Mtoto Juma Ramadhan mwanafunzi wa darasa la pili katika Shule ya Msingi ya Tabata Kimanga, akiwa amembeba mdogo wake Sara Sadiki wakati wakipita katika daraja la miti linalounganisha wakazi wa Tabata Kimanga na Tabata Chang'ombe Dar es Salaam , ambapo wakazi wa eneo hilo wanaiomba Manispaa ya Ilala iwajengee daraja la kudumu.
MTANDAO WA WIZI WA BAJAJI NA BODABODA WANASWA MBEYA
Mkutano wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya na Waandishi wa habari. |
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Dhahiri Kidavashali akionesha baadhi ya Bjajai na Pikipiki ziizokmatwa katika msako uliofanywa na jeshi hilo la POLISI Mbeya. |
Askari Polisi wakiwa wamebeba moja ya bajaji iliyokamatwa mara baada ya Jeshi la Polisi Kufanya masako . |
Bajaji zilizokamatwa na Jeshi la Polisi mara baada ya kufanya msako. |
JESHI
la Polisi Mkoani Mbeya limefanikiwa kuunasa mtandao uliokuwa ukihusika na
matukio mbalimbali ya wizi wa bajaji na Pikipiki (bodaboda) katika maeneo
mbalimbali ya Mkoa wa Mbeya.
Mtuhumiwa
anayehusika na matukio hayo imefahamika kwa jina la Getruda Mwakyusa Mkazi wa Mtaa
wa Manga Veta jijini hapa.
Akizungumza
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Dhahiri Kidavashari amesema jeshi la polisi
limeendelea kufanya misako katika maeneo
mbalimbali ya Mkoa wa Mbeya ili
kudhibiti uhalifu .
Amesema
Octobar 13 katika misako hiyo jeshi hilo la polisi lilifanikiwa kuunasa mtandao
wa wizi wa bajajai na pikipiki ambapo mtuhumiwa wa matukio hayo alifanikiwa
kutoroka ambapo nyumba yake mara baada ya kufanyiwa upekuzi
zilikutwa pikipiki 3,bajaji 3,bodi 7 za bajaji .
Amesema
kati ya mali hizo pikipiki mbili tayari zimekwisha tambuliwa na wamiliki wake
kuwa ziliibiwa wilayani Chunya septemba25 mwaka huu katika kijiji cha Isenyela
kata ya Mbugani.
Aidha
Kamanda wa Polisi Mkoani humo ametoa wito kwa jamii husasani vijana kuacha
tabia ya kutaka mali kwa njia ya mkato badala yake wafanye kazi kihalali ili
kijipatia kipato sanjali na kutumia fursa zilizopo ili kujitafutia ajira.
WAHITIMU ST. EMMANUEL CHAMAZI TEMEKE JIJINI DAR ES SALAAM WAASWA KUZINGATIA ELIMU
Mkurugenzi Mtendaji wa Shule ya ST. Emmanuel High School, Ernest Masaka, akizungumza katika mahafali ya saba ya Kidato cha Nne yaliyofanyika Chamazi jijini Dar es Salaam jana. Wengine kutoka kulia ni Mkuu wa shule hiyo, Khalid Simba, Diwani wa Kata ya Chamazi, Hemedi Karata ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye mahali hayo, Katibu wa Diwani huyo na Lucy Peter, mke wa Mkurugenzi wa shule hiyo.
Subscribe to:
Posts (Atom)