RAIS DKT. MAGUFULI AMUAPISHA MRISHO GAMBO KUWA MKUU WA MKOA WA ARUSHA, PIA AKUTANA NA RAIS MSTAAFU WA BENKI YA MAENDELEO YA AFRIKA (AfDB) DKT. DONALD KABERUKA IKULU JIJINI DAR ES SALAAM.

August 20, 2016

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Mrisho Gambo kuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Rais Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha na Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa pamoja na Mkuu mpya wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo mara baada ya tukio la Kiapo Ikulu jijini Dar es Salaam. Wengine katika picha ni Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi wa kwanza (kulia) na Naibu Waziri, Ofisi ya Rais Tawala za mikoa  na Serikali za Mitaa TAMISEMI Selemani Jafo wa kwanza (kushoto).
 Rais Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo mara baada ya kumuapisha Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan akimpongeza Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo mara baada ya kuapishwa Ikulu jijini Dar es Salaam.
  Rais Dkt. John Pombe Magufuli akimkaribisha Rais Mstaafu wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dkt. Donald Kaberuka aliyefika Ikulu kwa ajili ya mazungumzo.
 Rais Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Rais Mstaafu wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dkt. Donald Kaberuka mara baada ya kumaliza mazungumzo yao Ikulu jijini Dar es Salaam. Picha na IKULU.

JESHI LA POLISI LAPIGA MATIZI YA UTAYARI WA KUKABILIANA NA MATUKIO YA UHALIFU NA WAHALIFU NCHINI

August 20, 2016


Askari wa kikosi cha kutuliza ghasia wa wakiwa moja ya maozezi yao ya kupasha viungo kabla ya kuanza mazoezi ya kutuliza ghasia.
Askari Polisi wa kikosi maalum cha polisi (CRT) wa mkoa wa Iringa wakiwa katika mazoezi ya utayari wa kukabiliana na matukio yoyote yatakayojitokeza katika maeneo mbalimbali.
Askari wa vikosi vya kutuliza ghasia wa mikoa mbalimbali wakiwa na magari yao wakati wa mazoezi ya utayari wa kupambana na matukio mbalimbali ya uhalifu na wahalifu katika maeneo mbalimbali.
Askari wa vikosi vya kutuliza ghasia wa wakiwa na magari yao wakati wa mazoezi ya utayari wa kutuliza ghasia na kukabiliana na matukio yoyote ya uhalifu na wahalifu.
Askari wa kikosi cha kutuliza ghasia mkoa wa Lindi wakifanya mazoezi magumu ya kijiweka tayari kukabiliana na matukio yoyote yatakayojitokeza ikiwemo watu wasiotii amri za Jeshi la Polisi ikiwa ni pamoja na kutofuata sheria za nchi.
Askari Polisi wa vikosi vya kutuliza ghasia wa wa mikoa ya Lindi, Iringa, kanda maalumu ya Dar es salaam na mikoa mengine wakipokea maelekezo mbalimbali wakati wa mazoezi ya tayari katika kukabiliana na matukio mbalimbali ya uhalifu na wahalifu (Picha zote na makao makuu ya Jeshi la Polisi.)

MLEMAVU AOMBA AJIRA KWA WATANZANIA

August 20, 2016


Hujafa hujaumbika! Erasto Mketo (26) ni mkazi wa Lindi kijiji cha Mtondo Kimwaga, ni mlemavu wa miguu na mikono ambaye ana ndoto nyingi za kujikwamua kimaisha kama kijana mwingine wa Kitanzania, lakini ulemavu wake umekuwa changamoto kubwa ya yeye kuweza kufanikisha ndoto zake.

Moja ya changamoto zinazomkuta Erasto ni pamoja na unyanyapaa hasa kwenye sekta ya ajira jambo lililomfanya apaze sauti na kuwaomba Watanzania wajitokeze kumsaidia hata kwa kumpa mtaji au ajira ili aweze kujikwamua kimaisha.

Akiongea na mwandishi wa Blogs za Mikoa Tanzania, Erasto alisema anaamini anaweza kufanya biashara yoyote kama muajiriwa au kama atapewa mtaji wa kufungua biashara yake mwenyewe.

“Kwa huku kijijini nimekuwa nikipata tabu sana ya kupata ajira ambayo itaendana na ulemavu wangu na elimu yangu ya shule ya msingi, lakini ningependa sana nitimize ndoto zangu kwa sababu naweza sana kufanya biashara.

“Nawaomba watanzania wenzangu mnisaidie hata kwa kuniajiri ili mradi na mimi nijikwamue kiuchumi kama wenzangu na hata niweze kuwasaidia wazazi wangu,” alisema Erasto huku akiongeza kuwa baiskeli ya kutembelea atainunua mwenyewe kupitia ajira yake ikiwa atapata mtu wa kumuajiri.

Kutoa ni moyo si utajiri, kama umeguswa tafadhali msaidie Mtanzania mwenzako kwa hali na mali kupitia namba 0682755874, imesajiliwa kwa jina la Anastansi Ngomba.

                                              
Regards Tone Multimedia Company Limited Plot No.223/225 Block 46, Umoja Street Kijitonyama P.O Box 32529 Dar es salaam Tanzania Tel +255 22 2772919 Fax +255 22 2772892 E-Mail blogszamikoa@live.com Facebook: www.facebook.com/blogszamikoa Web: www.blogszamikoa.com 1458109219454_logo_blog_za_mikoi.png

MLIMBWENDE WA TAJI LA MISS MWANZA 2016 APATIKANA

August 20, 2016
Usiku wa jana Ijumaa Agost 19,2016 kuamkia leo Jumamosi Agost 20,2016, kulikuwa na mtifuano mkali wa kumtafuta mlimbwende wa taji la MISS MWANZA 2016 ambapo warembo 16 kutoka wilaya mbalimbali mkoani Mwanza walijitosa kusaka taji hilo.

Ilikuwa ni furaha kubwa kwa mrembo, Mary Peter (katikati), pale alipotangazwa kuwa MISS MWANZA 2016. Pia mwendelezo wa furaha uliwaendea warembo, Victoria Boniphace (kushoto) aliyetangazwa Miss Mwanza nambari mbili na Winnie Shayo (kulia), aliyetangazwa Miss Mwanza nambari tatu.

Kinyang'anyiro cha Miss Mwanza 2016, kiliandaliwa na Kampuni ya "Big D Entertainment" na baada ya kinyang'anyiro hicho, unafuata mtifuano wa MISS LAKE ZONE 2016 utakaofanyika Septemba 10,2016 ambapo washiriki wa Miss Mwanza 2016 waliongia nafasi tano bora, wanashiriki moja kwa moja kwenye shindano hilo.
Na BMG
Miss Mwanza 2015, Donny Roberty (kushoto), akimkabidhi taji Miss Mwanza 2016, Mary Peter (kulia) baada ya kuibuka mshindi wa shindano hilo.
Washiriki wa Miss Mwanza, walioingia nafasi tano bora
Warembo walioshiriki Miss Mwanza 2016
Warembo walioshiriki Miss Mwanza 2016.
Warembo walioshiriki Miss Mwanza 2016
Majaji walikuwa na Kazi pevu kuchagua mshindi
Baadhi ya waliohudhuria kwenye tukio
Msanii Elizayo HB kutoka Jijini Mwanza akidondosha burudani kwenye Miss Mwanza 2016
Burudani za kiafrika pia zilikuwepo
Mkali wa Moyo Mashine, Ben Pol, alidondosha burudani poa sana
Ben Pol kazini
Kupitia BMG, Ben Pol, aliwashukuru wakazi wa Jiji la Mwanza kwa namna wanavyopenda kazi zake na kuahidi kufanya kazi nzuri zaidi.
Miss Mwanza 2016 aliiambia BMG kwamba, maandalizi yake mazuri ndiyo yaliyompa fursa ya kunyakua taji hilo na kwamba amejiandaa vyema kwa ajili ya taji la Miss Lake Zone 2016 na pia Miss Tanzania 2016.
Miss Mwanza 2016 nambari mbili akibonga na BMG. Anasema shauku yake ni kuongeza juhudi zaidi ili kunyakua taji la Miss Lake Zone 2016.

Taswira;Uzinduzi rasmi wa msimu wa Tigo Fiesta 2016 jijini Mwanza

August 20, 2016
Waziri wa habari, utamaduni na michezo, Mhe. Nape Mnauye akiongea na wakazi wa mkoa wa Mwanza wakati wa uzinduzi wa msimu wa Tigo Fiesta 2016 kwenye viwanja vya Furahisha jana. 
 Waziri wa habari, utamaduni na michezo,  Mhe. Nape Mnauye akizindua rasmi msimu mpya wa Tigo Fiesta 2016 kwa kunyanyua juu bendera maalum kwa kushirikiana na wafanyakazi wa kampuni ya Tigo na viongozi mbalimbali kwenye viwanja vya furahisha jijini Mwanza jana. 

 Waziri wa habari, utamaduni na michezo,  Mhe. Nape Mnauye akizindua rasmi msimu mpya wa Tigo Fiesta 2016 kwa kunyanyua juu bendera maalum kwa kushirikiana na wafanyakazi wa kampuni ya Tigo na viongozi mbalimbali kwenye viwanja vya furahisha jijini Mwanza jana. 

IMOOOOO!

Wanakikundi wa chuo cha kilimahewa wakitumbuiza mara baada ya uzinduizi rasmi wa Fiesta Jijini Mwanza.

Wanakikundi wa utamaduni vijana wakitumbuiza mara baada ya uzinduizi rasmi wa Tigo  Fiesta 2016 Jijini Mwanza.

Wanakikundi wa utandawazi kutoka ukeerewe wakitumbuiza mara baada ya uzinduizi rasmi wa  Tigo Fiesta 2016 Jijini Mwanza jana.



photo Best Regards Krantz Mwantepele| Managing Director KONCEPT | Mikocheni B, House No 58. Opp Clouds Media. Dar es Salaam, Tanzania | M: + 255 624053989 / +255 712579102 E: Krantz.charles@koncept.co.tz Blog: www.mwanaharakatimzalendo.blogspot.co

SERIKALI YASEMA WANAOWAPA MIMBA WATOTO WA SHULE NA KUWAOA HATA MAGEREZA YAKIJAA WATAENDELEA KUKAMATWA

August 20, 2016
 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu (wa pili kulia), akikata utepe kuashiria uzinduzi wa  mradi wa kukusanya nguvu za pamoja kulinda haki za wasichana nchini Tanzania awamu ya pili Dar es Salaam leo. Kutoka kushoto ni Mkurugenzi kutoka Shirika la CDF, Kashuma Mtengeti, Mwakilishi wa Shirika la Comic Relief Uk, DFID, Jane Miller na Mwenyekiti wa Bodi ya Jukwaa la Utu wa Mtoto (CDF), Foturnata Temu.
 Wanahabari wakichukua taarifa hiyo.
 Mwakilishi wa Shirika la Comic Relief Uk, DFID, Jane Miller, akizungumza katika mkutano huo wakati akimkaribisha Wazir Ummy Mwalimu (kulia)
 Mwenyekiti wa Bodi ya Jukwaa la Utu wa Mtoto (CDF), Foturnata Temu (kulia), akizungumza katika hafla hiyo wakati akitoa taarifa ya mradi huo.
 Wadau mbalimbali na waandishi wa habari wakiwa kwenye hafla hiyo.
 Mwakilishi kutoka Shirika la MBE FORWARD UK-Naana Otoo Oyortey akitoa mada kwenye hafla hiyo ya uzinduzi wa mradi huo.
 Mwakilishi kutoka Shirika la CDF, Kambibi Kamugisha, akitoa mada.
 Waziri Ummy Mwalimu akihutubia kabla ya kuzindua rasmi 
mradi huo

 Mwakilishi kutoka Wadada Centre, Christian Noah akitoa mada kwenye uzinduzi huo
 Mkurugenzi kutoka Shirika la CDF, Kashuma Mtengeti, akichangia jambo.
 Waandishi wa habari wakiwa kazini.
 DK. Flora Myamba kutoka Repoa akitoa mada kwenye 
uzinduzi huo.
Christine Mwanukuzi kutoka shirika la UNFPA, akichangia jambo.


Na Dotto Mwaibale

SERIKALI imesema hata magereza zikijaa itaendelea kuwakamata na kuwachukulia sheria kali wanaume wote wataka0 bainika kuwaoa au kuwapa  mimba wanafunzi.

Hayo yalisema na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto wakati akizindua mradi wa kukusanya nguvu za pamoja kulinda haki za wasichana nchini Tanzania awamu ya pili Dar es Salaam leo.

Mwalimu alisema kuwa hata magereza yakijaa kwa kiasi gani serikali haitasita kuwakamata watuhumiwa hao bila ya kuwaonea huruma bila ya kujali mtuhumiwa ni mtu wa namna gani.

"Nawaagiza maofisa Ustawi wa Jamii wote katika ngazi ya mikoa, wilaya na Kata kuhakikisha haki za mtoto zinalindwa nchini kote hususan mtoto wa kike. Ninataka wahakikishe wale wote wanao wapa watoto wa shule mimba na wanao waozesha au kuoza wanakamatwa na kuchukuliwa hatua haraka kwani sheria za kuwalinda watoto zipo, kinachotakiwa sasa ni utekelezaji" alisema Mwalimu.

Waziri Mwalimu alisema Tanzania ni miongoni mwa nchi zenye kiwango cha juu cha ndoa za utotoni ambapo taarifa ya Demografia na Afya ya mwaka 2010 zimeonesha kuwa kwa wastani wanawake 2 kati ya watano Tanzania wa umri wa miaka 15-49 waliolewa kabla ya kufikisha umri wa miaka 18.

Aliongeza kuwa utafiti wa hali ya afya ya uzazi, mtoto na malaria wa mwaka 2015/16 unaonesha kuwa idadi ya wasichana wanaopata watoto katika umri wa miaka 15-19 imeongezeka kufikia asilimia 27 mwaka 2015 kutoka asilimia 23 mwaka 2010 na kuwa tatizo hilo lipo zaidi katika mikoa ya Katavi kwa asilimia 36.8, Tabora, asilimia 36.5, Simiyu asilimia 32.1, Geita asilimia 31.6 na Shinyanga kwa asilimia 31.2.

Mwenyekiti wa Bodi ya Jukwaa la Utu wa Mtoto (CDF), Foturnata Temu alisema katika kudumisha harakati za kupambana dhidi ya vitendo vya ukatili wa kijinsia na mimba za utotoni vinavyoendelea kuwakumba wasichana nchini Tanzania, CDF, Chama cha Uzazi na Malezi (Umati) na Kituo cha Wadada Centre wameamua kuzindua mradi huo kwa pamoja ili kulinda haki za wasichana hapa nchini.