CHRISTIAN BELLA AACHA HISTORIA VALENTINE'S DAY, DAR LIVE
Christian Bella akiimba na mashabiki wimbo wa Usilie.
Bella akiwakonga mashabiki jukwaani.
Wanenguaji wa Malaika Music wakifanya yao jukwaani.
Baadhi ya mashabiki wakijiachia kwa kucheza Wimbo wa Nakuhitaji wa Christian Bella.
Umati wa mashabiki wakimfuatilia Bella (hayupo pichani) alipokuwa akiimba Wimbo wa Usilie.
MFALME
wa masauti 'Christian Bella' akiwa na bendi yake ya Malaika Music
wameandika historia mpya ndani ya Uwanja wa Taifa wa Burudani, Dar Live,
Mbagala.
Bella
alianza kwa kuimba nyimbo zake kali za mapenzi kama vile Msaliti,
Usilie, Nakuhitaji sambamba na kutambulisha wimbo wake mpya wa
Nashindwa. Burudani ilinoga zaidi pale alipomaliza kwa Wimbo wa Nani
Kama Mama huku akiimba pamoja na wakinamama wote waliojumuika naye
jukwaani.
(Habari/Picha: Richard Bukos)
MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL, AKABIDHI TUNZO YA RAIS YA MZALISHAJI BORA MWAKA 2014
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na
wadau mbalimbali kwenye Ghafla ya utoaji Tunzo ya Rais ya mzalishaji
bora Mwaka 2014 wakati wa chakula cha jioni kilichoandaliwa na
Jumuiya ya wafanyabiashara (Cti). Ghafla hiyo imefanyika jana
usiku Februari 14,2015 katika Hoteli ya Serena jijini Dar es salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiangalia
maonesho mbalimbali kwenye Ghafla ya utoajio Tunzo ya Rais ya
mzalishaji bora Mwaka 2014 wakati wa chakula cha jioni kilichoandaliwa
na Jumuiya ya wafanyabiashara (Cti). Ghafla hiyo imefanyika
jana usiku Februari 14,2015 katika Hoteli ya Serena jijini Dar es
salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akikabidhi kikombe
kwa washindi bora wa Tunzo ya Rais ya mzalishaji bora Mwaka 2014
uongozi wa Kiwanda cha Saruji Tanga, wakati wa chakula cha jioni
kilichoandaliwa na Jumuiya ya wafanyabiashara (Cti). Ghafla hiyo
imefanyika jana usiku Februari 14,2015 katika Hoteli ya Serena jijini
Dar es salaam.
Washiriki waliohidhudhia kwenye
Ghafla ya utoaji Tunzo ya Rais ya mzalishaji bora Mwaka 2014
wakimsikiliza Makamu wa Rais Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal alipokua
akizungumza kwenye ghafla ya chakula cha jioni kilichoandaliwa na
Jumuiya ya wafanyabiashara (Cti). Ghafla hiyo imefanyika jana usiku
Februari 14,2015 katika Hoteli ya Serena jijini Dar es salaam. (Picha na
OMR)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal katikati akiwa
katika picha ya pamoja na washindi wa Tunzo ya Rais ya mzalishaji bora
Mwaka 2014, wakati wa ghafla ya chakula cha jioni kilichoandaliwa na
Jumuiya ya wafanyabiashara (Cti). Ghafla hiyo imefanyika jana usiku
Februari 14,2015 katika Hoteli ya Serena jijini Dar es salaam.
Tanzania yaipongeza China kwa misaada ya kimaendeleo.
Waziri wa Mambo ya Nje na
Ushirikiano wa Kimatafa Bernard Membe akitoa hotuba kwa niaba ya Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete ambaye alikuwa
Mgeni Rasmi katika sherehe ya mwaka mpya wa Kichina jana katika viwanja
vya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam.
Balozi wa China nchini Tanzania,
Dkt Lu Youqing akitoa hotuba ya kumkaribisha Waziri wa Mambo ya Nje na
Ushirikiano wa Kimatafa Bernard Membe kutoa hotuba kwa niaba ya Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete ambaye alikuwa Mgeni
Rasmi katika sherehe ya mwaka mpya wa Kichina jana katika viwanja vya
Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam.
Balozi wa China nchini Tanzania,
Dkt Lu Youqing (kushoto) na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Sadick Meck
Sadiki(kulia) wakicheza ngoma ya iliyoimbwa kwa lugha ya Kishwahili na
Kichina inayosema tupige jahazi iende mbali wakati wa sherehe ya mwaka
mpya wa Kichina iliyofanyika jana katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini
Dar es salaam.
Waziri wa Mambo ya Nje na
Ushirikiano wa Kimatafa Bernard Membe akizugumza jambo na Balozi wa
China nchini Tanzania, Dkt Lu Youqing wakati wa sherehe ya mwaka mpya wa
Kichina iliyofanyika jana katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es
salaam.
Waziri wa Mambo ya Nje na
Ushirikiano wa Kimatafa Bernard Membe(kushoto) na Balozi wa China nchini
Tanzania, Dkt Lu Youqing (katikati) wakati wa sherehe ya mwaka mpya wa
Kichina iliyofanyika jana katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es
salaam. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es SALAAM, Sadick Meck Sadiki.
Baadhi ya wageni waliaohudhuria
sherehe ya mwaka mpya wa Kichina iliyofanyika jana katika viwanja vya
Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam.
(Picha na Eleuteri mangi- MAELEZO)
………………………………………………………………………….
………………………………………………………………………….
Na Magreth Kinabo na Eleuteri Mangi- MAELEZO
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimatafa Bernard Membe,
ameipongeza Serikali Jamhuri ya China kwa msaada wake wa kuhakikisha
Tanzania imefungua idara ya maalum ya upasuaji wa moyo katika hospitali
ya Taifa ya Muhimbili (MNH).
Hayo yamesemwa na Waziri Membe jana katika viwanja vya Mnazi
Mmoja jijini Dar es salaam kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete ambaye alikuwa Mgeni Rasmi katika sherehe
ya mwaka mpya wa Kichina.
“Tuna mengi ya kusema kuhusu misaada ya maendeleo inayoletwa na
ndugu zetu Wachina Sasa hivi muhimbili, kwa mfamo wametusaidia kufungua
idara maalum ya upasuaji wa moyo, ambayo sasa unaweza kufanya upasuaji
wa moyo jambo ambalo lilikuwa hadithi ya kufikirika katika Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania.
“Lakini sasa hivi Watanzania wanaweza kwenda kutibiwa ugonjwa wa
moyo kwa kupasua na kufanyiwa matibabu. Tunawapongeza Serikali ya China
kwa kuleta msaada mkubwa wa aina hii nchini Tanzania,” alisema Waziri
Membe.
Katika sherehe hizo za mwaka mpya,Jumuiya ya Wachina waishio
nchini Tanzania waliungana pamoja na wageni wengine kusherehekea siku
kuu hiyo, ambayo itaanza rasmi February 18, mwaka huu.
Waziri Membe akifafanua kuhusu mwaka huo, alisema kuwa
utajulikana kama mwaka wa kondoo, ambapo mwaka jana 2014 ulijulikana
kama mwaka wa farasi.
Jumuiya hiyo wamechagua siku hiyo ya Februari 14 kwa kuwa ni
mwisho wa wiki tofauti na siku yao rasmi ya mwaka mpya ambayo
itaangukuia Jumatano ambayo ni katikati ya wiki na kuwanyima wengine
fursa ya kuhudhuria na wanasherehekea siku yao ya mwaka mpya 2015.
Aliongeza misaada mingine ya maendeleo ilitolewa na nchi hiyo ni
miradi ya maji Dodoma na Chalinze mkoani Pwani, mradi ya kilimo Dakawa
mkoani Morogoro, Uwanja wa Taifa wa Michezo na Ukumbi wa mikutano wa
Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere, uliopo jijini Dar es Salaam.
Kwa upande wake Balozi wa China nchini Tanzania, Dkt Lu Youqing
alisema sherehe hiyo kama alama ya kufahamu utamaduni wa nchi hiyo,
imeshafanyika kwa mafanikio mkubwa kwa miaka sita nchini Tanzania na
inapendeza, ambayo ni mfano mzuri wa ushirikiano kati ya nchi hizo mbili
katika sekta ya utamaduni.
“Uhusiano wa Tanzania na China
sasa uko katika kipindi kizuri cha Juu, mwaka 2014 uliopita ni miaka 50
ya uhusiano wa kidiplomasia baina ya Tanzania na China. Kwa nusu karne
uhusiano nchi hizi mbili zinasaidiana na urafiki wa baina ya nchi hizi
mbili umepata maendeleo makubwa,” alisema Balozi Dkt Youqing.
Balozi huyo aliishukuru Serikali Tanzania kwa kuunga mkono
sherehe hiyo na aliwaomba wananchi wa nchi hizo kushirikiana na
kusaidiana ili kupata maendeleo pande zote mbili.
Serikali hiyo ya China imepongezwa kwa kuwa nchi mfano wa kuigwa
kwa kutoa misaada mbalimbali Barani Afrika,ambapo imesaidia kutatua
migogoro na kutoa dola za Marekani milioni 35 kwa ajili ya kukabiliana
na ugonjwa wa ebola na kutoa madaktari 200 ili kukabiliana na janga hilo
katika nchi za Liberia,Guinea pamoja na Sierra Leone
MAKAMU WA KWANZA WA RAIS ZANZIBAR AREJEA NCHINI AKITOKEA QATARI KWA ZIARA YA KIKAZI.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa
Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akishuka ndege katika uwanja wa
Kimataifa wa Abeid Amani Karume baada ya kumaliza ziara ya Kiserikali
nchi Qatar.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa
Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akivishwa shada la maua alipowasili
uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume akitokea nchini
Qatar.
Waziri wa Biashara, Viwanda na
Masoko Nassor Ahmed Mazrui akisalimiana na Makamu wa kwanza wa Rais wa
Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad alipowasili uwanja wa ndege wa
Kimataifa wa Abeid Amani Karume akitokea nchini Qatar, wa kwanza
(kushoto) Waziri wa Nchi katika Ofisi yake Fatma Abdulhabib Ferej.
Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa
Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akizungumza na waandishi wa habari
katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Zanzibar mara baada ya kuwasili
kutoka ziara yake ya Qatar. Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar.
Mwandishi wa habari wa Radio
Adhana FM Said Mussa Makame akimuuliza swali Makamu wa Kwanza wa Rais
Maalim Seif Sharif Hamad alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari
Katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Zanzibar.
Maalim Seif Sharif Hamad akiagana na wananchi waliofika Uwanja wa ndege wa Zanzibar kumpokea akitokea Qatar.
Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar.
BALOZI WA PROMOSHENI YA JAYMILLIONS YA VODACOM'JAY'AWALIPIA ABIRIA WOTE NAULI WA KITUO CHA MAWASILIANO JIJINI
Balozi
wa Promosheni ya JayMillions inayoendeshwa na Vodacom Tanzania Hilary
Daud”Zembwela”(kushoto)akimkabidhi fedha mmoja wa abiria wa basi
linalofanya safari zake kutoka kituo cha mabasi cha mawasiliano cha
ubungo kwenda Mwananyamala jijini Dar es Salaam kwaajili ya kuwalipia
abiria wenzake nauli ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha wateja wa kampuni
hiyo kutuma neno Jay kwenda 15544 ili kujua kama wameshinda.
Mkazi
wa jijini Dar es Salaam Mudy Seleman(kushoto)akikabidhiwa fedha kwa
ajili ya nauli na Balozi wa Promosheni ya JayMillions inayoendeshwa na
Vodacom Tanzania Hilary Daud”Zembwela” wakati wa kuhamasisha wateja wa
kampuni hiyo kutuma neno Jay kwenda 15544 ili kujua kama wameshinda
iliyofanyika katika kituo cha mabasi cha Mawasiliano ubungo jijini Dar
es Salaam.
Baadhi
ya wanafunzi waliokuwa wakisubiria usafiri katika kituo cha mabasi cha
mawasiliano ubungo jijini Dar es Salaam wakipiga picha ya pamoja na
Balozi wa Promosheni ya JayMillions inayoendeshwa na Vodacom Tanzania
Hilary Daud”Zembwela”(kushoto)baada ya kuwalipia nauli wakati wa
kuhamasisha wateja wa kampuni hiyo kutuma neno Jay kwenda 15544 ili
kujua kama wameshinda iliyofanyika katika kituo hicho.
Meneja
uhusiano wa Vodacom Tanzania,Matina Nkurlu(kushoto)akitoa elimu kwa
mmoja wa abiria wa basi liendalo Gongolamboto kutoka kituo cha mabasi
cha mawasiliano ubungo jijini Dar es Salaam juu ya Promosheni ya
JayMillions inayoendeshwa na kampuni hiyo ambapo wateja wanatakiwa
kutuma neno Jay kwenda 15544 ili kujua kama wameshinda.
Baadhi
ya abiria wakiwa na watoto wao katika kituo cha mabasi cha Mawasiliano
ubungo jijini Dar es Salaam, wakifafanuliwa jambo na mfanyakazi wa
Vodacom Tanzania Joyce Mhina kuhusiana na Promosheni ya JayMillions
inayoendeshwa na kampuni hiyo wakati Balozi wa promosheni hiyo alipoenda
kituoni hapo kutoa elimu kuhusiana na promosheni hiyo na kuwalipia
wasafiri wote bure wa daladala nauli kulingana na sehemu wanayo kwenda
ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha wananchi kushirikia katika promosheni
hiyo.Ili mteja kujua kama ameshinda anatakiwa kutuma neno Jay kwenda
15544.
Balozi
wa Promosheni ya JayMillions inayoendeshwa na Vodacom Tanzania Hilary
Daud”Zembwela”(aliyesimama)akitoa elimu juu ya promosheni hiyo kwa
abiria waliopanda daladala zinazofanya safari za mlandizi kutoka kituo
cha mabasi cha mawasiliano ubungo jijini Dar es Salaam na aliwalipia
nauli abiria wote bure ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha wananchi
kushirikia katika promosheni hiyo.Ili mteja kujua kama ameshinda
anatakiwa kutuma neno Jay kwenda 15544.
Kondakta
wa basi linalofanya safari zake kutoka kituo cha mabasi cha
Mawasiliano ubungo kwenda Kawe jijini Dar es Salaam, Hamis
Omari(kushoto)akikabidhiwa nauli ya abiria wote waliopanda gari lake na
Balozi wa Promosheni ya JayMillions inayoendeshwa na Vodacom Tanzania
Hilary Daud”Zembwela”(kulia) wakati alipokuwa akihamasisha wateja wa
kampuni hiyo kituoni hapo kutuma neno Jay kwenda 15544 ili kujua kama
wameshinda. Ambapo abiria wote waliokuwepo kituoni hapo walilipiwa nauli
kulingana na safari zao.
Balozi wa promosheni ya Jaymilioni inayoendeshwa na Vodacom Tanzania Hillary Daud‘Jaymillions’ mwishoni mwa wiki alikuwa kivutio kwa wananchi wengi alipotembelea eneo kituo cha mabasi cha Ubungo Mawasiliano na kuwahimiza wananchi kuchangamkia fursa zinazojitokeza katika maisha yao ambapo pia alitoa ofa ya kuwalipia nauli wasafiri waliokuwa wamepanda mabasi kuelekea sehemu mbalimbali za jiji waliokuwa kituono hapo.
Ziara hiyo ilileta msisimko mkubwa wa wananchi waliokuwa eneo hilo ambapo baadhi yao walilazimika kuacha shughuli zao kumwangalia balozi huyo na wengine kuomba kupiga naye picha ikiwemo waliompiga picha kwa kutumia simu zao zao mkononi.
Balozi huyo alitumia fursa hiyo kuwaeleza wananchi kuwa wanaotumia mtandao wa Vodacom wahakikishe kila siku wameangalia kama namba zao zimeshinda mamilioni ya fedha kwa kutuma neno JAY kwenda namba 15544 na aliwataka wale ambao hawako kwenye mtandao wa Vodacom wajiunge nao ili washiriki kwenye promosheni hii kubwa iliyolenga kubadilisha maisha ya watanzania wengi kuwa mamilionea.
“Leo nimewafuata huku kuwapatia ofa na kuwafikishia ujumbe kwa maana naona wengi wenu bado hamjachangamkia fursa hii kwa kuangalia iwapo namba zenu zimeshinda kila siku,bado tunayo mabilioni ya fedha kwa ajili yenu hivyo changamkia fursa hii muweze kujishindia mamilioni ya fedha katika kipindi hiki cha promosheni.Kila siku kuna mshindi 1 wa shilingi milioni 100,000,washindi 10 wa milioni 10 na washindi 100 wa shilingi milioni 1 hivyo kazi kwenu na Vodacom”.Alisema
Naye Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Vodacom Tanzania Rosalynn Mworia, aliwahimiza wateja wote kuchangamkia promosheni hii kwa kuhakikisha wametuma neno JAY kwenda namba 15544 ili kutopoteza nafasi zao za kushinda pia alisema kuwa njia nyingine ya kushinda ni kutuma neno AUTO kwenda namba 15544 iwapo simu haina fedha ambapo mteja akiweka fedha anakatwa shilingi 300/-
Alisema kuwa tangu promosheni hii ianze mapema mwezi uliopita mteja mmoja ameishajishindia milioni 100, wateja 2 wamekwishajishindia milioni 10 na wateja kumi na moja wameisha jishindia shilingi milioni moja kila mmoja na maelfu ya wateja wengine tayari wamejishindia muda wa maongezi.
Wateja wa Vodacom ambao tayari wamejipatia mamilioni ya fedha kupitia promosheni hii ni Uwezo Magedenge mfanyakazi nyumba ya wageni wilayani Kilolo mkoani Iringa ambaye amejishindia milioni 100. Waliojishindia milioni kumi kila mmoja wao Hynes Petro Kanumba mkulima kutoka Inyonga mkoani Rukwa na James Mangu mfanyabiashara kutoka wilayani Magu.
Washindi wa milioni moja ni Chiphold Wanjara mjasiriamali wa Kutoka Mwanza ,Janeth Nganyange wa Njombe,Evarista Minja mwanafunzi kutoka Mwanza,Stanley Bagashe Mwalimu wa Shinyanga,Ramadhani Maulid Mkulima kutoka Dodoma, ,Lucas Masegese wa Shinyanga,Ayub Makonde mfanyabiashara wa Mbeya,Hyasinti Mlowe Fundi gereji kutoka Njombe,Florian Gwayu mchapishaji kutoka Arusha,Modesta Millanzi mjasiriamali kutoka Peramiho mkoani Ruvuma na Nobert Minungu mwanafunzi kutoka Mbwanga mkoani Dodoma.
“Promosheni hii itadumu kwa muda wa siku mia moja hivyo juma hili inaingia katika wiki ya nne na bado kuna mabilioni ya fedha yamewasubiri watanzania,wanachopaswa kufanya ni kuhakikisha kila siku wameangalia kama namba zao zimeibuka na ushindi kwenye droo ya siku kwa kutuma neno Jay kwenda namba 15544.”Alisisitiza.
Balozi wa promosheni ya Jaymilioni inayoendeshwa na Vodacom Tanzania Hillary Daud‘Jaymillions’ mwishoni mwa wiki alikuwa kivutio kwa wananchi wengi alipotembelea eneo kituo cha mabasi cha Ubungo Mawasiliano na kuwahimiza wananchi kuchangamkia fursa zinazojitokeza katika maisha yao ambapo pia alitoa ofa ya kuwalipia nauli wasafiri waliokuwa wamepanda mabasi kuelekea sehemu mbalimbali za jiji waliokuwa kituono hapo.
Ziara hiyo ilileta msisimko mkubwa wa wananchi waliokuwa eneo hilo ambapo baadhi yao walilazimika kuacha shughuli zao kumwangalia balozi huyo na wengine kuomba kupiga naye picha ikiwemo waliompiga picha kwa kutumia simu zao zao mkononi.
Balozi huyo alitumia fursa hiyo kuwaeleza wananchi kuwa wanaotumia mtandao wa Vodacom wahakikishe kila siku wameangalia kama namba zao zimeshinda mamilioni ya fedha kwa kutuma neno JAY kwenda namba 15544 na aliwataka wale ambao hawako kwenye mtandao wa Vodacom wajiunge nao ili washiriki kwenye promosheni hii kubwa iliyolenga kubadilisha maisha ya watanzania wengi kuwa mamilionea.
“Leo nimewafuata huku kuwapatia ofa na kuwafikishia ujumbe kwa maana naona wengi wenu bado hamjachangamkia fursa hii kwa kuangalia iwapo namba zenu zimeshinda kila siku,bado tunayo mabilioni ya fedha kwa ajili yenu hivyo changamkia fursa hii muweze kujishindia mamilioni ya fedha katika kipindi hiki cha promosheni.Kila siku kuna mshindi 1 wa shilingi milioni 100,000,washindi 10 wa milioni 10 na washindi 100 wa shilingi milioni 1 hivyo kazi kwenu na Vodacom”.Alisema
Naye Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Vodacom Tanzania Rosalynn Mworia, aliwahimiza wateja wote kuchangamkia promosheni hii kwa kuhakikisha wametuma neno JAY kwenda namba 15544 ili kutopoteza nafasi zao za kushinda pia alisema kuwa njia nyingine ya kushinda ni kutuma neno AUTO kwenda namba 15544 iwapo simu haina fedha ambapo mteja akiweka fedha anakatwa shilingi 300/-
Alisema kuwa tangu promosheni hii ianze mapema mwezi uliopita mteja mmoja ameishajishindia milioni 100, wateja 2 wamekwishajishindia milioni 10 na wateja kumi na moja wameisha jishindia shilingi milioni moja kila mmoja na maelfu ya wateja wengine tayari wamejishindia muda wa maongezi.
Wateja wa Vodacom ambao tayari wamejipatia mamilioni ya fedha kupitia promosheni hii ni Uwezo Magedenge mfanyakazi nyumba ya wageni wilayani Kilolo mkoani Iringa ambaye amejishindia milioni 100. Waliojishindia milioni kumi kila mmoja wao Hynes Petro Kanumba mkulima kutoka Inyonga mkoani Rukwa na James Mangu mfanyabiashara kutoka wilayani Magu.
Washindi wa milioni moja ni Chiphold Wanjara mjasiriamali wa Kutoka Mwanza ,Janeth Nganyange wa Njombe,Evarista Minja mwanafunzi kutoka Mwanza,Stanley Bagashe Mwalimu wa Shinyanga,Ramadhani Maulid Mkulima kutoka Dodoma, ,Lucas Masegese wa Shinyanga,Ayub Makonde mfanyabiashara wa Mbeya,Hyasinti Mlowe Fundi gereji kutoka Njombe,Florian Gwayu mchapishaji kutoka Arusha,Modesta Millanzi mjasiriamali kutoka Peramiho mkoani Ruvuma na Nobert Minungu mwanafunzi kutoka Mbwanga mkoani Dodoma.
“Promosheni hii itadumu kwa muda wa siku mia moja hivyo juma hili inaingia katika wiki ya nne na bado kuna mabilioni ya fedha yamewasubiri watanzania,wanachopaswa kufanya ni kuhakikisha kila siku wameangalia kama namba zao zimeibuka na ushindi kwenye droo ya siku kwa kutuma neno Jay kwenda namba 15544.”Alisisitiza.
Subscribe to:
Posts (Atom)