MAKAMU WA RAIS ATEMBELEA OFISI NDOGO YA CCM LUMUMBA LEO
Mjumbe
wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Mwenyekiti
wa CCM Taifa na Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kwenye Ofisi
ndogo ya CCM Lumumba jijini Dar es salaam leo Februari 02, 2016 wakati
Makamu wa Rais alipotembelea katika Ofisi hiyo (Picha na OMR)
Unilever yaendelea kuwazawadia wanafunzi shule mbambali Dar
Mwanafunzi wa darasa la tano wa shule ya msingi Maarifa, Gongo la Mboto, jijini Dar es Salaam Ester Lawrence akipokea fulana kutoka kwa Balozi wa Blue Band Neema Upendo shuleni hapo jana akiwa ni mmoja wa washindi wa shindano la Blue Band ‘Kula Tano’ linalowamasisha wanafunzi kutambua umuhimu wa kula vyakula vyenye virutubisho. Kushoto ni mwalimu wa michezo Edith Katundu.
SERIKALI ITAENDELEA KUWAFUNGIA MAGETI WATUMISHI
Serikali haitokuwa tayari kuwaona watumishi wa umma wachache wakinufaika na kufaidi pesa za walipa kodi hususani wa kipatao cha chini na wale maskinini.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kigwangalla.
Hayo yamesema wilayani hapa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kigwangalla alipokuwa akiwahutubia wananchi wa wilaya hiyo.
Dkt. Kigwangalla alisema serikali ya awamu ya tano inawataka watumishi wote nchini kufanya kazi za kuwahudumia wananchi na kuacha uzembe kwani awamu hii haiwezi kuwavumilia watumishi wa namna hiyo.
“Serikali haitowavumilia watumishi wazembe, hivyo tutaendelea kuwafungia mageti na kuwashughulikia wale wazembe, tunataka watumishi wa umma wafanye kazi ya kuwahudumia wananchi kwa ufanisi, mtumishi akizembea tutamtumbua majipu, akichelewa tunamfungia geti na akiiba tunafilisi pamoja na kumpeleka jela,hii ndiyo serikali ya hapa kazi tu,” alisema Dkt. Kigwangalla.
Aidha alisema serikali ya awamu ya tano inataka kero za wananchi zifanyiwe kazi na kutekeleza ahadi zote za ilani ya uchaguzi ya ccm zinatimizwa.
“Hatutomuonea mtu,lakini tutafanyia kazi pale penye matatizo,tunataka Tanzania mpya ya mwaka 2015 inakua,hatutaki hadithi wala ahadi,” alisema naibu waziri.
Hata hivyo aliwataka wazazi wote wenye watoto wenye umri wa kwenda shule kuwapeleka watoto wao kuanza masomo kwani elimu kwa sasa ni bure na hakuna michango yoyote.
“natoa wito kwa walimu wote wasitoze michango yeyote wala ushuru kwa wazazi wanaowapeleka kuwaandikisha watoto shule kwani shule zimepatiwa pesa za kuendeshea shule hizo,” alieleza Dkt. Kigwangalla.
Dkt. Kigwangwalla aliwakumbusha watumishi wa umma kujipanga na kama watagundulika ni majipu bali hawatosita kuwatumbua hadi kina kitoke,usaha na damu kutoka bila huruma.
MANISPAA YA ILEMELA YAWEKA MSIMAMO WAKE DHIDI YA WAFANYABIASHARA WA HOTEL NA NYUMBA ZA KULALA WAGENI.
Mkurugenzi wa Manispaa hiyo John Wanga akitoa ufafanuzi kwa Wanahabari juu ya tozo ya Kodi ya Malazi kwa wafanyabiashara wa hotel na nyumba za kulala wageni.
Wafanyabiashara wa Hotel na
Nyumba za Kulala Wageni katika Manispaa ya Ilemela Mkoani Mwanza, Wametakiwa kufanya
biashara zao kwa mjibu wa kanuni na sheria za biashara zao ikiwemo kulipa
ushuru na kodi mbalimbali kama ilivyoidhinishwa na Serikali.
Kauli
hiyo imetolewa hii leo na Mkurugenzi wa Manispaa hiyo John Wanga, katika Kikao
cha Viongozi wa Manispaa ya Ilemela na Wafanyabiashara hao, juu ya Ufafanuzi wa
Sheria ya Kodi ya Malazi, ambayo imeanza kukusanywa kwenye Hotel pamoja na
nyumba zote za kulala wageni.
“Kama
una wajibu wa kulipa kodi Majengo, leseni ya biashara, mabango, ushuru wa
malazi, ushuru wa huduma na kodi nyingine zote zilizo kisheria, ni vyema
ukalipa bila kushurutishwa. Kutokufanya hivyo utatufanya twende kwenye ule
mkono mwingine ambao tusingependa sana kuutumia ambao ni kushurutishana”.
Amesema Wanga.
Hata
hivyo licha ya agizo hilo, Wafanyabiashara katika Manispaa hiyo wameiomba
Serikali kuwapunguzia mzigo wa Kodi walionao kwa kuwa hivi sasa wanakabiriwa na
mzigo mkubwa wa kodi pamoja na Ushuru jambo ambalo wamesema ni tofauti na ahadi
ya kuondoa kero ya kodi mbalimbali aliyoitoa Mhe.Rais John Pombe Magufuli wakati
wa Kampeni zake.
“Kodi
zimekuwa nyingi sana kwa sisi wafanyabiashara wa Hotel na Guest Houses (nyumba
za kulala wageni), kwa mfano kodi ya majengo, leseni ya biashara, ardhi,
mabango na nyinginezo. Yaani nyumba moja inakuwa na kodi zaidi ya 11 sasa
itafika sehemu tutashindwa kufanya biashara. Sisi tuko tayari kulipa kodi ya majengo,
ardhi na leseni hivyo serikali iangalie namna ya kutusaidia”. Alisema Nuru
Ramadhan ambae ni mmoja wa wamiliki wa nyumba ya kulala wageni katika Manispaa
ya Ilemela na kuungwa mkono na wenzake.
Hawa
Waziri ambae ni Mwanasheria wa Manispaa ya Ilemela, amewasihi Wafanyabiashara
hao kuwa tayari kulipa kodi zilizopo kisheria, ikiwemo Kodi ya Malazi huku
wakiendelea kujenga hoja Serikalini ili Sheria hizo zifanyiwe marekebisho
bungeni na hatimae kupunguzwa.
Awali
Wafanyabiashara wa Hotel na Nyumba za Kulala Wageni, walikuwa wakilipa Kodi ya
Malazi ambayo ni asilimia 20 ya mapato yanayotokana na malipo ya kila mteja,
kabla ya kodi hiyo kusitishwa na Serikali ambapo hata hivyo imerejeshwa tena na
Wafanyabiashara hao wanatakiwa kulipa kodi ya asilimia 10 ya mapato
yanayotokana na mteja badala ya 20 kama ilivyokuwa awali.
Kikao juu ya tozo ya Kodi ya Malazi kwa wafanyabiashara wa hotel na nyumba za kulala wageni kikielendelea
Afisa biashara Manispaa ya Ilemela Mkoani Mwanza akitoa ufafanuzi juu ya tozo ya Kodi ya Malazi kwa wafanyabiashara wa hotel na nyumba za kulala wageni
Hawa Waziri ambae ni Mwanasheria wa Manispaa ya Ilemela Mkoani Mwanza akitoa ufafanuzi kwa wanahabari juu ya tozo ya Kodi ya Malazi kwa wafanyabiashara wa hotel na nyumba za kulala wageni
Cyprian Oyier ambae ni mmoja wa wafanyabiashara wa hotel Manispaa ya Ilemela akiwasilisha hoja zake katika kikao juu ya tozo ya Kodi ya Malazi kwa wafanyabiashara wa hotel na nyumba za kulala wageni
Lemmy Muganyizi Mboyelwa ambae ni mmoja wa wamiliki wa nyumba ya kulala wageni katika Manispaa ya Ilemela akiwasilisha hoja zake katika kikao juu ya tozo ya Kodi ya Malazi kwa wafanyabiashara wa hotel na nyumba za kulala wageni
Nuru Ramadhani ambae ni mmoja wa wamiliki wa nyumba ya kulala wageni katika Manispaa ya Ilemela akiwasilisha hoja zake katika kikao juu ya tozo ya Kodi ya Malazi kwa wafanyabiashara wa hotel na nyumba za kulala wageni
Melikior Fundi Minsa ambae ni mmoja wa wamiliki wa nyumba ya kulala wageni katika Manispaa ya Ilemela akiwasilisha hoja zake katika kikao juu ya tozo ya Kodi ya Malazi kwa wafanyabiashara wa hotel na nyumba za kulala wageni
Wafanyabiashara wa hotel na nyumba za kulala wageni katika Manispaa ya Ilemela wakiwa katika kikao cha ufafanuzi juu ya kuanza kutumika kwa kodi ya Malazi
Wafanyabiashara wa hotel na nyumba za kulala wageni katika Manispaa ya Ilemela wakiwa katika kikao cha ufafanuzi juu ya kuanza kutumika kwa kodi ya Malazi
Kushoto ni Stella Lwakatare ambae ni Afisa Biashara Mkuu katika Manispaa ya Ilemela Mkoani Mwanza akifafanua jambo kwenye kikao cha Wafanyabiashara wa hotel na nyumba za kulala wageni katika Manispaa ya Ilemela juu ya kuanza kutumika kwa kodi ya Malazi.
Katikani ni Mkurugenzi wa Manispaa hiyo John Paul Wanga na Kulia ni Peter Revelian ambae ni Mwekahazina wa Manispaa ya Ilemela.
Watumishi wa idara mbalimbali katika Manispaa ya Ilemela Mkoani Mwanza.
Imeandaliwa na George Binagi-GB Pazzo
LIGI KUU MZUNGUKO WA 17 KUENDELEA KESHO
Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara mzunguko wa 17 unatarajiwa
kuendelea kesho Jumatano kwa michezo sita kuchezwa katika viwanja
mbalimbali, huku kila timu ikisaka pointi tatu muhimu kwenye msimamo wa
ligi hiyo.
Kesho Jumatano, Simba SC watakua wenyeji wa maafande wa Mgambo
Shooting kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam, JKT Ruvu
watawakaribisha Mbeya City katika uwanja wa kumbukumu ya Karume Ilala,
huku Mtibwa Sugar wakicheza dhidi ya Toto Africans katika uwanja wa
Manungu – Turiani.
Jijini Mbeya, Tanzania Prisons watakua wenyeji wa vinara wa ligi hiyo
Young Africans katika uwanja wa Sokoine, Wana kimanumanu African Sports
watacheza dhidi ya Mwadui FC uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga, huku
wakata miwa wa Kagera Sugar wakiwakaribisha Majimaji FC katika uwanja wa
Kamabarage mjini Shinyanga.
Alhamisi ligi hiyo itaendelea kwa kuchezwa mchezo mmoja tu, Wagosi wa
Kaya Coastal Union watawakaribisha Ndanda FC katika uwanja wa Mkwakwani
jijini Tanga.
Michezo ya viporo ya Azam FC imepangiwa ratiba, mchezo dhidi ya
Tanzania Prisons utachezwa Februari 24 uwanja wa Sokoine jijini Mbeya,
huku mchezo dhidi ya Stand United ukichezwa Machi 16 katika uwanja wa
Azam Complex.
MALINZI AMPONGEZA KIKWETE
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanznaia (TFF), Jamal Malinzi
amempongeza Rais wa awamu ya nne Jakaya Kikwete kwa kukubali uteuzi wa
Shirikisho la Mpira wa Miguu barani Afrika (CAF) na GAVI utakaomfanya
kuwa bingwa wa chanjo na balozi wa mradi wa Africa United Duniani.
“Familia ya mpira wa miguu inajua umuhimu wa chanjo na hasa katika
maendeleo ya vipaji na wanamichezo kwa ujumla na jinisi chanjo
inavyoweza kuwapa watoto siyo tu fursa ya maendeleo bali pia haki ya
kuishi” ilisema sehemu ya barua hiyo iliyosainiwa na Rais wa TFF, Jamal
Malinzi.
Katika barua hiyo, Malinzi ameelezea furaha ya TFF kuona kiongozi wa
Tanzania akiongoza mapambano ya kuokoa afya na uhai wa kizazi cha sasa
na kijacho katika Afrika na dunia kwa ujumla.
“TFF itaunga mkono juhudi zako ili kufanikisha malengo yaliyowekwa na
ushirika wa chanjo” ilimalizia barua hiyo ambayo nakala yake imetumwa
kwa Rais wa Caf, Issa Hayatou.
fastjet yaongeza ndege ya tano
Dar es Salaam, Januari
28, 2016-Fastjet
Tanzania imeongeza ndege nyingine aina ya Airbus A319 kwenye idadi ya ndege zake nne na hivyo kuliweka shirika hilo la ndege la
gharama nafuu kuendelea na mipango yake ya kupanuka.
“Ndege
za fastjet kwa hivi sasa ni nne na zote zinatumika na ongezeko la ndege ya tano ni jibu kwenye mikakati yetu ya kupanuka pamoja na hitaji la kuongeza uwezo
wa kubeba kwenye safari zetu za ndani na za kimataifa”, alisema Meneja Mkuu wa fastjet Tanzania, John Corse.
Ndege
hiyo ya nyongeza inafanya jumla ya
nafasi inayokuwepo kwa siku kwenye safari kwa ajili ya wateja kufikia 1,000.
Fastjet
ilianza safari zake nchini mwaka 2012na hivi sasa inajiendesha kwa kutumia
ndege tano aina ya A319 kwenye mtandao
wake wa safari ambao unahusisha Dar es Salaam, Mbeya, Mwanza, Kilimanjaro na
Zanzibar na kuifanya ijikite kuufanya usafiri wa anga ndani ya Tanzania watu
wote waumudu.
Hali
kadhalika ilianzisha safari za kimataifa
kwenda Entebbe nchini Uganda, Nairobi Kenya, Harare Zimbabwe, Johannesburg Afrika Kusini
na Lusaka nchini Zambia katika kipindi cha miaka mitatu ya kuendesha shughuli
zake.
“Tangu
tuanze safari zetu tumeshabeba abiria
zaidi ya 1,800,000 ambapo utafiti wetu unaonesha kuwa zaidi ya theluthi moja ya abiria wetu walikuwa ndio mara yao ya kwanza
kumudu kusafiri kwa ndege”, anasema
Corse.
Aliendelea
kusema, “kuongeza ndege nyingine kwenye safari zetu kunatupa fursa muhimu ya kuongeza masafa kwa njia zetu zilizopo ili kukidhi
mahitaji ya wateja, na na inasaidia kwenye lengo letu la kuongeza njia
moja ya kimataifa kwenye mtandao wetu kwa mwaka huu 2016”.
Hali
kadhalika, Corse anabainisha kuwa ndege
hiyo mpya inamanisha kuwa fastjet ni sawia
na ni kubwa katika kutosheleza kupanuka kwa shughuli za fastjet.
Ndege
hiyo A319 ambayo ni Airbus ni ya injini mbili ambazo zinatoa kiwango cha juu cha ufanisi
pamoja na kiwango cha chini kabisa cha madhara kwenye mazingira, ikiwa ni
nyongeza kwenye viwango vya juu vya hali
ya kuliwaza ndani ya ndege hiyo ya kisiasa.
Ndege
hiyo ina uwezo wa kubeba abiria 156 ambaop wanamudu viwango vya chini vya
kuendesha mtindo wa maisha wa gharama nafuu ambao unaendeshwa na Fastjet
Tanzania.
Baadhi
ya njia muhimu ambazo ndege hiyo mpya
itakuwa inahudumia ni njia mpya
iliyoanzisjhwa hivi karibuni kati ya Dar es Salaam na Nairobi, Kilimanjaro na
Nairobi na Dar es Salaam kwenda Zanzibar
ambazo zote zilianza kwa mara ya kwanza Januari 11, 2016. njia hizi mpya zote ni kielelezo muhimu muda mrefu kwenye
upanuzi wa njia za fastjet kitaifa na
kimataifa.
Fastjet
inatarajia kuongeza ndege zaidi kwenye njia yake ya Kenya kutokana na mahitaji ya wateja kuongezeka
kunakosababisha na kumudu, usalama, kasi na huduma kwa wakati, na hali
kadhalika imeshajionesha kuwa kuna matarajio ya kuzindua
safari kati ya Zanzibar na Nairobi
na hali kadhalika kati ya Dar es Salaam na Mombasa baadaye mwaka 2016.
“Usafiri
wa anga unaoumudu ni muhimu kwenye
kukuza uchumi wa Tanzanoa, hususani kwenye kukuza sekta za biashara na utalii”, alisema
Corse.
Hali
kadhalika Corse alibainisha kuwa ndege
hiyo mpya inamaanisha kwamba ndege za
Fastjet zitatosheleza kiasi cha kutosha
kusaidia kwenye changamoto za usimamizi na uendeshaji iwapo
ndege moja miongoni mwake itakuwa
haifanyi kazi au kama ipo kwenye matengenezo au ukarabati wa lazima.
Mwisho
photo
Krantz Mwanteple
C.E.O & Founder, MWANAHARAKATI MZALENDO MEDIA
Phone: +255-712579102 /+255-767392840
Email: krantzcharles@gmail.com
Website: www.mwanaharakatimzalendo.blogspot.com
Whatsapp: 0712579102
"HABARI MAKINI KWA WATU MAKINI"
DC KINONDONI, PAUL MAKONDA APOKEA SARUJI MIFUKO 1640 KUTOKA KWA WADAU WA MAENDELEO KWA AJILI YA UJENZI WA SHULE ZA SEKONDARY
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Duma, Areeq Amran Mohamed (kulia), akimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda mfuko mmoja wa saruji kati ya 640 aliyoitoa kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa Shule za Sekondari za wilaya hiyo Dar es Salaam leo asubuhi. Katika makabidhiano hayo Makonda alipokea mifuko 500 ya saruji kutoka kwa Mwenyekiti wa Jumuia ya Wazazi Taifa ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Abdallah Bulembo na Askofu mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dk.Alex Malasusa aliyetoa mifuko 500.
Mwenyekiti wa Jumuia ya Wazazi Taifa ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Abdallah Bulembo (kulia), akimkabidhi saruji hiyo DC Makonda.
Lori lilibeba saruji hiyo likiwa eneo la tukio.
DC Makonda na wageni wake wakiwa eneo la tukio kabla ya makabidhiano ya saruji hiyo.
Mhe. Bulembo akihojiwa na waandishi wa habari baada ya kukabidhi msaada huo.
Wanahabari wakizungumza na watoa msaada huo.
Subscribe to:
Posts (Atom)