TIGO YAIBUA MAMILIONEA SABA ZAIDI KATIKA PROMOSHENI MURWA YA TIGO PESA

December 27, 2017
Mojawapo ya washindi 35 wa zawadi za kila siku za shilingi milioni moja na shilingi laki tano katika promosheni inayoendelea ya 'Tumia Tigo Pesa na Ushinde', Prochess Mroso (kulia) mkaazi wa Kimara Temboni jijini Dar es Salaam akielezea kuhusu ushindi wake katika mkutano na waandishi wa habari leo. Ameambatana na Meneja wa Wateja wa Tigo Pesa, Mary Rutta (kati) na mshindi mwengine Editha Malyamoto wa Kibamba(kushoto). Tigo pia inatoa zawadi kubwa za shilingi milioni 15, milioni 10 na milioni 5 kwa wateja wanaotumia Tigo Pesa. 

Mojawapo ya washindi 35 wa zawadi za kila siku za shilingi milioni moja na shilingi laki tano katika promosheni inayoendelea ya 'Tumia Tigo Pesa na Ushinde', Prochess Mroso (kulia) mkaazi wa Kimara Temboni jijini Dar es Salaam akielezea kuhusu ushindi wake katika mkutano na waandishi wa habari leo. Ameambatana na Meneja wa Wateja wa Tigo Pesa, Mary Rutta (kati) na  mshindi mwengine Editha Malyamoto wa Kibamba pamoja na Afisa Mawasiliano wa Tigo, Umi Mtiro (kushoto). Tigo pia inatoa zawadi kubwa za shilingi milioni 15, milioni 10 na milioni 5 kwa wateja wanaotumia Tigo pesa.  

Baadhi ya washindi 35 wa zawadi za kila siku za shilingi milioni moja na shilingi laki tano katika promosheni inayoendelea ya 'Tumia Tigo Pesa na Ushinde wakiwa na simu zao baada ya kupokea ujumbe wa simu uliothibitisha kupokea zawadi hizo  za pesa.Tigo inatoa zawadi ya shilingi milioni moja kila siku na zawadi nne za shilingi laki tano kila siku kwa wateja wanaotumia huduma ya Tigo Pesa, pamoja na zawadi kubwa za shilingi milioni 15, milioni 10 na milioni 5.

Mary Rutta, Meneja wa Wateja wa Tigo Pesa akizumgumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam katika hafla ya kukabidhi zawadi saba za shilingi milioni moja na zawadi 28 za shililingi laki tano kila mmoja kwa washindi wa wiki hii wa promosheni inayoendelea ya 'Tumia Tigo Pesa na Ushinde'. Kushoto ni Afisa Mawasiliano wa Tigo, Umi Mtiro.  




•             Wateja Wengine 28 Wajishindia Zawadi za TZS 500,000 Kila Mmoja. 
Dar es Salaam, 22 Desemba, 2017- Huduma ya kutuma na kupokea fedha inayoongoza nchini Tanzania, Tigo Pesa imewaibua jumla ya mamilionea saba (7) wapya  katika droo ya wiki hii ya promosheni yake inayoendelea ya ‘Tumia Tigo Pesa na Ushinde’. 
Washindi wengine 28 nao wamejinyakulia donge nono za kila siku za TZS 500,000 kila mmoja, na kufanya jumla ya wateja walipotakana hadi sasa kufikia 90. 
Akitangaza washindi wa wiki hii katika mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Meneja wa Wateja wa Tigo Pesa, Mary Rutta alisema kuwa pamoja na zawadi hizo za kila siku, wateja wa Tigo Pesa wana fursa kubwa ya kushinda zawadi kubwa za TZS 15 milioni, TZS 10 milioni na TZS 5 milioni ambapo washindi watajulikana usiku wa kuamkia mwaka mpya. 
Kufikia sasa tumetoa until now we have given out Tzs 69 Million to 90 winners and we expect  to give out Tzs 51Million more to remaining 63 winners
‘Kufikia sasa tumtoa jumla ya TZS 69 milioni kwa washindi 90 na bado tuna zawadi za TZS 51 milioni zitakazotolewa kwa washindi wengine 63, ikiwa pamoja na mamilionea wapya tutakaowapata usiku  wa kuamkia mwaka mpya wa 2018. Kushiriki katika promosheni hii ni rahisi na ni wazi kwa wateja wote wa Tigo Pesa. Kadri unavyotumia huduma ya Tigo Pesa ndivyo unavyojiongezea nafasi ya kushinda, kwa hiyo nawaasa wateja wote wa Tigo wachangamkie fursa hii ya kutimiza ndoto zao za sikukuu na mwaka mpya’ alisema. 
Tigo Pesa inajivunia kufanya miamala ya zaidi ya TZS 1.7bn kila mwezi kupitia mtandao wake mpana wa mawakala zaidi ya  70,000 waliosambaa nchini kote. 

SEKRETARIETi YA MAADILI YAHIMIZA VIONGOZI KUORODHESHA MALI ZAO KABLA YA DESEMBA 31 MWAKA HUU

SEKRETARIETi YA MAADILI YAHIMIZA VIONGOZI KUORODHESHA MALI ZAO KABLA YA DESEMBA 31 MWAKA HUU

December 27, 2017
umi1
Kamishna wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Jaji Mstaafu Harold Nsekela akizungumza na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo leo wakati alipowawataka Viongozi wote wa umma nchini  kuorodhesha mali zao  kisha kukabidhi kwa Sekretarieti kabla ya Desemba 31 mwaka huu Kulia ni Afisa Sheria Mkuu wa Sekretarieti hiyo Bw. Filotheus Manula.
umi2
Kamishna wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Jaji Mstaafu Harold Nsekela katikati  akikaribishwa na Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari Maelezo Bw. Rodney Thadeus ili kuzungumza na waandishi wa habari,  wa pili kutoka kulia ni Aisa Sheria Mkuu wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Bw. Filotheus Manula na kushoto ni Ofisa wa Sekretarieti hiyo Bw. Waziri Kipacha
………………………………………………………………………….
Kamishna wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Jaji Mstaafu Harold Nsekela amewahimiza  viongozi wote wa umma nchini  kuorodhesha mali zao  kisha kukabidhi kwa Sekretarieti kabla ya Desemba 31 mwaka huu.
Akizungumza na Waandishi wa habari leo katika ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo amesema  kufanya hivyo ni utaratibu ambao upo kwa mujibu wa sheria ,hivyo lazima watekeleze kwa wakati na watakaoshindwa hatua za kinidhamu  zitachukuliwa dhidi yao.
, Jaji Mstaafu  Nsekela ameongeza kwamba mwisho kwa viongozi wa umma kukabidhi tamko la mali zao na kufafanua  kuwa viongozi wanaotakiwa kuorodhesha mali zao na kisha kukabidhi Sekretarieti ya Maadili ni wale wa kuteuliwa na kuchaguliwa.
“Kila kiongozi wa umma ajaze tamko hilo kwa kuorodhesha mali zake, mwenza wake na watoto wake walio na umri chini ya miaka 18,”amesema.
Ameongeza kuwa viongozi ambao wanastaafu wakati wanaingia waliorodhesha mali zao, hivyo wanapostaafu ni lazima waoredheshe ili ifahamike wanatoka wakiwa na mali kiasi gani.
Ili kufikia malengo ya  tamko hilo kisheria linalowahusisha pia viongozi waliostaafu na wale wanaoelekea kustaafu, Ameongeza kwamba Fomu za tamko zipo kwenye tovuti ya sekretarieti ya maadili.
Amesema anaamini viongozi wanafahamu wajibu wao,hivyo wafanye haraka  iwezekanavyo na hasa kwa kuzingatia muda uliobakia ni mchache.
Kuhusu viongozi wanaostaafu ambao wamejaza tamko hilo amesema nao bado lakini katika eneo hilo kuna changamoto yake kidogo kwani viongozi wanapostaafu inakuwa ngumu kuwapata lakini nao watambue wanatakiwa kujaza tamko kwa mujibu wa sheria.
Kwa upande wake, Ofisa Sheria Mkuu wa Sekretarieti  ya maadili Bw. Filotheus Manula ameongeza kuwa ujazaji wa tamko la mali kwa viongozi wa umma ni takwa la kikatiba na kuna adhabu kwa wasiofuata.
Ametaja adhabu hizo ni kuonywa, kushushwa cheo, kusimamishwa kazi na wakati mwingine kufukuzwa kazi.

KAMANDA WA POLISI MKOA WA SINGIDA ASHIRIKI IBADA MAALUM YA KULIOMBEA TAIFA ILIYOANDALIWA NA UMOJA WA MAKANISA MKOA WA SINGIDA

December 27, 2017
 Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Singida, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), Deborah Magiligimba akizungumza na waumini wa Kikristo(hawapo pichani) kwenye ibada maalum ya kuliombea Taifa iliyoandaliwa na Umoja wa Makanisa Mkoa wa Singida  jana.
 Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Singida, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), Deborah Magiligimba( wa tano kulia) akifuatilia kwa makini mahubiri wakati wa Ibada maalum ya kuliombea Taifa iliyoandaliwa na Umoja wa Makanisa Mkoa wa Singida jana  wengine pichani ni viongozi wa madhehebu mbalimbali ya Kikristo  Mkoa wa Singida.
 Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Singida, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), Deborah Magiligimba akizungumza na waumini wa Kikristo kwenye ibada maalum ya kuliombea Taifa iliyoandaliwa na Umoja wa Makanisa Mkoa wa Singida  jana ambapo alisisitiza umuhimu wa wananchi kutii Sheria za nchi bila shuruti.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Singida, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), Deborah Magiligimba akizungumza na waandishi wa habari namna Jeshi la Polisi lilivyojipanga kuimarisha ulinzi katika nyumba za ibada na kumbi za starehe katika kipindi hiki cha sikukuu za Krismas na Mwaka Mpya.