MAFUNZO YA WAHE. MAJAJI YAMALIZIKA

MAFUNZO YA WAHE. MAJAJI YAMALIZIKA

March 28, 2018

1
Kaimu Jaji Mfawidhi, Mahakama Kuu-Kanda ya Arusha, Mhe. Sekela Moshi akitoa hotuba ya kufunga Mafunzo wa siku tano ya Waheshimiwa Majaji yaliyokuwa yakifanyika katika Ukumbi wa AICC jijini Arusha, kushoto ni Mhe. Sophia Wambura, Jaji wa Mahakama Kuu-Kitengo cha Ardhi.
2
Waheshimiwa Majaji wakimsikiliza mgeni rasmi alipokuwa akifunga mafunzo yao rasmi
3
Mhe. Sophia Wambura, Jaji wa Mahakama Kuu-Kitengo cha Ardhi akipokea cheti cha ushiriki kutoka kwa Kaimu Jaji Mfawidhi, Mahakama Kuu-Kanda ya Arusha, Mhe. Sekela Moshi aliyefunga mafunzo hayo.
4
Jaji wa Mahakama Kuu-Kanda ya Tabora, Mhe. John Utamwa akipokea cheti cha ushiriki wa Mafunzo kutoka kwa  Kaimu Jaji Mfawidhi-Mahakama Kuu Kanda ya Arusha, Mhe. Sekela Moshi.
5
Mhe. Haruna Songoro, Jaji wa Mahakama Kuu-Divisheni ya Biashara akipokea cheti cha ushiriki kutoka kwa Mgeni rasmi
6
Jaji wa Mahakama Kuu-Kanda ya Mwanza, Mhe. Joaquine De Mello akipokea cheti cha ushiriki wa Mafunzo.
7
Jaji wa Mahakama Kuu-Kanda ya Arusha, Mhe. Modesta Makopolo Opiyo akipokea cheti cha ushiriki, katika Mafunzo hayo Wahe. Majaji wametakiwa kuzingatia na kutekeleza yale yote waliyofunzwa ili kuboresha zaidi huduma ya utoaji haki nchini.
………………
REMARKS BY HON. S.C. MOSHI, ACTING JUDGE IN CHARGE OF THE HIGH COURT, ARUSHA ZONE AT THE CLOSING CEREMONY OF CONSTITUTIONAL LITIGATION AND THE USE OF ICT IN THE ADMINISTRATION OF JUSTICE PROGRAM FOR JUDGES OF THE HIGH COURT
TANZANIA HELD AT AICC, ARUSHA, FROM 24TH TO 28H MARCH, 2018.
Hon. Justice Dr. Paul Kihwelo, the Principal of the Institute of Lushoto Judicial Administration;
All Judges of the High Court;
Distinguished Facilitators;
All participants;
Ladies and Gentlemen.
Good Afternoon!
It gives me great pleasure to join you for the closing of this training on constitutional litigation and the use of ICT in the Administration of Justice.
Hon. Judges and other participants, we have now come to the end of the program which started on 24th March, 2018 and ends today, on 28th March, 2018. This has been a very informative and enriching week of training where all the topics were very inciting and well covered by the various facilitators.
I wish to thank all of you, on behalf of the Judiciary of Tanzania for making this training a success; specifically for your active participation in the program, valuable presentations and plenary discussions.
I also wish to thank the administration of the Institute of Judicial Administration for organising this training and the World Bank for funding the training.
Similarly, I wish to thank the secretariat which comprised staff from the the Judiciary of Tanzania led by the Assistant Director of Training (ADT), Institute of Judicial Administration Lushoto, the High Court of Tanzania in Arusha, the Police Force, the Management of AICC for hosting the program and providing other services.  
The Judiciary of Tanzania is implementing a Five Years Strategic Plan for the period of 2015/16 to 2019/2020 that is titled Towards citizens_ Centric Justice delivery Project. As I said during the opening of this training; this training was conducted as part of the implementation of the Judiciary Strategic Plan (JSP). The project is funded by the World Bank. I sincerely thank the Word Bank for funding this Project. We are indeed grateful.
The JSP has three main pillars, namely Governance, Accountability and Management of Resources, Access to Justice and Expeditiousness and Public Trust and Stakeholders Engagement. One of the strategic objectives for Governance is to increase efficiency in the judiciary business processes and enhance the use of ICT. This objective is in line with the Tanzanian Government ICT Policy of 2016. The judiciary is responsible for interpreting all laws and administering justice in the ICT environment and to ensure that ICT is mainstreamed in the justice framework in the country.
The Judiciary of Tanzania has already started to implement its ICT plan for efficient, effective and timely delivery of justice. The Judiciary has initiatives for e-justice like developing case management system, Electronic asset management, e- attendance register, e-complaints and court mapping. Plans are under way to formulate the ICT Policy Guidelines to guide ICT usage of equipment.
Marco Velicogna, a prominent researcher on ICT, in his paper which is titled Justice System and ICT, What can be learned from Europe he wrote that, “The use of information and technology is considered one of the key elements to significantly improve the administration of justice. The rapid development of technology opens up new opportunities that were unthinkable only a few years ago. Around the world, several statutory reforms have been introduced to allow the use of the exchange of electronic data and documents within national judicial systems, but also within supranational courts. The availability of web services, the possibility of consulting on_ line legislation and case laws, the use of electronic filing, the   of legal documents, are only some examples that are spurring the judicial administration around the world to rethink their current functions and activities.”
The presenters have shared with you the following topics; practice and procedures in constitutional rights and litigation, individual and collective rights in the context of constitutional rights litigation, remedies in constitutional rights, the use of expert evidence and amicus curiae , ICT and legal research; the presenter presented how to use the web and internet in judicial legal research, ICT in the administration of justice; basic issues in computer use were explained , e- justice; under this subject the presenters were able to explain the current electronic platform or information system and services which are in place in the judiciary of Tanzania like overall case management system, updated JSDS, judgement data base and records and archives system.
Other topics included ICT whereby presenters took you through the five years judiciary strategic plan and you shared experience from the East African Court of Justice. Last but not least, you had an opportunity to hear from the CEO of eGA on an ICT and Cyber Security Issues.
Iam aware that several ICT activities have already been implemented; for instance video conferencing facilities that have been installed at Mbeya High Court Zone and IJA Kisutu Training and Information Resource Centre, JSDS; the statistics data management, the judiciary web site and recording systems in High Court Zones.
I am told that the Government Mailing System (GMS) has already been developed; the consultant for installation of Local Area Network (LAN) for all existing court building by 2018/209 has been procured. The project also involves installation of Wide Area Net Work (WAN) and GON NET i.e. connecting court buildings to government Network.
I am also aware that you had time to discuss laws, case laws and rules which relate to constitutional matters and you noted some issues like contradicting provisions of law. There is need of harmonising the different pieces of legislations.  However, Iam firm that you have gained deeper understanding of the rules and practice obtained in as far as constitutional litigation is concerned.
I’m aware that the presenters have taken you through various activities. You had discussions, role plays, group works and you also had a chance of sharing of experiences on various topical issues. I am confident that the training has enriched you and increased your knowledge on ICT and constitutional litigation issues. I believe that you are now able to fully appreciate the use of ICT in performing your judicial work.
I wish you safe journey to your respective work places(chanzo FullshangweBlog)
I THANK YOU FOR YOUR KIND ATTENTION!
                SEKELA C. MOSHI
  1.         JUDGE IN CHARGE
                ARUSHA HIGH COURT ZONE
MHE.IKUPA: SERIKALI KUENDELEA KUBORESHA MAZINGIRA YA WATU WENYE ULEMAVU

MHE.IKUPA: SERIKALI KUENDELEA KUBORESHA MAZINGIRA YA WATU WENYE ULEMAVU

March 28, 2018

????????????????????????????????????
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (watu wenye Ulemavu) Mhe. Stella Ikupa akitoa maelezo kuhusu masuala ya watu wenye ulemavu kwa Kamati ya Kudumu ya Katiba na Sheria ili kujadili  Taarifa ya Utekelezaji wa Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa mwaka 2017/18 na Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka 2018/19 Kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Machi 28, 2018 Bungeni Dodoma.
????????????????????????????????????
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe.Jenista Mhagama akifafanua jambo wakati kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Machi 28, 2018 Bungeni Dodoma.
????????????????????????????????????
Baadhi ya Wajumbe wa kikao wakifuatilia mada zinazowasilishwa wakati wa Taarifa ya Utekelezaji wa Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa mwaka 2017/18 na Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka 2018/19 Kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Machi 28, 2018 Bungeni Dodoma.
????????????????????????????????????
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Katiba na Sheria Mhe.Najma Giga akiongoza kikao cha kamati yake wakati wa Uwasilishaji wa Taarifa ya Utekelezaji wa Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa mwaka 2017/18 na Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka 2018/19 kwa mafungu 27,62,65 na 15 ya Ofisi hiyo.
????????????????????????????????????
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Vijana), Mhe. Antony Mavunde akitoa hoja wakati wa Kikao cha Kamati hiyo.
????????????????????????????????????
Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Kailima Ramadhan akifafanua jambo wakati wa kikao cha kamati hiyo.
????????????????????????????????????
Baadhi ya Wajumbe wa kikao wakifuatilia mada zinazowasilishwa wakati wa kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria.
 (PICHA ZOTE NA OFISI YA WAZIRI MKUU – DODOMA)
…………………………………………………………………………………….
Na.MWANDISHI WETU
Serikali imedhamiria kuboresha mazingira ya watu wenye ulemavu ili kuwasaidia kujikwamua katika nyanja zote na kuchangia katika maendeleo nchini.
Hayo yameelezwa na Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya watu wenye ulemavu Mhe.Stella Ikupa wakati wa Uwasilishaji wa Taarifa ya Utekelezaji wa Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa mwaka 2017/2018 na Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka 2018/2019 kwa mafungu ya Taasisi zinazosimamiwa na Ofisi hiyo Mjini Dodoma.
Waziri Ikupa alieleza kuwa tayari Serikali imeanza mikakati ya kuboresha mazingira ya watu wenye Ulemavu kwa kuvifufua vyuo na vituo vyao ili kuwapa nafasi nzuri ya kujifunza katika mazingira yanayowapa uhuru na tija kulingana na aina za ulemavu walionao.
“Tayari tumeanza kuboresha mazingira ya vyuo vya ufundi ikiwemo kile cha Yombo kilichopo Mjini Dar es Salaam na Sabasaba ili kusaidia kuwapa fursa za kujifunza katika mazingira rafiki hii ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kuna kuwa na vifaa vya kutosha”.Aliongezea
Sambamba na hilo Serikali inaendelea na hatua za kuboresha mazingira ya Watu wenye ulemavu kwa kuwajengea uwezo, kuongeza wataalam wa kuwafundisha, kuwapa mafunzo maalumu yenye kuleta tija pamoja na kuwashirikisha katika fursa za maendeleo.
Aliongezea kuwa Ofisi yake itaendelea kushirikiana na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia pamoja na vyuo mbalimbali ili kupata taarifa sahihi za mahitaji halisi ya watu wenye ulemavu yatakayosaidia kuwa na kanzidata ya kudumu yenye taarifa hizo.
“Jitihada zilizopo ni pamoja na kushirikisha Wizara ya Elimu ili kuweza kupata taarifa muhimu za watu wenye ulemavu zitazosaidia kuwa na kanzi data ya uhakika inayowatambulisha kwa idadi, aina ya ulemavu na ujuzi alionao ili kuwapa nafasi wenye sifa za kushiriki katika programu za kukuza ajira”.Alisisitiza Mhe.Ikupa
Kwa upande wake mmoja wa wajumbe wa Kamati hiyo Mhe.Amina Mollel alishauri kuwe na mikakati madhubuti yenye tija kwa watu wenye ulemavu ikiwemo kutoa semina kwa watumishi wa serikali juu ya namna bora ya kuwahudumia watu wenye ulemavu kwa kuzingatia mahitaji yao.
“Ifike mahali kuwe na mikakati madhubuti ya kuwasaidia watu wenye mahitaji maalum hususani kwa kuwajengea uwezo watumishi kujua namna nzuri ya kuwahudumia watu wenye ulemavu pamoja na kusaidia kuzikabili changamoto wanazokabiliana nazo”.Alisema Mhe.Mollel.

RC MASENZA AWAPONGEZA RDO KWA KUTATUA TATIZO LA MAJI KWENYE BAADHI YA VIJIJI VYA WILAYA YA MUFINDI NA KILOLO

March 28, 2018



Mkuu wa mkoa wa Iringa Amina Masenza akiwahutubia wananchi wa kijiji cha Nandala alipokuwa ameenda kuzindua mradi wa maji ambao utasaidia kupunguza changamoto ya maji na kuchochea maendeleo kwa wananchi ambao watakuwa wananufaika na mradi huo ulifadhiliwa na shirika lisilo la kiserikali la Rural Development Organization (RDO) Tanzania ambao makao makuu yao yapo Mdabulo Mufindi.


Mkuu wa mkoa wa Iringa Amina Masenza akimtusha ndoo ya maji mmoja ya wananchi walihudhulia uzinduzi wa mradi maji ulifadhiliwa na shirika lisilo la kiserikali la Rural Development Organization (RDO) Tanzania

Mkuu wa mkoa wa Iringa Amina Masenza akiwa na mkurugenzi mtendaji wa shirika lisilo la kiserikali la Rural Development Organization (RDO) Tanzania Fidelis Filipatali wakibadilisha mawazo juu ya mradi huo ambao umegharibukiasi cha shilingi milioni tisini na tano,laki tano na elfu tatu mia moja ( 95,503,100)

Hapa ndio tank kubwa la mradi wa maji unaofadhiliwa na shirika lisilo la kiserikali la Rural Development Organization (RDO) Tanzania na
umegharibukiasi cha shilingi milioni tisini na tano,laki tano na elfu tatu mia moja ( 95,503,100)


Mkuu wa mkoa wa Iringa Amina Masenza akiwahutubia wananchi wa kijiji cha Nandala alipokuwa ameenda kuzindua mradi wa maji ambao utasaidia kupunguza changamoto ya maji na kuchochea maendeleo kwa wananchi ambao watakuwa wananufaika na mradi huo ulifadhiliwa na shirika lisilo la kiserikali la Rural Development Organization (RDO) Tanzania ambao makao makuu yao yapo Mdabulo Mufindi.


Na Fredy Mgunda,Iringa

MKUU wa mkoa wa Iringa Amina Masenza amelipongeza shirika lisilo la kiserikali la Rural Development Organization (RDO) Tanzania kwa kufanikisha kupatikana kwa maji katika baadhi ya vijiji vya wilaya ya Kilolo na Mufindi ambayo itakuwa njia moja wapo ya kuchochea maendeleo kwa wananchi.

Akizungumza wakati wa kuzindua mradi wa maji katika kijiji cha Nandala’ Masenza alisema kuwa amefurahishwa na mfumo ambao unatumiwa na shirika hilo kwa kutoa huduma ya maji kwa kushirikiana na wananchi wa maeneo husika.

“Mradi wowote ule ukiwa na ushirikiano mkubwa na wananchi mara nyingi wananchi wanautunza mradi huo kwa kuudhamini na kuulinda,hivyo nawapongeza RDO kwa kufanya maamuzi sahihi ya kubuni mradi huo pamoja na wananchi” alisema Masenza

Masenza alisema kuwa mradi huo wa maji utatoa huduma kwa wananchi wengi na taasisi binafsi nyingi hivyo wananchi wanatakiwa kuutunza na kuudhamini ili udumu kwa muda mrefu na kuondoa tatizo la maji ambalo limekuwa kero ya muda mrefu.

Nimesikia kwenye risala yenu kuwa mradi huu utahudumia kata zifuatazo Ifwagi,Mdabulo,Ihanu,Luhunga,Mtitu na Kising’a na vijiji vitakavyopata huduma hiyo ni Igonongo,Ludilo,Kidete,Ikanga,Nandala,Ibwanzi,Isipii,Mkonge,Lulanzi,Luhindo,Barabara mbili na Isele hivyo ukiangala utagundua kuwa mradi huu ni mkubwa na upaswi kupuuzwa kwa maendeleo kwa wananchi wa maeneo ambayo mradi huo umepita.

“Jamani wananchi ambao mmepata bahati ya kupitiwa na mradio huu mkubwa wa maji mnapaswa kuulinda na kuudhamini kwa kuwa ni mmoja ya mradi mkubwa ambao unapunguza adha ya upatikanaji wa maji ambayo hapo awali ilikuwa kero kubwa” alisema Masenza.
Kwa upande mkurugenzi mtendaji wa shirika lisilo la kiserikali la Rural Development Organization (RDO) Tanzania Fidelis Filipatali alisema kuwa mradi huo umegharibukiasi cha shilingi milioni tisini na tano,laki tano na elfu tatu mia moja ( 95,503,100) ambao ndani yake kuna pesa zilizochangwa na wananchi kwa ajili ya kusaidia kupata huduma ya maji.

“Sisi kama RDO ambao ndio wafadhili namba moja wa mradio huu wa maji tumechangia kiasi cha shilingi milioni themenini na sita,laki nane ishirini na moja elfu (86,821,000) na wananchi walichanga kiasi cha shilingi milioni nane,laki sita themenini na mbili na mia moja (8,682,100)” alisema Filipatali

Filipatali alisema kuwa mradi huo wa maji utazaliza ujazo wa lita 776 kwa vijiji vyote ambazo vinatumia huduma hiyo ya maji na pia wananchi watakao pata huduma hiyo ni 10,874 kwa vijiji vyote vilivyopitiwa na mradi huo na jumla ya taasisi 18 nazo zitanufaika na huduma hiyo.

“Mkuu wa mkoa sasa ukiangalia kwa ujumla ndio utagundua kuwa ni mradi ambao utakuwa unakomba wananchi wengi waliokuwa wanapata tabu juu ya kupata maji hivyo naomba pia nisisitize wananchi kuutunza na kuchangia kwa malipo kidogo kwa ajili ya ukarabati wa mashine na mitambo mingie inayosukuma maji hayo ili isihalibike” alisema Filipatali

Filipatali alisema kuwa mradi huo unakabiliwa na changamoto zifuatazo baadhi ya watumiaji maji kutochangia, viongozi kutotimiza majukumu yao kama kutohudhuria mikutano ya mapato na matumizi,watumiaji maji kutotilia mkazo elimu wanayopewa na wataalamu wa maji,siasa kuingia mfumo mzima wa mradi huu na baadhi ya serikali za vijiji kuchukulia mapato ya miradi ya maji kama sehemu ya mapato ya serikali kitu ambacho sio kweli mfano kjiji cha Lidilo

“Hizi changamoto zimekuwa kero sana kwenye miradi ambayo imekuwa inatekelezwa kwenye maeneo husika hivyo niwaombe viongozi wa kiasa wawe wa kwanza kutoa elimu juu ya miradi ambayo inafaida na kutatua changamoto za wananchi kwenye maeneo yao” Filipatali

SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR KUZINDUA UGAWAJI WA VYANDARUA VYENYE DAWA YA MUDA MREFU

March 28, 2018

Wizara ya afya Zanzibar kupitia Kitengo cha kumaliza Malaria katika juhudi zake za kupambana na ugonjwa wa Malaria kinakusudia kutoa vyandarua laki moja na 95 elfu kwa mama wajawazito na watoto waliochini ya miaka mitano nchi nzima .

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Zanzibar juu ya uzinduzi wa Kampeni ya kubwa ya matumizi ya vyandarua ambayo inatarajiwa kufanyika April nne mwaka huu visiwani Zanzibar Meneja wa utaribu wa kazi za kumaliza Malaria Zanzibar Abdallah Suleiman Ali amesema Zanzibar ni miongoni mwa nchi chache za Afrika ambazo zimokatika mchakato wa kumaliza Malaria ambapo kwa sasa ni zaidi ya miaka kumi Zanzibar imekuwa ikipambana na ugonjwa huo .

Amesema Zanzibar kila kipindi kinachomaliza mvua za masika kumekuwa na kiwango kikubwa ugonjwa Malaria lakini jitihada mbali mbali zinachukuliwa ikiwemo kupiga dawa majumbani, kuhakikisha dawa zinapatikana katika vituo vya afya, na kuwepo kwa vipimo cha kuchunguzia ugonjwa huo na matumizi ya vyandarua vilivyopigwa dawa.

Amesema vyandarua ndio kinga tahabiti ya kujikinga na Malaria ambapo kwa Zanzibar Asilimia 77 ya Wananchi wanatumia vyandarua kiwango ambacho bado hakijaridhisha kufikia vigenzo vya wizara ya afya zanizbar ya Asilimia 100 na shirika la afya ulimwenguni WHO Asilimia 85.

Hata hivyo Meneja Abdallah amesema kwa sasa licha ya Zanzibar kupunguza maambuzi ya wagonjwa wa Malaria lakini amekiri ugonjwa huo bado upo chini ya Asilimia moja na ambapo vigezo vinavyotumika kuhakikisha Wananchi wanaobainika kuwa na vimelea anafuatiliwa katika familia yake ili kuhakikisha anakuwa salama dhidi ya ugonjwa huo.

Aidha amesema bado kuna maeneo ambayo yanatoka wagonjwa wengi wanaobainika kuwa na vimelea vya Malaria ikiwemo Wilaya ya Maghariba A na B , Wilaya ya kati na Wilaya ya Micheweni Kisiwani Pemba na kwa wale Wananchi ambao wanatoka Tanzania bara katika mikoa ya Mwanza na Geita.

Kwa upande wake Waziri Nyoni Meneja Miradi wa VectorWorks amesema watakuwa na kazi ya kuhamasisha Jamii kuhakikisha vyandarua wanavyopatiwa wanavitumia ipasavyo ili kujikinga na ugonjwa na Malaria.

Kampeini ya kugawa vyandarua vyenye dawa ya muda mrefu umefadhiliwa na Shirika la Misaada la Marekani – USAID kupitia Mfuko wa Raisi wa Marekani wa kudhibiti malaria na kuratibiwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia Kitengo cha kumaliza Malaria Zanzibar - ZAMEP .




Meneja wa kitengo cha kupambana na Malaria Zanzibar Abdallah Suleiman Ally akiongea na waandishi wa habari leo Zanzibar wakati akitangaza kuanza kugawa vyandarua vyenye dawa ya muda mrefu ikiwa ni juhudi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuendelea kupambana na ugonjwa wa Malaria chini ya umefadhiliwa na Shirika la Misaada la Marekani – USAID kupitia Mfuko wa Raisi wa Marekani wa kudhibiti malaria.
Meneja Miradi kutoka VectorWorks akiongea na waandishi wa habari leo Zanzibar wakati akitangaza kuanza kugawa vyandarua vyenye dawa ya muda mrefu ikiwa ni juhudi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuendelea kupambana na ugonjwa wa Malaria chini ya umefadhiliwa na Shirika la Misaada la Marekani – USAID kupitia Mfuko wa Raisi wa Marekani wa kudhibiti

-- Ahmad Issa Michuzi Editorial Director P.O BOX 9033, DAR ES SALAAM. issamichuzi.blogspot.com www.michuzijr.blogspot.com othmanmichuzi.blogspot.com Phone:0713 422 313/ 0783 422 313 Tanzania- East Africa.

DK. KIGWANGALLA APOKEA WAWEKEZAJI KUTOKA CHINA WANAOTAKA KUWEKEZA KATIKA SEKTA YA UTALII

March 28, 2018
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akiwa kwenye picha ya pamoja na wawekezaji wa Kampuni ya Kimataifa ya Tibet Dexin Financia Leasing kutoka nchini China ofisini kwake mjini Dodoma jana wakati kampuni hiyo ilipowasilisha mpango wake wa kuwekeza apa nchini katika ujenzi wa mahoteli na huduma za utalii zenye ladha na mandhari ya kichina.

Na Hamza Temba - WMU-Dodoma

Kufuatia jitihada mbalimbali zinazofanywa na Serikali kutafuta wawekezaji wa Kimataifa kwa ajili ya kuwekeza katika sekta utalii hapa nchini, Kampuni ya Kimataifa ya Tibet Dexin Financia Leasing kutoka nchini China imejitokeza kwa lengo la kuwekeza katika utoaji wa huduma za kitalii zenye ladha na mandhari ya Kichina
Mwenyekiti wa Kampuni hiyo aliyejitambulisha kwa jina moja la Tony, amesema kampuni hiyo imepanga kujenga hoteli za kitalii za kichina katika mji wa Karatu jijini Arusha na Serengeti mkoani Mara.

Akizungumza na Waziri wa Maliasil na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla ofisini kwake mjini hapa jana kwa ajili ya kutambulisha mradi huo, Tony alisema mradi huo ni mahsusi kwa ajili ya kutoa huduma kwa watalii wa China wanaotembelea Tanzania

Alisema kupitia mradi huo jumla ya magari 500 ya safari za utalii yatanunuliwa (Safari Cars) kwa ajili ya kutoa huduma kwa watalii hao wakati wa kutembelea maeneo ya vivutio hapa nchini.

Pamoja na magari hayo alisema kampuni hiyo pia imepanga kuanzisha safari za moja kwa moja za ndege kutoka China hadi Tanzania ili kupunguza muda wa usafiri na gharama.

"Kupitia mradi huu, tunategemea kuhudumia watalii 200,000 kwa mwaka kutoka nchini China na kutengeneza ajira zaidi ya 200 kwa Watanzania" alisema Tony.

Alisema kwa sasa ni watalii 35,000 tu kutoka China wanaotembelea Tanzania kwa mwaka, na kwamba kupitia mradi huo idadi hiyo inatarajiwa kuongezeka.

Naye Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla alisema mradi huo umekuja wakati muafaka wakati huu Serikali kupitia Wizara yake imeshaweka mikakati mahususi ya kupanua wigo wa soko la utalii nchini China.

Alisema miongoni mwa mikakati hiyo inayolenga kuvutia watalii zaidi ya 200,000 kwa mwaka katika kipindi cha muda mfupi wa miaka mitatu, ni kuwakaribisha wachina wenyewe kuja kuwekeza kwenye mahoteli na huduma zenye ladha na mandhari ya kikwao. Mataifa mengine ni Israel, Urusi na Oman.






Alisema kwa sasa ni idadi ndogo tu ya watalii wa China wanaotembelea Tanzania ukilinganisha na ukubwa wa soko la nchi hiyo.






Aliahidi kuwapa ushirikiano wawekezaji hao ikiwa ni pamoja na kuwapa maeneo kwa ajili ujenzi wa hoteli hizo za kitalii ndani ya maeneo ya hifadhi ili kuwezesha ongezeko la watalii kutoka nchini humo.

"Kwa yale maeneo mtakayohitaji ambayo yapo nje na maeneo yetu ya hifadhi tunayoyasimamia, tutawasiliana na mamlaka husika ili muweze kuapatiwa maeneo ya kuanzisha uwekezaji huo muhimu kwa taifa" alisema Dk. Kigwangalla

Aliwataka pia wawekezaji hao kupitia taratibu zote za kuwekeza hapa nchini ikiwa ni pamoja na kujisajili katika Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Kusajili kampuni ya utalii hapa nchini na kuwasilisha andiko la mradi na namna ya utekelezaji wake.


Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akizungumza na wawekezaji wa Kampuni ya Kimataifa ya Tibet Dexin Financia Leasing kutoka nchini China ofisini kwake mjini Dodoma jana wakati kampuni hiyo ilipowasilisha mpango wake wa kuwekeza apa nchini katika ujenzi wa mahoteli na huduma za utalii zenye ladha na mandhari ya kichina.




Wawekezaji wa Kampuni ya Kimataifa ya Tibet Dexin Financia Leasing kutoka nchini China wakiwa kwenye mazungumzo na Waziri Kigwangalla ofisini kwake mjini Dodoma.



Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akimkabidhi flash yenye picha za wanyamapori wa Tanzania Mwenyekiti wa Kampuni ya Kimataifa ya Tibet Dexin Financia Leasing, aliyefahamika kwa jina moja la Tony kutoka nchini China ofisini kwake mjini Dodoma jana wakati kampuni hiyo ilipowasilisha mpango wake wa kuwekeza hapa nchini katika ujenzi wa mahoteli na huduma za utalii zenye ladha na mandhari ya kichina.


Waziri Kigwangalla akiendelea na mazungumzo na wakezaji hao.


Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akizungumza na wawekezaji wa Kampuni ya Kimataifa ya Tibet Dexin Financia Leasing kutoka nchini China ofisini kwake mjini Dodoma jana wakati kampuni hiyo ilipowasilisha mpango wake wa kuwekeza apa nchini katika ujenzi wa mahoteli na huduma za utalii zenye ladha na mandhari ya kichina.


Mazungumzo yakiwa yanaendelea.

Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akiagana na wawekezaji wa Kampuni ya Kimataifa ya Tibet Dexin Financia Leasing kutoka nchini China ofisini kwake mjini Dodoma jana baada ya kampuni hiyo kuwasilisha mpango wake wa kuwekeza apa nchini katika ujenzi wa mahoteli na huduma za utalii zenye ladha na mandhari ya kichina.

MILIONI 260 ZA TATU MZUKA KUNYAKULIWA KATIKA JACKPOT YA PASAKA

March 28, 2018

Tatu Mzuka, mchezo wa namba unaongoza hapa nchini unawapa fursa Watanzania kushinda kitita cha Shilingi milioni 260 katika droo itakayofanyika jumapili ya pasaka na kuonyeshwa moja kwa moja saa 3:30 usiku

Taifa linapojiandaa na sherehe za Pasaka, Tatumzuka imeungana na wateja wake kwa kutangaza fursa ya kushinda kitita cha shilingi 260 ambacho lazima kitolewe jumapili ya Pasaka.

Kitita hicho kinono cha milioni 260 ambacho hakijawahi kutolewa kwa mtu katika historia ya nchi hii sasa kitatolewa kwa mshindi mmoja atakayebahatika kwenye ‘PasakaMzukaJackpot’ siku ya tarehe 31/3/2018.

Bwana Sebastian Maganga, Mkuu wa kitengo cha mawasiliano wa Tatumzuka, ameuelezea umma namna ilivyo rahisi kuingia katika droo. “Wiki hii ukiwa na shilingi 500 tu, kwa kutumia; Mpesa, Tigo pesa au Airtel Money, ingiza namba ya kampuni ambayo ni 555111, kisha weka namba zako tatu za bahati na hapo utakuwa umeingia rasmi kwenye droo ya milioni 260 za PasakaMzukaJackpot” alielezea Maganga

Hicho sio kitu pekee ambacho Tatumzuka inatoa msimu huu wa sikukuu, pia una nafasi ya kushinda milioni 10 kila siku na milioni 6 kila saa.“Ukinunua tiketi moja ya shilingi 500, Tatumzuka inakupa nafasi ya kuingia katika droo 3 tofauti na hivyo kukuongezea nafasi za kushinda tofauti na michezo mingine ya namba” Maganga alisisitiza

Tatu Mzuka pia imetumia fursa hiyo kuwatambulisha washindi wa wiki iliyopita ambao walitokana na droo ya 34 ya Tatumzuka jackpot.Bi Hanifa kutoka Magomeni, Dar es Salaam alijishindia milioni 5. Bwana Juma Mkombozi kutoka Magomeni, Kagera alijishindia milioni 7. Bwana Prosper Munuo kutoka Bunju A alijinyakulia milioni 5 na Magreth Nkwabi wa Kahama, Shinyanga alipata milioni 3.

Washindi wote wakiwa wenye furaha baada ya ushindi walisisitiza kwamba wataendelea kucheza kujaribu bahati zao kwenye dau la kihistoria la milioni 260 jumapili hii.‘Droo hii ya kihistoria itaonyeshwa moja kwa moja kupitia ITV, Clouds TV na TV1 jumapili hii saa 3:30 usiku’ Bwana Maganga aliufafanulia umma.


Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano Sebastian Maganga akizungumza na Waandishi wa Habari mapema leo jijini Dar akielezea kuhusu Tatumzuka kuungana na wateja wake kwa kutangaza fursa ya kushinda kitita cha shilingi 260 ambacho lazima kitolewe jumapili ya Pasaka.




Mmoja ya washindi akikabidhiwa mfano wa Hundi yake yenye thamani ya shilingi milioni tano na la Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Sebastian Maganga.


Washindi wa Tatu Mzuka Jackpot wa wiki iliyopita kwa pamoja wakifurahi

AGPAHI YAKABIDHI MASHINE ZA KUCHUNGUZA SARATANI YA SHINGO YA KIZAZI,KOMPYUTA MKOA WA MWANZA

March 28, 2018




Shirika la Ariel Glaser Pediatric AIDS Healthcare Initiative (AGPAHI) limekabidhi mashine tano za kuchunguza saratani ya shingo ya kizazi kwa wanawake ‘cryotherapy machines’ mkoa wa Mwanza.


Msaada huo umetolewa Jumanne Machi 27,2018 katika ukumbi wa mikutano wa Gold Crest Hotel jijini Mwanza wakati wa kikao cha wadau wanaohusika katika mapambano ya VVU na Ukimwi mkoani Mwanza kwa ajili ya kupanga mipango na mikakati ya kupambana na VVU na Ukimwi.


Akizungumza wakati wa kukabidhi mashine hizo, Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la AGPAHI, Dk. Sekela Mwakyusa alisema mashine hizo ni kwa ajili ya vituo vya afya vya Katunguru na Kabila vilivyopo wilaya ya Sengerema, hospitali ya Ngudu iliyopo wilayani Kwimba na zahanati ya Kirumba na kituo cha afya cha Buzuruga vilivyopo wilayani Ilemela.
Dk. Sekela alisema mashine hizo tano zenye thamani ya shilingi milioni 6.8 zitatumika kutolea tiba mgando kwa akina mama wanaokutwa na dalili za mwanzo za kansa ya uzazi.


“Mbali na shirika letu kuendelea kuboresha huduma za kinga na matunzo pia tunatoa huduma ya uchunguzi wa dalili saratani ya mlango wa kizazi kwa akina mama”,alieleza.

Alisema huduma hiyo hutolewa katika vituo vya kutolea huduma ya afya 20 katika mkoa wa Mwanza.

Dk. Sekela alisema shirika hilo mpaka sasa limetoa msaada wa ‘cryotherapy machines’ 17 katika mikoa sita ambayo ni Mwanza,Shinyanga,Tanga,Geita,Simiyu na Mara zote zikiwa na thamani ya jumla ya shilingi milioni 115.6.

Dk. Sekela pia alikabidhi kompyuta 18 zitakazotumika kuhifadhi takwimu za wateja wa CTC katika vituo vya afya husika na kusaidia upatikanaji wa taarifa kwa haraka na kwa usahihi Zaidi mkoani Mwanza.
“Tangu tuanze mradi wa Boresha, tutakuwa tumetoa jumla ya kompyuta 82 kwa mkoa wa Mwanza ambazo zinatumika kutunza taarifa za watu wenye VVU na Ukimwi”,alisema.


Akizungumza kwa niaba ya wilaya zilizopokea mashine hizo,Mkuu wa wilaya ya Sengerema Emmanuel Kipole alilishukuru shirika la AGPAHI kwa kutoa msaada huo na kwamba watatumia vifaa vilivyotolewa kwa malengo yaliyokusudiwa.

Awali akizungumza katika kikao hicho, Mkuu wa mkoa wa Mwanza, John Mongella aliwataka wadau wote kuungana na kushirikiana ili kuhakikisha kuwa maambukizi ya VVU mkoa huo ambayo sasa ni asilimia 7.2 yanapungua.

AGPAHI ni shirika la Kitanzania linalofanya kazi kwa kushirikiana na serikali ya Tanzania kutoa huduma za afya hususani watu wanaoishi na Maambukizi ya Virusi vya Ukimwi na Ukimwi kwa fadhili wa Watu wa Marekani kupitia Centres for Disease Control (CDC).

ANGALIA PICHA ZA MATUKIO

Mkuu wa mkoa wa Mwanza, John Mongella akizungumza katika kikao cha wadau wanaohusika katika mapambano ya VVU na Ukimwi mkoani Mwanza kabla ya makabidhiano ya kompyuta na mashine tano za kuchunguza saratani ya shingo ya kizazi kwa wanawake ‘cryotherapy machines’.- Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog

Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la AGPAHI, Dk. Sekela Mwakyusa akielezea namna shirika hilo linavyotoa huduma ya kuwapima saratani ya shingo ya kizazi kwa wanawake.


Dk. Sekela akizungumza na wadau wa afya mkoani Mwanza.
Maboksi yenye kompyuta na mashine za kuchunguza saratani ya shingo ya kizazi kwa wanawake ‘cryotherapy machines’ zilizotolewa na shirika la AGPAHI kwa ajili ya vituo vya afya mkoani Mwanza.

Kulia ni Dk. Mwakyusa akiwa ameshikilia moja ya mashine inayotumika kuchunguza saratani ya shingo ya kizazi kwa wanawake ‘cryotherapy machines’.

Dk. Sekela akizungumza ukumbini.

Katikati ni Dk. Sekela Mwakyusa akikabidhi mashine kwa Mkuu wa mkoa wa Mwanza,John Mongella (wa pili kushoto) na viongozi wa wilaya ya Sengerema.


Zoezi la makabidhiano likiendelea. Wa kwanza kushoto ni Mwakilishi wa CDC nchini, Dk. Eva Matiko.




Kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Nyamagana, Mary Tesha akipokea cryotherapy machine.



Mkuu wa wilaya ya Sengerema Emmanuel Kipole akitoa neno la shukrani baada ya makabidhiano ya mashine tano za kuchunguza saratani ya shingo ya kizazi kwa wanawake na kompyuta 18 zilizotolewa na shirika la AGPAHI.

Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog