WENYE MAHITAJI MAALUM WAKUMBUKWA UDOM

November 29, 2023


Na Dotto Kwilasa,Dodoma

Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM)kimezindua Harambee ya kuwachangia wanafunzi wenye mahitaji maalum wanaosoma chuoni hapo ili kuchochea ari ya mafanikio yao ikiwa ni pamoja na kuongeza ushawishi kwa wanafunzi wengine wa kundi hilo kutokata tamaa ya kusoma. 

Hayo yamejiri November 29,2023 Jijini hapa kwenye Mkutano wa 14 wa Baraza la wahitimu wa Chuo hicho (UDOM) ambapo fedha zitazopatikana kupitia Harambee hiyo zitasaidia kukidhi mahitaji ya ada, magongo,vifaa wezeshi na mengineyo. 

Akizungumza kwenye Baraza hilo, Waziri wa Madini nchini Peter Mavunde ameipongeza hatua hiyo huku akitoa maelekezo kwa Uongozi wa UDOM kuandaa orodha ya wadau wa Chuo hicho na kuwaomba kuchangia ili kufikia malengo kwa kuwa kila mwenye ulemavu ana haki ya kuishi maisha mazuri.

Kwa kutambua umuhimu wa wenye mahitaji maalum Mavunde kwa upande wake amechangia shilingi milioni tano za kitanzania ambazo zitasaidia kuboresha baadhi ya mahitaji kwa wanafunzi hao.

"Mnatambua hapa nimemwakilisha Naibu Waziri Mkuu ambaye hajaweza kufika hapa kutokana na kuwa na majukumu mengine, yeye kwa upande wake ameahidi kutoa shilingi milioni kumi,na mimi binafsi natoa milioni tano naamini kabisa hii itaweza kusaidia kwa kiasi fulani," amesema

Kwa upande wake Naibu Makamu Mkuu wa UDOM anayeshughulikia Mipango,Fedha na Utawala Prof.Winesta Anderson ameeleza kuwa Chuo hicho kina jumla ya wanafunzi 160 wenye mahitaji maalumu . 

Amefafanua kuwa kati yao wenye uoni hafifu ni 12,walemavu wa ngozi 28,wenye ulemavu wa kutosikia ni 70 na wengine 46 waliosalia wapo kwenye kundi la ulemavu mwingine. 

"Amesema msingi wa jumuiya ya Tanzania unamtaka kila mwananchi kupata elimu bila kujali hali yake na kwamba kwa kulitambua hilo wao kama wadau wana mpango mkakati wake ambao utakamilika 2026 ukiwa umezingatia kwa undani mahitaji ya wanafunzi hao" amesema na kuongeza;

"UDOM kupitia convocation hii tumesema tulilete hili kama kampeni ya kuwasaidia wenye uhitaji kusoma na kufika chuo Kikuu,Wizara yetu mama ya elimu imeendelea kitusapoti kwa kutupatia bajaji nane,laptop 26, mafuta na bado tunaendelea kunapambana kuhakikisha kila sehemu inapitika ili wanafunzi wetu wawe salama,"amesema

Naye Mlezi wa wanafunzi wenye mahitaji maalum chuoni hapo kupitia Kurugenzi ya huduma za wanafunzi    Florida  Chambi ameeleza kuwa ili kufanikiwa katika kampeni hiyo,kiasi cha shilingi milioni 300 kinahitajika ambacho kitakusanywa kwa kipindi cha miezi 12 kuanzia sasa. 

Amesema fedha hizo zitasaidia pia kuboresha hali ya miundombinu ya wanafunzi hao ikiwa ni pamoja na kuboresha mazingira ya vyumba wanavyolala kuendana na hali yao. 

"Tunaishukuru Serikaki na Chuo hiki kwa jitihada zake mfano, Chuo kimeendelea kuwajali wanafunzi hawa kwa kuajiri madereva maalum wanaweza kuendesha bajaji na kuwarahisishia usafiri, Chuo pia kimetoa motisha kwa wanafunzi wanaowasaidia wenye mahitaji maalum kama Shukrani kwa kuwawekea mazingir wezeshi, "amesema

Chambi amesema Chuo hicho kinajali kuwatengea wanafunzi wenye mahitaji maalumu chumba cha mtihani na kueleza kuwa kupitia kurugenzi hiyo wanaendelea kuboresha zaidi kila eneo ili kuwawezesha wanafunzi hao kusoma kwa bidii kufikia malengo yao. 

Pamoja na hayo baadhi  ya wadau wa UDOM wameweza kuchangia harambee hiyo akiwemo Mkuu wa Mkoa wa Mbeya ambaye amemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Rosemary Senyamule ambaye ameahidi milioni mbili,Ridhiwan Kikwete milioni mbili,Kituo cha uwekezaji million mbili huku Makamu mkuu wa Chuo hicho Prof.Lughano Kusiluka akiahidi kuchangia shilingi milioni mbili. 

WANASAYANSI WATAKIWA KUFIKISHA TAARIFA ZA UTAFITI KWA JAMII ILI ZIWAFIKIE WALENGWA.

November 29, 2023

 


Naibu katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Grace Maghembe amewataka wana sayansi nchini na wadau wa afya kufanya tafiti zitakazosaidia kuleta suluhisho juu ya changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta ya afya hasa changamoto kubwa ya unyanyapaa katika jamii jambo linalochangia kwa kiasi kikubwa kuzorotesha juhudi za serikali na wadau wa maendeleo katika mapambano dhidi ya VVU na UKIMWI nchini.

Hayo yamesemwa na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt.Grace Maghembe wakati akifunga Kongamano la Kitaifa la Kisayansi lililofanyika katika Hoteli ya Nashera Mkoani Morogoro ambapo wadau na wataalamu wa masuala ya sayansi na tafiti walikutana kwa siku mbili kujadiliana kwa pamoja juu ya tafiti mbalimbali walizofanya zenye lengo la kutoa mwelekeo dhidi ya Maambukizi mapya ya virusi vya UKIMWI.

‘’Serikali itaendelea kujivunia wanataaluma wetu hasa wanaofanya tafiti za ndani zitakazoleta suluhisho katika jamii hasa kwenye sekta ya afya,na hakikisheni hizo tafiti mnazofanya ziwekwe kwenye lugha rahisi ambayo kila mtanzania ataelewa nini kimeandikwa na mzisambaze hadi ngazi ya chini kabisa ya serikali za Mitaa ilikusudi kila mtanzania aweze kunufaika na hayo machapisho yenu ya kitaalamu’’.AlisemaDkt Grace Maghembe Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Afya.

Aidha aliipongeza TACAIDS kwa uratibu wa kongamano hilo lililokutanisha wataalam na kujadili masuala muhimu yenye lengo la kutatua changamoto katika sekta ya afya hasa namna ya kujikinga na maambukizi mapya ya VVU na UKIMWI,alipongeza pia uwepo wa kongamano la vijana na wadau kusaidia uwezeshaji wa makongamano hayo yenye tija kubwa kwa vijana pia ni sehemu muhimu ya kupata maoni yao ili kujua ni namna gani serikali inaweza kuwekeza katika afua zinazowalenga. Hivyo kwa kufanya kungamano la vijana wa vyuo vikuu na hili lililofanyika hapa hoteli ya Nashera kwa siku mbili ambalo limekutanisha wataalamu na wadau mbalimbali wa masuala ya kisayansi katika kujadiliana kwa pamoja juu ya tafiti zilizofanywa zinatoa taswira gani kama taifa kwenye mapambano dhidi ya VVU na UKIMWI.

Dkt Grace Maghembe amesema kongamano hili lilikuwa na lengo la kukaa kwa pamoja kwa wadau na kujitathimini tunafanya kazi serikali pamoja na wadau wamaendeleo kutekeleza afua mbalimbali lakini pia na kufanya tafiti kwa wakati ilikuona namna ya kutekeleza afua mbalimbali katika kudhibiti maambukizi ya virusivya UKIMWI.

Amongeza kuwa, kupitia kongamano hili litasaidia serikali kuona kazi zilizofanyika mambo gani yaliyofanyika vizuri na mambo gani ambayo haya kufanyika vizuri na kutuonyesha mambo gani ya kujifunza kutoka taasisi mbalimbali,Aidha kupitia majadiliano haya yatatuwezesha kuandaa sera itakayotekelezwa kwa jamii kwasababu tayari tumeshafahamu nini jamii inahitaji huko ngazi za chini na kwakuwa tayari tumeshapata taarifa za kitaalamu za kitafiti.

Aidha ameongeza kwa kusema kuwa lazima tupambane kuhakikisha ili kufikia malengo ya 20/30 lazimatuangalietumefikiawapikwenyejitihadazamapambanokuanzialeolakini pia kuna changamoto kubwa kuhusiana na changamoto ya kukabiliana maambukizi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto lazima iende kwa vitendo na amesema tumepiga hatua kubwa kwenye unyanyapaa lakini bado kuna changamoto kubwa ya unyanyapaa hadi leo watu wanaogopa kujitokeza kujitangaza kuwa anamaambukizi wa na kuwa hawako huru kuzungumza kwa familia na marafiki na waathirika wanavyokaa kimya ndio kunasababisha kuongezeka kwa maambukizi mapya jambo ambalo linahitaji tafiti za kina kuhusu suluhisho la kupambana na unyanyapaa katika Jamii.

POLISI SHINYANGA WAJIWEKA TAYARI KUKABILIANA NA UHALIFU KUELEKEA CHRISMAS NA MWAKA MPYA... BUNDUKI YAKUTWA SHULENI

November 29, 2023

 

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Janeth Magomi akionesha silaha aina ya Pistol Browning ikiwa na risasi 12 ambayo ilitelekezwa au kusahauliwa na mmiliki wake katika  moja ya shule ya Mjini Shinyanga kutokana na uzembe katika kumiliki silaha hiyo.

Na Mwandishi wetu - Malunde 1 blog

Kuelekea kipindi cha Sikukuu za Krismas na Mwaka mpya, Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga limeendelea kujiweka katika hali ya utayari ili kukabiliana na vitendo mbalimbali vya kihalifu, na kuhakisha ulinzi na Usalama wa raia na mali zao unaendelea kuimarika.

Akizungumza na vyombo vya habari leo Jumatano Novemba 29,2023 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Janeth Magomi amesema  Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga limeendelea kufanya doria na misako katika maeneo yote ya Mkoa wa Shinyanga, kuimarisha vikundi vya ulinzi shirikishi ambapo hadi sasa kuna jumla ya vikundi hai 209 vinavyoshirikiana na Jeshi la Polisi. 


"Pia tunaendelea kutoa elimu kwa watumiaji wa barabara katika msimu huu wa sikukuu ili kuimarisha usalama barabarani, na kuwapeleka mahakamani wale wote wanaovunja sheria za usalama barabarani",amesema.

 Amefafanua kuwa, kwa kipindi cha mwezi mmoja uliopita, jumia ya madereva 06 wa magari walipelekwa mahakamani kwa makosa ya usalama barabarani, madereva 6,499 wa vyombo vya moto walitozwa fine na pia madereva 03 walifungiwa leseni zao. 

Hata hivyo amesema, kwa kipindi hicho cha mwezi mmoja uliopita, hakukuwa na ajali mbaya iliyojitokeza katika mkoa wa Shinyanga.


 "Kwa upande wa mahakama, jumla ya kesi 19 ziliweza kufanikiwa ambapo kesi 03 za makosa ya kubaka zilihukumiwa kifungo cha kati ya miaka 30 hadi kifungo cha maisha, kesi 01 ya kulawiti ilihukumiwa kifungo cha maisha jela, kesi 01 ya shambulio la aibu ilihukumiwa kifungo cha miaka 20 jela na fidia ya shilingi millioni moja, kesi 03 za wizi zilihukumiwa kifungo cha mwaka 01 jela, kesi 01 ya ukatili dhidi ya mtoto ilihukumiwa kifungo cha miaka 03 jela pamoja na fine ya shilingi laki tano, pia kesi 01 ya kumtorosha mwanafunz ilihukumiwa kifungo cha miaka 30 jela",ameeleza Kamanda Magomi.

"Vilevile kesi 01 ya kughushi nyaraka ilihukumiwa kifungo cha miaka 05 jela, kesi 01 ya wizi wa mtoto ilihukumiwa kifungo cha miaka 03 jela, kesi 02 za wizi wa mifugo zlihukumiwa kifungo cha mwaka 01hadi 05 jela na pia kesi 02 za kujeruhi zilihukumiwa kifungo cha mwaka 01 hadi 05 jela. Kesi zingine 02 za wizi wa Pikipiki ziliyohukumiwa kifungo cha miaka 02 na nyingine ya wizi ilihukumiwa kifungo cha miezi 06 jela na kulipa fidia ya shilingi milioni nane na kesi 01 ya kupatikana na bangi ilihukumiwa miaka 02 jela",ameongeza.

Ameongeza kuwa, katika mafanikio ya misako na doria wamefanikiwa kukamata jumla ya gramu 2205 pamoja na kete 61 za dawa za kulevya aina ya bangi, Pikipiki 11, mifuko 24 ya Cement, Ndoo 04 na makopo 04 ya rangi za majumba, Gypsum Powder na vifaa mbalimbali vya ramli chonganishi. 

Aidha kutokana na ushirikiano mwema kati ya Polisi na Jamii, amesema wananchi waliweza kutoa taarifa ya uwepo wa silaha aina ya Pistol Browning ikiwa na risasi 12 ambayo ilitelekezwa au kusahauliwa na mmiliki wake katika moja ya shule mjini Shinyanga kutokana na uzembe katika kumiliki silaha hiyo. 

Amesema jumla ya watuhumiwa 29 walikamatwa huku baadhi yao wakifikishwa mahakamani na wengine kupewa dhamana wakisubiri upelelezi wa kesi zao kukamilika.

 "Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga linatoa wito kwa wananchi wake kufuata Sheria na kutojihusisha na vitendo vya kiuhalifu, Madereva na watumia barabara kufuata sheria za Usalama barabarani ili kuepusha ajali zisizo za lazima, na litaendelea kuchukua hatua kali za Kisheria kwa yeyote atakayejihusisha na vitendo vya uhalifu",amesema.


GPE And CAMFED Host Roundtable On Education With Tanzanian CSOs

November 29, 2023

 Dar es Salaam, 29th November 2023 - The Chair of the Board of Directors of the Global Partnership for Education (GPE), H.E. Dr. Jakaya Mrisho Kikwete, Retired President of the United Republic of Tanzania, along with GPE’s Chief Executive Officer, Ms. Laura Frigenti, are set to participate in a significant roundtable discussion today at the Campaign for Female Education (CAMFED) Tanzania offices in Dar es Salaam.


According to Ms. Anna Sawaki, CAMFED Tanzania’s Director of Programs and Partnership, the primary objective of the roundtable is to collectively emphasise the importance of prioritising education on the political agenda.

Additionally, she said, the event aims to recognise the pivotal role of Civil Society Organisations (CSOs) in advocating for education and actively contributing to policy dialogue within local education groups.

“The roundtable will also provide an opportunity for CSO representatives to share their successful practices and experiences in supporting the transformation of education systems”, Ms Sawaki explained.

Among the CSOs expected to attend the roundtable are HakiElimu, PESTALOZZI, Shule Direct, UWEZO, Ubongo Kids, Lyra in Africa, World Vision, Binti Salha Foundation, TEN/MET, TEM/MET, CAMFED, CAMFED Tanzania, Transforming Life Tanzania, and Gender Networking (TGNP).

The Global Partnership for Education (GPE) is the largest global fund exclusively dedicated to reshaping education in lower-income countries. Operating as a unique, multi-stakeholder partnership, GPE works towards delivering quality education to ensure that every child, regardless of gender, has access to hope, opportunity, and agency.

For the past two decades, GPE has been actively disbursing funds and providing support to develop robust and resilient education systems in countries marked by extreme poverty or conflict. The focus is on enabling more children, particularly girls, to receive the education necessary for personal growth and contribution to building a more prosperous and sustainable world.

GPE's distinctive model has played a pivotal role in helping partner countries make significant strides in enhancing access, learning outcomes, and equity, resulting in improved educational opportunities for millions of boys and girls.

On the other hand, CAMFED, a pan-African movement, is leading a revolutionary approach to delivering girls' education. Through a gold-standard system of accountability to the young people and communities they serve, CAMFED has established a model that significantly improves the prospects of girls becoming independent and influential women.

CAMFED's work is driven at the grassroots level by local committees and teams comprising graduates, teachers, parents, government officials, and other volunteers who dedicate their time and expertise to ensure more girls successfully complete their education. The organisation’s governance structures include the boards of each national entity.

The roundtable represents a significant collaboration between GPE and CAMFED, bringing together key stakeholders and CSOs to reinforce the collective commitment to advancing education, particularly in regions facing the most pressing needs. This collaborative effort aligns with GPE's mission of transforming education systems and CAMFED's dedication to revolutionising girls' education across Africa.

The Chair of the Board of Directors of the Global Partnership for Education (GPE), H.E. Dr. Jakaya Mrisho Kikwete, Retired President of the United Republic of Tanzania, along with GPE’s Chief Executive Officer, Ms. Laura Frigenti, participate in a roundtable discussion with CSOs today at the Campaign for Female Education (CAMFED) Tanzania offices in Dar es Salaam.


The Chair of the Board of Directors of the Global Partnership for Education (GPE), H.E. Dr. Jakaya Mrisho Kikwete, Retired President of the United Republic of Tanzania, along with GPE’s Chief Executive Officer, Ms. Laura Frigenti, in a group photo with members of CSOs after their roundtable today at the Campaign for Female Education (CAMFED) Tanzania offices in Dar es Salaam.

FAO LA HUDUMA YA UTENGEMAO KUONGEZA FARAJA: PROFESA NDALICHAKO

November 29, 2023

 

 NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID

SERIKALI kupitia Mfuko wa Fidia kwa Wafanmyakazi (WCF) imetangaza Fao jipya la Huduma ya Utengemao wa Kijamii (Social Rehabilitation) kwa wafanyakazi wanaopata ulemavu na magonjwa yatokanayo na kazi na hivyo litawaongezea faraja, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Mhe. Profesa Joyce Ndalichako, amesema.

Akizungumza jijini Dar es Salaam,  Novemba 29, 2023, alipokutana na wanufaika wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Watu wenye Ulemavu Duniani inayotarajiwa kufanyika kitaifa jijini Dodoma, Desemba 2, 2023. 

Profesa Ndalichako mesema, “Ndugu zangu hivi karibuni tutaanza kutoa Fao la Huduma ya Utengamao wa Kijamii na kutoa mafunzo ya kujenga ujuzi kwa wafanyakazi wanaopata ulemavu wakiwa kazini na aina ya ujuzi tutakaotoa utategemea uhitaji.” Alisema

Alisema lengo la Serikali ni kumpatia mfanyakazi ujuzi ambao utaendana na hali ya ulemavu wake, mfano alikuwa dereva na akapata ajali iliyopelekea ulemavu wa miguu, huyu anaweza kubadilisha ujuzi na kusomea kazi nyingine. 

Sambamba na kuwajengea ujuzi, fao hilo pia litatoa fursa ya kumjengea miundombinu inayoendana na hali yake, na hivyo kumuwezesha kumudu maisha katika mazingira anayoishi.” Alifafanua Profesa Ndalichako.

Kwa upande wao, wanufaika wa WCF wameishukuru Serikali kwa huduma wanazopokea kutoka katika Mfuko huo licha ya kupata ulemavu na wengine kuondokewa na wapendwa wao.

“Naomba kuhamasisha waajiri kuweza kuwachangia wafanyakazi wao, kwani viwango vya uchangiaji ni vidogo, tunaishukuru Serikali imepunguza viwango vya uchangiaji hadi kufikia asilimia 0.5” Alisema Norbert Tesha, ambaye amepata ulemavu wa kudumu baada ya kupata ajali akiwa kazini mwaka 2016.

“Hatuwezi kujua kesho yetu, lakini kama kuna misingi mizuri iliyowekwa leo, basi kesho yetu itakuwa njema, kila mtu ni mlemavu mtarajiwa.” Alisema, Bw. Tesha.

Mnufaika mwingine Bi. Emmaculet Nhigula, ambaye alimpoteza mumewe kwa ajali ya gari, amesema, “Mimi na watoto wangu wanne, tunanufaika sana na Mfuko huu, rafiki yetu kwa sasa ni WCF, huwa nikipita kwenye barabra hii na kuliona jengo lenu, ninasema hawa ni rafiki zangu wanaotembea na mimi nyakazi ngumu." Alisema

Alisema yale mafao ya kila mwezi yamekuwa na msaada mkubwa sana, yamesaidia kusomesha watoto wangu na sikuweza kuwahamisha kutoka shule walizokuwa wanasoma kabla ya kufariki baba yao.” Alisema Bi. Emaculate. 

Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Watu Wenye Ulemavu, yanalenga kuwahamasisha viongozi wa taasisi za kibiashara Duniani kutambua mchango maridhawa wa watu wenye ulemavu.

Kwamujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO), kwasasa inakadiriwa kuwa watu bilioni 1.3 duniani wanaishi na changamoto ya ulemavu, hii ni sawa na asilimia 16% ya Watu wote duniani.

Kauli mbiu ya maadhimisho ya mwaka huu ni “ Tuungane katika hatua za Kuokoa na kufikia Malengo ya SDGs kwa Watu wenye Ulemavu”.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Mhe. Profesa Joyce Ndalichako (wapili kushoto) akiwa na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Dkt. John Mduma (wakwanza kushoto), wakati akizungumza na wanufaika wa Fidia inayotolewa na WCF, kwenye Ofisi za Mfuko huo, jijini Dar es Salaam. 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Mhe. Profesa Joyce Ndalichako akizunguzma kwenye mkutano na waandishi w ahabari jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Mhe. Profesa Joyce Ndalichako, akizungumza kwenye mkutano na waandishi w ahabari jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa WCF, Dkt. John Mduma.
 Mkurugenzi Mkuu wa WCF, Dkt. John Mduma, akizungumza mwanzoni mwa mkutano huo.
Bw. Norbert Tesha (kushoto), Mnufaika wa WCF, akitoa ushuhuda mbele ya waandishi wa habari jinsi anavyonufaika baada ya kupata ulemavu wa kudumu kufuatia kuumia katika ajali iliyotokana na kazi
Bw. Kelvin Cameroon,  mnufaika wa WCF, akitoa ushuhuda mbele ya waandishi wa habari jinsi anavyonufaika baada ya kupata ulemavu wa kudumu kufuatia kuumia katika ajali iliyotokana na kazi
Bi. Emmaculat Nzigula, Mtegemezi anayenufaika na mafao yanayotolewa na WCF baada ya kumpoteza mumewe aliyefariki katika ajali ya gari wakati akitekeleza majukumu ya mwajiri wake.
Profesa Ndalichako, akisalimiana na mmoja wa wategemezi wanaonufaika na mafao ya Fidia. Kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa WCF.
Profesa Ndalichako, akizungumza na waandishi wa habari kwenye ofisi za WCF jijini Dar es Salaam. Katikati ni Mkurugenzi Mkuu wa WCF, Dkt. John Mduma na Bw. Rasheed Maftah, Mkurugenzi wa Kitengo cha Huduma kwa  Wenye Ulemavu, Ofisi ya Waziri Mkuu.

Picha ya pamoja.