Imewekwa Saa 12:01mchana leo Desemba 29.
MABINGWA
watetezi wa kombe la Mapinduzi, klabu ya Azam FC imetamba kwenda
kutetea taji hilo kwa mara ya tatu mfululizo katika michuano inayoanza
kutimua vumbi januari mosi mwakani.
Jafari
Idd Maganga, Afisa habari wa klabu hiyo amesema panapo majaaliwa timu
hiyo inatarajia kung`oa nanga jijini Dar e salaam januari 1 mwaka huu
kuelekea visiwani Zanzibar tayari kuanza harakati za kutafuta kombe
hilo.
“Michuano
hii ni muhimu sana kwetu. Kocha mkuu Mcameroon, Joseph Marius Omog
atakuwa na nafasi nyingine ya kupima kikosi chake na kuelewa wapi kuna
matatizo ili kuiandaa timu kwa ajili ya mzunguko wa pili wa ligi kuu
soka Tanzania bara na michuano ya kimataifa”. Alisema Jafar.
Jafar aliongeza kuwa tangu timu ipate kocha mpya, wachezaji wamekuwa wakipambana kutafuta nafasi katika kikosi cha kwanza.
“Mapinduzi
Cup itawajenga wachezaji wetu. Kila mchezaji anataka kuonekana mbele ya
kocha, ushindani umeongezeka zaidi, bila shaka baada ya kumalizika kwa
michuano hii muhimu, Kocha Omog atakuwa amepata kikosi chake”.