TABATA KIMANGA JIJINI DAR ES SALAAM WAIOMBA MANISPAA YA ILALA KUWAJENGEA DARAJA LITAKALO WAUNGANISHA NA TABATA CHANG'OMBE

October 16, 2016

 Mtoto Juma Ramadhan mwanafunzi wa darasa la pili katika Shule ya Msingi ya Tabata Kimanga, akiwa amembeba mdogo wake Sara Sadiki wakati wakipita katika daraja la miti linalounganisha wakazi wa Tabata Kimanga na Tabata Chang'ombe Dar es Salaam , ambapo wakazi wa eneo hilo wanaiomba Manispaa ya Ilala iwajengee daraja la kudumu.

MTANDAO WA WIZI WA BAJAJI NA BODABODA WANASWA MBEYA

October 16, 2016
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Dhahiri Kidavashali akizungumza na waandishi wa habari jijini Mbeya kuhusiana na tukio la kuunasa mtandao wa wizi wa Bajaji na Pikipiki (BodaBoda) Mkoani Mbeya.(JamiiMojaBlog)

Mkutano wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya na Waandishi wa habari.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Dhahiri Kidavashali akionesha baadhi ya Bjajai na Pikipiki ziizokmatwa katika msako uliofanywa na jeshi hilo la POLISI Mbeya.

Askari Polisi wakiwa wamebeba moja ya bajaji iliyokamatwa mara baada ya Jeshi la Polisi Kufanya masako .

Bajaji zilizokamatwa na Jeshi la Polisi mara baada ya kufanya msako.



JESHI la Polisi Mkoani Mbeya limefanikiwa kuunasa mtandao uliokuwa ukihusika na matukio mbalimbali ya wizi wa bajaji na Pikipiki (bodaboda) katika maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Mbeya.
Mtuhumiwa anayehusika na matukio hayo imefahamika kwa jina la Getruda Mwakyusa Mkazi wa Mtaa wa Manga Veta jijini hapa.
Akizungumza Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Dhahiri Kidavashari amesema jeshi la polisi limeendelea  kufanya misako katika maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Mbeya  ili kudhibiti uhalifu .
Amesema Octobar 13 katika misako hiyo jeshi hilo la polisi lilifanikiwa kuunasa mtandao wa wizi wa bajajai na pikipiki ambapo mtuhumiwa wa matukio hayo alifanikiwa kutoroka ambapo nyumba yake mara baada ya kufanyiwa  upekuzi  zilikutwa pikipiki 3,bajaji 3,bodi 7 za bajaji .
Amesema kati ya mali hizo pikipiki mbili tayari zimekwisha tambuliwa na wamiliki wake kuwa ziliibiwa wilayani Chunya septemba25 mwaka huu katika kijiji cha Isenyela kata ya Mbugani.
Aidha Kamanda wa Polisi Mkoani humo ametoa wito kwa jamii husasani vijana kuacha tabia ya kutaka mali kwa njia ya mkato badala yake wafanye kazi kihalali ili kijipatia kipato sanjali na kutumia fursa zilizopo ili kujitafutia ajira.

WAHITIMU ST. EMMANUEL CHAMAZI TEMEKE JIJINI DAR ES SALAAM WAASWA KUZINGATIA ELIMU

October 16, 2016

 Mkurugenzi Mtendaji wa Shule ya ST. Emmanuel High School, Ernest Masaka, akizungumza katika mahafali ya saba ya Kidato cha Nne yaliyofanyika Chamazi jijini Dar es Salaam jana. Wengine kutoka kulia ni Mkuu wa shule hiyo, Khalid Simba, Diwani wa Kata ya Chamazi, Hemedi Karata  ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye mahali hayo, Katibu wa Diwani huyo na Lucy Peter, mke wa Mkurugenzi wa shule hiyo.