SKYLIGHT YAENDELEA KUKONGA NYOYO MASHABIKI WAKE NDANI YA ESCAPE ONE MIKOCHENI NI KILA SIKU YA JUMAPILI

September 27, 2015

Wanaume wa shoka wakilisakata rhumba wakati wa kuwafurahisha mashabiki wa bendi ya Skylight wakati wa mkesha wa eid
Mwimbaji wa bendi ya Skylght Natasha akiwa anawapa mashabiki vionjo vya nyimbo za taratibu (kistaarabu) wakati wa mkesha huo wa Eid ndani ya kiwanja cha Escape One Mikocheni
Bendi ya waimbaji wakali wa Skylight ikirindimisha baadhi ya nyimbo zao huku mbele kabisa akiwa anawaongoza wenzake katika uimbaji wa nyimbo hiyo Sony Samba.
Ashura Kitenge (kushoto) akiwa na Kasongo Junior wa Skylight band wakitoa burudani ya kukata na shoka kwa mashabiki wao ndani ya kiwanja cha Escape One Mikocheni
Sam Mapenzi ni muimbaji mashuhuri na huwa anajua kukonga nyoyo za watu hususani katika ule muziki wa Afrika magharibi weee utampenda hata kwa mkopo, hapo akiwa anaimba kwa kushirikiana na wenzake ndani ya bendi ya Skylight siku ya mkesha wa Eid.
Hii siku zote huwa inapatikana ndani ya Skylight tu na sio kwingineko maana ukihitaji kuburudika njoo tuungane pamoja katika bendi yetu inayoenda kwa kusikiliza mashabiki zaidi na sio kubagua mashabiki.
Mashabiki sasa zamu yao kulisakata wakati bendi ya Skylight ikiwa inatoa burudani hiyo ndani ya Escape One Mikocheni
Rapa mkongwe kwenye muziki wa Live Joniko Flower akiwa katika hatua yake ya kukusanya mashabiki ili tu waende sawa aisee huyu jamaa ni hatari jumapili hii atakuwepo pale Escape One Mikocheni bila kukosa sogea taratibu uje ushuhudie vitu kutoka Skylight band.
Sam Mapenzi (kushoto) akiwa na Ashura Kitenge wakitoa burudani ya nguvu ndani ya Skylight band wakati wa mkesha wa kuamkia sikukuu ya Eid
 Mmoja wa viongozi wa Bendi ya Skylight Joshua Ndege (katikati) akionyesha umahiri wake sambamba na waimbaji wa bendi hiyo.
INAWEZEKANA KUPIGA VITA UMASKINI KWA USHIRIKIANO-UN

INAWEZEKANA KUPIGA VITA UMASKINI KWA USHIRIKIANO-UN

September 27, 2015
IMG_2370
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez akizungumza wakati akizindua Malengo Endelevu 17 ya Maendeleo nchini (SDG’s) Tanzania katika shule ya Uhuru mchanganyiko, katika hafla ambayo pia benki ya Standard Chartered Tanzania ilishiriki na kugawa vitu mbalimbali kwa ajili ya wanafunzi wa shule hiyo. (Picha na Zainul Mzige wa Modewjiblog)
Na Mwandishi wetu
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez, amesema uondoaji umaskini nchini unawezekana kwa ushirikiano kati ya wadau mbalimbali wa maendeleo.
Kauli hiyo ameitoa mwishoni mwa wiki wakati akizindua Malengo Endelevu 17 ya Maendeleo nchini (SDG’s) Tanzania katika shule ya Uhuru mchanganyiko, katika hafla ambayo pia benki ya Standard Chartered ilishiriki na kugawa vitu mbalimbali kwa ajili ya wanafunzi wa shule hiyo.
Katika hafla hiyo ambayo ilitengenezwa mahususi kuanzisha utekelezaji wa Malengo Endelevu (SDG’s) yakiwemo ya elimu, afya na mazingira Standard walipeleka miti 150 ya kupanda, kompyuta na pia kutumia muda kuangalia afya za wanafunzi.
Alisema katika kukabiliana na umaskini kwa kuangalia Maendeleo Endelevu hakuna kitu kigumu ukilinganisha na ugumu wa mwanafunzi asiyeona kujifunza kwa kupitia vitabu vya nukta nundu na asiyesikia kuwasiliana na mtu mwingine lakini pamoja na ugumu huo watoto hao wanaweza.
Alisema kwa ushirikiano wa wadau kama walivyofanya wao na benki ya Standard Chartered Tanzania anaamini kwamba maendeleo yatafikiwa na Tanzania itafanikiwa kuzika umaskini ifikapo mwaka 2030.
Alisema kutiwa saini kwa Malengo Endelevu na viongozi wa nchi 190 kumeonesha wazi nia ya seriakli mbalimbali duniani kushughulikia umaskini na kuuzika kwa kutekeleza malengo hayo endelevu.
IMG_2313
Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Benki ya Standard Chartered Tanzania, Charles Katongole akitoa salamu za Mkurugenzi wake ambapo benki hiyo imeahidi kushiriki kikamilifu katika kuhakikisha utekelezaji wa malengo mapya ya Maendeleo Endelevu (SDG's) yanafanikiwa nchini Tanzania. Kushoto ni Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez, Mtaalam wa Mahusiano na Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) Tanzania Hoyce Temu (kulia) pamoja na Mkuu wa Mahusiano wa benki ya Standard Chartered Tanzania, Juanita Mramba (wa pili kulia).
Naye Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Benki ya Standard Chartered Tanzania, Charles Katongole, alisema kwamba ni lengo la benki hiyo ni kurejesha faida kwa jamii kupitia miradi yake mbalimbali na kwamba kusaidia shule hiyo ya Uhuru mchanganyiko iliyoanzishwa 01-01-1921 awali ikiitwa Government African secondary school kabla ya kuhamishiwa Mzumbe Morogoro 01-01-1953 na kubadilishwa jina kuwa Kichwele African boys middle school ikiwa na madarasa ya V-VII, ni sehemu ya kurejesha faida kwa jamii.
Alisema ni lengo la benki hiyo kwa mwaka huu kuwezesha kupatikana kwa dola za Marekani milioni 5 kusaidia mambo mbalimbali ya watoto kwa mwaka huu kwa nchi za Afrika mashariki huku Tanzania pekee watoto milioni 10 wakifikiwa.
Benki hiyo yenye matawi Dar es salaam, Mwanza na Arusha katika miradi yake ya afya, vijana na elimu wamekusudia kushirikiana na Umoja wa Mataifa kutekeleza malengo mbalimbali endelevu ikiamini kwamba jamii ikiboreshwa itakuwa katika mfumo mzuri wa maendeleo na kupiga vita umaskini.
Malengo ya SDG’s yamepangwa kutekelezwa katika kipindi cha miaka 15.
IMG_2324
Mwalimu Mkuu wa Shule ya msingi Uhuru mchangayiko, Anna Mshana akitoa risala fupi ya shule yake sambamba na changamoto zinazoikabili shule yake kwa ugeni huo kutoka Umoja wa Mataifa na Benki ya Standard Chartered Tanzania.
Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Anna Mshana alisema shule hiyo ambayo ilianzisha kitengo cha wanafunzi wasioona 1962 na kubadilishwa kuwa Shule ya msingi Uhuru mchanganyiko mwaka 1964, inakabiliwa na changamoto mbalimbali.
Miongoni mwa matatizo ni miundombinu ya shule hiyo isiyokidhi mahitaji halisi, ukosefu wa ukuta, mashine za kufundishia watoto wasioona, upungufu wa mabweni, magodoro, vitanda na gari la kuwakimbiza hospitalini inapotokea dharura.
Alisema ingawa kuna taasisi hutoa msaada wa gari na matibabu kwa watoto mchana, lakini nyakati za usiku kukitokea dhararu inabidi shule igharamie ingawaje wakati mwingine hatuna fedha inakuwa ni changamoto kwetu.
Alisema Shule ya msingi Uhuru mchanganyiko yenye kutoa elimu jumuishi ina vitengo vya ufundi seremala (1975) wanafunzi wenye mahitaji maalumu ulemavu wa akili (1984) na viziwi na wasioona (Deafblidn) kilichoanzishwa mwaka 1994.
IMG_2346
Wanafunzi ambao ni viziwi nao walipata fursa ya kuja kila kinachoendelea kutoka kwa mkalimani wao.
IMG_2470
Mkuu wa Mahusiano wa benki ya Standard Chartered Tanzania, Juanita Mramba akitangaza wanafunzi 17 ambao walishiriki shindano la kuhifadhi malengo mapya ya Maendeleo Endelevu (SDG's) wakati wa kukabidhi zawadi kwa wanafunzi hao wa shule ya Uhuru mchanganyiko.
IMG_2480
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez akikabidhi zawadi zilizotolewa na Benki ya Standard Chartered Tanzania kwa wanafunzi hao, sambamba na Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Benki ya Standard Chartered Tanzania, Charles Katongole.
IMG_2428
Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Benki ya Standard Chartered Tanzania, Charles Katongole akimkabidhi Mwalimu Mkuu wa Shule ya msingi Uhuru Mchanganyiko, Anna Mshana (wa pili kushoto) moja kati ya kompyuta tano zilizolotolewa na Benki hiyo ikiwa ni kama ishara ya utekelezaji wa lengo namba nne “Quality Education” wakati wa uzinduzi wa Malengo mapya ya Maendeleo Endelevu (SDG’s) uliofanywa na Benki ya Standard Chartered Tanzania kwa kushirikiana na Umoja wa Mataifa katika shule ya msingi Uhuru mchanganyiko jijini Dar mwishoni mwa wiki. Kulia ni Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez na kushoto ni Mjumbe wa Bodi ya Shule ya msingi Uhuru Mchanganyiko, Bw. Abubakar Mwambungu wakishuhudia tukio hilo.
IMG_2407
Kompyuta tano zilizotolewa na Benki ya Standard Chartered Tanzania kwa shule ya Uhuru mchanganyiko.
IMG_2448
Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Benki ya Standard Chartered Tanzania, Charles Katongole (wa tatu kushoto), Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez (katikati), Mwalimu Mkuu wa Shule ya msingi Uhuru Mchangayiko, Anna Mshana (wa pili kushoto), Mjumbe wa bodi ya kamati ya Shule ya msingi Uhuru Mchanganyiko, Abubakari Mwambungu (kushoto) pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Benki ya Standard Chartered Tanzania katika picha ya pamoja huku wakiwa wameshikilia miche ya miti mbalimbali ikiwemo ya matunda ambapo zaidi ya miche 150 ya miti ilipandwa kuzunguka mazingira ya shule hiyo kulinda mazingira ikiwa ni ishara kwa vitendo ya utekelezaji wa lengo namba 13 "Climate Action" kati ya Malengo 17 mapya ya Maendeleo Endelevu (SDG’s) nchini Tanzania.
IMG_2338
Pichani juu na chini baadhi ya wanafunzi na walimu wa shule ya msingi Uhuru mchanganyiko waliohudhuria uzinduzi huo.
IMG_2393
IMG_2541
Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Benki ya Standard Chartered Tanzania, Charles Katongole sambamba na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez wakishiriki zoezi la upandaji miti kuzunguka maeneo ya shule ya Uhuru mchanganyiko jijini Dar mwishoni mwa wiki.
IMG_2563
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez akishiriki zoezi la upandaji miti sambamba na baadhi ya wanafunzi wa shule Uhuru mchanganyiko.
IMG_1924
Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Uhuru Mchangayiko, Anna Mshana akitoa maelezo kwa Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez (aliyeinama) na Mkuu wa Mahusiano wa benki ya Standard Chartered Tanzania, Juanita Mramba (kulia) walipotembelea darasa la awali la watoto wenye ulemavu wa macho (upofu) katika shule hiyo. Nyuma ya Mwalimu Mkuu ni Mjumbe wa Kamati ya Shule ya Msingi Uhuru Mchangayiko, Abubakar Mwambungu.
IMG_1942
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez akicheza na mtoto Fatuma Haji wa darasa la awali katika shule hiyo ambaye ni mlemavu wa macho alipotembelea darasa hilo kabla ya kuzindua wa Malengo mapya ya Maendeleo Endelevu (SDG’s) hafla iliyoandaliwa na Benki ya Standard Chartered Tanzania kwa kushirikiana na Umoja wa Mataifa katika shule ya msingi Uhuru Mchanganyiko jijini Dar mwishoni mwa wiki.
IMG_2032
Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Benki ya Standard Chartered Tanzania, Charles Katongole, Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez, Mkuu wa Mahusiano wa benki ya Standard Chartered Tanzania, Juanita Mramba pamoja na ujumbe wao katika nyuso za masikitiko walipotembelea darasa la watoto wenye ulamavu wa macho (vipofu) na matatizo ya kutosikia (viziwi) katika shule ya msingi Uhuru mchanganyiko.
IMG_2075
Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Benki ya Standard Chartered Tanzania, Charles Katongole, Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez, Mkuu wa Mahusiano wa benki ya Standard Chartered Tanzania, Juanita Mramba na ujumbe wao katika picha ya pamoja na wanafunzi ambao ni walemavu wa macho ambao pia ni viziwi katika shule ya msingi Uhuru mchanganyiko.
IMG_1995
Walimu wa darasa la watoto wenye ulemavu wa macho ambao ni viziwi wakicheza ngoma na wanafunzi wao.
IMG_2082
Maana ya ulemavu wa macho na kuwa kiziwi.
IMG_1844
Mkutubi wa maktaba ya shule ya Uhuru mchanganyiko, Masanja akitoa maelezo ya namna mashine za kukuzia maandishi kwa wale wanafunzi wenye uono hafifu katika shule hiyo kwa Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Benki ya Standard Chartered Tanzania, Charles Katongole (kushoto) na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez walipotembelea maktaba hiyo.
IMG_1833
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez akipitia Katiba maalum kwa watu wenye ulemavu wa macho iliyopo kwenye maktaba ya shule hiyo. Kushoto kwake ni Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Benki ya Standard Chartered Tanzania, Charles Katongole.
IMG_2119
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez na Ujumbe wa Benki ya Standard Chartered Tanzania ulioongozwa na Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Benki ya Standard Chartered Tanzania, Charles Katongole wakitembelea mambweni ya wanafunzi katika shule ya msingi Uhuru Mchanganyiko.
IMG_2696
Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Benki ya Standard Chartered Tanzania, Charles Katongole, Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Benki ya Standard Chartered Tanzania katika picha ya pamoja na baadhi ya wanafunzi wa shule ya Msingi Uhuru Mchanganyiko.
IMG_2723
Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Benki ya Standard Chartered Tanzania, Charles Katongole (kulia) na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez katika picha ya pamoja na wanafunzi wa shule ya msingi Uhuru mchanganyiko Issa Abasi Wenge w darasa la pili (wa pili kushoto) mlemavu wa ngozi na Fatuma Haji (wa pili kulia) wa shule ya awali mwenye ulemavu wa macho.
IMG_2742
Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Benki ya Standard Chartered Tanzania, Charles Katongole (kulia) na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez na Mwanafunzi Mariana Alex (Mariana the voice of the SDGs in TZ) wa darasa la tano katika shule ya msingi Uhuru mchanganyiko jijini Dar. about the
IMG_2672
Mtaalam wa Mahusiano na Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) Tanzania Hoyce Temu akiserebuka na baadhi ya wanafunzi wa shule ya Uhuru mchangayiko.
IMG_2264
Bango lililoorodhesha Malengo 17 mapya ya Maendeleo Endelevu (SDG’s).
IMG_2874
Siku ilimazika kwa mechi ya kirafiki baina ya Shule ya msingi Uhuru mchanganyiko na wafanyakazi wa Benki ya Standard Chartered Tanzania katika viwanja vya shule ya sekondari Benjamin Mkapa ambayo ilizinduliwa na Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Benki ya Standard Chartered Tanzania, Charles Katongole (kulia) na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez.
DStv YAJA NA CHANELI YA MAISHA MAGIC BONGO, KWA AJILI YA WATANZANIA

DStv YAJA NA CHANELI YA MAISHA MAGIC BONGO, KWA AJILI YA WATANZANIA

September 27, 2015
D3A_5097
Mkurugenzi M-Net Kanda ya Afrika Magharibi, Wangi Mba-Uzoukwu akifafanua jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) kutoka nchi za Afrika waliokusanyika kwenye jukwaa kubwa la kuonesha vitu mbalimbali vinavyoburudisha katika chaneli za DStv na GoTv kupitia MultiChoice hivi karibuni nchini Mauritius.
D3A_5116
Mkurugenzi wa M-Net kwa nchi za Afrika Mashariki na SADC, Theo Erasmus akifurahi jambo kwenye mkutano na waandishi wa habari (hawapo pichani) kutoka nchi mbalimbali za Afrika.
Na Modewjiblog, Mauritius
Moja ya makampuni yanayoongoza katika utoaji wa vipindi vya burudani barani Afrika M-Net imesema kwamba itazindua chaneli maalumu kwa ajiri ya wakazi wa Tanzania itakayojulikana kama maisha Magic Bongo.
MAISHA MAGIC BONGO itaruka hewani kupitia chaneli 160 ya DStv kuanzia Alhamisi ya Oktoba Mosi mwaka huu na itapatikana katika vifurushi vyote vya Access, Family, Compact, Compact Plus na Premium.
Imeelezwa kuwa ingawa mambo yametengenezwa mahsusi kwa ajili ya Watanzania mataifa jirani yaAfrika Mashariki ikiwamo Kenya, Uganda, Ethiopia na DRC wanaweza kuona.
Uamuzi huo wa M-Net umefanyika wakati mchakato unaendelea wa kuboresha zaidi ulaji kwa wateja wake.
Hata hivyo wamesema kwamba MAISHA MAGIC EAST ambayo kwa sasa inaruka kupitia chaneli 158 itajiimarisha zaidi katika soko la Kenya huku ikiendelea na mara moja kwa wiki kwa ajili ya soko la Uganda ndani ya Luganda.
D8A_1979
Pichani ni waandishi wa habari kutoka nchi mbalimbali za Afrika waliokusanyika kwenye jukwaa hilo lililoandaliwa na MultiChoice Africa hivi karibuni.
MAISHA MAGIC BONGO imelenga kuhudumia soko la Tanzania likionesha vipindi vya Kiswahili kwa ajili ya kutimiza pia lengo la taasisi la kuhudumia soko kwa kuangalia makundi.
Mkurugenzi wa M-Net kwa nchi za Afrika Mashariki na SADC, Theo Erasmus amesema ingawa kwa miaka mingi wamekuwa wakitoa vipindi vyenye lugha mchanganyiko kwa sasa wamepania kutoa vipindi kwa lugha ya eneo kutokana na soko kuruhusu.
“Tumefanya mabadiliko kwa nchi za Afrika Mashariki kwa siku za karibuni. Kasi ya mabadiliko hayo yanaonesha kujali kwetu. Na tutaangalia mafanikio katika MAISHA MAGIC BONGO, kuona uwezekano wa kuendelea kutengeneza chaneli zinazokidhi mahitaji Fulani.” Amesema Erasmus.
Chaneli mpya itakuwa na matangazo ya saa sita ambayo yatarejewa mara tatu kwa siku na inatarajiwa saa za vipindi kuongezeka zaidi.
Katika chaneli hiyo kutakuwa na kipindi cha saa moja cha muziki Mzooka, ambayo itakuwa mwishoni mwa wiki majira ya jioni na itakuwa kipindi cha miziki ya karibuni kutoka Tanzania. Kitakuwa ni kipindi cha wapenzi wa hip hop na Bongo.
D3B_8767
Mkurugenzi M-Net Kanda ya Afrika Magharibi, Wangi Mba-Uzoukwu (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na Movie Stars wa nchini Nigeria, Rita Dominic na Desmond Elliot mara baada ya mkutano na waandishi wa habari.
Pia kutakuwa na michezo ya kuigiza ambayo ni tamthilia Talaaka itakayokuwa ikizungumzia masuala ya ndoa na talaka na kupeleka ujumbe kwanini kunakuwa na talaka. Pia kutakuwa na kipindi cha mapishi cha Jikoni na Marion. Kwenye kipindi hiki tutawaona masupastaa wa Tanzania wakipika chakula huku wakizungumzia mambo yao.
MAISHA MAGIC BONGO kutakuwa na sinema za Kiswahili kama Nusra iliyochezwa na Ashura Iddy, Ammar Ruweth, Riyama Ally na Zuberi Mohammed. Pia kutakuwa na sinema ya Hard Price iliyochezwa na akina Sabrina Tamim na Jacqueline Wolper .
Ikiwa imebaki mwezi mzima kabla ya MAISHA MAGIC BONGO kuingia katika runinga za watanzania kwa sasa angalia kipindi gani kipo hewani ukipendacho kupitia www.dstv.com.
D3A_5080
Mkuu wa chaneli ya Maisha Magic, Margaret Mathore akisisitiza jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani).

WANAKIMANUMANU WAKINUKISHA MKWAKWANI WAIPIGA BAO 1-0 NDANDA SC

September 27, 2015


 Kikosi Cha Ndanda FC kilichobugizwa bao 1 na Arfican Sports wana Kimanumanu leo Uwanja wa Mkwakwani Tanga
 Tangakumekuchablog
Timu ya African Sports ya Tanga, imewaondoa aibu wakazi wa Tanga na washabiki wake baada ya kuibamiza bao moja timu ya Ndanda FC ya Mtwara.
Timu hiyo ambayo imeonyesha kandanda safi la ufundi wa hali ya juu tofauti na timu nyengine za Tanga ambazo zimekuwa hazionyeshi ushindani na badala yake zimekuwa zikipokea vipigo mfululizo.
Kuanzia dakika ya kwanza ya mchezo hadi kipenga cha mwisho African Sports walionyesha kandanda safi na kuwakonga washabiki wake wakiwemo wakazi wa Tanga ambao kipindi cha pili cha mchezo walifanikiwa kutingisha nyavu kwa bao la ufundi.
Baadhi ya washabiki waliofika kuishangilia timu hiyo walizungumza na tangakumekuchablog na kudai kuwa huo ni mwanzo wa safari ya ushindi na kusema kuwa wanatoa salamu kwa timu nyengine ambazo zitakutana nazo.
Walisema katika safari hiyo kwao kila timu inayokutana nayo wataichukulia   sawa na fainal hivyo kuwataka washabiki na wapenzi wa timu hiyo kuishangilia kwa nguvu zote ili kuweza kupata ushindi mfululizo.