DAS KOROGWE AFUNGUA MAFUNZO YA MRADI WA SHULE BORA ATOA NENO WANAHABARI MKOANI TANGA

December 07, 2022


KATIBU Tawala wa wilaya ya Korogwe (DAS) Rahel Mhando akizungumza wakati akifungua mafunzo ya mradi wa shule Bora kwa waandishi wa habari mkoa wa Tanga.


Na Oscar Assenga,KOROGWE

MAFUNZO ya mradi wa Shule Bora kwa waandishi wa Habari Mkoani Tanga yamefanyika wilayani Korogwe huku Katibu Tawala wa wilaya ya Korogwe Rahel Mhando akiwataka wanahabari kutumia kalamu zao vizuri katika kuelimisha jamii juu ya mradi wa shule bora wakizingatia taratibu, kanuni sheria zinazowaongoza katika taaluma yao

Ambapo alisema ili kuweza kuboresha na kufanikisha malengo ya mradi wanaamini mawasiliano kupitia vyombo vya habari ni nyenzo muhimu sana ili kuifikia jamii kubwa zaidi.

Alisema hivyo ni jukumu lao kuhakikisha taarifa zote za shughuli za mradi na maendeleo yake katika mkoa wa Tanga ni lao wote hivyo kila anatakiwa kutekeleza jukumu hilo kwa uhakika , weledi na kwa uadilifu kwa lengo la kuhakikisha watoto wetu wanapata elimu iliyobora "alisema Mhando.

Hata hivyo akizungumza wakati wa mafunzo hayo, Afisa Elimu Mkoa wa Tanga Newaho Mkisi alisema ujio wa mradi huo utakuwa chachu ya kwenda kusaidia na kuongeza kiwango cha ufaulu hatua ambayo itakwenda kuuwezesha mkoa kupata fedha zaidi zinazotolewa na serikali kupitia mradi wa lipa kwa matokeo 'Ep for

Alisema fedha hizo hutolewa kulingana na vigezo na masharti yaliyowekwa na seikali zikiwa na lengo la kuendelea kuweka mazingira rafiki katika sekta ya elimu hapa nchini.

Hata hivyo alisema kwa mkoa huo wa Tanga ufaulu umeongezeka ukilinganisha na wa mwaka jana ukilinganisha na mwaka huu japo sio kwa wastani mkubwa kwenye mradi wa EpforR walikuwa wanashindwa kupata fedha nyingi kwa sababu ya kushindwa kufikia vile vigezo vilivyowekwa ikiwemo ufaulu .

Aliongeza kwamba ili waweze kupata ufaulu mzuri lazima wafanye kazi kwa kushirikiana tukikidhi hivyo vigezo tunapata fedha zaidi abazo zitasaidia katika maswala ya elimu

Mikoa itakayonufaika na mradi huo wa shule bora kwa kipindi chote cha utekelezaji kwa miaka 6 ni Tanga, Dodoma , Pwani , Katavi, Kigoma , Mara, Rukwa , Singida na Simiyu

Naye kwa upande wake Mratibu wa Mradi wa Shule Bora Mkoa wa Tanga Thomas Aikaruwa alisema lengo la mradi huo ni kuboresha na kuinua kiwango cha elimu kwa wanafunzi kuanzia ngazi ya awali hadi darasa la saba unatarajiwa kutekelezwa kwenye mikoa tisa nchini kwa kwa kipindi cha miaka 6 .

Utekelezaji wa mradi huo unafanywa na serikali ya Tanzania kwa ufadhili wea serikali ya uingereza umelenga pia kuboresha ufundishaji kwa walimu, kuboresha elimu jumuishi kwa makundi ya watoto wenye mahitaji maalum , kuboresha ujifunzaji kwa wanafunzi pamoja na kuboresha mfumo wa usimamiaji wa sekta ya elimu katika kuhakikisha kila kiongozi anawajibika ipasavyo kwa nafasi yake ili kufikia adhima iliyokusudiwa.

Alisema mradi huo unakusudia kuongeza muda wa miaka mitatu ambapo itatokana na matokeo yatakayopatikana kwa kipindi chote cha utekelezaji.

Alisema kwamba mradi huo una lengo la kuondoa changamoto zinazowakabili watoto wengi kushindwa kusoma, kuandika na kuhesabu vizuri, tatizo la utoro mashuleni, kupambana na mimba za za utotoni.

Alieleza pia mradi huo utawapa fursa watoto wenye mahitaji maalumu katika kuendelea na elimu ya sekondari ambapo wengi wao wamekuwa wakishindwa kuendelea kutokana na vikwazo mbalimbali.

“Hivyo kwa kutambua mchango wenu kama wana habari kwani ni wadau muhimu katika mradi huo na maendeleo ya sekta ya elimu kwa ujumla hapa nchini tunatarajia kuifikia jamii katika kuwaelimisha, kuhamasisha kwa kupitia vyombo vya habari matarajio yakiwa ni kuweza kuleta matokeo chanya ili kuhakikisha malengo yaliyokusudiwa yanapatikana”Alisema

Aidha alisema matarajio yao makubwa ni kuona elimu ya msingi inaboreka hivyo wanategemea baada ya miaka ya utekelezaji wa mradi wuone hali tofauti kwenye mikoa hii 9 katika sekta ya elimu ikiwemo mahudhurio ya watoto mashuleni yanaboreka,kujua kusoma na kuandika vizuri kabisa , tuone watoto wa kike wakiwa wanapata fursa sawa sawa na watoto wa kiume na watoto wenye mahitaji maalumu wanaendeleea na elimu ya sekondari.

Akizungumzia lengo la kutoa semina kwa waandishi wa habari alisema kwamba wameona wafanye hivyo kutokana na kwamba ni wadau muhimu hivyo wakaona ipo haja ya kufanya nao kazi katika kuelimisha kuhusiana na mradi huo ili nao waweze kuieleza jamii.


Hata hivyo Makamu Mwenyekiti wa Klabu ya waandishi wa Habari mkoa wa Tanga( Tanga Press Club) Burhan Yakub alitoa shukrani kwa waandaaji wa mafunzo hayo ambayo yataleta tija kwa waandishi katika kuendelea kuuhabarisha umma.


Alisema kwa uzoefu uliopo kwa waandishi katika kuandika habari za elimu, imeonekana Tanga kuingia kwenye mradi huo ni tofauti ya matokeo ya darasa la saba.

Makamu Mwenyekiti huyo alisema tatizo ni  kwamba wananchi wengi wanaona shule siyo zao kwamba shule ni ya mwalimu na mwenyekiti wa kijiji, na hii inatokana na kukosekana kwa uwazi na ushirikishwaji, unaweza ukakuta hata hizo fedha zinzoletwa kutoka serikalini hawapati taarifa na ndiomaana wanaona hakuna umuhimu wa kuchangia hata chakula shuleni.

DC TANGA ALISHUKURU SHIRIKA LA BRAC MAENDELEO TANZANIA KWA KUWAKOMBOA WASICHANA KIELIMU

December 07, 2022




Mkuu wa Wilaya ya Tanga Hashim Mgandilwa akizungumza wakati akifungua wa kikao cha wadau cha kujadili na kutathimini mafanikio ya utekelezaji wa mradi wa miaka minne uliokuwa unaotoa elimu, uwezeshaji na stadi za maisha ( Education Empowerment and Life Skills for Adolescent and Young Children -EELAY) Mkoa wa Tanga tangu Juni 2018 hadi Desemba 2022. kulia ni Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga Abdurhaman Shiloo 
Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga Abdurhaman Shiloo wakati akifungua wa kikao cha wadau cha kujadili na kutathimini mafanikio ya utekelezaji wa mradi wa miaka minne uliokuwa unaotoa elimu, uwezeshaji na stadi za maisha ( Education Empowerment and Life Skills for Adolescent and Young Children -EELAY) Mkoa wa Tanga tangu Juni 2018 hadi Desemba 2022
Meneja awa Mradi huo kutoka Shirika la Brac Maendeleo Tanzania Hope Jassson akizungumza wakati wa kikao hicho
Meneja awa Mradi huo kutoka Shirika la Brac Maendeleo Tanzania Hope Jassson akizungumza wakati wa kikao hicho
Afisa Elimu Msingi Jiji la Tanga Kassim Kaonekana akizungumza
Mmoja wa wanafunzi walionufaika na mradi 
Maafisa wa Shirika la Brac Maendeleo Tanzania mkoani Tanga wakiwemo na wadau wengine
Wadau wakiwa kwenye kikao hicho
Sehemu ya wadau wa kikao hoicho
Waheshimiwa madiwani wakiwa kwenye kikao hicho


Na Oscar Assenga,TANGA.


Mkuu wa Wilaya ya Tanga Hashim Mgandilwa amelishukuru Shirika la BRAC Maendeleo Tanzania kwa kuwakomboa Mabinti na Wasichana ambao hawakupata elimu kupitia mfumo maalumu,

Mgandilwa aliyasema hayo wakati wa kikao cha wadau cha kujadili na kutathimini mafanikio ya utekelezaji wa mradi wa miaka minne uliokuwa unaotoa elimu, uwezeshaji na stadi za maisha ( Education Empowerment and Life Skills for Adolescent and Young Children -EELAY) Mkoa wa Tanga tangu Juni 2018 hadi Desemba 2022.

Mradi huo ulikuwa na vipengele viwili muhimu,kipengele cha kwanza kinalenga wasichana walioko kwenye rika balehe wenye umri kati ya miaka 15-24 kwa kutoa elimu ya Sekondari ,mafunzo ya stadi za maisha na fursa za ajira kwa wasichana walio nje ya mfumo rasmi wa elimu kwa kutumia programu ya muda mfupi yenye matokeo chanya kusaidia wasichana katika kukamilisha miaka minne ya elimu ya Sekondari ndani ya miaka miwili.

Alisema kwamba wanashukuru sana kwa mradi huo ambao unawaachia urithi mkubwa wa elimu kwa Watoto hivyo wap kama Serikali wanawaomba wakakae chini watathmini upya kisha warudi tena katika Mkoa huo na Halmashauri ya Jiji la Tanga kuendelea.

Alisema miradi yote ambayo inaachwa na mradi huo itaendelezwa na kwamba hakuna mradi hata mmoja ambao utatelekezwa huku akiwakikishia kuwa miradi yote itaendelezwa kwa gharama yoyote ile na Serikali itasimamia kuhakikisha watoto wanaendelea kupata elimu.

Awali akizungumza Meneja awa Mradi huo kutoka Shirika la Brac Maendeleo Tanzania Hope Jassson alisema kwamba hadi sasa zaidi ya Wasichana 900 ambao hawakufanikiwa kupata Elimu katika mfumo maalumu wa Elimu ya upili ( Sekondari) wamefanikiwa kupata Elimu hiyo kupitia Mradi wa Elimu na Stadi za Maisha unaotekelezwa  katika Mkoa wa Tanga.

Hope alisema Shirika hilo Chini ya Ufadhili wa Shirika la Norad la Nchini wamefanikiwa kuwapatia Elimu ya Sekondari Mabinti hao zaidi ya 900 chini ya Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia,

" Asilimia 86.8 ya Wasichana walioko kwenye Rika Balehe wamefaulu na kupewa Cheti Cha Elimu ya Sekondari kuanzia Mwaka 2017 Hadi 2021, Vituo 30 vya Masomo vinaendelea ya Elimu chini ya usimamizi wa Jamii ambapo Kati ya hivyo Vituo 20 vipo katika Halmashauri ya Jiji la Tanga na 10 vipo Wilaya ya Korogwe " Alisisitiza Hope

Alisema Wasichana zaidi ya 1161 walipatiwa Mafunzo ya kuanzisha Biashara ndogo pamoja na Mitaji kupitia SIDO,VETA na Ustawi wa Jamii,

"Zaidi ya asilimia 65 ya Wasichana hususani katika Halmashauri ya Jiji la Tanga Wanajishughulisha na shughuli za kujiongezea kipato na kubadili mfumo wao wa Maisha ya awali kabla ya kupata Elimu " Alisisitiza Hope

Aliongeza kuwa Wasichana 10 wa wamefanikiwa kujiunga na Chuo kikuu kwa kozi za Shahada ya Kwanza huku Wasichana 22 Walioko kwenye Rika Balehe Wamehitimu ngazi ya Cheti kutoka Chuo Cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) Kampasi ya Tanga Wakati,


"Wasichana wengine 3 waliandikishwa katika Vyuo mbalimbali vikiwamo chuo Cha maji,chuo Cha Taifa Cha Zanzibar na Chuo Cha Usimamizi wa Fedha, Watoto 1670 wa miaka 3-5 walipata Elimu ya Makuzi ,Malezi na Maendeleo ya awali, nafasi za kazi zaidi ya 450, Ujenzi wa Madara mapya 22 na Ukarabati wa madarasa 13 pamoja na Walimu 41 wa Elimu ya Awali kutoka Shule za Serikali walipatiwa Mafunzo juu ya Mtaala wa Elimu ya Awali pamoja na kutoa Vifaa vya kufundishia" Alisisitiza Hope