BENKI YA CRDB YAZINDUA KADI ya Kimataifa ya ‘TembocardVisa Infinite’

September 06, 2016

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa Kituo cha kutolea huduma "Premier Club" pamoja na Kadi ya Kimataifa ya TemboCardVisa Infinite uliofanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam. (Picha na Francis Dande)
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB, Ally Laay akizungumza wakati wa uzinduzi wa TemboCard Visa Infinite pamoja na uzinduzi wa Kituo cha Huduma kwa Wateja Wakubwa cha Premier Club.
Naibu Spika Dk. Tulia Ackson akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi huo. 
Naibu Spika Dk. Tulia Ackson akipeana mkono na Dk. Kimei.
Naibu Spika Dk. Tulia Ackson akipeana mkono na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Ally Laay.
Mkurugenzi wa Masoko, Utafiti na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Tully Mwambapa akizungumza katika hafla hiyo.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB, Ally Laay (kulia), akimkabidhi Naibu Spika, Dk. Tulia Ackson kadi ya kimataifa ya ‘TembocardVisa Infinite’, wakati wa uzinduzi wa kadi hiyo uliokwenda sambamba na kituo cha kutolea huduma ‘Premier Club’ jijini Dar es Salaam, mwishoni mwa wiki. 

MATUKIO YA BUNGENI MJINI DODOMA LEO.

September 06, 2016

 Baadhi ya Wabunge wakiingia katika ukumbi wa bunge kuhudhuria mkutano wa nne(4) wa  bunge la kumi na moja (11) la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo Mjini Dodoma.
 Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Job Ndugai akiingia kwenye ukumbi wa Bunge kwa ajili ya kuendesha mkutano wa nne(4) wa  bunge la kumi na moja (11) la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo Mjini Dodoma.
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Job Ndugai Akiwaongoza Wabunge wa kuimba wimbo wa Taifa wakati wa mkutano wa nne(4) wa  bunge la kumi na moja (11) la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo Mjini Dodoma.
 Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakiwa katika ukumbi wa bunge wakati wa mkutano wa nne(4) wa  bunge la kumi na moja (11) la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo Mjini Dodoma.
 Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. George Masaju akimueleza jambo Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa  wakati wa mkutano wa nne(4) wa  bunge la kumi na moja (11) la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo Mjini Dodoma
 .Naibu Waziri, Ofisi ya Rais (TAMISEMI) Mhe. Selemani Said Jafo (MB) akieleza mpango wa kuendelea kuimarisha hospitali za Serikali Nchini.
 Katibu wa Bunge Dkt. Thomas Kashililah akiwaeleza jambo Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. George Masaju na Waziri Wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira, Vijana,Wazee na Wenye Ulemavu wakati wa mkutano wa nne(4) wa  bunge la kumi na moja (11) la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo Mjini Dodoma.
                 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye                (MB) akieleza mipango ya Serikali katika kuimarisha michezo nchini                   na kuwataka wadau mbalimbali kujitokeza kusaidiana na Serikali                                                                      kuwekeza katika Michezo. 
Mbunge wa Jimbo la Chemba Mhe. Juma Nkamia akiwaeleza jambo Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye (MB) na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais(Muungano na Mazingira) Mhe. January Makamba (MB), wakati wa mkutano wa nne(4) wa  bunge la kumi na moja (11) la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo Mjini Dodoma. 
PICHA NA HASSAN SILAYO-MAELEZO.

MAKAMU WA RAIS MAMA SAMIA SULUHU HASSAN AZUSHIWA KUOMBA KUJIUZULU, OFISI YAKE YAKANUSHA VIKALI UZUSHI HUO

September 06, 2016
MAMA SAMIA
Dar es Salaam, Tanzania
Ofisi ya Makamu wa Rais imekanusha vikali kuwa taarifa inayosambazwa kwenye baadhi ya mitandao kuwa Makamu wa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan ameomba kujiuzulu wadhifa wake,  ni ya uongo.

Taarifa ilyotolewa hivi punde leo, na Ofisi ya Makamu wa Rais, imesema, taarifa hiyo ni ya uzushi na uongo na kuomba wananchi kuipuuza mara moja kwa kuwa mbali ya kupotosha wananchi lakini pia ina lengo la uchochezi na kuliweka taifa kwenye taharuki.

"Taarifa hiyo ni ya uchochezi inayolenga kuliweka Taifa kwenye taharuki.  Mhe. Makamu wa Rais yuko bega kwa bega na Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kufanya kazi zao kwa mujibu wa Katiba ya nchi ili kuwaletea wananchi maendeleo", imesema sehemu ya Taarifa hiyo na kuongeza;-

"Ofisi ya Makamu wa Rais inawataka wananchi na Watanzania kwa ujumla kupuuza taarifa hiyo ambayo inalenga kupotosha umma kuhusu ushirikiano mzuri uliopo baina ya Viongozi wetu". 
TAARIFA  RASMI
 
TAARIFA  RASMI

WASHIRIKI 29 WA SHINDANO LA MAISHA PLUS EAST AFRIKA 2016 WAINGIA RASMI KIJIJINI KUANZA SAFARI YA KUISAKA MIL.30

September 06, 2016
 Ally Masoud  maarufu kwa jina la Kipanya akiwa katika kijiji na Babu mwenyeji wa kijiji cha Maisha Plus wakijadili jambo wakati wakiwangoja washiriki wa shindano hilo hapo jana ambapo pia ilikuwa ikirushwa live na kituo cha Luninga cha AZAM TWO chaneli 102
 Babu mwenyeji wa kijiji cha Maisha Plus akiwa anaandaa mazingira ya kijijini hapo
 Haya ni Baadhi ya maeneo katika kijiji cha Maisha Plus ambapo washiriki hao kutoka Nchi Tano za Afrika Mashariki watakaa kwa wiki 8
 Washiriki wa shindano la Maisha Plus Msimu wa tano wakiwa wanaingia kijijini huku kila mmoja akiwa amefungwa kitambaa usoni wasijue wapo wapi.
Mwenyeji wa Kijiji Babu wa Maisha Plus akiwa anawakaribisha washiriki kwa namna yake
 Hapa Washiriki wakiendelea kuingia katika kijiji cha Maisha Plus huku wasifahamu wapo wapi.
 Masoud Kipanya akiwapa maelekezo washiriki wa Shindano la Maisha Plus kabla hawajafugua rasmi vitambaa na kujua wapo wapi
 Hivi ni Baadhi ya Vifaa na vitu ambavyo vijana wa Maisha Plus watakuwa wakivitumia kipindi wapo kijijini kwa Muda wa Wiki8
 Masoud Kipanya akitoa msisitizo wa Jambo kwa washiriki wa shindano la Maisha Plus Msimu wa tano
Washiriki wa wa Shindano la Maisha Plus Msimu wa tano wakiwa wanafungua vitambaa kuona rasmi kijiji ambacho wataishi kwa wiki 8
Hapa ilikuwa ni kasheshe baada ya kufungua vitambaa na kukuta wapo porini sehemu wasiyo ijua huku kukiwa hakuna jengo lolote.
Hapa washiriki wa shindano la Maisha Plus wakiwa wanajipanga kuanza kufanya mchakato wa kuanza kujenga nyumba zao
Bado shughuli ilikuwa ni Pevu sana hawaelewi kabisa wanaanzia wapi wanaishia kujishauri kwanza huku kila mmoja akiwaza Milioni 30 atazipata vipi?
Hapa bado shughuli ndio kwanza ilikuwa inaanza washiriki hawa pia walikuwa wakibadilishana mawazo wafanyaje.
Babu wa Kijiji cha Maisha Plus akiwa anatoa maelezo ya kina kwa washiriki wa shindano hilo ambao wanatoka katika Nchi 5 Afrika Mashariki jinsi gani wataishi, watakavyojenga nyumba zao na watakavyo ishi katika kijiji cha Maisha Plus
Wakiwa wanaleta mizigo yao ndani ya Kijiji cha Maisha Plus
Mmoja wa washiriki wa Shindano la Maisha Plus akinoa panga kwa ajili ya kujiandaa kwenda kukata miti kwa ajili ya kujenga nyumba zao za kuishi ambapo kila nyumba moja watakuwa wanaishi washiriki watatu.
Baadhi ya Mizigo ya washiriki baada ya kuwasili katika kijiji cha Maisha Plus
Washiriki wa Shindano la Maisha Plus wakiwa wameanza kuandaa makazi yao
Kazi Ikiendelea ya Kuandaa sehemu ya Kuishi
Hapa kazi tuu yani kila mtu yupo na yake alimradi tuu wapate kujenga nyumba za kuishi katika kijiji hicho cha Maisha Plus.
Kulikuwa hakuna namna lazima kila mmoja afanye kazi ili wapate sehemu ya kulala
Wakati wenzake wamekwenda tafuta Miti ya Kujengea nyumba yeye alikuwa anatengeneza mpini
Babu wa Kijiji cha Maisha Plus akiwa anatoa maelekezo na kutoa vipimo vya jinsi watakavyokujenga nyumba zao
Kila mshiriki akiwa ameshika nyenzo yake kwa ajili ya kujenga nyumba zao zakuishi
Kazi zinaendelea hapa na sasa ilikuwa ni mwendo wa kukata miti ili kuwahi kumaliza kujenga nyumba na kuanza kuishi.
Babu wa Maisha Plus akiwa anafatilia jambo kijijini hapo.
Bila kuchakalika na kazi ya kujiandaa kutafuta miti na kujenga nyumba unaweza kujikuta unalala nje
Baadhi yao walikuwa wamesha anza kuweka nguzo za nyumba zao
Akionekana akikomaa kuchimba kitu kabla hajawekea mpini
Ukiwa katika kijiji cha Maisha Plus  lazima upate na ubunifu sana .. hawa jamaa washiriki wa Shindano la Maisha plus msimu wa 5 2016 wakiwa wanakata miti kwa ajili ya kujenga nyumba ambapo wataishi kwa wiki 8
Pori kwa pori
Kazi kwa kwenda mbele 

MAISHA PLUS EAST AFRICA 2016 itakuwa ikionyeshwa na AZAM Two Chaneli 102 
#HapaKaziTuu
#VijanaNdioNgazi