Mvua ya mabao yatawala uwanja wa CCM Kirumba Mwanza

October 14, 2017

Ni kwenye mchezo wa kirafiki baina ya EFM Vs Mwanza Veterans!
BMG

DK. KESSY AWAPIGA MSASA WASIMAMIZI WA MASHAMBA YA MKIKITA NCHINI

October 14, 2017
 Daktari wa Mifugo na Kilimo, Dk.  Aloyce Kessy akitoa mafunzo ya jinsi ya kuandaa vitalu vya miche ya papai katika kikao cha mpango kazi kwa watalaamu wa kilimo wa Mtandao wa Kijani Kibichi Tanzania (MKIKITA) watakaokuwa wanasimamia mashamba makubwa yaliyoanzishwa na mtandao huo maeneo ya Ruaha mkoani Iringa, Kibaha na Vikindu mkoani Pwani. Kikao hicho kimefanyika leo eneo la Goba, Dar es Salaam.PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG
 Dk. Kessy akifafanua jambo wakati wa kikao hicho. Kutoka kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Mkikita, Adam Ngamange, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mtandao huo, Dk. Kissui S Kissui na  Mkurugenzi wa Miradi na Maendeleo ya Biashara wa Mkikita, Edwin Mkwanga
 Washiriki wakisikiliza kwa makini wakati Dk. Kessy akitoa mafunzo hayo
 Mkurugenzi Mtendaji wa Mkikita, Adam Ngamange akiwaelea watalaaamu hao kuhusu majukumu yao
 Watalaamu wa kilimo wa Mkikita wakiwa makini kusikiliza maelekezo ya jinsi ya kuboresha kilimo cha papai





TAMASHA LA WAANDISHI WA HABARI MKOA WA ARUSHA KUFANYIKA KESHO

October 14, 2017

 
wakwanza kulia ni Katibu wa TASWA mkoa wa Arusha, Mussa Juma katikati ni Mwenyekiti wa TASWA Arusha, Jamila Omar akioongea na waandishi wa habari
Na  Woinde Shizza,Arusha
Tamasha la waandishi wa habari, kanda ya kaskazini, linatarajiwa kufanyika jumapili, octobar 15 katika uwanja wa General Tyre ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Mkuu wa mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo.

Katika tamasha hilo, ambalo litashirikisha wanahabari zaidi ya 500, kutoka mikoa ya Arusha, Tanga, Manyara na Kilimanjaro,limedhaminiwa na shirika la hifadhi za Taifa(TANAPA) Mifuko ya hifadhi ya Jamii ya LAPF na PSPF, Mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro, kampuni ya vinywaji baridi ya Coca cola na kampuni ya ya vinywaji baridi ya SBC (T) Limited na Palace Hoteli.

Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari, Katibu wa TASWA mkoa wa Arusha, Mussa Juma, alisema tamasha hilo, limeandaliwa na TASWA kwa kushirikiana na kampuni ya Arusha media na maandalizi yote yamekamilika.

Juma alisema katika tamasha hilo, bingwa atazawadiwa kikombe na fedha taslimu jumla ya shilingi 500,000, mshindi wa pili fedha taslimu 100,000 na kwa upande wea mpira wa pete mshindi ni kikombe na fedha taslimu jumlaya sh 300,000 na mshindi wa pili sh 50,000.

Alisema pia kutakuwa na michezo ya mbio za magunia, kuvuta kamba, mbio za vijiko, riadha na masumbwi ambapo tayari waambuzi wanaotambuliwa na mashirika mbali mbali ya michezo watakuwepo.

Hata hivyo, alisema wadhamini wengine wa tamasha hilo wanatarajiwa kutangazwa, ili kuhakikisha wanahabari wanaburudika ambapo pia kuwa kuwa na benki maalum ambayo itatumnbuiza siku za tamasha.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa TASWA Arusha, Jamila Omar alitoa wito kwa wanahabari wote na familia zao kujitokeza katika tamasha hili ambalo hufanyika kila mwaka mkoani Arusha.

Alisema kauli mbio ya tamasha hilo, ambalo linaendama na maadhimisho ya kumbukumbu ya mwalimu nyerere ni michezo ni ajira, michezo ni kazi tufanye kazi kwa bidii kuunga mkono jitihada za serikali ya awamu ya tano ya Tanzania ya viwanda.

Mratibu wa Tamasha hilo, Andrea Ngobole alizitaja timu ambazo zitashiriki kuwa ni TASWA Dar es Salaam, Triple A,RadioSunrise , chuo cha uandishi habari cha Arusha(AJTC)timu ya Arusha One Fm, TASWA Arusha,Radio ORS ya Manyara ,NSSF na timu ya Wazee Klabu.

KONGAMANO LA MAADHIMISHO YA SIKU YA CHAKULA LAFANA MKOANI GEITA

October 14, 2017
Mkuu wa Mkoa wa Geita Meja Jenerali Mstaafu Ezekiel Kyunga akizungumza wakati wa kongamano katika maadhimisho ya siku ya Chakula ambayo Kitaifa yanafanyika Mkoani Geita.
Baadhi ya washiriki wa Kongamano la maadhimisho ya siku ya Chakula ambayo Kitaifa yanafanyika Mkoani Geita wakifatilia kwa makini mada mbalimbali zikiwasilishwa.
Mkuu wa Mkoa wa Geita Meja Jenerali Mstaafu Ezekiel Kyunga akizungumza wakati wa kongamano katika maadhimisho ya siku ya Chakula ambayo Kitaifa yanafanyika Mkoani Geita.
Mchambuzi na mshauri wa sera katika Wizara ya kilimo Ndg Revelian Ngaiza Akiwasilisha mada kuhusu mchango wa sera za kilimo katika mageuzi ya uchumi wa viwanda wakati wa kongamano la maadhimisho ya siku ya Chakula Duniani ambayo Kitaifa yanafanyika Mkoani Geita.
Meneja wa Muendelezo wa wakulima wadogo TADB Ndg Joseph Mabula Akiwasilisha mada kuhusu Mikopo nafuu kwa mapinduzi ya kilimo na viwanda wakati wa kongamano la maadhimisho ya siku ya Chakula Duniani ambayo Kitaifa yanafanyika Mkoani Geita.
Afisa uendeshaji Mwandamizi Utoaji Mikopo na kudai madeni Kutoka Mfuko wa Pembejeo Ndg Joshua Kalab akiwasilisha mada kuhusu Mchango wa mfuko wa pembejeo katika kuongeza uzalishaji wa chakula, kupambana na njaa na kupunguza umasikini hususani vijijini wakati wa kongamano la maadhimisho ya siku ya Chakula Duniani ambayo Kitaifa yanafanyika Mkoani Geita.
Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano serikalini kutoka Wizara ya Kilimo Ndg Issa Sabuni akichangia mada wakati wa kongamano la maadhimisho ya siku ya Chakula Duniani ambayo Kitaifa yanafanyika Mkoani Geita.
Katibu wa Chama cha Biashara Tanzania Mkoa wa Kagera (TWCC) Bi Paskazia Sebastian akichangia mada wakati wa kongamano la maadhimisho ya siku ya Chakula Duniani ambayo Kitaifa yanafanyika Mkoani Geita.
Afisa Mfawidhi kutoka Taasisi ya udhibiti wa mbegu TOSCI Mkoa wa Mwanza Ndg Ngura Joseph Akiwasilisha mada kuhusu Mchango wa mbegu bora katika usalama wa chakula wakati wa kongamano la maadhimisho ya siku ya Chakula Duniani ambayo Kitaifa yanafanyika Mkoani Geita.

Afisa Kilimo Mkuu kutoka Wizara ya kilimo Bi Mwanaid Kiya Akiwasilisha mada kuhusu Sumu kuvu kwenye mahindi: Madhara katika sekta ya kilimo, Biashara na afya ya binadamu wakati wa kongamano la maadhimisho ya siku ya Chakula Duniani ambayo Kitaifa yanafanyika Mkoani Geita.

UJUMBE WA BABA WA TAIFA, MWALIMU JULIUS KAMBARAGE NYERERE KUHUSU UHIFADHI

October 14, 2017

BONANZA LA MICHEZO JIJINI TANGA LAHUDHURIWA NA MAMIA YA WAKAZI WA JIJI HILO

October 14, 2017
Wapenzi wa mchezo wa mpira wa kikapu wakishuhudia baadhi ya timu zilizoshiriki bonanza hilo zikichuana leo kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani mjini Tanga ambalo lilikuwa na msisimuko mkubwa likiwakutanisha mamia ya wananchi kutoka maeneo mbalimbali Jijini Tanga
TIMU za mpira wa Pete (netball) za Bandari na Jiji zikichuano katika bonanza hilo ambapo kwenye mchezo huo,Jiji iliweza kuibuka na ushindi wa  mabao 30-1 dhidi ya wapinzania wao ambapo kipindi cha kwanza Jiji iliweza kuongoza kwa mabao 18-0 dhidi ya Bandari
Wachezajji wakichuana katika mechi ya mpira wa pete kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani mjini Tanga leo katika bonanza la michezo ambalo limeandaliwa na Radio ya TK FM kwa kudhaminiwa na Tanga City Lounge,Tanga Fresh,Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya mkoani Tanga (NHIF),Vodacom,Amic Design,Chuo cha Utumishi wa Umma(TPSC) Tawi la Tanga,Katani Limited,Leen Events Planner,Shirika la Maendeleo la BRAC Tanzania,Jaysen Studio 
Wananchi wa mkoa wa Tanga wakishuhudia uhondo wa michezo mbalimbali katika bonanza hilo
Wachezaji wa timu ya mpira wa pete ya chuo cha Utumishi Mkoani Tanga wakitoka uwanjani mara baada ya mechi yao kumalizika
Wachezaji wa timu ya Maveterani ya Tanga Middle Age wakipasha kabla ya kuwavaa wapinzani wao Kilombero Veterani ambapo Tanga Middle Age walishinda kwa bao 1-0

Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga (NHIF) Ally Mwakababu kulia akitoa elimu kwa mkazi wa Jiji la Tanga aliyetembelea banda lao waliloweka kwenye bonanza hilo kwa lengo la kuhamasisha jamii kujiunga na mfuko huo ili kuweza kunufaika na matibabu


Wachezaji wa timu za maveterani wakichuana katika Bonanza hilo ambalo lilikuwa la aina yake kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani Mjini Tanga ambalo liliandaliwa na kituo cha Radio cha Jijini Tanga (TK)

Mashabiki wa michezo wakifuatilia kwa umakini bonanza hilo
Afisa wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga (NHIF) Denis Kapinga akitolea ufafanuzi baadhi ya huduma wanazozitoa wakati wa bonanza hilo

Msimamizi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Mkoani Tanga,Dinna Mlwilo kushoto akisisitiza jambo kwa wananchi waliofika kwenye banda lao leo kwenye bonanza la Michezo ambalo lilifanyika kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani mjini Tanga
Wafanyakazi wa Radio TK FM ya Jijini Tanga kushoto ni Mamy Mohamed ambaye ni Meneja wa Kituo hicho kulia ni George Kivumbi ambaye ni Program Manager katikati ni DJ Rogger Kiss wakiwa katika bonanza hilo
 Mamy Mohamed ambaye ni Meneja wa Kituo cha Radio cha TK FM ya Jijini Tanga akitoa utaratibu wa zawadi kwa washindi mara baada ya kumalizika bonanza hilo
Mkuu wa wilaya ya Korogwe Mkoani Tanga,Mhandisi Robert Gabriel akiwa na Mkurugenzi wa Radio TK ya Jijini Tanga,Saidi Othumani kushoto wakati alipokwenda kumwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martini Shigella katika Bonanza hilo
 Mkurugenzi wa Radio TK ya Jijini Tanga,Saidi Othumani kushoto akiwa na Mkuu wa wilaya ya Korogwe,Mhandisi Robert Gabriel
 Ally Choki mzee wa Farasi kulia akiwa na Luiza Mbutu kwenye jukwaa wakitumbuiza katika Bonanza la Michezo ambao liliandaliwa na Radio TK FM ya Jijini Tanga
 Wasanii wanaounda Bendi ya Twanga Pepeta wakitumbuiza Jukwaani
 Wasanii wanaounda Bendi ya Twanga Pepeta wakitumbuiza Jukwaani
 Baadhi ya washiriki  waliojitokeza katika bonanza hilo wakipiga picha ya pamoja

RAIS DKT MAGUFULI AONGOZA SHEREHE ZA KUZIMA MWENYE, NYERERE DAY NA WIKI YA VIJANA ZANZIBAR LEO

October 14, 2017
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akikvishwa skafu baada ya kuwasili kuongoza sherehe za Kilele cha Mbio za Mwenge wa uhuru, Kumbukumbu ya Baba wa Taifa na Wiki ya Vijana katika uwanja wa Amaan mjini Zanzibar leo Oktoba 14, 2017

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana na mwakilishi wa familia ya Mwalimu, Mhe. Makongoro Nyerere wakati akiwasili kwenye sherehe za Kilele cha Mbio za Mwenge wa uhuru, Kumbukumbu ya Baba wa Taifa na Wiki ya Vijana katika uwanja wa Amaan mjini Zanzibar leo Oktoba 14, 2017.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli na Rais wa Zanzibar na Mwnyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein wakiteta jambo wakati wa sherehe za Kilele cha Mbio za Mwenge wa uhuru, Kumbukumbu ya Baba wa Taifa na Wiki ya Vijana katika uwanja wa Amaan mjini Zanzibar leo Oktoba 14, 2017.
Vijana wa Halaiki wakitumbuiza kwenye sherehe za Kilele cha Mbio za Mwenge wa uhuru, Kumbukumbu ya Baba wa Taifa na Wiki ya Vijana katika uwanja wa Amaan mjini Zanzibar leo Oktoba 14, 2017.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akipokea Mwenge wa uhuru wakati wa sherehe za Kilele cha Mbio za Mwenge wa uhuru, Kumbukumbu ya Baba wa Taifa na Wiki ya Vijana katika uwanja wa Amaan mjini Zanzibar leo Oktoba 14, 2017.