KINANA AWASILI MOSHI VIJIJINI KWA KISHINDO, MSAFARA WAKE WAPOKELEWA NA FARASI

KINANA AWASILI MOSHI VIJIJINI KWA KISHINDO, MSAFARA WAKE WAPOKELEWA NA FARASI

March 24, 2015

Msafara wa katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana ukipokelewa kwa farasi wakati alipowasili katika kijiji cha Mikocheni TPC wakati alipoanza ziara yake ya kukagua na kusimamia ilani ya uchaguzi ya CCM katika jimbo la Moshi Vijijini akitokea jimbo la hai ambapo alimaliza ziara kama hiyo jana, Kinana akiwa katika jimbo la Moshi vijijini atashiriki shughuli mbalimbali za maendeleo pamoja na wananchi na kuhimiza uhai wa Chama Cha Mapinduzi CCM jimboni humo akiongozana na Nape Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM.(PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-MOSHI VIJIJINI- KILIMANJARO) 3 4 
Farasi wakiongoza msafara huo ulipowasili kijiji cha Mikocheni TPC Moshi vjijini. 5 
Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM akisalimiana na Mbunge wa viti maalum kutoka mkoa wa Kilimanjaro Mh. Betty Machangu. 7 
Msafara wa katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiongozana na Mbunge wa jimbo la Moshi Vijijini Mh. Cyril Chami kulia wakati alipowasili katika kijiji cha Mikochenzi. 8 
Umati wa wananchi wakimpokea. 10 
Mbunge wa jimbo la Moshi Vijijini Mh. Dr. Cyril Chami akizungumza na wananchi katika kijiji cha Mikocheni. 13 
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Ndugu Leonidas Gama akwasalimia wananchi katika kijiji cha Mikochenzi. 14 
Rais Kikwete akagua waathirika wa Mafuriko Buguruni

Rais Kikwete akagua waathirika wa Mafuriko Buguruni

March 24, 2015

1
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akikagua kazi ya kuondoa maji ya mafuriko kutoka katika nyumba za watu katika eneo la Buruguruni Mnyamani wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam leo wakati Rais na Mkewe Mama Salma Kikwete na viongozi mbalimbali walipotembelea eneo hili kujionea athari za mafuriko na kuwafariji wananchi.
3
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimfariji mmoja wa wakazi wa Buguruni Mnyamani Bi.Halima Hamza ambaye nyumba yake imeathiriwa vibaya na maji ya mafuriko wakati Rais na Mkewe Mama Salma Kikwete na viongozi mbalimbali walipotembelea eneo hili kujionea athari za mafuriko na kuwafariji wananchi.
4
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimsalimia mtoto Irene ambaye nyumba yao imeathiriwa na mafuriko huko Buguruni Mnyamani leo.
5 6
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Mack Sadik akimuonesha Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete mfereji ulioziba kutokana na uchafu na kusababisha mafuriko katika makazi ya watu eneo la Buguruni Mnyamani jijini Dar es Salaam leo.
7 8
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwahutubia wakazi wa Buguruni Mnyamani waloathiriwa na mafuriko kufuatia mvua kubwa zinazoendelea kunyesha jijini Dar es Salaam.Rais Kikwete ameahidi kuwasaidia wananchi hao
9 10
Rais Kikwete na Mama Salma Kikwete wakipita katika mitaa mbalimbali ya Buguruni leo wakati wa zoezi la kuwafariji waathirika wa mafuriko huko Buguruni Mnyamani leo.
(picha na Freddy Maro)

WIZARA YA NISHATI NA MADINI YATANGAZA UFADHILI WA MASOMO NCHINI CHINA KWA MWAKA 2015

March 24, 2015

 Msemaji wa Wizara ya Nishati na Madini, Badra Masoud akizungumza na wanahabari.
  Msemaji wa Wizara ya Nishati na Madini, Badra Masoud akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo asubuhi, kuhusu ufadhili wa masomo nchini China kwa mwaka 2015. Kulia ni Ofisa Habari wa Maelezo, Fatma Salum.
 Mwanahabari Salome Kitomari kutoka gazeti la Nipashe, akiuliza maswali katika mkutano huo.
 Wanahabari kutoka vyombo mbalimbali wakichukua taarifa hiyo.
Hapa mkutano ukiendelea. ……………………………………….

Na Dotto Mwaibale
WIZARA ya Nishati na Madini imetangaza nafasi za masomo kwa vijana wa Tanzania kwa ufadhili wa Serikali ya Watu wa China kwa kipindi cha mwaka 2015.
Hayo yalibainishwa na Msemaji wa Wizara hiyo Badra Masoud Dar es Salaam leo wakati akizungumza na wanahabari.
Alisema nafasi hizo za masomo ni ngazi ya Shahada ya Juu ya Uzamili katika fani ya gesi katika Chuo Kikuu cha Jiosayansi cha China ambapo muda wa kutuma maombi hayo umeongezewa hadi kufikia Machi 30 mwaka huu.
Alisema waombaji wa ufadhili huo wanatakiwa kuwa na Shahada ya Sayansi ya Ardhi au Uhandisi kutoka vyuo vinavyotambuliwa na serikali, na muombaji awe na miaka kati ya 35 na 40.
Katika hatua nyingine Masoud alisema mitambo ya kuchakata gesi imekamilika kwa asilimia 96.
Alisema kukamilika kwa mitambo hiyo inamanufaa makubwa ikiwemo umeme wa uhakika na gharama nafuu kwani utekelezaji wa mradi huo utaliwezesha taifa kuokoa trilioni 1.6 kwa mwaka zinazotumika kununua mafuta kwa ajili yua kuzalisha umeme.
Masoud  alisema kukamilika kwa mradi huu kutachochea  maendeleo ya viwanda nchini kwani viwanda vingi vimeonyesha nia ya kutumia nishati  ya gesi asilimia  katika  kuendesha mitambo  yake  ya uzalishaji.aidha umeme wa uhakika utapunguza gharama za uzalishaji na kufanya  bidhaa za tanzania kukuzika katika masoko mbalimbali duniani.
Alisema tatizo la ajira nalo litapungua kutokana na kukamilika kwa mradi huu ambao utapelekea ajira  mpya  nyingi  kupatikana na kutokana na kuwepo kwa umeme wa kutosha na uhakika katika viwanda ambapo  viwanda  vingi vitaanzishwa vilevile umeme utakwenda mashambani na kwenye biashara nyingine hivyo kwa namna moja ama nyingine ajira  zitaongezeka.
Alisema gesi hiyo asilia pia hutumika kama malighafi katika viwanda mbalimbali kama,mbolea, kemikali,aluminiamu pamoja na kutengeneza vifaa vya plastiki uanzishaji wa viwanda vipya kutokana na matumizi ya gesi  asilimia kutachochea .
kukua kwa uchumi  wa nchi yetu na kwa upatikanaji wa ajira mpya nyingi kwa vijana wetu.
Aliongeza kuwa Serikali kupitia wizara hiyo chini ya Mradi Endelevu wa Usimamizi wa Rasilimali Madini (SMMRP), inakaribisha maombi ya Ruzuku Awamu ya pili kwa wachimbaji wadogo nchini.
(Imeandaliwa na mtandao wa www.habari za jamii.com)

Diamond Motors wazindua gari jipya la Mitsubishi 2015 ASX jijini Dar es Salaam

Diamond Motors wazindua gari jipya la Mitsubishi 2015 ASX jijini Dar es Salaam

March 24, 2015

1
Hili ndilo gari la ASX Mitsubish jipya lililozinduliwa hivi karibuni katika hoteli ya serena jijini Dar es Salaam.
2 3
Wema Sepetu akiwasha gari Jipya la ASX Mitsubishi katika uzinduzi wa gari hilo jijini Dar es Salaam.
………………………………………………………………………..
Na Mwandishi wetu Dar es Salaam
Mtangazaji wa Clouds FM, Millard Ayo na mwigizaji maarufu nchini, Wema Sepetu wamesifia gari jipya la Mitsubishi ASX la mwaka 2015 linalouzwa na kusambazwa na kampuni ya Diamond Motors (Hansa Group). Katika uzinduzi wa kutambulisha gari hilo uliofanyika mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam, pamoja na mambo mengine Kampuni ya Diamond Motors wauzaji pekee wa magari kutoka Mitsubishi waliwaalika Millard Ayo na Wema Sepetu kujaribu gari hilo toleo jipya Mitsubishi ASX kabla ya uzinduzi. Mastaa hao walivutiwa na mwonekano wa Mitsubishi ASX lenye vioo vya kisasa juu vyenye mwanga unaomwezesha dereva na abiria kufurahia mwonekano wa pande zote. Meneja mauzo wa Diamond Motors, Reena Ganatra alisema Gari hilo lenye luninga ndogo inayocheza DVD, iPods, Bluetooth na sauti kutoka vyanzo mbalimbali ni maalumu kwa vijana wa kisasa na familia kwani Mitsubish ASX limetengenezwa na teknolojia ya MIVEC yenye kulifanya liwe na nguvu ya 150 ps katika 6,000 rpm na nguvu ya kuzunguka kwa mwendokasi mkubwa na kwamba limetengenezwa maalum kutumia mafuta kidogo. “ASX ni mwanzo tu, tunazo aina nyingine za magari kama kama Pajero ambayo tunakaribia kuyatambulisha sokoni ili kuwapatia watanzania magari imara na yenye kuaminika kutoka Mitsubishi” Alisema Ganatra. ASX toleo la 2015 limebuniwa kwa ubora wa hali ya juu na imara likiwa na bodi gumu pia lina mfumo maalumu usiotegemea funguo hivyo kumfanya mwendeshaji kuwasha injini kwa kubofya kitufe. “ASX kutoka Mitsubishi, imetengenezwa maalumu kukidhi mazingira ya Tanzania hasa mijini kama Dar es Salaam ambapo muda wowote dereva wa kawaida anatoka kwenye barabara nzuri na kuingia kwenye barabara zenye makorongo” alisema Ganatra Injini ya gari hilo ambayo ni 2.0-liter imeunganishwa INVECS-III CVT inayoisaidia mwendelezo wake katika kubadili mwendo pamoja na uimara wa usukani unaosaidia mikono ya dereva kuwa salama hata anapokuwa katika mwendo mkali. Hansa Group inayofanya biashara kama Diamond Motors Limited, imekuwa ikifanya kazi ya katika sekta ya usafirishaji tangu mwaka 1980, ikitoa huduma kwa wasambazaji na wadau wa usafiri.Kampuni hiyo huhusika na bidhaa/ huduma mbalimabali. Shughuli za Hansa Group zimesambaa karibu nchi zote za jumuia ya Africa ikitoa huduma kama vile za uchimbaji, Umeme, Mafuta na Gesi, Reli,Ulinzi, Ujenzi, Usafiri, kimataifa na jumuhia za kimataifa.
MATUKIO BUNGENI MJINI -DODOMA

MATUKIO BUNGENI MJINI -DODOMA

March 24, 2015

001
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Jenista Mhagama akisoma Muswada wa Sheria ya Udhibiti na Umamizi wa Dawa za Kulevya wa mwaka 2014 , Bungeni mjini DOdoma Machi 24, 2015
002
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiteta na Waziri wa Maendeleo ya jamii, Jinsia na Watoto, Sophia Simba Bungeni mjini Mjini Dodoma Machi 24, 2015.
(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
003
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akifurahia jambo katika mazungumzo na waandishi wa habari kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma  Machi 24, 2015. Kushoto ni Naibu Waziri wa Fedha, Adam Malima.

BULEMBO AGEUKWA NA WAJUMBE WAKE SAKATA LA KWENDA KWA LOWASSA.

March 24, 2015

Mjumbe wa Baraza la Wazazi, Taifa na Mbunge wa Korogwe, Steven Ngonyani ‘Prof .Maji Marefu’ akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma hii leo juu ya tuhuma za yeye kutajwa na mmoja wa wajumbe wa baraza hilo kuwa aliratibu na kulazimisha baadhi ya wajumbe wa baraza hilo kwenda kumuona Mbunge wa Munduli na Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa. 
Naye Mbunge wa Korogwe
Vijijini, Stephen Ngonyani, alisema yeye alielezwa kuhusiana na safari hiyo na rafiki yake Vioroka Kajoko.
“Nimekuwa katika jumuiya hii
kwa miaka 15. Siko tayari kuchaguliwa kiongozi, marafiki wala maadui. Mimi siko
tayari  uomba radhi kwasababu sina kosa
nililotenda,”alisema Ngonyani. 
Alisema hajawahi kumshawishi
mtu wala kumlazimisha mtu kumpenda mtu anayempenda yeye.
 Jackline Ngonyani aliyejitambulisha kwa Lowassa kama ‘Maji mafupi’ na kutoa salam za shukrai kwa wana Ruvuma kwa jinsi Lowassa alivyo shiriki katika mazishi ya Capt.John Komba lakini jana aliwaambia waandishi wa habari kuwa alilazimishwa kushiriki katika msafara huo. Lakini wenzake wanasema yeye alikuwa mmoja wa waratibu.
Mjumbe wa Baraza Kuu la Wazazi mkoa wa Njombe, Evarist Lupenza,  akizungumza na waandishi wa habari juu ya safari yao kwenda kwa Lowassa. Pamoja nae ni Mwenyekiti wa Jumuia ya Wzazi mkoa wa Mwanza, Malila Lugoye.
  Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo Mkoa wa Dodoma, Dk.
Damas Mukassa, akiwaonesha waandishi wa habari picha ambayo mjumbe mwenzao alisema wamelazimishwa kwewnda kwa Lowassa jinsi alivyo kula pozi na Lowassa.
*********************
VIONGOZI waliotajwa na Mwenyekiti
wa Jumuiya ya Wazazi ya CCMTaifa, Abdallah Bulembo, kuratibu safari ya baadhji
ya wajumbe wa jumuia hiyo na baraza la Wazazi Taifa kwenda kumsalimia Waziri
Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Monduli Edward Lowassa leo wamekanusha vikali
kuhusika na uratibu wa baraza hilo.
Jana Bulembo aliwashukia wajumbe
waliokwenda nyumbani kwa Waziri Mkuu wa Zamani, Edward lowassa,na kumchakingaia
fedha na kumshawishi  agombee Urais na
kuwataka waombe radhi kutumia jina la baraza hilo na kasha kusubiri  kamati ya maadili.
Wakizungumza hii leo baadhi ya
wajumbe hao wamewataja waratibu walioongoza msafara wao kuwa ni pamoja na
Katibu wa CCM Wilaya ya Hanang, Vioroka Kajoro na Mjumbe wa baraza hilo kutoka mkoani
Ruvuma, Jackline Ngonyani na Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo Mkoa wa Dodoma, Dk.
Damas Mukassa.
Mjumbe wa jumuiya hiyo kutoka
Mkoa wa Njombe, Evarist Lupenza, alisema aliyekuwa akiandika majina ya wajumbe
waliokwenda katika ziara hiyo ni Jackline Ngonyani. 
“Niliwasikia wakisema kwa Mzee
ni saa tatu, nikawauliza mnataka kwenda wapi, wakaniambia kuwa wanataka kwenda
kumsalimia Lowassa, name nikaandikisha jina kwa ajili ya kwenda huko,”alisema
Lupenza.
Nae Mwenyekiti wa Jumuia ya
Wazazi mkoa wa Mwanza, Malila Lugoye alibainisha kuwa hakuna mtu
aliyeshinikizwa katika safari hiyo na ilikuwa ni huru kuamua kwenda au kubaki.
 “Hakuna mtu aliyeshinikizwa kwenda kwa Lowassa
kila mtu alikwenda kwa mapenzi yake. Na hakuna mtu aliyetumia jina la Jumuiya
wakati tulipokwenda bali watu walijitambulisha mmoja mmoja,”alisema na kuungwa
mkono na Mwenyekiti wa jumuiya hiyo Mkoa wa Mwanza, Malila Lugoye.
Naye Mbunge wa Korogwe
Vijijini, Stephen Ngonyani, alisema yeye alielezwa kuhusiana na safari hiyo na
rafiki yake Vioroka Kajoko.
“Nimekuwa katika jumuiya hii
kwa miaka 15. Siko tayari kuchaguliwa kiongozi, marafiki wala maadui. Mimi siko
tayari  uomba radhi kwasababu sina kosa
nililotenda,”alisema Ngonyani.
Alisema hajawahi kumshawishi
mtu wala kumlazimisha mtu kumpenda mtu anayempenda yeye. 
 Dk Mukassa alisema yeye aliratibu ziara hiyo
kama mwenyeji wa mkoa wa  Dodoma ambaye
anakufahamu nyumbani kwa Lowassa.
 Alisema fedha walizotoa kwa ajili ya
kumchangia kuchukua fomu za Sh 600,000 zimetokana na mchango wao wenyewe kama
wanachama wa kikundi cha kusaidia cha wajumbe wa jumuiya hiyo.
“Fedha zile hazikutoka kwenye
jumuiya ya chama wala hakuna aliyekwenda pale kuwakilisha jumuiya na
niliwaeleza pale mliponiuliza na kila mtu alijitambulisha kama yeye,”alisema
AMBASADA LU YOUQING NA MHE .MASELE WAZUNGUMZA JUU YA MKUTANO WA JUKWAA LA VIONGOZI VIJANA AFRIKA NA CHINA

AMBASADA LU YOUQING NA MHE .MASELE WAZUNGUMZA JUU YA MKUTANO WA JUKWAA LA VIONGOZI VIJANA AFRIKA NA CHINA

March 24, 2015

001
Balozi wa China nchini Tanzania Mheshimiwa Dr.Lu Youqing (kushoto) akizungumza na Naibu waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) Mhe. Stephen Masele walipokutana kwenye ukumbi wa ubalozi huo kuzungumzia mkutano wa kimataifa wa viongozi vijana wa Afrika na China unatorajiwa kufanyika kuanzia Machi 27 na kumalizika Machi 31 katika Ukumbi wa Hoteli ya Ngurdoto, mkoani Arusha.
002
Balozi wa China hapa nchini Mheshimiwa Dr.Lu Youqing akipeana mkono na Naibu waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) Mhe. Stephen Masele mara baada ya kikao chao kufikia tamati ambapo walijadili hatua walizozifikia katika kuandaa mkutano huo wa kimataifa wa viongozi vijana wa Afrika na China unatorajiwa kufanyika kuanzia Machi 27 na kumalizika Machi 31 katika Ukumbi wa Hoteli ya Ngurdoto, mkoani Arus
003
Balozi wa China hapa nchini Mheshimiwa Dr.Lu Youqing akijibu swali aliloulizwa na mwandishi wa habari (Hayupo pichani) wakati wa kujadili mustakabali wa uandaaji wa mkutano wa kimataifa wa viongozi vijana wa Afrika na China unatorajiwa kufanyika kuanzia Machi 27 na kumalizika Machi 31 katika Ukumbi wa Hoteli ya Ngurdoto, mkoani Arusha. (Kushoto) ni Naibu waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) Mhe. Stephen Masele ambaye ni mwenyekiti wa maandalizi ya mkutano huo.

WAFANYAKAZI MGODI WA NORTH MARA WATUZWA KWA UMAHIRI NA UMAKINI KATIKA KAZI

March 24, 2015

Meneje Mkuu wa Mgodi wa North Mara, Gary Chapman, akizungumza kwenye hafla ya awamu ya pili ya utoaji tuzo za umahiri mwaka 2014 (CEO Excellence Awards 2014), iliyofanyika Jumanne usiku Machi 23, 2014, kwenye mgodi huo ulioko Nyamongo, wilayani Tarime mkoa wa Mara.
Meneja mkuu wa mgodi wa North Mara, Gary Chapman, (kushoto), akishuhudia wakati Le Poer Trench, (katikati) na Albert Rudman, wakionyesha tuzo za umahiri za mwaka 2014, (CEO ECellence Aawards 2014), walizopokea kwa niaba ya idara ya huduma za kiufundi ya mgodi huo, kwenye hafla ya awamu ya pili ya utoaji tuzo hizo iliyofanyika kwenye mgodi huo ulioko Nyamongo wilayani Tarime mkoa wa Mara, Jumanne usiku Machi 23, 2015
Meneja Mkuu wa Mgodi wa North Mara, Gary Chapman, (kushoto), akimkabidhi Aziz Rashid, kwa niaba ya idara anayofanyia kazi ya Matengenezo, tuzo ya umahiri ya mwaka 2014, itolewayo na kampuni ya uchimbaji madini ya Acacia, kwenye hafla ya awamu ya pili ya utoaji tuzo hizo iliyofanyika kwenye mgodi huo wilayani Tarime mkoa wa Mara Jumatatu usiku Machi 23, 2015. Tuzo hizo utolewa kila mwaka kwa mfanyakazi binafsi au idara, kutokana na umahiri katika kutekeleza majukumu yao kwa weledi na nidhamu ya hali ya juu.
Meneja Mkuu wa Mgodi wa North Mara, Gary Chapman, (katikati), akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa idara ya matenegenezo ya mgodi huo, baada ya kuwapatia tuzo na vyeti kwenye hafla ya awamu ya pili ya utoaji tuzo za umahiori mwaka 2014, zilizofanyika kwenye mgodi huo Jumanne usiku Machi 23, 205. Tuzo hizo utolewa kila mwaka kwa mfanyakazi binafsi au idara, kutokana na umahiri katika kutekeleza majukumu yao kwa weledi na nidhamu ya hali ya juu.
Meneja Mkuu wa Mgodi wa North Mara, Gary Chapman, akionyesha wafanyakazi wenzake wa mgodi huo, tuzo ya umahiri ya mwaka 2014, (CEO Excellence Awards 2014), waliyonyakua kwa kuwa mgodi wenye kuzingatia usalama kwa kiwango cha juu, wakati wa utoaji tuzo hizo awamu ya pili iliyofganyika kwenye mgodi huo Jumanne usiku Machi 23, 2015.
Stanley Harding, Meneja wa Liability, mgodi wa North Mara, (kushoto), akimkabidhi tuzo ya umahiri ya mwaka 2014, Adam Charles, kwa niaba ya idara ya operesheni ya mgodi huo, kwenye sherehe za awamu ya pili ya utoaji tuzo hizo (CEO Excleence Awards 2014), zilizofanyika Jumanne usiku Machi 23, 2015, kwenye mgodi huo ulioko Nyamongo, wilayani Tarime mkoa wa Mara. Tuzo hizo utolewa kila mwaka kwa mfanyakazi binafsi au idara, kutokana na umahiri katika kutekeleza majukumu yao kwa weledi na nidhamu ya hali ya juu.
Stanley Harding, Meneja wa Liability, mgodi wa North Mara, (aliyechuchumaa katikati), akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa idara ya operesheni ya mgodi huo mara baada ya kuwatunuku tuzo ya umahiri ya mwaka 2014, kweney sherehe ya awamu ya pili ya utoaji tuzo hizo iliyofanyika kwenye mgodi huo ulioko Nyamongo, wiklayani Tarime mkoa wa Mara, Jumanne usiku Machi 23, 2015. Tuzo hizo utolewa kila mwaka kwa mfanyakazi binafsi au idara, kutokana na umahiri katika kutekeleza majukumu yao kwa weledi na nidhamu ya hali ya juu.