MASHINDANO YA MAJESHI KUFUNGULIWA KESHO JWTZ WAWASILI SALAMA RWANDA

MASHINDANO YA MAJESHI KUFUNGULIWA KESHO JWTZ WAWASILI SALAMA RWANDA

August 07, 2016
jei1
Mkuu wa Majeshi ya Rwanda (CDS) Jenerali Patrick Nyamvumba (Kushoto)akiongea na Waandishi habari Hawapo Pichani katika Ukumbi wa Uwanja wa Amahoro Juu ya maandalizi ya mashindano ya majeshi  kwa Nchi za Afrika mashariki yanayotarajia kufungulia Kesho(Jumatatu Agosti  8)Kulia ni Mwenyekiti wa kamati ya Mandalizi Brigedia Jenerali martin Kemwanga wa JWTZ. .(Picha na Selemani Semunyu).
jei2
Mwenyekiti wa kamati ya Mandalizi ya Mashindano ya 10 ya Majeshi kwa Nchi za Afrika mashariki Brigedia Jenerali Martin Kemwanga wa JWTZ kifafanua jambo Mbele ya Waandishi wa habari (Hawapo Pichani)Mjini Kigali kuhusu Maandalizi ya mashindano hayo kushoto ni Mkuu wa Majeshi wa Rwanda (CDS) Jenerali Patrick Nyamvuba ).(Picha na Selemani Semunyu).
jei3
Baadhi ya Viongozi  na Wachezaji wa Timu za Jeshi wanaoshikiri Michuano ya Kumi ya Majeshi kwa Nchi za Afrika mashariki yanayotaraji kufunguliwa Kesho katika Uwanja Wa Amahoro Mara walipowasili  katika Mji wa KigalI Nchini Rwanda .(Picha na Selemani Semunyu).
…………………………………………………………………………………………………..
Na Selemani Semunyu ,JWTZ
Timu ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzani limewasili Salama katika Mji wa Kigali Nchini Rwanda kuungana na Wanajeshi wa Nchi Za Afrika Masahariki katika Mashindano ya majeshi kwa nchi hizo yanayotajiwa kufunguliwa Rasmi kesho(Leo).
Kiongozi wa Msafara wa Timu hiyo Brigedia Jenerali Jairos Mwaseba Alisema muda mfupi baada ya Timu hiyo kuwasili kuwa Timu iko salama na Wameanza mazoezi mepesi kwa Ajili ya Kujiandaa na Michuano hiyo sambamba na kuzoea hali ya hewa.
“Timun yetu iko vizuri kilizhobaki watanzania waendelee kuiombea Timu yetu kwani maombi yao yakichanganyika na jitihada za Timu basi ushindi utapatikana na ni vema Watanzania walioko Rwanda kujitokeza kushangilia Timu zao,Alisema Brigedia Jenerali mwaseba.
Wakati huo huo Mkuu wa majeshi wa Rwanda Jenerali Patrick Nyamvumba akizungumza Na Waandishi wa Habari alisema Maandalizi yote yamekamilika na kinachosubiriwa ni kuanza kwa Michezo hiyo huku Timu zikimalizia hatua za Mwisho za Usajili kwa ajili ya Michuano hiyo
Alisema Wanajeshi 500 kutoka katika Majeshi ya Nchi Nne za Tanzania,Rwanda,Uganda, na Kenya wanatarajiwa kushiriiki katika Mashindano ya Kumi  ya Majeshi ya Nchi za Afrika Mashariki huku Burundi ikiwa imeshindwa kushiriki kutokana na hali ilivyo katika Nchi yake.
Jenerali Nyamvumba alisema anamatumani makubwa na mazungumzo yanayoendelea kuhusu Burundi hivyo Matarajio yake yataifikisha Burundi katika Hatua Nzuri na Hivyo kushiriki katika Michezo hiyo ambayo aliita Muhumi kwa Ushirikiano.
“Michezo hii ni Muhimu kwa Ushirikiano wetu kwani hakuna Mshindi mwisho wa mashindano sote tunakuwa washindi kutokan na kufanikisha kuwa pamoja,Urafiki kama kamajeshi yaliyo katika Ukanda wa Afrika Mashariki,” Alisema Jenerali  Nyamvumba.
Kwa Upande Wake Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi kutoka Tanzania Brigedia Jenerali Martin Kemwanga  amesema kama kamati waliridhia kuwepo kwa Michezo Mitano ambayo ni Mpira wa miguu,Kikapu,Pete,Mikono na Mbio za Nyika
MASHINDANO YA MAJESHI KUFUNGULIWA KESHO JWTZ WAWASILI SALAMA RWANDA

MASHINDANO YA MAJESHI KUFUNGULIWA KESHO JWTZ WAWASILI SALAMA RWANDA

August 07, 2016
jei1
Mkuu wa Majeshi ya Rwanda (CDS) Jenerali Patrick Nyamvumba (Kushoto)akiongea na Waandishi habari Hawapo Pichani katika Ukumbi wa Uwanja wa Amahoro Juu ya maandalizi ya mashindano ya majeshi  kwa Nchi za Afrika mashariki yanayotarajia kufungulia Kesho(Jumatatu Agosti  8)Kulia ni Mwenyekiti wa kamati ya Mandalizi Brigedia Jenerali martin Kemwanga wa JWTZ. .(Picha na Selemani Semunyu).
jei2
Mwenyekiti wa kamati ya Mandalizi ya Mashindano ya 10 ya Majeshi kwa Nchi za Afrika mashariki Brigedia Jenerali Martin Kemwanga wa JWTZ kifafanua jambo Mbele ya Waandishi wa habari (Hawapo Pichani)Mjini Kigali kuhusu Maandalizi ya mashindano hayo kushoto ni Mkuu wa Majeshi wa Rwanda (CDS) Jenerali Patrick Nyamvuba ).(Picha na Selemani Semunyu).
jei3
Baadhi ya Viongozi  na Wachezaji wa Timu za Jeshi wanaoshikiri Michuano ya Kumi ya Majeshi kwa Nchi za Afrika mashariki yanayotaraji kufunguliwa Kesho katika Uwanja Wa Amahoro Mara walipowasili  katika Mji wa KigalI Nchini Rwanda .(Picha na Selemani Semunyu).
…………………………………………………………………………………………………..
Na Selemani Semunyu ,JWTZ
Timu ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzani limewasili Salama katika Mji wa Kigali Nchini Rwanda kuungana na Wanajeshi wa Nchi Za Afrika Masahariki katika Mashindano ya majeshi kwa nchi hizo yanayotajiwa kufunguliwa Rasmi kesho(Leo).
Kiongozi wa Msafara wa Timu hiyo Brigedia Jenerali Jairos Mwaseba Alisema muda mfupi baada ya Timu hiyo kuwasili kuwa Timu iko salama na Wameanza mazoezi mepesi kwa Ajili ya Kujiandaa na Michuano hiyo sambamba na kuzoea hali ya hewa.
“Timun yetu iko vizuri kilizhobaki watanzania waendelee kuiombea Timu yetu kwani maombi yao yakichanganyika na jitihada za Timu basi ushindi utapatikana na ni vema Watanzania walioko Rwanda kujitokeza kushangilia Timu zao,Alisema Brigedia Jenerali mwaseba.
Wakati huo huo Mkuu wa majeshi wa Rwanda Jenerali Patrick Nyamvumba akizungumza Na Waandishi wa Habari alisema Maandalizi yote yamekamilika na kinachosubiriwa ni kuanza kwa Michezo hiyo huku Timu zikimalizia hatua za Mwisho za Usajili kwa ajili ya Michuano hiyo
Alisema Wanajeshi 500 kutoka katika Majeshi ya Nchi Nne za Tanzania,Rwanda,Uganda, na Kenya wanatarajiwa kushiriiki katika Mashindano ya Kumi  ya Majeshi ya Nchi za Afrika Mashariki huku Burundi ikiwa imeshindwa kushiriki kutokana na hali ilivyo katika Nchi yake.
Jenerali Nyamvumba alisema anamatumani makubwa na mazungumzo yanayoendelea kuhusu Burundi hivyo Matarajio yake yataifikisha Burundi katika Hatua Nzuri na Hivyo kushiriki katika Michezo hiyo ambayo aliita Muhumi kwa Ushirikiano.
“Michezo hii ni Muhimu kwa Ushirikiano wetu kwani hakuna Mshindi mwisho wa mashindano sote tunakuwa washindi kutokan na kufanikisha kuwa pamoja,Urafiki kama kamajeshi yaliyo katika Ukanda wa Afrika Mashariki,” Alisema Jenerali  Nyamvumba.
Kwa Upande Wake Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi kutoka Tanzania Brigedia Jenerali Martin Kemwanga  amesema kama kamati waliridhia kuwepo kwa Michezo Mitano ambayo ni Mpira wa miguu,Kikapu,Pete,Mikono na Mbio za Nyika
MASHINDANO YA MAJESHI KUFUNGULIWA KESHO JWTZ WAWASILI SALAMA RWANDA

MASHINDANO YA MAJESHI KUFUNGULIWA KESHO JWTZ WAWASILI SALAMA RWANDA

August 07, 2016
jei1
Mkuu wa Majeshi ya Rwanda (CDS) Jenerali Patrick Nyamvumba (Kushoto)akiongea na Waandishi habari Hawapo Pichani katika Ukumbi wa Uwanja wa Amahoro Juu ya maandalizi ya mashindano ya majeshi  kwa Nchi za Afrika mashariki yanayotarajia kufungulia Kesho(Jumatatu Agosti  8)Kulia ni Mwenyekiti wa kamati ya Mandalizi Brigedia Jenerali martin Kemwanga wa JWTZ. .(Picha na Selemani Semunyu).
jei2
Mwenyekiti wa kamati ya Mandalizi ya Mashindano ya 10 ya Majeshi kwa Nchi za Afrika mashariki Brigedia Jenerali Martin Kemwanga wa JWTZ kifafanua jambo Mbele ya Waandishi wa habari (Hawapo Pichani)Mjini Kigali kuhusu Maandalizi ya mashindano hayo kushoto ni Mkuu wa Majeshi wa Rwanda (CDS) Jenerali Patrick Nyamvuba ).(Picha na Selemani Semunyu).
jei3
Baadhi ya Viongozi  na Wachezaji wa Timu za Jeshi wanaoshikiri Michuano ya Kumi ya Majeshi kwa Nchi za Afrika mashariki yanayotaraji kufunguliwa Kesho katika Uwanja Wa Amahoro Mara walipowasili  katika Mji wa KigalI Nchini Rwanda .(Picha na Selemani Semunyu).
…………………………………………………………………………………………………..
Na Selemani Semunyu ,JWTZ
Timu ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzani limewasili Salama katika Mji wa Kigali Nchini Rwanda kuungana na Wanajeshi wa Nchi Za Afrika Masahariki katika Mashindano ya majeshi kwa nchi hizo yanayotajiwa kufunguliwa Rasmi kesho(Leo).
Kiongozi wa Msafara wa Timu hiyo Brigedia Jenerali Jairos Mwaseba Alisema muda mfupi baada ya Timu hiyo kuwasili kuwa Timu iko salama na Wameanza mazoezi mepesi kwa Ajili ya Kujiandaa na Michuano hiyo sambamba na kuzoea hali ya hewa.
“Timun yetu iko vizuri kilizhobaki watanzania waendelee kuiombea Timu yetu kwani maombi yao yakichanganyika na jitihada za Timu basi ushindi utapatikana na ni vema Watanzania walioko Rwanda kujitokeza kushangilia Timu zao,Alisema Brigedia Jenerali mwaseba.
Wakati huo huo Mkuu wa majeshi wa Rwanda Jenerali Patrick Nyamvumba akizungumza Na Waandishi wa Habari alisema Maandalizi yote yamekamilika na kinachosubiriwa ni kuanza kwa Michezo hiyo huku Timu zikimalizia hatua za Mwisho za Usajili kwa ajili ya Michuano hiyo
Alisema Wanajeshi 500 kutoka katika Majeshi ya Nchi Nne za Tanzania,Rwanda,Uganda, na Kenya wanatarajiwa kushiriiki katika Mashindano ya Kumi  ya Majeshi ya Nchi za Afrika Mashariki huku Burundi ikiwa imeshindwa kushiriki kutokana na hali ilivyo katika Nchi yake.
Jenerali Nyamvumba alisema anamatumani makubwa na mazungumzo yanayoendelea kuhusu Burundi hivyo Matarajio yake yataifikisha Burundi katika Hatua Nzuri na Hivyo kushiriki katika Michezo hiyo ambayo aliita Muhumi kwa Ushirikiano.
“Michezo hii ni Muhimu kwa Ushirikiano wetu kwani hakuna Mshindi mwisho wa mashindano sote tunakuwa washindi kutokan na kufanikisha kuwa pamoja,Urafiki kama kamajeshi yaliyo katika Ukanda wa Afrika Mashariki,” Alisema Jenerali  Nyamvumba.
Kwa Upande Wake Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi kutoka Tanzania Brigedia Jenerali Martin Kemwanga  amesema kama kamati waliridhia kuwepo kwa Michezo Mitano ambayo ni Mpira wa miguu,Kikapu,Pete,Mikono na Mbio za Nyika
MASHINDANO YA MAJESHI KUFUNGULIWA KESHO JWTZ WAWASILI SALAMA RWANDA

MASHINDANO YA MAJESHI KUFUNGULIWA KESHO JWTZ WAWASILI SALAMA RWANDA

August 07, 2016
jei1
Mkuu wa Majeshi ya Rwanda (CDS) Jenerali Patrick Nyamvumba (Kushoto)akiongea na Waandishi habari Hawapo Pichani katika Ukumbi wa Uwanja wa Amahoro Juu ya maandalizi ya mashindano ya majeshi  kwa Nchi za Afrika mashariki yanayotarajia kufungulia Kesho(Jumatatu Agosti  8)Kulia ni Mwenyekiti wa kamati ya Mandalizi Brigedia Jenerali martin Kemwanga wa JWTZ. .(Picha na Selemani Semunyu).
jei2
Mwenyekiti wa kamati ya Mandalizi ya Mashindano ya 10 ya Majeshi kwa Nchi za Afrika mashariki Brigedia Jenerali Martin Kemwanga wa JWTZ kifafanua jambo Mbele ya Waandishi wa habari (Hawapo Pichani)Mjini Kigali kuhusu Maandalizi ya mashindano hayo kushoto ni Mkuu wa Majeshi wa Rwanda (CDS) Jenerali Patrick Nyamvuba ).(Picha na Selemani Semunyu).
jei3
Baadhi ya Viongozi  na Wachezaji wa Timu za Jeshi wanaoshikiri Michuano ya Kumi ya Majeshi kwa Nchi za Afrika mashariki yanayotaraji kufunguliwa Kesho katika Uwanja Wa Amahoro Mara walipowasili  katika Mji wa KigalI Nchini Rwanda .(Picha na Selemani Semunyu).
…………………………………………………………………………………………………..
Na Selemani Semunyu ,JWTZ
Timu ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzani limewasili Salama katika Mji wa Kigali Nchini Rwanda kuungana na Wanajeshi wa Nchi Za Afrika Masahariki katika Mashindano ya majeshi kwa nchi hizo yanayotajiwa kufunguliwa Rasmi kesho(Leo).
Kiongozi wa Msafara wa Timu hiyo Brigedia Jenerali Jairos Mwaseba Alisema muda mfupi baada ya Timu hiyo kuwasili kuwa Timu iko salama na Wameanza mazoezi mepesi kwa Ajili ya Kujiandaa na Michuano hiyo sambamba na kuzoea hali ya hewa.
“Timun yetu iko vizuri kilizhobaki watanzania waendelee kuiombea Timu yetu kwani maombi yao yakichanganyika na jitihada za Timu basi ushindi utapatikana na ni vema Watanzania walioko Rwanda kujitokeza kushangilia Timu zao,Alisema Brigedia Jenerali mwaseba.
Wakati huo huo Mkuu wa majeshi wa Rwanda Jenerali Patrick Nyamvumba akizungumza Na Waandishi wa Habari alisema Maandalizi yote yamekamilika na kinachosubiriwa ni kuanza kwa Michezo hiyo huku Timu zikimalizia hatua za Mwisho za Usajili kwa ajili ya Michuano hiyo
Alisema Wanajeshi 500 kutoka katika Majeshi ya Nchi Nne za Tanzania,Rwanda,Uganda, na Kenya wanatarajiwa kushiriiki katika Mashindano ya Kumi  ya Majeshi ya Nchi za Afrika Mashariki huku Burundi ikiwa imeshindwa kushiriki kutokana na hali ilivyo katika Nchi yake.
Jenerali Nyamvumba alisema anamatumani makubwa na mazungumzo yanayoendelea kuhusu Burundi hivyo Matarajio yake yataifikisha Burundi katika Hatua Nzuri na Hivyo kushiriki katika Michezo hiyo ambayo aliita Muhumi kwa Ushirikiano.
“Michezo hii ni Muhimu kwa Ushirikiano wetu kwani hakuna Mshindi mwisho wa mashindano sote tunakuwa washindi kutokan na kufanikisha kuwa pamoja,Urafiki kama kamajeshi yaliyo katika Ukanda wa Afrika Mashariki,” Alisema Jenerali  Nyamvumba.
Kwa Upande Wake Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi kutoka Tanzania Brigedia Jenerali Martin Kemwanga  amesema kama kamati waliridhia kuwepo kwa Michezo Mitano ambayo ni Mpira wa miguu,Kikapu,Pete,Mikono na Mbio za Nyika

STARTIMES YACHANGIA MADAWATI MKOANI MTWARA

August 07, 2016
 Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mh. Bi. Anastazia Wambura (kushoto) pamoja na Makamu wa Rais wa StarTimes Tanzania, Bi. Zuhura Hanif (kulia) wakiwa kwenye baadhi ya madawati yaliyochangiwa na kampuni hiyo ikiwa ni jitihada za kuunga mkono kampeni ya kuchangia madawati nchi nzima iliyoanzishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Dkt. John Pombe Magufuli. Zoezi hio la uchangiaji wa madawati lilifanyika katika ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Mtwara mwishoni mwa wiki hii.


 Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mh. Bi. Anastazia Wambura (kushoto) pamoja na Makamu wa Rais wa StarTimes Tanzania, Bi. Zuhura Hanif (kulia) wakiwa wamekaa kwenye madawati hayo. 

 Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mh. Bi. Anastazia Wambura (kulia) , akizungumza wakati wa kupokea madawati hayo. Katikati ni Mkuu wa Wilaya ya Mtwara, Mh. Dkt. Khatib Malimi Kazungu
Makamu wa Rais wa StarTimes Tanzania, Bi. Zuhura Hanif (kushoto), akizungumza wakati wa kukabidhi madawati hayo.

Na Mwandishi Wetu

Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mh. Bi. Anastazia Wambura amepokea madawati hamsini yenye thamani ya shilingi milioni tano kutoka kwa kampuni ya matangazo ya dijitali ya StarTimes ikiwa ni jitihada za kuunga mkono kampeni ya kuchangia madawati iliyoanzishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Dkt. John Pombe Magufuli.

Akizungumza mara baada ya hafla fupi ya makabidhiano iliyofanyika mwishoni mwa wiki moani Mtwara, Mh. Bi. Wambura amebainisha kuwa zoezi la kuchangia madawati ili kuwawezesha wanafunzi kusoma katika mazingira mazuri linawahusu watu wote na sio serikali pekee.

“Ningependa kuchukua fursa hii kuzipongeza taasisi za umma na sekta binafsi kwa mwitikio wao mkubwa wa kumuunga mkono Mheshimiwa Rais katika kampeni ya kuchangia madawati. Wote tunafahamu ni kwa kiasi gani shule nyingi nchini zinavyokabiliwa na uhaba wa madawati jambo linalopelekea mazingira magumu ya kufundishia na kujinzia. Lakini kwangu mimi suala la wanafunzi kuongezeka sioni kama ni tatizo bali ni changamoto kwa serikali yetu na jamii kwa ujumla kuendana na mwamko mkubwa wa wazazi na walezi kuwapeleka watoto wao shule. Kwa muda mrefu sana serikali imekuwa ikiwahamasisha wananchi wake wawapeleke watoto shule na wakafanya hivyo, sasa suala hilo tumefanikiwa kwa kiasi kikubwa na vivyo jinsi walivyoitikia mwamko huo basi waitikie na wa huu wa kuchangia madawati.” Alisema Mh. Bi. Wambura

Naibu Waziri huyo aliendelea kwa kuelezea kuwa serikali ina wajibu wa kuhamasisha maendelea kwa wananchi wake kwa njia mbalimbali ikiwemo hii ya kuwasilisha maeneo ambayo yanapaswa kupewa kipaumbele kama vile suala la elimu nchini.

“Elimu ndio suala la msingi katika taifa lolote duniani iwe lililoendelea au linaloendelea na ndio maana kwa nchi za wenzetu wanawekeza fedha nyingi katika sekta hii. Nchi yoyote yenye wasomi wengi lazima itakuwa na maendeleo makubwa kutokana na raia wake kuelimika lakini hayo yote haya hayatowezekana kama tusipowawekea mazingira mazuri wanafunzi wetu tangu ngazi ya msingi,” alisema Mh. Naibu Waziri na kumalizia, “Ningependa kumalizia kwa kuwapongeza na kuwashukuru wenzetu wa kampuni ya StarTimes kwa kuguswa na suala hili na kuamua kuja huku Mtwara kuchangia madawati kwani huku ndiko kwenye changamoto kubwa hasa kutokana na taasisi na makampuni mengi kuwepo sehemu za mijini. Tunawashukuru sana na tunawaomba muendelee na moyo huo huo na mfike sehemu nyingine amabko makampuni mengine hayafiki.”

Kwa upande wake Makamu wa Rais wa StarTimes Tanzania, Bi. Zuhura Hanif amesema kuwa kampuni hiyo imekuwa ni mdau mkubwa wa masuala ya kijamii hususani elimu kwa inafahamu umuhimu wake katika kuleta mapinduzi ya kimaendeleo.

“StarTimes ni mdau mkubwa sana wa masuala ya elimu na kwa muda mrefu tumekuwa tukisaidia shule zenye wanafunzi wenye mahitaji maalumu. Uchangiaji wa madawati ni kampeni ya aina yake iliyoanzishwa na Mh. Rais Magufuli na inahitaji kuungwa mkono kwa nguvu zote kwani yeye aliamini kabisa watanzania tunao uwezo huo ila tulikosa tu uhamasishaji. Na ni kweli uhamasishaji ndio uliokosekana kwani mara baada ya kutoa tamko hilo taasisi, makampuni, mashirikia, wananchi na watu binafsi wameonyesha mwitikio mkubwa. Hii ni dalili njema kwamba watanzania tunaweza kuleta maendeleo yetu wenyewe bila ya kungojea msaada kutoka kwa watu wa nje.” Alisema Bi. Hanif

“Leo hii tumekuja huku Mtwara kuja kukabidhi madawati haya, tunafahamu kwamba ni machache lakini yatakuwa ni msaada mkubwa kwa watoto wetu kusoma katika mazingira mazuri. Wanafunzi wanaposoma katika mazingira mazuri hupelekea kuhudhuria vipindi, kuipenda shule, kuelewa vizuri na hatimaye kupelekea kufaulu masomo yao,” alisema na kuhitimisha Bi. Hanif kuwa, “Wananfunzi wanapowekewa mazingira mazuri ya kusomea pia hutoa hamasa kwa walimu kufanya kazi yao kwa ufanisi mkubwa kwani ufundishaji unakuwa ni rahisi na vivyo hivyo uelewa kwa wanafunzi. Hivyo basi, ningependa kutoa wito kwa wanafunzi wayatunze madawati haya ili yaje kuwanufaisha na wenzao watakaokuja siku za usoni na tunawaahidi kuwa tuko pamoja nao katika kutatua changamoto zinazowakabili.”

Serikali ya Brazil yaonyesha nia ya kufanikisha azma ya Rais. Dkt. Magufuli kuifanya Tanzania kuwa nchi ya Viwanda

August 07, 2016

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (Kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Brazil nchini Tanzania, Carlos Alfonso Puente, wakati Balozi huyo alipomtembelea ofisini kwake jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
Balozi wa Brazil nchini Tanzania, Carlos Alfonso Puente (Kushoto), akisaini Kitabu cha Wageni ofisini kwa Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (Kulia), alipomtembelea Waziri na kufanya naye mazungumzo kuhusu ushirikiano baina ya nchi hizo mbili hususan katika uwekezaji kwenye sekta ya nishati.
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (Kushoto), akimsikiliza kwa makini Balozi wa Brazil nchini Tanzania, Carlos Alfonso Puente (Kulia), wakati Balozi huyo alipomtembelea Waziri Ofisini kwake jijini Dar es Salaam hivi karibuni na kufanya mazungumzo naye kuhusu masuala ya uwekezaji katika sekta za nishati na madini. Wengine pichani ni Maafisa wa Wizara waliohudhuria mkutano huo.

Na Veronica Simba

Serikali ya Brazil imeonesha nia kuwekeza katika sekta ya nishati nchini hususan katika kuzalisha umeme kwa kutumia maji na mabaki ya miwa. Hayo yameelezwa jana jijini Dar es Salaam na Balozi wa Brazil nchini Tanzania, Carlos Alfonso Puente, alipomtembelea Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo ofisini kwake na kufanya mazungumzo naye.

Balozi Puente alimweleza Profesa Muhongo kuwa nchi yake inao ujuzi na uzoefu wa kutosha katika uzalishaji wa umeme kwa kutumia vyanzo mbalimbali hususan maji.

Alisema, Brazil ingependa kuchangia kufanikisha azma ya Rais John Magufuli kuifanya Tanzania kuwa nchi ya Viwanda.

“Kutekeleza mchakato wa kuifanya nchi kuwa ya Viwanda, unahitaji umeme mwingi unaotokana na vyanzo mbalimbali. Ni bahati nzuri kwamba Tanzania inazo njia za kufanikisha azma hiyo,” alisema.

Alisema kuwa, nchini Brazil, kuna Kampuni kubwa zenye uzoefu wa muda mrefu unaofikia miaka 20 hadi 40 katika kazi hiyo, ambazo huzalisha umeme wa maji nchini mwao na hata nje ya nchi.

Pia, alitaja eneo jingine ambalo nchi yake ina nia ya kuwekeza kuwa ni uzalishaji wa umeme unaotumia mabaki ya miwa ambayo aliielezea kuwa chanzo kizuri cha nishati safi.

Balozi Puente alisisitiza kuwa, Brazil ikiwa ni nchi inayozalisha miwa kwa kiwango kikubwa duniani, itasaidia kuleta mabadiliko katika sekta ya nishati kwa kuzalisha umeme unaotokana na mabaki ya miwa kwa kutumia teknolojia za kisasa.

Kwa upande wake, Waziri Muhongo, akimjibu Balozi Puente, alikiri kuwa kuwa Brazil ina ujuzi, uzoefu na uwezo mkubwa hususan katika maeneo ambayo Balozi aliyataja na hivyo akamwambia nchi hiyo inakaribishwa kuwekeza Tanzania kwa kufuata masharti na utaratibu uliowekwa na Serikali.

Akizungumzia zaidi kuhusu utaratibu wa uwekezaji, Waziri Muhongo alieleza kwamba Serikali ya Tanzania, kupitia Wizara yake, inabadilisha utaratibu wa kupokea wawekezaji katika sekta husika.

Alisema, kunaandaliwa utaratibu maalum utakaokuwa wa wazi na kuruhusu ushindani kwa wenye nia ya kuwekeza kwa malengo ya kupunguza au kuondoa kabisa mazingira ya rushwa na muda mrefu unaotumika katika majadiliano pasipo sababu za msingi.

Profesa Muhongo alifafanua zaidi kwamba, Serikali itaweka mazingira mazuri zaidi ya ushindani kwa kuandaa maelezo ambayo pamoja na mambo mengine yatabainisha aina mbalimbali za vyanzo vya umeme vilivyopo nchini pamoja na maeneo vilipo.

Alisema, Kampuni zenye nia ya kuwekeza zitakaribishwa kupendekeza viwango vya bei vitakavyotumika kuuza umeme utakaozalishwa na zitashindanishwa, ambapo washindi wachache watachaguliwa kwa ajili ya majadiliano kabla ya kuingia mkataba wa uwekezaji husika.

“Kwa hivyo, tunaandaa kabrasha maalum litakalokuwa na maelezo husika na litakuwa tayari mwezi wa Septemba mwaka huu. Kabrasha hilo lenye maelezo litatumika kama mwongozo wa ushindanishaji maombi mbalimbali ya uwekezaji hususan katika kuzalisha umeme kwa kutumia vyanzo mbalimbali kwa uwazi,” alisisitiza.

Alivitaja vyanzo hivyo kuwa ni pamoja na gesi asilia, makaa ya mawe, maji, jua, upepo, jotoardhi, mawimbi ya bahari pamoja na nishati mbadala. Waziri Muhongo alisema kuwa maelezo hayo maalum yatasambazwa kwa wadau mbalimbali wa sekta husika wakiwemo wale wote wenye nia ya kuwekeza ikiwa ni pamoja nan chi ya Brazil kupitia Ubalozi wake hapa nchini.

“Kwa kutumia Kabrasha hilo maalum lenye maelezo husika, wewe Balozi utaweza kuwashawishi wafanyabiashara kutoka nchini kwako kutoa mapendekezo ya uwekezaji ambayo yana vigezo vyote muhimu vinavyoshawishi wapate fursa husika za uwekezaji katika sekta ya nishati,” Profesa Muhongo alimweleza Balozi Puente.

Kuhusu Mradi mkubwa wa ujenzi wa Bomba la kusafirisha mafuta kutoka Uganda hadi Tanzania, ambao pia Brazil imeonesha nia kuwa ingependa kuwekeza kwa kushirikiana na Tanzania; Profesa Muhongo alisema Serikali itaweza kulisemea hilo baada ya kipindi cha miezi takribani 45 kupita, ambapo mambo yote ya kisheria kuhusu Mradi huo yanatarajiwa kuwa yamekamilika.

Aidha, Profesa Muhongo alitumia fursa hiyo kuomba nafasi za masomo nchini Brazil kwa wanafunzi wa kitanzania katika ngazi za Shahada za Uzamili na Uzamivu katika sekta ya Nishati hususan Mafuta na Gesi, kwa kuzingatia kuwa Brazil imeendelea sana katika sekta hiyo.

“Ninyi mnazo Taasisi bora kabisa za Utafiti duniani. Mnafanya vizuri sana katika maeneo mbalimbali.”

Kwa mujibu wa Profesa Muhongo, Brazil ni miongoni mwa nchi Tano (5) bora duniani zinazozalisha umeme kwa kutumia nishati jadidifu kwa sababu umeme mwingi wanaozalisha unatokana na maji, kutoka katika Mito mikubwa waliyonayo.

KATIBU MKUU MALIASILI NA UTALII AONGOZA WATUMISHI WA WIZARA HIYO KUMUAGA ALIYEKUWA MKURUGENZI WA UTAWALA NA RASILIMALI WATU, SAID MSAMBACHI

August 07, 2016

Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii, Maj. Gen. Gaudence Milanzi (kushoto) akizungumza katika hafla fupi iliyoandaliwa na watumishi wa Wizara hiyo kumuaga aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Utumishi, Said Msambachi (kulia) aliyestaafu rasmi kwa mujibu wa sheria tarehe 16 Juni, 2016. Hafla hiyo ilifanyika juzi tarehe 05 Agosti, 2016 katika ukumbi wa mikutano wa Selous, Makao Makuu wa Wizara hiyo, Jengo la Mpingo, jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mstaafu wa Idara ya Utawala na Rasilimali Watu, Wizara ya Maliasili na Utalii, Said Msambachi (kulia) akitoa nasaha zake kwa watumishi wa Wizara hiyo katika hafla fupi ya kumuaga iliyoandaliwa na watumishi hao tarehe 05 Agosti, 2016. Aliwaasa watumishi hao kutekeleza majukumu yao kwa kufanya kazi kwa bidii, uadilifu na uaminifu kama chachu ya maendeleo yao kazini. Aliwataka pia kufanya kazi kwa ushirikiano kujiepusha na majungu, vitendo vya rushwa na ubaguzi pahala pa kazi. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Maj. Gen. Gaudence Milanzi.
 Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Utumishi, Ziana Mlawa (kushoto) akitoa shukurani kwa niaba ya watumishi wote kwa ushirikiano walioupata kutoka kwa Bw. Said Msambachi (kulia) katika kipindi chote cha miaka mitano alichofanya kazi katika Wizara hiyo.
Mkurugenzi Msaidizi wa Rasilimali Watu, Idara ya Utawala na Utumishi, Aurelia Matagi, akitoa ufafanuzi wa ratiba na kuongoza utambulisho katika hafla hiyo.
Mkurugenzi Mstaafu wa Idara ya Utawala na Rasilimali Watu, Wizara ya Maliasili na Utalii, Said Msambachi na Mama Msambachi wakikata Keki ya kuagwa waliyoandaliwa na watumishi wa Wizara hiyo.
Taswira ya keki hiyo.
Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii, Maj. Gen. Gaudence Milanzi (wa tatu kushoto) akimkabidhi Mkurugenzi Mstaafu wa Idara ya Utawala, Said Msambachi (wa pili kulia) risiti ya friji (pichani kulia) aliyozawadiwa na watumishi wa Wizara hiyo.
 Baadhi ya watumishi wa Wizara hiyo katika hafla hiyo.
 Baadhi ya watumishi wa Wizara walioshiriki hafla hiyo.
 Baadhi ya watumishi wa Wizara katika hafla hiyo.
 Sehemu ya watumishi katika hafla hiyo.
 Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii, Maj. Gen. Gaudence Milanzi (kushoto) akizungumza na watumishi walihudhuria hafla hiyo.
 Picha ya pamoja kati ya Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii, Maj. Gen. Gaudence Milanzi (wa pili kushoto, msatari wa mbele), Mkurugenzi Mstaafu wa Idara ya Utawala na Rasilimali Watu, Said Msambachi (wa tatu kushoto), Mkurugenzi anayekaimu nafasi yake kwa sasa ambaye pia ni Mkurugenzi Msaidizi wa Utawala, Ziana Mlawa (kulia), Mkurugenzi Msaidizi wa Rasilimali Watu, Aurelia Matagi na Watumishi wa Wizara walioshiriki hafla hiyo (mstari wa pili na wa tatu nyuma) .
Picha ya pamoja kati ya Mkurugenzi Mstaafu wa Idara ya Utawala na Rasilimali Watu, Wizara ya Maliasili na Utalii, Said Msambachi (katikati) na Mkurugenzi anayekaimu nafasi yake kwa sasa ambaye pia ni Mkurugenzi Msaidizi wa Utawala, Ziana Mlawa (kulia) na Mkurugenzi Msaidizi wa Rasilimali Watu, Aurelia Matagi (kushoto).(Picha na Hamza Temba - WMU)

RAIS DKT. MAGUFULI ASALI KATIKA KANISA LA BIKIRA MARIA PAROKIA YA CHATO, PIA ATEMBELEA KANISA LA ANGLIKANA, AIC PAMOJA NA MSIKITI WA OMAR BIN-L-KHATTAB CHATO MKOANI GEITA

August 07, 2016

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mke wake Mama Janeth Magufuli wakisali katika ibada ya Jumapili katika Kanisa la Bikira Maria Parokia ya Chato mkoani Geita.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na waamini wa kanisa Katoliki wa Parokia ya Chato mara baada ya Ibada katika kanisa hilo Chato Mkoani Geita.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akihamasisha mchango wa ujenzi wa Kanisa jipya la la Bikira Maria Parokia ya Chato mkoani Geita.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Padre wa Kanisa la Bikira Maria Parokia ya Chato Henry Mulinganisa mara baada ya kushiriki Ibada katika Kanisa hilo.
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akisalimiana na na Padre wa Kanisa la Bikira Maria Parokia ya Chato Henry Mulinganisa mara baada ya kuwasili kwenye kanisa hilo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwapungia mkono waamini wa Kanisa Katoliki Kanisa la Bikira Maria Parokia ya Chato mkoani Geita hawapo pichani mara baada ya kushiriki Ibada katika kanisa hilo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mkewe Mama Janeth Magufuli wakimsikiliza Mchungaji wa Kanisa la Anglikana Chato Zacharia Samson mara baada ya kuwasili katika kanisa hilo la Anglikana Chato Mkoani Geita.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiimba wimbo wa Amani pamoja na Kwaya ya Kanisa la African Inland Church la Chato Mkoani Geita mara baada ya kuwasili katika kanisa hilo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimsalimia Mwalimu wake wa zamani wa Shule ya Msingi Chato Mkoani GeitaMwalimu Mkuu Mstaafu Jackson Nyamwaga mara baada ya kumuona wakati akitoka katika Kanisa la African Inland Church la Chato Mkoani Geita.

Shekhe wa Bakwata Wilaya ya Chato Hassan Issa Mnubi akiongoza dua ya Kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na Mkewe Mama Janeth Magufuli nje ya Msikiti wa Omar Bin-L-Khattab Chato Mkoani Geita. PICHA NA IKULU

WANANCHI WAZIDI KUFURAHIA MAONESHO YA NANENANE KANDA YA KASKAZINI

August 07, 2016
Mmoja wa wananchi waliotembelea maonesho ya Kilimo na Mifugo ya Nanenane Kanda ya Kaskazini yanayofanyika kwenye uwanja wa Taso Themi akipata maelezo kwenye banda la kampuni ya Simba Cement

Meneja Mauzo wa Simba Cement mkoa wa Arusha,Christopher Mgonja(kulia)akimkabidhi mmoja wa wananchi waliotembelea banda hilo,Thomas Mollel kofia na tisheti .

Bwana Shamba wa kampuni ya mbegu ya Seed Co,Lukinga Miho akizungumzia kampuni hiyo kuanza kuzalisha mbegu za mbogamboga ambazo zina soko kubwa ndani na nje ya nchi.

Wananchi wakipata maelezo ya kilimo cha Mbogamboga na Matunda kwenye banda la taasisi ya TAHA inayojihusisha na kuhamasisha wakulima kuzalisha kwa wingi kwaajili ya soko la ndani na masoko ya Ulaya .

Wananchi wakipata elimu ya kilimo kwenye uwanja wa maonesho ya Wakuma na wafugaji Kanda ya Kaskazini  uwanja Taso, Themi mkoani Arusha.

Wajasiriamali hawakua nyuma kwenye banda la Halmashauri ya Jiji la Arusha kuonyesha bidhaa zao kwa wananchi waliotembelea maonesho ya mwaka huu.

Wanafunzi nao ni sehemu ya wananchi wanaotembelea maonesho ya Wakulima na Wafugaji ya Nanenane pamoja na mambo mengine hujifunza mambo mengi yanaendana na masomo yao kwa vitendo.

Maafisa wa Benki ya NMB mjini Arusha wakitoa huduma kwa wananchi wanaofika kwenye banda lao.