Rais
Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akifanya mazoezi leo katika viwanja vya Ikulu
kufuatia ushauri wa madaktari waliomtaka afanye hivyo mara tatu kwa
siku ili kuendelea kuimarisha afya yake baada ya kufanyiwa upasuaji
mwezi uliopita katika hospitali ya Johns Hopkins nchini Marekani.(Picha
na Freddy Maro)
TAIFA STARS MABORESHO YAREJEA DAR
Kikosi cha Taifa Stars Maboresho kinarejea leo Dar es Salaam
kutoka Bulyanhulu mkoani Shinyanga ambapo kiliweka kambi kwa ajili ya mechi ya
kimataifa dhidi ya Burundi itakayochezwa Desemba 9 mwaka huu.
Timu hiyo ambayo leo asubuhi imefanya mazoezi kwenye Uwanja wa CCM
Kirumba jijini Mwanza, itatua Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere
(JNIA) kwa ndege ya Fastjet saa 12.30 jioni na kwenda moja kwa moja kambini
hoteli ya Tansoma.
Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager kesho (Desemba 7
mwaka huu) itafanya mazoezi asubuhi na jioni kwenye viwanja vya Gymkhana wakati
keshokutwa (Desemba 8 mwaka huu) itafanya mazoezi jioni kwenye Uwanja wa Taifa.
Nayo timu ya Taifa ya Burundi inatua nchini keshokutwa (Desemba 8
mwaka huu) saa 10 jioni kwa ndege ya Kenya Airways. Kikosi hicho kitafikia
hoteli ya Tiffany Diamond kitakwenda moja kwa moja Uwanja wa Taifa, Dar es
Salaam ambapo kitafanya mazoezi kuanzia saa 11 jioni.
Kiingilio cha mechi kati ya Tanzania na Burundi itakayochezwa
Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 10 jioni kitakuwa sh. 3,000 kwa viti
vya raungi ya chungwa, bluu na kijani wakati VIP B na C ni sh. 5,000 tu.
IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)
WEMA SEPETU, DIAMOND WATARUDIANA NA KUFUNGA NDOA!
!
Mtabiri maarufu Bongo, Maalim Hassan Yahya ambaye ni mrithi wa kazi za
marehemu Shehe Yahya amesema kuwa, penzi la mastaa wa Kibongo,Wema
Sepetu na Nasibu Abdul ‘Diamond’ bado halijafika mwisho, watarudiana na
kufunga ndoa. Mbongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’.
Akizungumzia penzi la wawili hao ambao siku chache zilizopita
wameripotiwa kumwagana alisema, hali hiyo ni ya mpito tu haimaanishi
kuwa hiyo ndiyo tamati ya mapenzi yao, sababu nyota zao zinategemeana
japo ya Wema ina nguvu kubwa kuibeba ya Diamond.Staa
wa Bongo Movies, Wema Sepetu. “Msifikiri kwamba penzi lao ndiyo
limefika mwisho, hakuna kitu kama hicho ni mara ngapi wameachana na
kurudiana hata hili la sasa natabiri watarudiana,” alisema Malim.
MBOWE:TUTAZUIA UCHAGUZI WA MITAA MAHAKAMANI IKIWA................
Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amesema kama hali ya kuwaengua wagombea wa chama hicho katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa itaendelea kama ilivyo sasa, basi wataupinga uchaguzi huo mahakamani.
Mbowe alisema hayo jana katika mkutano wa hadhara wa operesheni mshikemshike mzizima uliofanyika Vijibweni Kigamboni.
“Tangu kampeni zianze kumekuwa na tabia ya kuengua wagombea wetu kiholela. Tumeshaweka angalizo mahakamani na kama hali ikiendelea hivyo tutaupinga uchaguzi mahakamani.”
Alisema baada ya kuibuka kwa tabia ya wagombea kuenguliwa aliwasiliana na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akimsihi alitizame kwa kina suala hilo kwa sababu wagombea walienguliwa kimakosa.
“Alisema atalifanyia kazi lakini naona bado hali hiyo inaendelea na alisema atazungumza na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana kuhusu jambo hili.
Nilipowasiliana naye mara ya pili alisema kama tunataka ushindi uchaguzi uwe wa haki. Kuona hivyo tumekwenda kutoa angalizo mahakamani,” alisema.
Aliongeza, “Tukutane katika uchaguzi na tuone nani ni bingwa kati ya CCM na Ukawa baada ya kutumia njia za mkato kama wao wanavyofanya.
Hata sisi hatutaki ushindi wa dezo ila wakitumia dola kutuyumbisha kamwe hatutokubali maana polisi wamekuwa wakitumika kama mawakala wa uchaguzi. Hilo halitakubalika.”
Aliwataka wananchi kutokaa mbali na vituo vya kupigia kura mara baada ya kuwachagua viongozi wanaowataka huku akisisitiza, “Msikubali kura zikahesabiwe sehemu nyingine watazichakachua.
Hata katika sheria za Uchaguzi hakuna sehemu inayosema baada ya kupiga kura, mpigakura anatakiwa kukaa umbali wa mita 100 kutoka katika kituo cha kupiga kura. Tumeweka mawakala nchi nzima kuhakikisha kila kitu kinakuwa sawa.”
Alisema hakuna dhambi mbaya kama wananchi kushindwa kuleta mapinduzi ndani ya nchi yao, hasa nchi kama Tanzania ambayo ina kila aina ya umasikini.
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amesema kama hali ya kuwaengua wagombea wa chama hicho katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa itaendelea kama ilivyo sasa, basi wataupinga uchaguzi huo mahakamani.
Mbowe alisema hayo jana katika mkutano wa hadhara wa operesheni mshikemshike mzizima uliofanyika Vijibweni Kigamboni.
“Tangu kampeni zianze kumekuwa na tabia ya kuengua wagombea wetu kiholela. Tumeshaweka angalizo mahakamani na kama hali ikiendelea hivyo tutaupinga uchaguzi mahakamani.”
Alisema baada ya kuibuka kwa tabia ya wagombea kuenguliwa aliwasiliana na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akimsihi alitizame kwa kina suala hilo kwa sababu wagombea walienguliwa kimakosa.
“Alisema atalifanyia kazi lakini naona bado hali hiyo inaendelea na alisema atazungumza na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana kuhusu jambo hili.
Nilipowasiliana naye mara ya pili alisema kama tunataka ushindi uchaguzi uwe wa haki. Kuona hivyo tumekwenda kutoa angalizo mahakamani,” alisema.
Aliongeza, “Tukutane katika uchaguzi na tuone nani ni bingwa kati ya CCM na Ukawa baada ya kutumia njia za mkato kama wao wanavyofanya.
Hata sisi hatutaki ushindi wa dezo ila wakitumia dola kutuyumbisha kamwe hatutokubali maana polisi wamekuwa wakitumika kama mawakala wa uchaguzi. Hilo halitakubalika.”
Aliwataka wananchi kutokaa mbali na vituo vya kupigia kura mara baada ya kuwachagua viongozi wanaowataka huku akisisitiza, “Msikubali kura zikahesabiwe sehemu nyingine watazichakachua.
Hata katika sheria za Uchaguzi hakuna sehemu inayosema baada ya kupiga kura, mpigakura anatakiwa kukaa umbali wa mita 100 kutoka katika kituo cha kupiga kura. Tumeweka mawakala nchi nzima kuhakikisha kila kitu kinakuwa sawa.”
Alisema hakuna dhambi mbaya kama wananchi kushindwa kuleta mapinduzi ndani ya nchi yao, hasa nchi kama Tanzania ambayo ina kila aina ya umasikini.
CHANZO:CHADEMA BLOG
WAGANDA WAMSHANGAA ZARI KUMGANDA DIAMOND
Mitandao
ya kijamii na vyombo vya habari vya Uganda vimemgeuka nyota wa vipindi
vya runinga na Mwanamuziki Zari ‘The Boss Lady’ kwa madai kwamba
amemganda mwanamuziki wa Tanzania Diamond Platnumz.
Mitandao
hiyo ilimshambulia Zari kwa kumwambia kuwa kavuruga uhusiano baina ya
Wema na mkali huyo wa video ya ‘Ntampata Wapi’, huku ikiponda picha
ambayo Zari aliiweka mitandaoni ikimwonyesha akiwa na Diamond.
Mitandao hiyo imeponda kuwa Zari ana tabia ya kuwanadi wanaume anaotoka nao.
Wiki tatu zilizopita Zari amekuwa bega kwa bega na mwanamuziki
Diamond, baada ya kutengeneza wimbo wa pamoja katika studio za Tuddy
Thomas. Zari alionekana akipiga picha kadhaa na nyota huyo kabla ya
kumsindikiza katika tuzo za CHOAMVA, Afrika Kusini na baadaye kurudi
naye nchini.
Diamond
ambaye alinyakua tuzo tatu za Channel O 2014, anatarajiwa kuwa mgeni
rasmi katika hafla inayoandaliwa na Zari, ijulikanayo kama ‘Zari All
White Ciroc Party’, itakayofanyika Desemba 18, mwaka huu.
NHIF Yanyakuwa Tuzo tatu za Ubunifu Hifadhi ya Jamii Barani Afrika
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Bima ya Taifa ya Afya Bw. Khamis Mdee akipokea tuzo tuzo tatu za ubunifu
katika sekta ya hifadhi ya Jamii Barani Afrika zinazosimamiwa na
Shirikisho la Mifuko ya Hifadhi ya Jamii Duniani (ISSA)
katika sekta ya hifadhi ya Jamii Barani Afrika zinazosimamiwa na
Shirikisho la Mifuko ya Hifadhi ya Jamii Duniani (ISSA)
Kaimu
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Bima ya Taifa ya Afya Bw. Khamis Mdee
katikati akionyesha tuzo hizo pamoja na washiriki we ngine wa mkutano
huo.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Bima ya Taifa ya Afya Bw. Khamis Mdee na washiriki wengine wakiwa katika mkutano huo.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Bima ya Taifa ya Afya Bw. Khamis Mdee akiwa na maofisa wengine wa mfuko huo wakiwa katika picha ya pamoja.
Kaimu
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Bima ya Taifa ya Afya Bw. Khamis Mdee na
washiriki wengine kutoka mataifa mbalimbali wakiwa katika mkutano huo.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Bima ya Taifa ya Afya Bw. Khamis Mdee akielezea jambo katika mkutano huo.
Mandhari ya jiji la Cassablanca Morocco
……………………………………………………………………………………………….
Mwandishi Maalum Casablanca, Morocco
Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, NHIF umenyakua tuzo tatu za ubunifu katika sekta ya hifadhi ya Jamii Barani Afrika zinazosimamiwa na Shirikisho la Mifuko ya Hifadhi ya Jamii Duniani (ISSA).
Halfa ya kukabidhi tuzo hizo ilifanyika Jijini Casablanca nchini
Morocco usiku wa tarehe 3 Desemba, 2014 katika hoteli ya Serana jijini Casablanca ambapo washiriki zaidi ya 360 kutoka taasisi 75 katika mataifa 45 ya Afrika zilihudhuria.
Tuzo ambazo NHIF ilikabidhiwa ni katika eneo la utoaji wa huduma zamatibabu za kibingwa maeneo magumu kufika, kazi ambayo mfuko umefanyakwa kushirikiana na wataalamu wa hospitali za rufaa nchini.
tuzonyingine ni katika eneo la TEHAMA katika utayarishaji madai na hudumaza matibabu kwa wanachama wastaafu.
Ujumbe wa Tanzania katika mkutano huo wa Kanda ya Afrika ambacho piakilijadili mambo muhimu kuhusu sekta ya hifahi ya jamii na kutambuakazi za ubunifu uliongozwa na Waziri wa kazi Mheshimiwa GaudensiaKabaka pamoja na Viongozi waandamizi wa Mamlaka ya Usimamizi naUdhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii nchini (SSRA) na baadhi ya
Watendaji wakuu wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii nchini.
Tangu kuanza kutolewa kwa ambazo hushindaniwa kila baada ya miakamitatu, NHIF imeng’ara mara zote.Mwaka 2008 ilipata tuzo ya cheti chaheshima cha ubunifu mjini Kigali kwa kuwashirikisha wadau wake katikautoaji wa elimu kwa makundi mbalimbali ngazi ya mkoa. Mwaka 2011ulikuwa mshindi wa kwanza wa jumla barani Afrika na mwaka huu umeibuka tena na ushindi huo muhimu unaoitangaza Tanzania kimataifa kupitia Bima ya Afya.
Mbali ya NHIF, Tanzania pia imengara kwa kuzoa jumla ya tuzo 6 mbapoMamlaka ya Udhibiti ya SSRA, Mfuko wa Pensheni wa PPF na Mfuko wa PSPSpia ilijizolea tuzo moja moja kwa kila mmoja hivyo kufanya Tanzaniakuwa na jumla ya tuzo 6 na kuifanya kuwa kinara katika ukanda wa nchiza Afrika mashariki na ya Kati.
Mifuko ya Hifadhi ya Jamii katika nchi nne ilipata heshima ya pekeekwa kazi zao za ubunifu. Mifuko hiyo ni kutoka Cameroon yenyewe
iliyonyakua tuzo 8, Gabon, Maurtania, wenyeji Morocco.
Washindi wa jumla wa kwa mwaka 2014 ni wenyeji Morocco na Jirani zaowa Mauritania ambao kwa pamoja wamepata tuzo ya jumla kwa kutoa huduma bora, kuongeza uwigo wa wanaonufaika na huduma za mifuko hiyo hasa wasio na uwezo, matumizi ya TEHAMA na huduma kwa wateja na ufanisi kwa
ujumla.
MAONYESHO YA KIMATAIFA YA ELIMU KUANZA DISEMBA 17-21, 2014 JIJINI DAR
Mkurugenzi Mtendaji wa Global Education Link, Abdulimalik Mollel, akisisitiza jambo kwa wanahabari (hawapo pichani)
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.
Kampuni ya Global Education Link
(GEL) kwa kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Wizara ya
Elimu na Ufundi pamoja na Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania
(Tantrade) wameandaa maonyesho ya kwanza ya kimataifa ya elimu (TIEE)
yanayotarajiwa kufanyika Disemba 17 hadi 21 mwaka huu katika viwanja
vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
Akizungumza jijini Dar es
Salaam, Mkurugenzi Mkuu wa Global link Education, Abdulmalik Mollel,
alisema lengo la maonyesho hayo ni kutambulisha wadau wa elimu kwa
pamoja ili kuweza kutoa huduma ya pamoja kwa wananchi na kuwaelimisha
juu ya mambo muhimu yaliyopo katika kila sekta.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (Tan Tred), Jacqueline Mneney, akizungumza jambo.
Alisema ushiriki wa asasi
mbalimbali kwa kushirikiana na sekta binafsi utakuwa na chachu ya
mabadiliko ya elimu kwa kupitia mpango wa matokeo makubwa sasa.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya
Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade), Jacqueline Mneney, alisema
wakati umefika kwa Watanzania kujua umuhimu wa maonyesho ya Elimu maana
yamekuja kutatua matatizo mbali mbali waliyokuwa wakiyapata wazazi pindi
wanapokuwa wanawatafutia shule na vyuo watoto wao.
Aidha alisema maonyesho hayo
yataleta manufaa makubwa na changamoto chanya hasa katika kuongeza
ushindani katika sekta ya elimu ambayo itasaidia mpango wa matokeo
makubwa sasa.
Maonesho hayo yanatarajiwa kupata washiriki zaidi ya 500 na wananchi mbalimbali zaidi ya 350,000 kutoka ndani na nje ya nchi.
Kauli mbiu ya maonesho hayo ni ‘KUWEKA JITIHADA ZA PAMOJA KATIKA KUBORESHA MFUMO WA ELIMU TANZANIA NI NJIA THABITI YA KULETA MAENDELEO ENDELEVU KATIKA TAIFA.’
MAMA SALMA KIKWETE AFANYA KAMPENI KATIKA KATA ZA MTANDI NA MWENGE HUKO LINDI MJINI
Mke wa Rais na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi, CCM,
anayewakilisha Lindi Mjini, Mama Salma Kikwete akisalimiana na viongozi
wa Kata ya Mtandi iliyoko Lindi Mjini wakati alipotembelea Kata hiyo kwa
ajili ya kufanya mkutano wa kampeni katika uchaguzi wa viongozi wa
serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika nchini kote tarehe 14.12.2014.
Mjumbe
wa Halmashauri Kuu ya CCM anayewakilisha Lindi mjini na Mke wa Rais
Mama Salma Kikwete akionyesha ishara ya vidole viwili kuashiria kuunga
mkono pendekezo la muundo wa serikali mbili nchini wakati alipozungumza
na viongozi wa Chama Cha Mapinduzi wa Kata ya Mtandi tarehe 5.12.2014.
Mjumbe
wa Halmashauri Kuu ya CCM anayewakilisha wilaya ya Lindi Mjini na Mke
wa Rais Mama Salma Kikwete akiwahutubia viongozi wa Chama Cha Mapinduzi
wa Kata ya Mtandi katika mkutano uliofanyika katika Mtaa wa Maisara kwa
ajili ya uchaguzi wa viongozi wa serikali za mitaa nchini unaotarajiwa
kufanyika tarehe 14.12.2014.
Mjumbe
wa Halmashauri Kuu ya CCM anayewakilisha wilaya ya Lindi Mjini na Mke
wa Rais Mama Salma Kikwete akiwahutubia viongozi wa Chama Cha Mapinduzi
wa Kata ya Mtandi katika mkutano uliofanyika katika Mtaa wa Maisara kwa
ajili ya uchaguzi wa viongozi wa serikali za mitaa nchini unaotarajiwa
kufanyika tarehe 14.12.2014.
Mama Salma Kikwete, Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi
anayewakilisha Lindi Mjini akishiriki kucheza na baadaye kuwahutubia
wananchi wa Kata ya Mwenge huko Lindi Mjini wakati akishiriki kuwapigia
kampeni za uchaguzi wa viongozi wa serikali za mitaa unaotarajiwa
kufanyika nchini kote tarehe 14.12.2014.
Baada
ya kuhutubia mkutano wa kampeni kwenye Kata ya Mwenge huko Lindi Mjini
Mama Salma Kikwete anaonekana akimbeba mtoto Juma Selemani ambaye naye
alikuwa miongoni mwa watu waliohudhuria mkutano wa kampeni.
…………………………………………………..
Na Anna Nkinda – Lindi
Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi
(CCM) wilaya ya Lindi mjini wametakiwa kutokubali kurubuniwa kwa kitu
chochote kile ili wawapigie kura wagombea wa vyama vya upinzani bali
waungane kwa pamoja katika kampeni na kuhakikisha chama hicho kinapata
ushindi wa kishindo.
Mwito huo umetolewa jana na
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM kupitia wilaya ya Lindi
mjini Mama Salma Kikwete wakati akiwanadi kwa wananchi wagombea wa
chama hicho wanaowania nafasi za uongozi kwenye uchaguzi wa Wenyeviti na
Wajumbe wa Serikali za Mitaa katika Kata ya Mwenge.
Mama Kikwete ambaye ni Mke wa Rais
Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete alisema lengo la chama chochote cha Siasa ni
kushika Dola kuanzia ngazi ya mtaa hadi Taifa hivyo basi wanachama
hao wasikubali kurubuniwa bali waendelee kukitetea na kukipigania Chama
chao ili kipate ushindi katika mitaa yote 117 ya Kata hiyo.
“Viongozi wanaogombea tena
wamechaguliwa kutokana na kazi yao nzuri. Nanyi ambao kura zeu
hazikutosha wakati wa mchakato wa kuchagua msilaumu, bali muwapiganie
wagombea wote na kuhakikisha wanashinda angalieni maslahi ya chama
kwanza mambo binafsi baadaye”, alisema Mama Kikwete.
Aidha Mama Kikwete aliwaomba
wananchi wa wilaya hiyo kutumia maarifa na ujuzi waliopewa na Mwenyezi
Mungu wa kutambua mema na mabaya na kutokubali kudanganywa na kundi la
watu wachache ili waipoteze amani yao.
Mama Kikwete alisema, “Wenzenu
wamepiga hatua kubwa za maendeleo katika mikoa yao huku Lindi Mwenyezi
Mungu katupa neema maendeleo yanakuja sasa. Wanakuja huku kuwadanganya
ili mfanye vurugu na kurudisha maendeleo yenu nyumba, msifuate mkumbo na
kuchezea amani kwani vurugu zinarudisha nyuma maendeleo”.
Aliwasihi wananchi waliohudhuria
mkutano huo kuhakikisha watoto wao wanaenda shule ili wapate viongozi
wazuri wa baadaye ambao watawaletea maendeleo kwani bila ya kuwa na
elimu ni vigumu kupata maendeleo.
MNEC huyo pia aliwashukuru wanaume
waliowaruhusu wake zao kugombea nafasi mbalimbali za uongozi na
kuwapongeza wanawake kwa kutokukubali kubaki nyuma na kuomba kugombea
nafasi hizo.
Mama Kikwete yupo wilayani humo
kwa ajili ya shughuli za kichama ikiwa ni pamoja na kushiriki kwenye
kampeni na kuwanadi wagombea wa chama hicho wanaowania nafasi mbalimbali
za uongozi katika uchaguzi wa viongozi wa Serikali za Mitaa, Vijiji na
Vitongoji utakaofanyika tarehe 14 mwezi huu.
MICHUANO YA WANAWAKE TAIFA CUP KUANZA DESEMBA 28
Michuano ya Taifa ya mpira wa
miguu kwa wanawake ya Proin Women Taifa Cup inaanza rasmi Desemba 28
mwaka huu kwa mechi ya ufunguzi kati ya timu za mikoa ya Mara na Mwanza
itakayochezwa Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.
Kombaini za mpira wa miguu za
mikoa yote ya Tanzania Bara zitashiriki mashindano hayo yatakayochezwa
kwa raundi mbili mwanzoni, na baadaye hatua ya robo fainali hadi
fainali.
Mashindano hayo yanayodhaminiwa na
kampuni ya Proin Promotions Limited, kuanzia hatua ya robo fainali,
mechi zote zitafanyika jijini Dar es Salaam.
Meneja Biashara wa Shirikisho la
Mpira wa Miguu Tanzania, Peter Simon Shankunkuli aliishukuru kampuni ya
Proin ambao ni watengenezaji, wazalishaji na wasambazaji wa filamu za
kitanzania kwa kuwezesha mashindano hayo kufanyika kwa mara ya kwanza
Proin Promotions imekua ikivumbua
vipaji mbalimbali vya uigizaji na sasa imeamua kujikita katika mpira wa
miguu ili kuweza kuvumbua vipaji kwa wachezaji wa kike.
Shankunkuli alisema nafasi bado
zipo kwa wadhamini watakaoguswa na mashindano hayo, kwa kuwasiliana na
TFF au Proin Promotions Limited kwa maelezo zaidi.
Waziri Mwakyembe awapongeza fastJet Kwa Huduma Nzuri kwa Wateja.
Ofisa
wa Mahusiano na Masoko wa kampuni ya ndege ya FastJet Lucy Mbogoro
akitoa maelezo kwa ujumbe kwa Waziri wa Uchukuzi Harrison Mwakyembe na
ujumbe wake wakati wa maadhimisho ya siku ya anga duniani kushoto kwake
ni Mwenyekiti wa Bunge ya Miundombinu, Peter Serukamba.
Wafanyakazi wa kampuni ya ndege ya Fast Jet wakiwa kwenye picha ya pamoja
Wafanyakazi
wa kampuni ya FastJet wakipita mbele ya mgeni rasmi ambae ni Waziri wa
Uchukuzi Mh.Harrison Mwakyembe wakati wa maadhimisho ya siku ya anga
duniani
Waziri
wa Uchukuzi Harrison Mwakyembe akizungumza na wafanyakzi wa kampuni ya
ndege ya FastJet wakati wa maadhimisho ya siku ya anga duniani ambapo
aliipongeza kampuni hiyo kwa kutoa huduma kwa bei rahisi kwa wasafiri
pembeni yake ni Mwenyekiti wa Bunge ya Miundombinu, Peter Serukamba.
Meneja
Biashara wa FastJet, Jean Uku akitoa maelekezo kwa Waziri wa Uchukuzi
HarrisonMwakyembe kuhusiana na utendaji kazi wa kampuni hiyo wakati wa
maadhimisho ya siku ya anga duniani pembeni ya Mwakyembe ni Mwenyekiti
wa Bunge ya Miundombinu, Peter Serukamba.
Waziri
wa Uchukuzi HarrisonMwakyembe akizungumza na wafanyakzi wa kampuni ya
ndege ya FastJet wakati wa maadhimisho ya siku ya anga duniani ambapo
aliipongeza kampuni hiyo kwa kutoa huduma kwa bei rahisi kwa wasafiri.
Serikali kuendelea kunufaisha Vijana katika kutengeneza ajira
Serikali imeahidi kuendelea kusaidia kuwajengea Vijana uwezo wa kujitambua na kufanya kazi kwa hari ikiwemo kujitolea.
Hayo yamebainishwa katika Hotuba
ya Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara
iliyosomwa kwa niaba yake na Kaimu Mkurugenzi wa Maendeleo ya Vijana
wakati wa hafla ya madhimisho ya Siku ya Kimataifa yakujitolea
iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Akihutubi baadhi ya Vijana
wanaofanya kazi za Kujitolea katika taasisi mbalimbali Kajugusi amesema
vijana wanapaswa kufanya kazi za kujitolea ili kujenga uwezo wa utendaji
kazi na kupata uzoefu utakaopelekea kuajirika kwa ulahisi.
“Jengeni tabia ya kujitolea kwa
kuwa kutawajenga na kuwapa fursa kubwa ya kupata ajira zenye staha
zitakazo kidhi matarajio yenu”
Aidha Mkurugenzi huyo alitoa rai kwa vijana kujunga tabia ya kujifunza na kutumia kwa manufaa yao na taifa kwa jumla wake
Kajugusi aliongeza kuwa Serikali
ipo mbioni kuboresha mkakati wa Taifa wa kushirikisha Vijana katika
shughuli za maendeleo hapa nchini ambapo vijana watapa fursa ya
kushiriki moja kwa moja katika kutekeleza mipango ya maendeleo ya nchi
yao.
Kwa upande wake Afisa Habari wa
Kituo cha Habari cha Umoja wa Matifa (UNIC) Bibi. Stella Vuzo amesema
kuwa kadri vijana wanavyofanya kazi za kujitolea ndipo wanapopata fursa
ya kujijengea uwezo utakapoelekea waajirike katika sjira zenye staha
Aliongeza kuwaidi ya vijana
asilimia 80 wanajitolea katika taasisi mbalimbali duniani kote, ambapo
kati yao asilimia 30 ujitolea ndani ya nchi zao hivyo kusaidia kuongeza
nguvu kazi katika shughuli za maendeleo.
Akisoma ujumbe mahususi wa Katibu
Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon kwa ajili ya maadhimisho hayo,
Bibi. Vuzo alisema kuwa Katibu Mkuu huyo anawashukuru zaidi ya watu
6,300 wanaofanya kazi kwa kujitolea katika Umoja wa Mataifa na na 11,000
wanaojitolea kupitia Mtandao kwa kuweza kuwasidia zaidi ya mamilioni ya
watu katika kufanya mabadiliko kwa kuwapa sauti katika maendeleo
endelevu na jitihada za utunzaji wa amani duniani kote’Alisema Stella
Vuzo.
Siku ya Kujitolea duniani
uadhimishwa kila mwaka tarehe 5 Desemba duniani kote ambapo kwa Tanzania
kitaifa maadhimisho haya yamefanyika jijini Dar es Salaam
Subscribe to:
Posts (Atom)