Na Oscar Assenga,Lushoto.
MSANII Gwiji wa filamu Tanzania, Charles Magari maarufu kama "Mzee wa Magari" amewaasa wasanii chipukizi wa tasnia hiyo nchini kutambua kuwa sanaa ni kazi kama zilivyo nyingine ambayo inaweza ‘kumtoa’ kijana kutoka kwenye umaskini na kuwa katika hali nzuri ya kimaisha.
Aliyasema
hayo mwishoni mwa wiki kwenye sherehe za uzinduzi wa Filamu mpya iitwayo “Hulka”
iliyofanyika mjini Lushoto, Mkoani Tanga ambapo iliwashirikisha wasanii
wengine nguli kama Mzee Jengua, Davina, Birigita na Sekuti.
Magari
alisema vijana wengi wanaonekana wakipoteza muda kwenye vijiwe wakipiga
porojo zisizo na tija huku wakilalamikia hali duni ya maisha yao
wakidai kuwa hawana ajira.
“
Ajira huwezi kuipata kwa kukaa tu na kulalamika kwani fursa ya
kujiajiri imepanuka sana”, alisema Magari na kuongeza, tasnia ya sanaa
bado inahitaji vijana wengi wenye kujituma.
Alieleza
kuwa nia ya kuja kuzindua filamu hiyo ni kutaka kuwapa fursa
vijana wa wilaya ya Lushoto kujifunza maudhui yaliyomo katika filamu
hiyo na kuchukua hatua ya kujisahihisha.
Katika
filamu hiyo washiriki wanaigiza tabia ya kabila fulani ambalo
halikutajwa ambapo mwanamke aliyeolewa huona hapendwi asipopigwa na muwe
mara kwa mara.
Nafasi ya mume anacheza Sekuti ambapo Biligita anachukua nafasi ya mke,Mume ni mtoto wa Mzee Jengua na mke ni binti ya Mzee Magari.
Akizindua
filamu hiyo kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Lushoto,Majid Mwanga, Ofisa Utamaduni wa
wilaya hiyo, Ezekiel Almas alisema wakati sanaa inaanza kukubalika
katika jamii, upo umuhimu kwa washiriki hao kujali na kudumisha tamaduni
za kiafrika.
Almas
aliitaka jamii kuondoa dhana iliyojengeka katika baadhi ya watu kwamba
usanii ni uhuni ambapo alieleza uhuni ni tabia ya mtu binafsi sio fani
yake.
Meneja wa Creator Entertainment iliyoandaa sherehe hizo, Mwanahawa Chongole alisema
kampuni yake ilikubali kuchukua jukumu la kuandaa sherehe hizo kutokana
na kutambua umuhimu wa maudhui yaliyomo ndani ya filamu hiyo kwani
inatoa ujumbe utakaoelimisha jamii kwa ufasaha.
Mwisho.
|
Tanga Warriors yaiadhiri City Kings yaibamiza Vikapu 46-37.
Na Oscar Assenga,Tanga.
|
Subscribe to:
Posts (Atom)