TUME YA UCHAGUZI TAIFA YASIKITISHWA NA MANENO MAKALI JUKWAANI

October 17, 2015




Tangakumekuchablog
Tanga, KAMISHNA wa Tumeya Taifa ya Uchaguzi, Mjaka Mchanga, amesikitishwa na mwenendo wa kampeni za uchaguzi majukwaani na kuwaomba wagombea kuacha kutoa maneno makali na badala yake kutangaza sera za vyama vyao.
Akizungumza katika kongamano leo na viongozi wa vyama vya siasa ukumbi wa mikutano jengo la Mkuu wa Mkoa, Mchanga, alisema Tume inasikitishwa kuona baadhi ya vyama kutumia majukwaa vibaya.
Alisema kipindi kilichobaki kuelekea uchaguzi mkuu wa Urais, Ubunge na Udiwani ni fursa ya kipekee kwa wagombea kujinadi kwa sera nzuri ambazo zitawavutia wananchi.
“Ni fursa ya kipekee kwa viongozi wa siasa hapa Tanga kukutana hapa na kujadili mambo ya msingi kuelekea uchaguzi----natambua wengi  wenu hapa ni wagombea au wakikilishi wa wawagombea” alisema Mchanga na kuongeza
“Tume inasikitishwa na mwenendo wa kampeni majukwaani ----baadhi ya vyama vimekuwa vikitoa maneno yasiyo mazuri kwa washindani----hebu zitumieni siku hizi chache zilizobaki kutoa sera zitakazowavutia wapiga kura” alisema
Mchanga amewataka wagombea pamoja na wanasiasa kuyatumia majukwaa yao kuzungumzia suala zima la amani pamoja na kunadi sera zao kwa wananchi ili kuweza kuwavutia na kuvuna wapiga kura.
Kwa upande wake Mgombea Udiwani kata ya Mwanzange, Rashid Jumbe wa Chama Cha Wananchi (CUF) ameitaka tume hiyo kusimamia uchaguzi kwa haki na amani bila ushabiki wa chama chochote.
Alisema vipindi vya uchaguzi  Tume ya Uchaguzi imekuwa ikilalamikiwa katika mchakato mzima wa uchaguzi na hivyo kuitaka tuhuma hizo kuzifuta na badala yake kusimamia kwa haki .
“Mheshimiwa kamishna wa tume ya uchaguzi taifa kwa heshima na taadhima naiomba tume yako kusimamia kwa haki uchaguzi huu kwani tumezoea kuona uvurugwaji kuanzia upigaji kura hadi uhesabuji na utangazaji” alisema Rashid na kuongeza
“Hapa kwetu hakuna dalili za viashiria vya fujo wala zogo----ila natoa angalizo simamieni uchaguzi ili uwe huru na haki kwa kila chama kinachoshiriki uchaguzi kiridhike” alisema
Alisema uchaguzi wa mwaka huu ni wa ushindani mkubwa kuliko chaguzi zote zilizopita hivyo kuitaka tume hiyo kusimamia kwa haki  bila upendeleo wa chama kimoja .
                                          


 Kamishna wa Chama Cha NCCR Mageuzi Mkoa wa Tanga, Ramadhani Manyeko, akichangia wakati wa mdahalo wa viongozi wa vyama vya siasa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi uliofanyika leo ukumbi wa Mkuu wa Mkoa.

 Mgombea Udiwani kata ya Mwanzange kupitia CUF, Rashid Jumbe, akichangia wakati wa kongamano la viongozi wa vyama vya siasa na Tume ya Taifa ya  Uchaguzi lililofanyika leo ukumbi wa Mkuu wa Mkoa.



 Kamishna wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Mjaka Mchanga akifungua kongamano la viongozi wa vyma vya siasa leo ikiwa ni kuelekea uchaguzi mkuu

MAMIA WAMUAGA MBUNGE WA LUDEWA DEO FILIKUNJOMBE NA NDUGU ZAKE NYUMBANI KWAKE KIJICHI JIJINI DAR ES SALAAM

October 17, 2015

 Aliyekuwa Mbunge wa Ludewa, Deo Filikunjombe enzi za Uhai wake.
 Msaidizi wa Mbunge huyo, Casablanga Haule enzi za Uhai wake.
 Padri Plasdus Ngabuma enzi za Uhai wake.
 Waombolezaji wakiwa wamebeba jeneza lenye mwili wa aliyekuwa Mbunge wa Ludewa, Deogratias Filikunjombe wakati wa ibada ya kuuaga iliyofanyika nyumbani kwake Kijichi Dar es Salaam leo mchana.
 Majeneza yenye miili ya aliyekuwa Mbunge wa Ludewa, Deogratias Filikunjombe na ndugu zake, Plasdus Ngabuma na Casablanga Haule yakiwa yamewekwa mbele wakati wa ibada ya kuiombea iliyofanyika nyumbani kwa mbunge huyo Kijichi Dar es Salaam leo, kabla ya kusafirishwa kwenda Ludewa kwa mazishi.
 Mjane wa Deo Filikunjombe, Sarah (katikati) akisaidiwa na jamaa zake wakati wa ibada hiyo.
 Waombolezaji wakiwa kwenye ibada hiyo.
 Padri Maxmillian Wambura kutoka Parokia ya Mtakatifu Wote Kiluvya akiyamwagia mafuta ya baraka majeneza hayo.
 Waombolezaji wakiwa katika ibada hiyo.
 Waombolezaji wakiwa wamebeba jeneza la Plasdus Haule.

 Jamilia ya Filikunjombe ikiwa katika ibada hiyo.
 Waombolezaji wakiwa kwenye ibada hiyo.
Nyumba ya Filikunjombe ambayo inadaiwa amekaa wiki mbili tangu ahamie baada ya kukamilika ujenzi wake 'Hakika tumuache mungu aitwe mungu"
(Imeandaliwa na mtandao wa habari za jamii.com

ACACIA YADHAMINI PAMBANO LA SOKA LA VIONGOZI WA DINI NA MABALOZI KUHAMASISHA AMANI

October 17, 2015

 Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, ambaye ni
nahodha wa timu ya viongozi wa dini, Alhadi Mussa Salum, akinyanyua juu kikombe
cha ushindi wa pili baada ya kumalizika kwa pambano la soka kati ya viongozi
hao na mabalozi kwenye uwanja wa taifa jijini Dar es Salaam leo Oktoba 17, 2015. Mabalozi walishinda kwa mikwaju ya penati 3-2 na kutwaa kombe. Katikati ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe, na wakwanza ushoto ni Meneja Mkuu wa kampuni ya Acacia,
anayeshughulikia ustawi wa kampuni, Assa Mwaipopo
 ………………………………………………………
NA K-VIS MEDIA
KAMPUNI ya Acacia imedhamini pambano la soka kati ya viongozi wa dini na mabalozi
wanaowakilisha nchi zao hapa Tanzania, pambano lililopigwa uwanja wa Taifa
jijini Dar es Salaam jana Oktoba 17, 2015
Katika pambano hilo, mabalozi waliibuka washindi kwa njia ya mikwaju ya penalty 3-2 na
kutwaa kombe.
Akitoa nasaha zake kabla ya kuanza pambano hilo la kuenzi amani taifa linapoelekea
kwenye uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25 mwezi huu, Waziri wa
Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe, aliwaambia washiriki kuwa, serikali
inaunga mkono jitihada za viongozi wa dini na mabalozi katika kuwaleta pamoja
wananchi hususan katika kipindi hiki ambacho taifa linaelekea kwenye uchaguzi.
Pambano hilo la soka lililodumu kwa muda wa dakika 40, lilikuwa la utangulizi kabla ya
pambano la ligi kuu soka Tanzania bara kati ya Yanga na Azam FC.
Akizungumza mwishoni mwa mchezo huo, Meneja Mkuu wa Acacia anayeshugulikia  a ustawi wa kampuni,  Assa Mwaipopo, alisema, kampuni yake
imedhamini pambano hilo kwa kutambua umuhimu wa amani hapa nchini, ambapo
Acacia kama wawekezaji wanao wajibu wa kuunga mkono jitihada zozote za kijamii
katika kuhakikisha amani inakuwepo hapa nchini inakuwepo.
“Sote tunatambua kuwa hivi karibuni taifa litaingiankwenye uchaguzi mkuu wa kuchagua
viongozi wetu, hivyo pambano hili la soka la viongozi wa dini na mabalozi
ambalo nia yake kubwa ni kuhamasisha amani miongoni mwa Watanzania katika
kipindi hiki cha uchaguzi limekuja wakati muafaka nasi kama Acacia tumeona
tuchangie katika jambo hili muhimui.” Alisema Assa.
Katika pambano hilo lililofana, wachezaji wa timu zote mbili walionyesha ukakamavu wa
hali ya juu kwa kumudu kucheza kwa nguvu na umahiri mkubwa na kuwapa burudani
safi wapenzi wa soka.
 Balozi wa Jumuiya ya Ulaya hapa nchini, Filiberto Sebregondi, ambaye alikuwa nahodha wa timu ya soka ya
mabalozi, akinyanyua juu kombe baada ya timu yake kuishinda timu ya mabalozi
kwenye uwanja wa taifa jijini Dar es Salaam Oktoba 17, 2015. Wanaoshuhudia
kushoto ni Meneja Mkuu wa kampuni ya Acacia, anayeshughulikia ustawi wa
kampuni, Assa Mwaipopo, na Mkuu wa Mahusiano ya Serikali, Alex Lugendo (wapili
kushoto)
 Waziri Chikawe, (kushoto), akisalimiana na Assa Mwaipopo
 Chikawe, akisalimiana na Alex Lugendo
 “Ball Boys” wakiwa wamebeba bendera ya Acacia, wakati timu zikiingia uwanjani
 Sheikh Alhadi akiwa kwenye mazoezi ya viungo na viongozi wenzake wa dini kabla ya mpambano huo
 Sheikh Alhadi akifumua shuti

WAKAZI WA JIJI LA MWANZA WAIPOKEA CCM KWA MIKONO MIWILI, WASEMA MAGUFULI NI RAIS AJAYE

October 17, 2015
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea na wakazi wa jiji la Mwanza na vitongoji vyake katika uwanja wa Fraisha kwenye mkutano wa hadhara wa Kampeni za CCM zilizohudhuriwa na Maelfu ya watu.Picha na Cathbert Kajuna wa Kajunason Blog.
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea na wakazi wa jiji la Mwanza na vitongoji vyake katika uwanja wa Fraisha kwenye mkutano wa hadhara wa Kampeni za CCM zilizohudhuriwa na Maelfu ya watu.Picha na Cathbert Kajuna wa Kajunason Blog.
Wakazi wa jiji la Mwanza na vitongoji vyake waliojitokeza katika mkutano wa hadhara wa Kampeni za CCM zilizohudhuriwa na Maelfu ya watu.
-- ---- Cathbert Angelo Kajuna, Founder and Mananging Director Kajunason Blog, P.O Box 6482, Dar es Salaam. Tel: +255 787 999 774 Alt: +255 765 253 445 www.kajunason.blogspot.com "Everything is Possible Through Peace & Stability''

DKT MAGUFULI ASHIRIKI KUTOA HESHIMA ZA MWISHO KWA MAREHEMU DEO FILIKUNJOMBE NA WENZAKE WAWILI WALIOFARIKA KATIKA AJALI YA HELIKOPTA..

October 17, 2015

Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi CCM,Dkt John Pombe Magufuli  akitoa heshima za mwisho mbele ya majeneza ya aliyekuwa Mbunge wa Ludewa(CCM) Marehemu Deo Filikunjombe na wenzake wawili waliofariki katika ajali ya helikopta juzi katika pori la akiba la mbuga ya Selous. Marehemu aliagwa katika hospitali ya jeshi Lugalo jijini Dar es Salaam Oktoba 17, 2015.PICHA NA MICHUZI JR.
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi CCM,Dkt John Pombe Magufuli akimfariji Mke wa Marehemu Bi Sarah Filikunjombe wakati wa kuaga mwili wa marehemu katika hospitali ya jeshi Lugalo jijini Dar es Salaam Oktoba 17, 2015.
 Mke wa Marehemu Bi Sarah Filikunjombe akilia kwa uchungu kufuatia kifo cha Mumwe Deo Filikunjombe,wakati wa kuaga katika hospitali ya jeshi Lugalo jijini Dar es Salaam Oktoba 17, 2015.
 Dkt Magufuli akifarijiana na Mh.Zitto Kabwe  wakati wa kuaga mwili wa marehemu katika hospitali ya jeshi Lugalo jijini Dar es Salaam Oktoba 17, 2015.
 Dkt Magufuli alishindwa kujizuia kutoa machozi ya huzuni  wakati wa kuaga mwili wa marehemu katika hospitali ya jeshi Lugalo jijini Dar es Salaam Oktoba 17, 2015.
 Majeneza yenye miili ya aliyekuwa Mbunge wa Ludewa, Deogratias Filikunjombe na ndugu zake, Plasdus Ngabuma na Casablanga Haule yakiwa yamewekwa mbele ya waombolezaji  wakati wa kuaga katika hospitali ya jeshi Lugalo jijini Dar es Salaam Oktoba 17, 2015. kabla ya kusafirishwa kwenda Ludewa kwa mazishi mkoani Njombe.

DKT SHEIN AMNADI DKT MAGUFULI KISIWANI UNGUJA LEO,ASEMA ANATOSHA KUWA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

October 17, 2015


Mgombea Urais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Dkt Mohamed Shein akimnadi Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya chama cha Mapinduzi CCM Dkt John Pombe Magufuli mbele ya maelfu ya wananchi waliohudhuria mkutano wa kampeni uliofanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja,kisiwani Unguja jioni ya leo.

Dkt Shein emebainisha wazi kwenye mkutano huo wa kampeni kuwa Dkt Magufuli ni mtu sahihi na anatosha kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,amesema kuwa iwapo atachaguliwa kuwa Rais wa awamu ya tano atashirikiana nae kwa kila jambo kuhakikisha Tanzania inapiga hatua zaidi kimaendeleo.
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya chama cha Mapinduzi CCM Dkt John Pombe Magufuli akihutubia maelfu ya wananchi waliohudhuria mkutano wa kampeni uliofanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja,kisiwani Unguja jioni ya leo.PICHA  ZOTE NA MICHUZI JR-KISIWANI UNGUJA.
Sehemu ya umati wa wakazi wa Kisiwani Unguja na vitongoji vyake wakiwa wamejitokeza kwa wingi katika mkutano wa kampeni uliofanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja mjini humo,ambapo Mgombea Urasi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha CCM Dkt John Pombe Magufui aliwahutubia.
Mgombea Urais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Dkt Mohamed Shein akimsikiliza kwa makini Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya chama cha Mapinduzi CCM Dkt John Pombe Magufuli kabla ya kupanda jukwaani na kuwahutubia maelfu ya wakazi wa kisiwani Unguja kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja,kisiwani humo.
Wananchi wa kiswani Unguja wakishangilia jambo kwenye mkutano huo wa kampeni.
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya chama cha Mapinduzi CCM Dkt John Pombe Magufuli akihutubia maelfu ya wananchi waliohudhuria mkutano wa kampeni uliofanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja,kisiwani Unguja jioni ya leo.
Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ,Mh Al Hassan Mwinyi  akiwahutubia Wananchi (hawapo pichani) ,kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja,kisiwani Unguja jioni ya leo.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mjini,Ndugu Boraafya Silima akizungumza machache kwenye mkutano wa kampeni kabla ya kumkaribisha Mgombea Urais wa CCM Dkt Magufuli kuwahutubia wananchi wa kisiwani Unguja.


Nyomi la wakazi wa Kisiwani Unguja ndani ya mkutano wa kampeni.
Sehemu ya umati wa wakazi wa kisiwani Unguja na vitongoji vyake wakiwa  wamekusanyika kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja,kisiwani Unguja jioni ya leo.
Baadhi ya Wafuasi wa chama hicho wakishangilia jambo kwenye mkutano wa kampeni wa Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli
Wadau wakifuatilia mkutano wa kampeni ndani ya uwanja wa Mnaji Mmoja kisiwani Unguja.
Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ,Mh Al Hassan Mwinyi  akiwahutubia Wananchi (hawapo pichani) ,kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja,kisiwani Unguja jioni ya leo.

wakifuatilia mkutano wa kampeni.
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano Dkt Jonh Pombe Magufuli akiwapungia wananchi wa Kisiwani Unguja (hawapo pichani),alipokuwa akiwasili kwenye mkutano wa kampeni katika viwanja vya Mnazi Mmoja mjini humo.
Balozi Seif Ali Iddi akiwahutubia wananchi wa Kisiwani Unguja kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika katika viwanja vya Mnazi mmoja.


Baadhi ya Wafuasi wa chama hicho wakifurahia jambo kwenye mkutano wa kampeni wa Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli
Sehemu ya umati wa wakazi wa kisiwani Unguja na vitongoji vyake wakiwa  wamekusanyika kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja,kisiwani Unguja jioni ya leo.
Wananchi wa Kisiwani Unguja wakifuatilia mkutano wa kampeni ndani ya viwanja vya Mnazi Mmoja.