), alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum Mhe. Shally Raymond aliyetaka kufahamu wakati ambapo kampuni za simu zitalazimishwa kutoa elimu kwa wananchi kabla ya kutoa mikopo, kwa kuwa kampuni za simu ndizo zinazoongoza kutoa mikopo kwa haraka bila kujaza fomu au chochote ambapo vijana na wajasiriamali wengi wakiwemo wakina mama huvutiwa nayo.

Dkt. Nchemba alisema, kwa mujibu wa sheria za fedha zinazosimamiwa na Benki Kuu ya Tanzania, hakuna kampuni ya simu iliyopewa leseni ya kutoa mikopo kwa wananchi kwa kuwa ili kampuni, taasisi au mtu binafsi aweze kutoa mikopo kwa wananchi anapaswa kuwa na leseni kutoka Benki Kuu ya Tanzania na kukidhi matakwa ya Sheria ya Benki na Taasisi za Fedha (The Banking and Financial Institutions Act, 2006) na Sheria ya Huduma Ndogo za Fedha (Microfinance Act, 2018).

Aliongeza kuwa, Kampuni za simu zinazotoa huduma za fedha zimepewa leseni ya kutoa huduma za mifumo ya malipo kulingana na matwaka ya sheria ya Mifumo ya Malipo ya Taifa ya mwaka 2015 (The National Payment Systems Act, 2015) pamoja na kanuni zake. Kampuni hizo zipo sita (6) ambazo ni: M-Pesa Limited, Honora Tanzania Mobile Solution Limited (Tigopesa), Airtel Money Tanzania Limited (Airtel Money), Viettel Ecommerce Limited (Halopesa), TTCL Pesa Limited (T-Pesa), na Azam Pesa Tanzania Limited (AzamPesa).

“Mikopo inayotolewa kwa wananchi kupitia simu za kiganjani hutolewa kwa ushirikiano kati ya taasisi zilizopewa leseni ya kutoa mikopo na kampuni za simu zilizopewa leseni ya mifumo ya malipo, ushirikiano huu unaainisha majukumu ya kila mtoa huduma ambapo taasisi zinazotoa mikopo hutoa mikopo hiyo kulingana na sheria na kanuni za leseni za utoaji mikopo huku kampuni za simu zikitoa mifumo, wateja na mwenendo wao wa kutumia huduma za kifedha” alisema Dkt. Nchemba.

Aidha, Dkt. Nchemba aliongeza kuwa mikopo yote hutolewa kupitia benki na watoa huduma ndogo za fedha ambapo inawafikia wananchi wote wenye uhitaji na wenye kutumia huduma za kifedha kupitia simu za mkononi kwa kutumia mifumo ya malipo ya kampuni za simu ambayo wateja wao wapo nchi nzima. 

Alisema kuwa hatua hiyo imewasaidia wananchi kupata mikopo bila uhitaji wa kuwa na akaunti ya benki wala dhamana ya mkopo husika.

Dkt. Nchemba alisema kuwa, kwa mujibu wa Kanuni za Kumlinda Mtumiaji wa Huduma za Fedha za mwaka 2019, watoa huduma wote wa fedha wanaosimamiwa na Benki Kuu ya Tanzania wanatakiwa kutoa elimu ya fedha kwa wateja wao juu ya huduma zao wanazotoa, ikiwemo elimu ya mikopo ambapo kanuni hizo zinawataka kutoa mikopo baada ya mkopaji kuridhia masharti ya mkopo husika.  

Alisema kuwa pamoja na Benki Kuu kuwahimiza watoa huduma za fedha kutoa elimu kwa wateja wao, Benki Kuu ya Tanzania katika nyakati tofauti imekuwa ikitoa elimu kwa wananchi juu ya huduma za fedha na kuwataka kutojihusisha na huduma za kifedha kutoka kwa watoa huduma wasio na leseni kutoka Benki Kuu ya Tanzania.

“Mikopo iliyopata umaarufu wa kuitwa “Kausha Damu” hutolewa na taasisi ambazo hazina leseni ya Benki Kuu ya Tanzania, Serikali kupitia Benki Kuu ya Tanzania imechukua hatua mbalimbali za kuzuia mikopo hii ikiwa ni pamoja na kuzitaka kampuni za simu kuhakikisha mifumo yao haitumiki katika shughuli zozote zinazohusiana na mikopo hiyo pamoja na kuendelea kutoa elimu kwa wananchi ili waepukane na kuchukua mikopo hiyo. Vile vile, Serikali inaendelea kuwafuatilia wahusika ili hatua stahiki ziweze kuchukuliwa dhidi ya wanaokiuka taratibu zilizowekwa” alisema Dkt. Nchemba.

Dkt. Nchemba alitoa rai kwa Benki Kuu ya Tanzania kuimarisha usimamizi wa sekta ya fedha hususan watoa huduma ndogo za fedha pamoja na watoa huduma za mifumo ya malipo kuhakikisha wanazingatia matakwa ya Sheria ya Benki na Taasisi za Fedha ya mwaka 2006, Sheria ya Mifumo ya Malipo ya mwaka 2015 pamoja na Sheria ya Huduma Ndogo za Fedha ya mwaka 2015. 

Aidha aliwasihi wanachi wapate huduma za fedha kwa watoa huduma rasmi wanaosiimamiwa na Benki Kuu ya Tanzania ili kuepuka kutumia huduma za fedha kutoka kwa watoa huduma wasio rasmi na masharti magumu ikiwemo riba kubwa. 

DKT TULIA ATOA RAI KWA WAANDISHI KUHABARISHA JAMII KUHUSU MAZINGIRA.

May 02, 2024

 Na Janeth Raphael -MichuziTv -Dodoma


Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Raisi wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) Dkt Tulia Ackson amaetoa Rai kwa Waandishi wa habari na Watangazaji Nchini kutumia muda wao kuandika na kuhabarisha Umma kuhusiana na Mazingira pamoja na Mabadiliko ya tabia ya Nchi.

Dkt Tulia ameyasema hayo mapema Leo hii May 2 Jijini Dodoma wakati akifungua Kongamano la wana habari kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa vyombo vya habari Duniani ambayo hufanyika May 3 kila mwaka.

"Nitoe Rai kwa Waandishi wa habari na Watangazaji kutumia muda wenu kuandika habari za kuhabarisha Umma kuhusiana na mazingira na mabadiliko ya tabia ya Nchi,hasa katika kipindi ambacho tunakipitia ambacho wakati mwingine sio mara zote watu huusisha na kila jambo linalotokea katika jamii ili mradi nila mazingira basi tunalihusisha na mabadiliko ya tabia ya nchi,Tunawategemea sana katika kuhabarisha na kuelimisha Umma kuhusu mabadiliko ya tabia ya nchi ".

Aidha Dkt Tulia amesema kuwa takwimu za Watafiti zinaonesha kuwa takribani watu milioni 16 nchini Tanzania wanategemea rasilimali za pwani kwaajili ya kuendesha maisha yao hivyo uharibifu ukitokea unaathiri hao watu wote milioni 16 hivyo wasimame hapo kuokoa mazingira pia".

"Takwimu za watafiti zinaonesha kuwa takribani watu milioni 16 nchini Tanzania wanategemea rasilimali za pwani kwaajili ya kuendesha maisha yao,na kwahiyo uharibifu wote unaotokea unahatarisha maisha ya hao watu milioni 16, Katika Muktatha huo tunawagemea Waandishi wa habari kusaidia kuokoa haya mazingira ambayo na ninyi kwa kuona umuhimu wake tunaamjni mtafanya uchunguzi lakini pia ninyi mmeweka kwenye kauli mbiu yenu kuonesha kwamba mtashiriki pamoja na sisi kwenye jambo hilo".

Awali akimkaribisha Mgeni Rasmi, Waziri wa Habari,Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe Nape Nnauye yeye amesema kuwa kazi ya vyombo vya habari hapa Nchini ni nzuri hata kama hatujafika tunakokutaka lakini tumepiga hatua sana katika sekta hii.

"Kwa kifupi niseme kazi ya ya vyombo vya habari ni nzuri hapa Nchini kama nilivyotangulia kusema, inawezekana hatujafika tunakotaka kwenda lakini tumepiga hatua kubwa na tunaendelea kusonga mbele na Serikali ya awamu ya 6 chini ya usimamizi wa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ameruambia tuache milango wazi kila tunapohitajika na kila panapohitajika kufanya marekebisho ya hapa na pale".

Kongamano hili limehudhuriwa na wadau wa Sekta ya Habari Nchini wapatao 300 wakiongozwa na Kauli mbiu isemayo:Uandishi wa habari katikati ya Changamoto za Mazingira.






CDF MKUNDA AELEZA UMUHIMU WA JKT KATIKA ULINZI WA TAIFA

May 02, 2024

MKUU wa Mkoa wa Tanga Balozi Batilda Burian akikagua gwaride kabla ya kufunga mafunzo ya  awali ya ya Kijeshi kwa vijana wa kujitolea Operesheni miaka 60 ya JKT kikosi cha Jeshi 838 Maramba 

MKUU wa Mkoa wa Tanga Balozi Batilda Burian akikagua gwaride kabla ya kufunga mafunzo ya  awali ya ya Kijeshi kwa vijana wa kujitolea Operesheni miaka 60 ya JKT kikosi cha Jeshi 838 Maramba 

MKUU wa Mkoa wa Tanga Balozi Batilda Burian akizungumza wakati  alipofunga mafunzo ya  awali ya ya Kijeshi kwa vijana wa kujitolea Operesheni miaka 60 ya JKT kikosi cha Jeshi 838 Maramba 

Mwakilishi wa Mkuu wa Majeshi la Ulinzi Tanzania Brigedia Jenerali Abubakari Charo akizungumza wakati wa ufungaji wa mafunzo ya awali ya ya Kijeshi kwa vijana wa kujitolea Operesheni miaka 60 ya JKT kikosi cha Jeshi 838 Maramba 


Mwakilishi wa Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa Kanali Elias Sikaponda akizungumza wakati wa ufungaji wa mafunzo ya awali ya ya Kijeshi kwa vijana wa kujitolea Operesheni miaka 60 ya JKT kikosi cha Jeshi 838 Maramba

MKUU wa Kikosi cha Jeshi 838 JKT Maramba Kanali Ashraf Hassan akizungumza  wakati wa mafunzo hayo



Na Oscar Assenga,MKINGA.


MKUU wa Majeshi la Ulinzi Tanzania Jenerali Jacob Mkunda amesema mafunzo ya awali ya ya Kijeshi kwa vijana wa kujitolea Operesheni miaka 60 ya JKT kikosi cha Jeshi 838 Maramba huku akieleza umuhimu wa vijana hao ni mkubwa kutokana na kwamba wanaingia kwenye Jeshi la akiba ambalo inapotokea hitajiko la ulinzi wa Taifa wanaitwa kwa mujibu wa sheria.

Mkunda aliyasema hayo Jumanne Aprili 30 mwaka huu wakati wa ufungaji wa mafunzo hayo ambapo aliwakilishwa na Brigedia Jenerali Abubakari Charo ambapo alisema kutokana na miongozo mbalimbali iliyopo kwa mafunzo hayo ya vijana hasa kwa kuzingatia kwamba vijana hao wanapohitimu mafunzo yao wanaingia kwenye jeshi la akiba.

Alisema kwamba linapotokea hitajiko la ulinzi wa Taifa na Rais na Amri Jeshi Mkuu akatangaza hali ya hatari vijana hao wanaitwa kwa mujibu wa sheria kwenda kuungana na Jeshi la Wananchi (JWTZ) kulinda ulinzi wa Taifa.

Aidha alisema kutokana na umuhimu wa vijana kwenye Jeshi hilo wanapenda kuona wanafikia viwango na malengo ya mafunzo hayo na amewaona wamefikia viwango vinavyotakiwa huku akieleza yanawajenga kwenye nidhamu, ukakamavu, uzalengo, uhodari wa kujiamini na kulipenda taifa lao.

“Nichukue fursa hii kwa niaba ya Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi kutoa shukrani kwa dhati kwa Serikali kwa juhudi zinazofanyika kuhakikisha mazingira ya mafunzo kwa vijana ndani ya JKT yanaboreshwa”Alisema

“Kwani katika mwaka wa fedha 2023/2024 Serikali imetoa kiasi cha sh Milioni 950 kwa ajili ya ujenzi wa mabweni kwa vijana wanaojiunga na JKT fedha hizo zimeweza kujenga mabweni 12 kila moja lenye uwezo wa kuchukua vijana 120 hivyo kusaidia kikosi kuongeza uwezo kuchukua vijana 1440 na hii ni ishara za wazi kwamba serikali inatambua na kuthamini mafunzo ya vijana wa JKT”Alisema

“Lakini pia ujenzi wa vyoo vitano ambapo kila choo kina matundu 22 vitatumika kwa vijana hilo sio suala dogo ni jambo kubwa ambalo serikali imefanya kwa mazingira hayo wanawaomba vijana ambao hawapati fursa kujiunga na JKT wasije kufikiria wametengwa na kunyimwa fursa bali lengo vijana wote wapite Jkt na wale vijana wanaomaliza kidato cha sita”Alisema

Hata hivyo alisema kwamba Jeshi la Kujenga Taifa litakuwa likiendelea kuongozewa uwezo huku akieleza wanathamini juhudi za serikali katika kuboresha mazingira ya jeshi hilo ambapo mafunzo ambayo wameyapata yatawawezesha kuajiriwa kwenye vyombo vya ulinzi na usalama,sekta mbalimbali za serikali au makampuni mbalimbali .

Awali akizungumza wakati akifunga mafunzo hayo Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi Batilda Burian alisema mafunzo hayo kwa vijana wa JKT ni muhimu sana kwa vijana kwa maana wao ndio tegemeo la Taifa.

Balozi Batilda alisema Rais Dkt Samia Suluhu kupitia falsafa yake ya 4R ameendelea kusimamia na ndio maana juzi chadema walikuwa na maandamano yao wakasimamiwa vizuri na jeshi la Polisi wakafanya mkutano wao wakatembea.

Alisema kwa hakika wakawa na matumaini watapata mambo ya msingi yatakayowasaidia kujenga nchi lakini wakasikia mambo tofauti kwanini wakuu wa mikoa hawapigiri kura, kama madiwani sasa akasema hata RC akipigiwa kura atachaguliwa Tanga na RC ni msaidizi wa Rais anaweza kuhamishwa kila eneo .


“Tulitegemea kwamba hivi sasa nchi ipo kwenye kipindi kigumu na mvua zinanyesha madhara maeneo mengi barabara nyingi zimepata changamoto na maeneo mengi lami zimepasuka changamoto ni nyingi vita vya israel vinaendelea duniani gharama zinapanda bei ya dola ipo kubwa kulingana na bei yetu sisi tukaona haja hoja zao za za kwamba hazikuwasaidia wakapata mawazo mbadala hazipo"Alisema

Hata hivyo Mwakilishi wa Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa Kanali Elias Sikaponda alisema kwamba alisema mafunzo hayo ni muhimu kwa sababu yanaleta tija kwa vijana katika shughuli za kujitegemea huku akiwataka kujiepusha na matumizi ya dawa za kulevya

Aliwataka pia vijana hao kutumia elimu waliyoipata wakaweze kutatua changamoto mbalimbali pasipo kuvunja sheria na taratibu zilizowekwa hapa nchini huku akisiistiza watumie nidhamu pekee kama silaha kwenye jambo lolote mbeleni.