Na Mwandishi Wetu,Korogwe.
MKUU wa Mkoa wa Tanga,Chiku Gallawa amewataka maafisa Elimu ya msingi na Sekondari ambao watashindwa kwenda na kasi ya uboreshaji wa elimu wasisite kuandika barua za kuomba kuacha kazi ili wenye uwezo wachukue nafasi zao.
Alitoa agizo hilo wakati wa kikao cha kazi alichoitisha kujua
mikakati ya Halmashauri zilizopo mkoa wa Tanga iliyojiwekea kutekeleza malengo ya kupandisha ufaulu kutoka asilimia 45 hadi 75 katika mitihani ya kitaifa ya kidao cha nne na darasa la saba ya mwaka huu.
Alisema kila Halmashauri inatakiwa kuhakikisha imetekeleza kwa vitendo malengo ya kupandisha ufaulu wa watahiniwa wake watakaofanya mitihani ya kidato cha nne,sita na darasa la saba wa mwaka 2013.
Alitoa agizo hilo baada ya kutoridhishwa na baadhi ya taarifa
zilizotolewa na maafisa elimu ya msingi na Sekondari katika kutekeleza mikakati ya kuhakikisha ufaulu unapanda katika mitihani ya mwaka huu.
“Baadhi ya taarifa mlizotoa hapa hazionyeshi kama mko makini katika kutekeleza malengo,lazima mfahamu kuwa mkoa wa Tanga sasa umeondokana na kufanya kazi kwa mazoea badala yake tubadilike na twende na kasi inayohitajika”alisema Gallawa.
Miongoni mwa taarifa zilizohimizwa kufanyiwa kazi kwa haraka ni pamoja na ile ya kuwazoesha wanafunzi kufanya mitihani kwa kutumia fomu zijulikanazo kwa jina la OMR zilizopitishwa na baraza la mitihani la Taifa na kusababisha idadi kubwa ya wanafunzi kufeli mitihani mwaka jana.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga,Benedikt Ole Kuyan aliwaagiza maafisa elimu wa Wilaya zote za mkoa wa Tanga kujifunza kwa Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga ambayo imekuwa ikiwafanyia mazoezi wanafunzi wake ya namna ya kujibu maswali kwa kutumia OMR.
MWISHO
Alitoa agizo hilo wakati wa kikao cha kazi alichoitisha kujua
mikakati ya Halmashauri zilizopo mkoa wa Tanga iliyojiwekea kutekeleza malengo ya kupandisha ufaulu kutoka asilimia 45 hadi 75 katika mitihani ya kitaifa ya kidao cha nne na darasa la saba ya mwaka huu.
Alisema kila Halmashauri inatakiwa kuhakikisha imetekeleza kwa vitendo malengo ya kupandisha ufaulu wa watahiniwa wake watakaofanya mitihani ya kidato cha nne,sita na darasa la saba wa mwaka 2013.
Alitoa agizo hilo baada ya kutoridhishwa na baadhi ya taarifa
zilizotolewa na maafisa elimu ya msingi na Sekondari katika kutekeleza mikakati ya kuhakikisha ufaulu unapanda katika mitihani ya mwaka huu.
“Baadhi ya taarifa mlizotoa hapa hazionyeshi kama mko makini katika kutekeleza malengo,lazima mfahamu kuwa mkoa wa Tanga sasa umeondokana na kufanya kazi kwa mazoea badala yake tubadilike na twende na kasi inayohitajika”alisema Gallawa.
Miongoni mwa taarifa zilizohimizwa kufanyiwa kazi kwa haraka ni pamoja na ile ya kuwazoesha wanafunzi kufanya mitihani kwa kutumia fomu zijulikanazo kwa jina la OMR zilizopitishwa na baraza la mitihani la Taifa na kusababisha idadi kubwa ya wanafunzi kufeli mitihani mwaka jana.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga,Benedikt Ole Kuyan aliwaagiza maafisa elimu wa Wilaya zote za mkoa wa Tanga kujifunza kwa Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga ambayo imekuwa ikiwafanyia mazoezi wanafunzi wake ya namna ya kujibu maswali kwa kutumia OMR.
MWISHO