DJ TEE AZIDI KUTAKATA, SASA SHUJAAZ RADIO SHOW KUSIKIKA KUPITIA VITUO 4 NCHINI TANZANIA.

June 16, 2016
Kama ni mfuatiliaji mzuri wa vipindi vipya vya redio nchini Tanzania, basi lazima utakuwa umekutana na Shujaaz Radio Show inayoendeshwa na kijana anayejiita DJ Tee. Kitu kimoja tofauti sana ambacho kijana huyu anakifanya kwenye shoo yake ni kuelimisha vijana wengine, kuwapa meseji mbali mbali kuhusiana na mapenzi, mahusiano, na fursa mbali mbali, kwa njia rahisi sana ya burudani.
Wiki iliyopita katika harakati zangu za kutafuta vitu vipya, nilijikuta nikisikiliza TBC FM kwa muda mrefu na pasipo kutegemea, nilijikuta nikiisikia Shujaaz Radio Show. Nilidhani nimebadilisha frequency, lakini nilikuja kuhakikishiwa baadae na shabiki mmoja wa DJ Tee ambaye nimekuwa nikimuona akiizungumzia sana shoo hii kwenye akaunti yake ya Twitter.
Nilijikuta nikijiuliza – Hivi kuna shoo gani nyingine nchini Tanzania ambayo inarushwa na redio stesheni nne tofauti tofauti? Jibu sahihi ni HAKUNA! Ukiangalia alipotokea kijana huyu tangu nilipoanza kufuatilia stori yake kwenye kijarida cha SHUJAAZ, nimeona ni jinsi gani amefanikiwa sana kwa kufikia watu wengi ndani ya muda mfupi sana.
Kwa ufahamu wangu nikikurudisha nyuma kidogo, SHUJAAZ ilizinduliwa nchini Tanzania mwezi Februari mwaka jana 2015 (mwaka mmoja uliopita), na redio shoo za SHUJAAZ tulianza kuzisikia mwezi Novemba mwaka jana 2015 kupitia East Africa Radio. Mwaka huu 2016 ulipoanza (Januari) tuliweza kusikia redio stesheni nyingine mbili zikirusha shoo hii kali ya vijana, Chuchu FM ya Zanzibar na Kings FM kwa mikoa ya kusini mwa Tanzania.
Habari zilizopo ni kwamba hivi sasa shoo hii pia inasikika kupitia TBC FM kila Jumamosi saa kumi na moja jioni. Hii inafanya shoo hii kusikika kupitia vituo 4 vya redio nchini Tanzania. Kilichonivutia zaidi ni utofauti wa maudhui kwa shoo za kila kituo kwa kuwa kama utapata nafasi ya kuzisikiliza zote, utagundua kuwa kila stesheni ina kitu chake tofauti kabisa kupitia Shujaaz Radio Show.
Vijana wengi wamekiri waziwazi kuwa SHUJAAZ kwa ujumla imewasaidia kwa kiasi kikubwa kubadilisha mitazamo na fikra zao kuelekea mafanikio kwa staili rahisi na yenye kuburudisha.
Kijarida cha SHUJAAZ hutoka kila Jumamosi ya mwisho wa mwezi na husambazwa na gazeti la Mwanaspoti na wauzaji maalum wa Coca Cola nchi nzima. Vipindi vya redio vya SHUJAAZ husikika kupitia East Africa Radio kila Jumamosi saa TISA kamili alasiri, Chuchu FM kila Jumamosi saa KUMI jioni, TBC FM kila Jumamosi saa KUMI NA MOJA jioni na Kings FM kila Jumamosi saa KUMI NA MBILI jioni.
Pia, DJ Tee anapatikana kwenye mitandao ya kijamii kwa jina @djtee255

Allan Lucky
Media Personality & Media Content Producer

SERIKALI MKOANI MBEYA YASITISHA MATUMIZI YA DARAJA LA MBAKA WILAYANI RUNGWE MPAKA LITAKAPO KAMILIKA

June 16, 2016
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amosi Makalla mwenye miwani akitizama maendeleo ya ujenzi wa daraja Mbaka katika kijiji cha Kibhundughulu  wilayani Rungwe Mkoani Mbeya ambalo ujenzi wake ulikwama kutokana na ukosefu wa fedha hali ambayo iliwalazimu wananchi wa kijiji hicho kupita juu ya daraja hilo kwa kutumia kamba kitendo ambacho kilikuwa kikihatarisha maisha yao.(PICHA E.MADAFA JAMIIMOJABLOG) .

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amosi Makalla mwenye miwani akijaribu kupita kwa lengo  kukagua maendeleo ya ujenzi wa daraja la Mbaka katika kijiji cha Kibhundughulu  katika Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe ambalo  ujenzi wake ulianza toka mwaka 2015 na  ulishindwa kukamilika kutokana na ukosefu wa fedha kiasi cha shilingi milioni 58 ambapo katika ziara hiyo mkuu huyo wa mkoa wa mbeya aliambatana na baadhi ya viongozi wa halmashauri hiyo.

Mafundi wa kampuni ya Richer Ivestment ya Mkoani Mbeya ambao ndio wanajenga daraja hilo wakiendelea na ujenzi daraja hilo ambapo hadi kukamilika kwakwe linataji kukagharimu kiasi cha shilingi milioni 58 .

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amosi Makalla akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Kibhundughulu  Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe Mkoani Mbeya ambao ndio watumiaji wa daraja hilo la Mbaka ambalo lilikwama kukamilika kutokana na ukosefu wa fedha hali iliyopelekea wananchi wa kuanza kutumia daraja hilo kwa kupita juu kwa kutumia kamba hali ambayo iliatalisha maisha yao.

Katika mkutano huo Mkuu huyo wa Mkoa aliwataka wananchi wa kijiji hicho kuwapa ushirikiano mafundi wanaojenga daraja hilo ili liweze kukamilika kwa wakati .

Aidha Makalla amekemea baadhi watu wasio waaminifu ambao walikuwa wakipita juu ya daraja hilo kabla ya kukamilika kwakwe kitendo ambacho kilikuwahatari kwa maisha ya wananchi hao.

Aidha amemtaka mkarandasi anaye jenga daraja hilo kuhakikisha anakamilisha ujenzi huo katika kipindi cha wiki mbili ili kutoa fursa kwa wananchi hao kuanza kulitumia . 

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amosi Makalla akisiadiana na mafundi wa kampuni ya Richer Investment ambao wanajenga daraja la Mbaka kwa kiasi cha fedha shilingi Milioni 58 mara baada ya kuzungumza na wananchi wa kijiji cha Kibhundughulu ambao ndio watumiaji wa daraja hilo.
 
Baadhi ya akinana wakazi wa kijiji cha Mbaka Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe wakikatiza katika ya mto kutokana na Daraja walilokuwa wakitumia kuzuiwa na serikali ili kupisha ujenzi wake.



MICHUANO YA COPA AMERICA YAFIKIA ROBO FAINALI

June 16, 2016


Na Mwandishi Wetu

 MICHUANO ya Copa America inayoonekana moja kwa moja kupitia visimbuzi vya StarTimes Tanzania imefikia hatua ya robo fainali ambayo itaanza kutimua vumbi kesho Juni 16 mpaka 19.

Timu zilizotinga hatua hiyo ni Argentina, Chile, Mexico, Marekani, Venezuela, Peru, Colombia na Ecuador huku mashabiki wa soka wakishuhudia miamba ya soka ya timu za Brazil na Uruguay wenye nyota lukuki kama vile Luis Suarez, Edinson Cavani, Willian, Countinho na wengineo wakishindwa kuzisaidia timu zao.

Katika michuano hii ya kusisimua kikosi cha timu ya taifa cha Argentina kikiongozwa na mchezaji bora wa dunia mara tano, Lionel Messi, ambacho kinapewa nafasi kubwa ya kutwaa ubingwa huo kimeingia kwa kishindo hatua ya robo fainali baada kushinda michezo yote mitatu na kuongoza kundi D kwa alama tisa.

Kupitia chaneli za Sports Focus na World Football wateja na watanzania wanatazama michezo yote moja kwa moja huku wakiwa na nafasi ya kusinda zawadi mbalimbali kama vile vifurushi vya bure pamoja na pesa taslimu na safari kwenda Ujerumani kutazama mechi za Bundesliga za msimu ujao unaotarajiwa kuanza mwezi wa nane.

Akitoa ufafanuzi juu ya michuano hiyo Makamu wa Rais wa StarTimes Tanzania, Bi. Zuhura Hanif amesema kuwa, “Mbali na kufurahia matangazo ya moja kwa moja ya mechi zinazochezwa nchini Marekani pia tuna kampeni inayoendelea ya ‘Tabiri na Ushinde’ inayoenedelea kupitia mitandao yetu ya facebook na instagram. Kupitia kampeni hiyo mteja anaebashiri kwa usahihi matokeo ya mechi ya siku husika hupata fursa ya kujishindia kifurushi cha Mambo pamoja na cha michezo cha Sports Plus cha jumla ya shilingi 36,000/-.”

“Mbali na hapo pia kuna zawadi zingine zinazotokana na kampeni ya hashtag ya #CopaAmericaonStarTimes kupitia mitandao yetu pia. Mshindi wa kampeni hii hupatikana kwa kushea mara nyingi zaidi post atakayoiona kuwekwa na kurasa za StarTimes na kufikia watu wengi zaidi. Mshindi wa kwanza wa kampeni atapatiwa tiketi VIP ya kwenda ya kwenda Ujerumani kutazama mechi za Bundesliga msimu ujao pamoja na dola za Kimarekani 1500/-, huku wa pili na wa tatu watapatiwa simu za mkononi za kisasa aina ya Solar 5. Tumefanya hivi ili kuwazawadia wateja wetu waaminifu na wanaofuatilia huduma zetu ili kunogesha zaidi shamra shamra za kombe la Copa America.” Alimalizia Bi. Hanif 

Hatua ya robo fainali itakayoanza kupigwa kesho itazijumuisha timu zote zilizoshika nafasi ya pili katika makundi yao.

Wapenzi wa soka ulimwenguni wanazidi kusononeshwa na mwenedo mbovu wa kikosi cha taifa cha Brazil ambacho kimeshindwa kutinga hatua hiyo kwa kufanikiwa kushinda mechi moja tu kati ya tatu. Matokea hayo mabovu yamepelekea kocha wa taifa timu hiyo Dunga kutimuliwa kazi.

Timu na ratiba kwa timu zitakazopambana ni  pamoja na Marekani na Ecuador (Juni 16), Peru na Colombia (Juni 17), na mechi za mwisho ni Argentina na Venezuela; Mexico na Chile (Juni 18). Timu zitakazopita hatua hii zitakutana katika hatua ya nusu fainali siku ya Juni 21.


JIJI LA MWANZA LATAKIWA KUWAONDOA WATOTO OMBAOMBA MITAANI.

June 16, 2016
Watoto kutoka taasisi ya "Pamoja Youth and Children Foundatio" ya jijini Mwanza wakionyesha michezo ya sarakasi katika Maadhimisho ya miaka 40 ya Mtoto wa Afrika, yaliyofanyika katika Uwanja wa Shule ya Msingi Mabatini kwa wilaya ya Nyamagana mkoani Mwanza.
Imeandaliwa na BMG

Tigo yatoa dola 12,000 (26.4m/-) kwa C-Sema kuboresha kituo cha Huduma ya simu kwa Mtoto

June 16, 2016
Meneja wa Huduma za Jamii wa Tigo Woinde Shisael akimkabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya dola za Kimarekani 12,000(26.4m/-) Ofisa Mtendaji Mkuu wa C-Sema Kiiya kwa  ajili ya kuboresha kituo cha kutoa cha kupokelea simu cha Huduma ya Simu kwa Mtoto kilicho mjini Zanzibar, zoezi hili limefanyika leo katika viwanja vya JMK, Dar es Salaam kwa ajili ya kuadhimisha siku ya mtoto wa Afrika.


Dar es Salaam, Juni 16, 2016 - Kampuni ya Tigo Tanzania imeshiriki katika kumbukumbu ya Siku ya Mtoto wa Afrika 2016 kwa kuchangia  zaidi ya shilingi 26.4m/-($12,000) kwa asasi isiyo ya kiserikali ya  C-Sema  ambayo inaendesha kituo cha kupokelea simu cha Huduma ya Simu kwa Mtoto (Child Helpline Call Centre)  mjini Zanzibar ambacho kinatoa ushauri na kuwaunganisha watoto kupata huduma sahihi za kijamii  kikishirikiana na serikali.
Tigo na asasi ya C-Sema  watafanya maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika  mwaka huu katika Kituo cha Michezo cha JMK Park jijini Dar es Salaam Alhamisi Juni 16. Siku ya Mtoto wa Afrika ni tukio linalofanyika duniani kote  kila Juni 16 ya kila mwaka. 
Akizungumza wakati wa kukabidhi  msaada huo, Meneja wa Huduma za Jamii wa Tigo, Woinde Shisael  alisema  msaada huo ni sehemu ya  mkakati wa kampuni  wa kuwekeza katika  ajenda ya kumlinda mtoto iwe kwa njia ya mtandao  na hata nje ya mtandao.
Akitoa shukrani  kutokana na msaada, huo Ofisa Mtendaji Mkuu wa C-Sema, Kiiya JK aliishukuru kampuni hiyo ya simu kwa  kutoa mchango sahihi katika  kuwekeza rasilimali zake  ili kuhakikisha kwamba watoto na wazazi wanakuwa na uhakika wa kupata jukwaa ambalo wanaweza kutoa taarifa  kuhusu aina yoyote ya ukatili dhidi yao.
“Ninaishukuru  Tigo kwa msaada huu wakati leo tunasherehekea watoto wa Afrika kwa kuzisikiliza sauti zao wakati wakitueleza  kile wanachokifikiria kuhusu masuala mbalimbali yanayowasibu na nini kitu gani kifanyike  kutokomeza  matendo mabaya ambayo yanaweza   kukwamisha maendeleo yao.”
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mheshimiwa Nape Nnauye anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika tukio la mwaka huu la Siku ya Mtoto wa Afrika.
Kituo cha taifa cha kupokelea simu za huduma ya simu kwa mtoto (Child Helpline call centre) kilianzishwa rasmi Juni 15, 2013  kikiwa na kituo cha Dar es Salaam na Zanzibar.
 Mwisho 
photo Krantz Mwantepele Founder & CEO , KONCEPT Phone: +255-712579102 /+255-767392840 Email: krantzcharles@gmail.com Blog: www.mwanaharakatimzalendo.blogspot.com Website;www.koncept.co.tz
OSHA kuja na mbinu mpya za kuwasaidia wafanyakazi

OSHA kuja na mbinu mpya za kuwasaidia wafanyakazi

June 16, 2016
Wakiwa kama wakaguzi wa huduma za afya na usalama kwa wafanyakazi katika maeneo ya kazi, Wakala wa Afya na Usalama sehemu za Kazi (OSHA) wameeleza kuwa wataboresha ukaguzi wao hasa kwa wafanyakazi walio na UKIMWI jinsi wanavyohudumiwa na waajiri wawapo kazini.

Akizungumza na Mo Blog katika mafunzo ya jinsi ya kufanya kaguzi sehemu za kazi kwa watu walio na UKIMWI, Kaimu meneja usajili na takwimu za afya na Usalama OSHA, Dk. Abdalssalaam Omary, alisema kupitia mafunzo hayo wanataraji kuboresha ukaguzi zao ambazo zifanywa katika maeneo ya kazi ambazo zinakuwa zinawahusu watu walio na UKIMWI.

“Tunaamini kuwa baada ya mafunzo tutakuwa na maboresho katika kaguzi zetu sababu tumepata nafasi ya kukutana na wenzetu kutoka sehemu nyingine na kubadilishana uelewa kwahiyo tutakuwa tofauti na awali,” alisema Dk. Omary.

Alisema pamoja na kujipanga kuboresha kaguzi zao alisema kuwa bado wamekuwa wanakabiliwa na changamoto mbalimbali ambazo kwa muda mwingine zinaweza kuwa zinawafanya wakwame na kueleza changamoto hizo ni pamoja na fedha na madaktari kwa ajili ya kuwafanyia uchunguzi wafanyakazi.

Kwa upande wa serikali kupitia Kaimu Kamishna wa Kazi Msaidizi, Rehema Moyo alisema kuna sheria ambazo zimewekwa ambazo zinakataza waajiri kufanya vitendo vya ubaguzi kwa wafanyakazi na hivyo kama kuna waajiri wanawafanyia vitendo ambavyo havikubaliki kisheria basi watachukuliwa hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kufikishwa mahakani kujibu mashitaka yanayowakabili.

“Sera zipo utekelezaji ndiyo mgumu kuna vitendo vya ubaguzi lakini kujua ndiyo inakuwa changamoto maana ni mpaka muhusika aseme na sheria zipo kama mwajiriwa akikutwa na hatia anaweza hata kufungwa gerezani au kupigwa faini,” alisema Bi. Moyo.

Nae Mratibu wa maswala yanayohusiana na UKIMWI maeneo ya kazi kutoka Shirika la Kazi (ILO), Getrude Sima, alisema kupitia mafunzo hayo wanaamini washiriki wataweza kupata kitu kipya ambacho kitawasaidia katika kaguzi wanazozifanya ili waweze kutambua zaidi matatizo yanayowakuta wagonjwa wa UKIMWI wawapo kazini na jinsi ya kuwasaidia.

Washiriki wa mafunzo hayo wakimsikiliza mwendeshaji wa mafunzo hayo, Andrew Christian ambaye yupo Geneva, Switzerland aliyekuwa akitoa elimu kuhusu ukaguzi kwa wafanyakazi.



Mwendeshaji wa mafunzo, Andrew Christian akiwa Geneva, Switzerland ambaye alikuwa akitoa elimu kuhusu ukaguzi kwa wafanyakazi.
Wafanyakazi wakiwa katika picha ya pamoja.

KAMATI YA MAWASILIANO MKOA WA MWANZA YATOA ELIMU KWA WATUMIAJI WA HUDUMA ZA MAWASILIANO

June 16, 2016
Mwenyekiti wa Kamati ya Mawasiliano Mkoa wa Mwanza, Jonathan Abdallah Kasibu, akizungumza katika Semina kwa Watumiaji wa Huduma za Mawasiliano Jijini Mwanza iliyofanyika jana katika Ukumbi wa Shule ya Sekondari Mwanza.
Katika semina hiyo, watumiaji wa hudumza za mawasiliano ikiwemo simu pamoja na vyombo vya habari ambao waliwakilisha makundi mbalimbali kama vile wanahabari, wajasiriamali na walemavu, walipewa elimu juu ya uwepo wa Kamati hiyo pamoja na uwepo wa Baraza la Ushauri la Watumiaji wa huduma za Mawasiliano kutoka Mamlaka ya Mawasiliano nchini (TCRA-CCC).

Pia walielimishwa juu ya mwongozo wa kuwasilisha malalamiko ya watumiaji wa huduma za mawasiliano, haki na wajibu wa mtumiaji wa huduma za mawasiliano pamoja na sheria ya makosa ya mitandao ya mwaka 2015.

Semina hiyo pia ilihudhuriwa na viongozi wa Baraza la Ushauri la Watumiaji wa Huduma za Mawasiliano, kutoka Mamlaka ya Mawasiliano nchini (TCRA-CCC) ambapo iliambatana na viongozi wa Kamati ya Mawasiliano mkoani Mwanza kujitambulisha kwa baraza hilo.

Watumiaji wa huduma za mawasiliano walielezwa kwamba ni wajibu wao kuwasilisha malalamiko yao ikiwa wanapokea huduma zilizo chini ya kiwango ama ikiwa wana malalamiko ya aina yoyote kuhusu huduma za mawasiliano.

Walihimizwa kuwasilisha malalamiko yao kwa kuanza na mtoa huduma, yasiposhughulikiwa wanawayawasilisha katika Kamati ya Huduma za Mawasiliano mkoa, yasipotatuliwa yatawasilishwa katika Baraza la Ushauri la Watumiaji wa Huduma za Mawasiliano kutoka TCRA na hata ngazi nyingine zaidi hadi pale utatuzi utakapofanyika.

Semina hiyo ilionekana kuwafungua ufahamu watumiaji wa huduma za mawasiliano jijini Mwanza kwani baadhi yao walieleza kuwa awali walikuwa hawatambui haki na wajibu wao katika kutumia huduma za mawasiliano.
Baadhi ya Watumiaji wa Huduma za Mawasiliano Jijini Mwanza, wakiwa katika semina ya kuwaelimisha juu ya Matumizi ya Huduma za Mawasiliano.

UVCCM WAPANGISHA JENGO LAO LA MAJESTIC LA JIJINI TANGA

June 16, 2016


JUMUIYA YA UMOJA WA VIJANA YA CHAMA CHA MAPINDUZI (UVCCM) MKOA WA TANGA INAWATANGAZIA WAFANYABIASHARA NA WATANZANIA WOTE KUWA WANAKODISHA JENGO LAO LA BIASHARA LA MAJESTIC JIJINI TANGA

JENGO HILO LIPO ENEO ZURI KWA AJILI YA KUFANYIA BIASHARA NA KUWEZA KUPATA MAFANIKIO KAMA ILIVYOKUWA MAENEO MENGINE.

KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA KWA SIMU NAMBA 0714113900.
AU  0716001191

NYOTE MNAKARIBISHWA!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!