FASTJET SEEKS ZIMBABWE DOMESTIC ROUTES

FASTJET SEEKS ZIMBABWE DOMESTIC ROUTES

June 21, 2015
IMG_3933
Head of Marketing, Fastjet, PLC, Ms. Jai Gilbert, speaking to the Tanzanian Journalists who have been sponsored by Fastjet Airline to attend the 8th edition of the Sanganai/Hlanganani–World Tourism Expo which was held in Harare at the Rainbow Towers Hotel. Standing at the centre is Mpilo Nyathi a representative from Fastjet branch in Harare, Zimbabwe.(All photos by Zainul Mzige of modewjiblog).
IMG_3926
Head of Marketing Fastjet, PLC, Ms. Jai Gilbert, during the interview Journalists.
By Modewjiblog team
A low cost airline operating in Tanzania, Fastjet, is trying to get a license to operate Zimbabwe domestic routes.
Speaking with Tanzania journalist here in Harare, Zimbabwe, Head of Marketing Fastjet, PLC, Ms. Jai Gilbert said discussions are in advanced stage and in four months they expect to be given a license.
She said they are looking to operate Victoria Falls, Johannesburg, Harare and Bulawayo routes.
Fastjet which started business in Tanzania 2012 is now flying four times to Harare, Zimbabwe via Lusaka, Zambia.
In Tanzania, this low cost airline operates in main cities of Dar es salaam, Mwanza, Arusha. Mbeya and Moshi. On international routes Fastjet is operating Johannesburg, Entebbe, Harare and Lusaka and now are seeking Nairobi route.
Since they have started operating Dar, Lusaka, Harare route the response is terrific gunning 70 percent of the capacity. They normally fly from Dar es salaam on Monday, Wednesday, Friday and Sunday.
She said most of the passengers are business people and some of them are drivers who come to Dar es Salaam to pick their car and drive back.
Speaking to Modewjiblog Executive Director, Destination Marketing of Zimbabwe Tourism Authority (ZTA), and Mr. Jeffrey Manjengwa said Fastjet’s entry into Zimbabwe helped the country to reach another market segment that has been ignored for so long.
“The Government of Zimbabwe is thrilled with the coming of Fastjet and it is bringing it’s affordable price, reliable and safe service to the people of Zimbabwe,” Manjengwa said.
Mr. Manjengwa added that the initiative would go a long way in increasing connectivity and would also improve trade and tourism between Zimbabwe and Tanzania.
IMG_3915
A Tanzanian Journalist who writes for Daily News Paper, Ms. Mariam Said, is asking question during the Interview session with Head of Marketing Fastjet, PLC, Ms. Jai Gilbert, at the 8th edition of the Sanganai/Hlanganani–World Tourism Expo which was held in Harare at the Rainbow Towers Hotel.
Fastjet that started operating in the country in 2012 carried 1.2 million passengers, 38 percent first time flyers by last year; currently has three aircraft and expects to have 2 more by the end of this year.
Ms. Gilbert thanked the government of Tanzania for helping Fastjet to become number one.
Fast jet has sponsored 5 Tanzanian journalists to attend the 8th edition of the Sanganai/ Hlanganani World tourism Expo held recently. Those journalists are from Daily News, The African, The Guardian, East Africa Business Week and Modewjiblog.
The journalists have been invited by Zimbabwe Tourism Authority (ZTA) to attend the 8th edition of the Sanganai/Hlanganani–World Tourism Expo which was held from 18 – 20 June 2015 at the Rainbow Towers Hotel in Harare, Zimbabwe.
IMG_3952
Head of Marketing Fastjet, PLC, Ms Jai Gilbert, listening attentively to the guests who visited Fastjet booth during the 8th edition of the Sanganai/Hlanganani–World Tourism Expo 2015 which was held in Harare at Rainbow Towers Hotel.
IMG_4378
Tanzanian Journalist on their way back to Dar es Salaam inside the Fastjet Tanzania Africa's trusted low cost airline (Airbus FN0205) which is taking route Harare, Zinbabwe via Lusaka, Zambia. From Left is Mr. Timothy Kitundu (East Africa Business Week), Mr. Justin Damian (The African) and Frank Aman (The Guardian).
IMG_4388
Ms. Mariam Said who writes for Daily News Paper poses for a selfie with Modewjiblog Operations Manager, Zainul Mzige, inside the Fastjet Tanzania Airline returning back to Dar es Salaam after attending the 8th edition of the Sanganai/Hlanganani–World Tourism Expo 2015 which was held from 18 – 20 June 2015 in Harare at Rainbow Towers Hotel and the trip was sponsored by Fastjet Tanzania Airline. IMG_4444
Fastjet Cabin Crew, Maureen Mwaisaka, serving the passenger.
MAONESHO YA UTALII YA SANGANAI/HLANGANANI–(WORLD TOURISM EXPO) ZIMBABWE YAFUMBUA MACHO WATANZANIA

MAONESHO YA UTALII YA SANGANAI/HLANGANANI–(WORLD TOURISM EXPO) ZIMBABWE YAFUMBUA MACHO WATANZANIA

June 21, 2015
IMG_4145
Pichani juu na chini ni Afisa Habari Mwandamizi wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Esther Solomon (kushoto) akitoa maelezo ya shughuli mbalimbali za utalii na vivutio vyake nchini Tanzania kwa baadhi ya wanafunzi wa vyuo mbalimbali vikiwemo vya utalii nchini Zimbabwe waliofika katika banda la Tanzania kwenye maonyesho ya nane ya Kimataifa ya Utalii Sanganai/Hlanganani–(World Tourism Expo) kupata taarifa mbalimbali za vivutio vya utalii wa Tanzania yaliyomalizika jana jijini Harare katika ukumbi wa hoteli ya Rainbow Towers.(Picha zote na Zainul Mzige wa modewjiblog)
IMG_4137 IMG_4168
Afisa Habari Mwandamizi wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Esther Solomon (kulia) akibadilishana mawazo na wananfunzi wa Belvedere Technical Teachers College nchini Zimbabwe, Francisca Chipuriro (kushoto) na Natalie Takavarasha (katikati) wakati walipotembelea banda la Tanzania kwa ajili ya kupata taarifa mbalimbali za utalii wa Tanzania na vivutio vyake siku ya ufunguzi rasmi wa maonyesho hayo yaliyomalizika juzi jijini Harare katika hoteli ya Rainbow Towers.
IMG_4185
Wageni mbalimbali waliovutiwa na vivutio vya utalii nchini Tanzania wakiendelea kumiminika katika banda la Tanzania na kupata taarifa mbalimbali kutoka kwa Afisa Habari Mwandamizi wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Esther Solomon (kulia) ambapo hivi sasa Shirika la ndege la Fastjet limeanza safari zake jijini Harare kupitia Lusaka hadi Dar es Salaam kwa gharama nafuu kabisa itakayowezesha wananchi wa Zimbabwe kufanya safari za Tanzania kwa gharama nafuu kabisa.
IMG_4229
Meneja Masoko na Tehama wa kampuni ya Best Northern Tours and safaris nchini Tanzania, Mary Joel akitoa maelezo ya shughuli mbalimbali za utalii zinazofanywa na kampuni yake kwa wageni waliofika katika banda la Tanzania wakati wa maonyesho hayo yaliyomalizika juzi jijini Harare.
IMG_4241
Mkurugenzi wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Bw. Samwel Diah (wa pili kulia) akitoa maelezo yaliyomo kwenye vipeperushi vyenye taarifa mbalimbali za vivutio vya utalii nchini Tanzania kwa wageni waliotembelea banda la Tanzania kwenye maonyesho nane ya utalii ya Sanganai/Hlanganani–(World Tourism Expo) jijini Harare.
IMG_4191
Wakala wa utalii kutoka kampuni ya Cordial Tours and Travel ya nchini Tanzania, Joseph Waryoba (kulia) akipata picha ya kumbukumbu na Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Utalii nchini Zambia, Felix Chaila aliyembelea banda la Tanzania wakati wa maonesho ya siku tatu ya utalii ya Sanganai/Hlanganani–(World Tourism Expo) jijini Harare katika hoteli ya Rainbow Towers ambayo yamemalizika juzi.
IMG_4195
Wakala wa utalii kutoka kampuni ya Cordial Tours and Travel nchini Tanzania, Joseph Waryoba katika picha ya pamoja na Mkurugenzi wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Bw. Samwel Diah ambaye pia ni Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya Tanzania Travel Company ambayo pia imeshiriki maonyesho ya utalii nane ya Sanganai/Hlanganani–(World Tourism Expo) jijini Harare.
IMG_4205
Timu kutoka Tanzania ambayo imeshiriki maonyesho ya utalii nane ya Sanganai/Hlanganani–(World Tourism Expo) jijini Harare ikiongozwa na Afisa Habari Mwandamizi wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Esther Solomon (wa pili kulia). Kutoka kushoto ni Wakala wa utalii kutoka kampuni ya Cordial Tours and Travel nchini Tanzania, Joseph Waryoba, Meneja Masoko na Tehama wa kampuni ya Best Northern Tours and safaris nchini Tanzania, Mary Joel pamoja na Mkurugenzi wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Bw. Samwel Diah (kulia).
Na Modewjiblog team, Harare
TIMU ya watanzania walioenda kuhudhuria maonesho ya utalii nchini Zimbabwe wamesema Tanzania ina nafasi kubwa ya kujifunza uendeshaji wa sekta ya utalii.
Walisema katika ziara yao hiyo wamegundua kwamba Wazimbabwe kuanzia wanapompokea mgeni hadi anapofika hotelini wanaonesha kujali hali ambayo mgeni hawezi kusahau hata kidogo.
Aidha amesema kwamba hata mipangilio ya kwenda kwenye vivutio inafanyika katika hali ambayo huwezi kusahau hata kidogo.
Kutokana na mazingira hayo, wamesema Tanzania ina nafasi kubwa ya kujifunza namna ya kupokea na kuishi na wageni na kuwatengenezea taswira ambayo hawatakaa wakisahau.
Hayo yamesemwa na Ofisa Habari Mwandamizi wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Esther Solomon katika mahojiano maalum na mtandao wa habari wa modewjiblog yaliyofanyika mjini Harare siku ya ufunguzi rasmi wa maonesho ya siku tatu ya utalii ya Sanganai/Hlanganani–(World Tourism Expo) jijini Harare katika hoteli ya Rainbow Towers jijini Harare.
Solomon amesema ingawa hali ya Tanzania si mbaya, watendaji katika viwanja vya ndege na mahotelini wanaweza kuangalia namna Wazimbabwe wanavyojali kazi zao na tabasamu zao nyakati zote kwa wageni .
“Si kwamba kwetu kuna shida lakini unaona watu wanavyojituma hapa” alisema Esther Solomon na kuongeza kuwa aliona jinsi walivyojipanga vizuri na wafanyakazi walikuwa na uelewa wa hali ya juu.
Esther aliongoza kundi la watu watano wa Kitanzania walioalikwa na mamlaka ya utalii Zimbabwe (ZTA) kuhudhuria maonesho hayo.Tanzania iliweka banda lake pia katika maonesho hayo ya siku tatu yaliyomalizika juzi.
Makampuni ya mawakala wa utalii aliyoambatana nayo katika safari hiyo ni pamoja na Tanzania Travel Company, Cordial Tours and Travel, Mberesero Tented Camp na Best Northern Tours and safaris .
Alisema safari yao Zimbabwe pamoja na ushiriki wao katika maonesho pia walifika katika maeneo mbalimbali ya kitalii nchini yakiwemo maporomoko ya Victoria.
Aidha walipewa nafasi ya kukagua sehemu za malazi kwa ajili ya wageni.
Alisema katika maonesho hayo wamefanikiwa kupata wageni wengi wanaoulizia namna ya kufika Tanzania na pia ushirikiano wa makampuni katika sekta ya utalii.
“ Watu wengi wamekuja kututembelea. Na wengi ni watu weusi. Mwamko wao wa kutembelea vivutio ni mkubwa.” Alisema Esther na kuongeza kuwa wamebaini kwamba ipo haja ya watanzania kuhimizwa kutembelea vivutio kwani hata nchini Zimbabwe wanaotembelea vivutio ni wananchi wenyewe.
Alisema wengi waliofika katika banda la Tanzania waliulizia namna ya kufika visiwa vya Zanzibar na pia mbuga za Tanzania.
Aidha mawakala wengi waliulizia namna ya kushirikiana na Tanzania katika kuimarisha utalii katika bara la Afrika.
Asilimia 80 ya watalii nchini Zimbabwe wanatoka bara la Afrika na waliobaki ndio wanatoka nje ya bara hili.

MFUKO WA PESHNI WA PSPF WATOA ELIMU KWA MADEREVA TAXI WA WILAYA YA ILALA NA MADEREVA KUJIUNGA NA MPANGO WA HIARI

June 21, 2015
Afisa Masoko wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Ismail Juma  akitoa maelezo ya kina kuhusu faida na huduma zitolewazo na Mfuko wa Pensheni wa PSPF hasa katika uchangiaji wa hiari ambapo mtu yeyote anaweza kujionga alipokuwa akiongea na madereva wa taxi wa wilaya Ilala jijini Dar 
 Mkuu wa Kitengo Cha Elimu wa Jeshi la Polisi, Kikosi cha Usalama Barabarani Makao Makuu, Abel Swai akizungumza na madereva wa taxi wa wilaya ya Ilala(Hawapo pichani) kuhusu kutii sheria za barabarani na kuwasisitiza kujiunga na mfuko wa Peisheni wa PSPF.
 Mkaguzi Msaidizi wa Jeshi la Polisi kanda maalum ya Dar es Salaam, Josephat Sylvery Tirumanywa azungumza jambo na madereva wa taxi wakati wa mkutano wao uliofanyika katika shule ya Sekondari ya Tambaza jijini Dar
Afisa Masoko wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Abdalla Mohamed akijibu maswali ya baadhi ya madereva 
 
 
 
 Madereva wa Taxi wa wilaya ya Ilala wakiuliza maswali kwa Maofisa  wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF wakati wa mkutano wao
 Afisa Masoko wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Abdalla Mohamed akiwaelekeza madereva wa Taxi jinsi yakujiunga na mfuko huo
Afisa wa mfuko wa pensheni David.M.Mgaka akimpa maelezo mmoja wa madereva wa Taxi wilaya ya Ilala aliyeamua kujiunga na mfuko wa Peisheni wa PSPF
 Afisa Masoko wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Abdalla Mohamed akimtolea ufafanuzi kuhusu faida za mfuko wa PSPF wakati wa mkutano wao uliofanyika katika shule ya Sekondari ya Tambaza jijini Dar

Afisa wa mfuko wa pensheni David.M.Mgaka(kushoto) akimuonesha mmoja wa madereva ili aweke alama ya dole gumba kwenye fomu za Uchangiaji wa Hiari
Afisa wa mfuko wa pensheni David.M.Mgaka akielezea jinsi ya ujazaji fomu za Uchangiaji wa Hiari kwa baadhi ya madereva waliovutiwa kujiunga na mfuko wa Peisheni wa PSPF
Baadhi ya Madreva wa Taxi wilaya ya Ilala wakiendelea kufuatilia kkwenye mkutano wao



Na Mwandishi Wetu
Madereva taxi katika wilaya ya Ilala jijini dar es salaam wapokea elimu kutoka kwa mfuko wa pensheni wa PSPF na kuweza kujiunga na mfuko huo ili kuhakikisha wanawekeza katika mfuko huo kwa manufaa yao hapo baadae kutokana na kazi zao wanazozifanya kila siku za udereva kuwa ni kazi za kawaida na kuona kuwa Pspf ndio kimbilio kwa madereva hao

Akizungumza wakati wa mkutano huo Afisa masoko wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF Bw. Ismail Juma amesema wameamua kuungana na madeeva Tax ili kuweza kuwapa elimu katika suala la kuwekeza na kufaidika na mafao mbalimbali yanayo tolewa na PSPF kwani Pindi watakapo jiunga na mfuko huo wataona matunda mengi hasa kutokana na kuwa ni watu ambao wanategemewa na familia hivyo kama Pspf wana mafao ambayo wataweza kujikwamua kama mafao ambayo wanaweza kuwasomesha watoto,vilevile fao la uzazi hata fau la nyumba pia ujiungapo na mfuko huu utafaidika na wala hauto jutia 

Mkuu wa kitengo cha elimu wa jeshi la polisi,kikosi cha usalama barabarani makao makuu , Abel Swai wakati akitoa elimu ya usalama barabarani amewaasa madereva wote nchini hususani kwa madereva walio weza kufika katika mkutano huo wa madereva tax kuweza kuwekeza katika mifuko ya jamii ni jambo muhimu hasa ukizingatia kwa hali ya sasa maisha kuwa ya kawaida na uchumi wanchi yetu kuporomoka amewaomba madereva kutumia fursa zinazo tolewa na mfuko wa pensheni wa PSPF ili wawe na akiba ya mafao yao pindi kazi zinapo isha na hata kuweza kufaidika na mambo mbalimbali katika mfuko huo

Pia mkaguzi msaidizi wa polisi kanda maalumu ya dare s salaam Josephat Sylvery Tirumanywa amewasisitiza madereva kutii sheria za barabarani maana wamepewa dhamana ya kuwasafirisha abiria kwa amani na upendo ,hivyo kati ya jeshi la polisi na madereva husaidiana kufanya kazi kwa umoja na hivyo kuweka mahusiano mazuri katika kufanikisha nchi yetu iajengwa na sisi watanzania kwa kuendeleza upendo na amani pindi tuwapo barabarani,aliongeza kuwapa shukrani mfuko wa pensheni wa Pspf kwa hatua ya kuwahamasisha watu mbalimbali kuweza kujiunga na mfuko huo ili kuhakikisha mabadiliko ya wananhi mbalimbali yanatokea kimaisha ,elimu,afya na mengine mengi.

Miongoni mwa madereva waliohudhuria katika mkutano huo wameupongeza  mfuko wa pesheni wa PSPF kwa kuweza kuwajali kwa kuwapa elimu juu ya mfuko huo pia wameahidi kushiriki vilivyo katika kujiunga na mfuko huo ili  kuhakikisha maisha yao yanaenda sambamba na hadhi ya jina na ubora wa kazi zinazofanywa na PSPF,
”kwani tumeiona fursa kutoka PSPF hivyo hatuna budi kujiunga na mfuko huu kwani fursa ni kuthubutu,kuhiari, kutendana kuamua  na uamuzi tulio uchukua ni kujiunga na PSPF kwa manufaa ya kwetu pia ya taifa kwa ujumla “pia wawasisitiza kuendelea kueneza elimu katika mkoa wa dar es salaam wote na hata nje ya mkoa ili watu watambue fursa zinazo tolewa na PSPF.