WANASAYANSI WATAKIWA KUFIKISHA TAARIFA ZA UTAFITI KWA JAMII ILI ZIWAFIKIE WALENGWA.
POLISI SHINYANGA WAJIWEKA TAYARI KUKABILIANA NA UHALIFU KUELEKEA CHRISMAS NA MWAKA MPYA... BUNDUKI YAKUTWA SHULENI
Na Mwandishi wetu - Malunde 1 blog
Kuelekea kipindi cha Sikukuu za Krismas na Mwaka mpya, Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga limeendelea kujiweka katika hali ya utayari ili kukabiliana na vitendo mbalimbali vya kihalifu, na kuhakisha ulinzi na Usalama wa raia na mali zao unaendelea kuimarika.
Akizungumza na vyombo vya habari leo Jumatano Novemba 29,2023 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Janeth Magomi amesema Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga limeendelea kufanya doria na misako katika maeneo yote ya Mkoa wa Shinyanga, kuimarisha vikundi vya ulinzi shirikishi ambapo hadi sasa kuna jumla ya vikundi hai 209 vinavyoshirikiana na Jeshi la Polisi.
"Pia tunaendelea kutoa elimu kwa watumiaji wa barabara katika msimu huu wa sikukuu ili kuimarisha usalama barabarani, na kuwapeleka mahakamani wale wote wanaovunja sheria za usalama barabarani",amesema.
Amefafanua kuwa, kwa kipindi cha mwezi mmoja uliopita, jumia ya madereva 06 wa magari walipelekwa mahakamani kwa makosa ya usalama barabarani, madereva 6,499 wa vyombo vya moto walitozwa fine na pia madereva 03 walifungiwa leseni zao.
Hata hivyo amesema, kwa kipindi hicho cha mwezi mmoja uliopita, hakukuwa na ajali mbaya iliyojitokeza katika mkoa wa Shinyanga.
"Kwa upande wa mahakama, jumla ya kesi 19 ziliweza kufanikiwa ambapo kesi 03 za makosa ya kubaka zilihukumiwa kifungo cha kati ya miaka 30 hadi kifungo cha maisha, kesi 01 ya kulawiti ilihukumiwa kifungo cha maisha jela, kesi 01 ya shambulio la aibu ilihukumiwa kifungo cha miaka 20 jela na fidia ya shilingi millioni moja, kesi 03 za wizi zilihukumiwa kifungo cha mwaka 01 jela, kesi 01 ya ukatili dhidi ya mtoto ilihukumiwa kifungo cha miaka 03 jela pamoja na fine ya shilingi laki tano, pia kesi 01 ya kumtorosha mwanafunz ilihukumiwa kifungo cha miaka 30 jela",ameeleza Kamanda Magomi.
"Vilevile kesi 01 ya kughushi nyaraka ilihukumiwa kifungo cha miaka 05 jela, kesi 01 ya wizi wa mtoto ilihukumiwa kifungo cha miaka 03 jela, kesi 02 za wizi wa mifugo zlihukumiwa kifungo cha mwaka 01hadi 05 jela na pia kesi 02 za kujeruhi zilihukumiwa kifungo cha mwaka 01 hadi 05 jela. Kesi zingine 02 za wizi wa Pikipiki ziliyohukumiwa kifungo cha miaka 02 na nyingine ya wizi ilihukumiwa kifungo cha miezi 06 jela na kulipa fidia ya shilingi milioni nane na kesi 01 ya kupatikana na bangi ilihukumiwa miaka 02 jela",ameongeza.
Ameongeza kuwa, katika mafanikio ya misako na doria wamefanikiwa kukamata jumla ya gramu 2205 pamoja na kete 61 za dawa za kulevya aina ya bangi, Pikipiki 11, mifuko 24 ya Cement, Ndoo 04 na makopo 04 ya rangi za majumba, Gypsum Powder na vifaa mbalimbali vya ramli chonganishi.
Aidha kutokana na ushirikiano mwema kati ya Polisi na Jamii, amesema wananchi waliweza kutoa taarifa ya uwepo wa silaha aina ya Pistol Browning ikiwa na risasi 12 ambayo ilitelekezwa au kusahauliwa na mmiliki wake katika moja ya shule mjini Shinyanga kutokana na uzembe katika kumiliki silaha hiyo.
Amesema jumla ya watuhumiwa 29 walikamatwa huku baadhi yao wakifikishwa mahakamani na wengine kupewa dhamana wakisubiri upelelezi wa kesi zao kukamilika.
"Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga linatoa wito kwa wananchi wake kufuata Sheria na kutojihusisha na vitendo vya kiuhalifu, Madereva na watumia barabara kufuata sheria za Usalama barabarani ili kuepusha ajali zisizo za lazima, na litaendelea kuchukua hatua kali za Kisheria kwa yeyote atakayejihusisha na vitendo vya uhalifu",amesema.
GPE And CAMFED Host Roundtable On Education With Tanzanian CSOs
Dar es Salaam, 29th November 2023 - The Chair of the Board of Directors of the Global Partnership for Education (GPE), H.E. Dr. Jakaya Mrisho Kikwete, Retired President of the United Republic of Tanzania, along with GPE’s Chief Executive Officer, Ms. Laura Frigenti, are set to participate in a significant roundtable discussion today at the Campaign for Female Education (CAMFED) Tanzania offices in Dar es Salaam.
According to Ms. Anna Sawaki, CAMFED Tanzania’s Director of Programs and Partnership, the primary objective of the roundtable is to collectively emphasise the importance of prioritising education on the political agenda.
Additionally, she said, the event aims to recognise the pivotal role of Civil Society Organisations (CSOs) in advocating for education and actively contributing to policy dialogue within local education groups.
“The roundtable will also provide an opportunity for CSO representatives to share their successful practices and experiences in supporting the transformation of education systems”, Ms Sawaki explained.
Among the CSOs expected to attend the roundtable are HakiElimu, PESTALOZZI, Shule Direct, UWEZO, Ubongo Kids, Lyra in Africa, World Vision, Binti Salha Foundation, TEN/MET, TEM/MET, CAMFED, CAMFED Tanzania, Transforming Life Tanzania, and Gender Networking (TGNP).
The Global Partnership for Education (GPE) is the largest global fund exclusively dedicated to reshaping education in lower-income countries. Operating as a unique, multi-stakeholder partnership, GPE works towards delivering quality education to ensure that every child, regardless of gender, has access to hope, opportunity, and agency.
For the past two decades, GPE has been actively disbursing funds and providing support to develop robust and resilient education systems in countries marked by extreme poverty or conflict. The focus is on enabling more children, particularly girls, to receive the education necessary for personal growth and contribution to building a more prosperous and sustainable world.
GPE's distinctive model has played a pivotal role in helping partner countries make significant strides in enhancing access, learning outcomes, and equity, resulting in improved educational opportunities for millions of boys and girls.
On the other hand, CAMFED, a pan-African movement, is leading a revolutionary approach to delivering girls' education. Through a gold-standard system of accountability to the young people and communities they serve, CAMFED has established a model that significantly improves the prospects of girls becoming independent and influential women.
CAMFED's work is driven at the grassroots level by local committees and teams comprising graduates, teachers, parents, government officials, and other volunteers who dedicate their time and expertise to ensure more girls successfully complete their education. The organisation’s governance structures include the boards of each national entity.
The roundtable represents a significant collaboration between GPE and CAMFED, bringing together key stakeholders and CSOs to reinforce the collective commitment to advancing education, particularly in regions facing the most pressing needs. This collaborative effort aligns with GPE's mission of transforming education systems and CAMFED's dedication to revolutionising girls' education across Africa.
FAO LA HUDUMA YA UTENGEMAO KUONGEZA FARAJA: PROFESA NDALICHAKO
NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID
SERIKALI
kupitia Mfuko wa Fidia kwa Wafanmyakazi (WCF) imetangaza Fao jipya la Huduma ya
Utengemao wa Kijamii (Social Rehabilitation) kwa wafanyakazi wanaopata ulemavu na magonjwa
yatokanayo na kazi na hivyo litawaongezea faraja, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na
Wenye Ulemavu), Mhe. Profesa Joyce Ndalichako, amesema.
Akizungumza jijini Dar es Salaam, Novemba 29, 2023, alipokutana na wanufaika wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Watu wenye Ulemavu Duniani inayotarajiwa kufanyika kitaifa jijini Dodoma, Desemba 2, 2023.
Profesa Ndalichako mesema, “Ndugu zangu hivi karibuni tutaanza kutoa Fao la Huduma ya Utengamao wa Kijamii na kutoa mafunzo ya kujenga ujuzi kwa wafanyakazi wanaopata ulemavu wakiwa kazini na aina ya ujuzi tutakaotoa utategemea uhitaji.” Alisema
Alisema
lengo la Serikali ni kumpatia mfanyakazi ujuzi ambao utaendana na hali ya ulemavu wake,
mfano alikuwa dereva na akapata ajali iliyopelekea ulemavu wa miguu, huyu anaweza kubadilisha ujuzi na kusomea kazi nyingine.
Sambamba
na kuwajengea ujuzi, fao hilo pia litatoa fursa ya kumjengea miundombinu inayoendana
na hali yake, na hivyo kumuwezesha kumudu maisha katika mazingira
anayoishi.” Alifafanua Profesa Ndalichako.
Kwa
upande wao, wanufaika wa WCF wameishukuru Serikali kwa huduma wanazopokea
kutoka katika Mfuko huo licha ya kupata ulemavu na wengine kuondokewa na
wapendwa wao.
“Naomba
kuhamasisha waajiri kuweza kuwachangia wafanyakazi wao, kwani viwango vya
uchangiaji ni vidogo, tunaishukuru Serikali imepunguza viwango vya uchangiaji
hadi kufikia asilimia 0.5” Alisema Norbert Tesha, ambaye
amepata ulemavu wa kudumu baada ya kupata ajali akiwa kazini mwaka 2016.
“Hatuwezi
kujua kesho yetu, lakini kama kuna misingi mizuri iliyowekwa leo, basi kesho
yetu itakuwa njema, kila mtu ni mlemavu mtarajiwa.” Alisema, Bw. Tesha.
Mnufaika mwingine Bi. Emmaculet Nhigula, ambaye alimpoteza mumewe kwa ajali ya gari, amesema, “Mimi na watoto wangu wanne, tunanufaika sana na Mfuko huu, rafiki yetu kwa sasa ni WCF, huwa nikipita kwenye barabra hii na kuliona jengo lenu, ninasema hawa ni rafiki zangu wanaotembea na mimi nyakazi ngumu." Alisema
Alisema yale mafao ya kila mwezi yamekuwa na msaada
mkubwa sana, yamesaidia kusomesha watoto wangu na sikuweza kuwahamisha kutoka
shule walizokuwa wanasoma kabla ya kufariki baba yao.” Alisema Bi. Emaculate.
Maadhimisho
ya Siku ya Kimataifa ya Watu Wenye Ulemavu, yanalenga kuwahamasisha viongozi wa
taasisi za kibiashara Duniani kutambua mchango maridhawa wa watu wenye ulemavu.
Kwamujibu
wa Shirika la Afya Duniani (WHO), kwasasa inakadiriwa kuwa watu bilioni 1.3
duniani wanaishi na changamoto ya ulemavu, hii ni sawa na asilimia 16% ya Watu
wote duniani.
Kauli
mbiu ya maadhimisho ya mwaka huu ni “ Tuungane katika hatua za Kuokoa na
kufikia Malengo ya SDGs kwa Watu wenye Ulemavu”.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu
(Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Mhe. Profesa Joyce Ndalichako (wapili
kushoto) akiwa na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Dkt.
John Mduma (wakwanza kushoto), wakati akizungumza na wanufaika wa Fidia
inayotolewa na WCF, kwenye Ofisi za Mfuko huo, jijini Dar es Salaam.
Picha ya pamoja.