April 09, 2014


NA FATNA MFALINGUNDI,KOROGWE.
 Halmashauri ya wilaya ya Korogwe imetoa kilo 500 za mbegu ya mtama kwa Wananchi wake walioathiriwa na mafuriko na ukame katika msimu huu wa kilimo ili kukabiliana na njaa  kwa kuwa zao hilo linahimili ukame na hivyo kuwahakikishia usalama wa  chakula kwa mwaka huu.
Akikabidhi mbegu hizo juzi katika kijiji cha Mapangoni
kata ya Kerenge kilichoathiriwa na mafuriko, Afisa Kilimo wa wilaya Kakulu Lugembe aliwaambia viongozi na wakulima wa kijiji hicho kuwa halmashauri imetoa mbegu hiyo ili kuwakinga na upungufu wa chakula unaoweza kutokea kutokana  na mahindi yao kusombwa na maji yaliyosababishwa na mvua kubwa iliyonyesha mwishoni mwa wiki.
April 09, 2014

*SERIKALI YAKANUSHA TAARIFA ZA UPOTOSHAJI KUHUSU MATUMIZI YA MASHINE ZA KIELEKTRONIKI (EFD's)

Kaimu Mkurugenzi Huduma na Elimu kwa Mlipakodi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Julius Mjanga akiwaeleza waandishi wa Habari(Hawapo Pichani) kuhusu Taaarifa za Upotoshaji kuwa matumizi ya mashine za kielektroniki(EFD’s) yamesitishwa ila mashine hizo zinaendelea kutumika kwa mujibu wa Sheria na wafanyabiashara wanapaswa kuendelea kuzitumia il kuisaidia serikali katika ukusanyaji wa Kodi. Kushoto ni Afisa Uhusiano Mkuu wa Mamlaka hiyo Bi Oliver Njunwa.
Baadhi ya Waandishi wa Habari waliohudhuria Mkutano wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) leo Jijini Dar es Salaam.
(Picha Hassan Silayo)
April 09, 2014

VYOMBO VYA HABARI VYAASWA KUTOA KIPAUMBELE KWA HABARI ZINAZOJENGA JAMII

Msemaji wa Serikali na Mkurugenzi wa Idara ya Habari Bw. Assah Mwambene (kushoto) akizungumza na wahariri wa Gazeti la Jamhuri Bw. Deodatus Balile, Muhariri Mtendaji (katikati) na Bw. Manyerere Jackton , Naibu Muhariri Mtendaji (kulia) alipotembelea Ofisi za gazeti hilo mtaa wa Samora leo jijini Dar es salaam ikiwa ni sehemu ya utaratibu wa watendaji wa Idara ya Habari kuvitembelea vyombo vya habari kwa lengo la kuimarisha ushirikiano na kutatua changamoto zinazoikabili tasnia ya Habari nchini.
Muhariri Mtendaji wa Gazeti la Jamhuri Bw. Deodatus Balile (kulia) akizungumza jambo na viongozi wa Idara ya Habari waliotembelea ofisi za gazeti hilo leo jijini Dar es salaam. Kutoka Kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari-Usajili wa Magazeti Bw. Raphael Hokororo,Afisa habari wa Idara ya Habari Bi. Jovina Bujulu na Mkurugenzi wa Idara ya Habari na Msemaji wa Serikali Bw. Assah Mwambene.
April 09, 2014

YANGA YAIBUKA NA POINTI TATU KWA MABAO 2-1 DHIDI YA KAGERA, AZAM v/s RUVU MCHEZO UMEAHIRISHWA

 Wachezaji wa Yanga, wakishangilia bao la pili lililofungwa na Didier Kavumbagu (pichani wa pili kushoto) katika dakika ya 34 ya kipindi cha kwanza, huku bao la kwanza likifungwa na Hamis Kiiza katika dakika ya 3, mabao yaliyodumu hadi mwisho wa mcheo huo. 

Bao la kufutia machozi la Kagera Sugar, lilifungwa na Daud Jumanne, katika dakika ya 63 baada ya beki wa Yanga Oscar Joshua, kujaribu kumrudishia kipa wake mpira wa kichwa uliokuwa mfupi na kunaswa na mshambuliaji huyo aliyemchambua kipa wa Yanga, Deogratias Minishi. 

Hadi mwisho wa mchezo huo Yanga ya Jijini Dar es Salaam, 2 na Kagera Sugar ya Mjini Bukoba 1. Na katika habari kutoka Mlandizi zinasema kuwa mchezo kati ya Azam Fc na Ruvu Shooting, umeahirishwa kutokana na Uwanja wa Mlandizi Mabatini kujaa maji kutokana na mvua iliyonyesha leo, na mchezo huo sasa unatarajiwa kuchezwa kesho.
 Mabeki wa Kagera Sugar, akimdhibiti Simon Msuva.
April 09, 2014

MVUA YAAHIRISHA MECHI YA AZAM NA RUVU SHOOTING

Na Mahmoud Zubeiry, Mlandizi

MCHEZO wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kati ya wenyeji Ruvu Shooting na Azam FC ya Dar es Salaam uliokuwa ufanyike jioni ya leo Uwanja wa Mabatini Mlandizi mkoani Pwani umeahirishwa hadi kesho kufuatia mvua kubwa.
Timu hazikuwahi hata kuingia uwanjani kupasha misuli moto kutokana na mvua kubwa na Uwanja kujaa maji na ilipowadia Saa 10:20 waamuzi wa mechi hiyo waliingia uwanjani kukagua na kuvunja mchezo.
April 09, 2014

*NYANGWINE KUWASHITAKI KWA KINANA MAKADA WANAOMHUJUMU JIMBONI


 
NA MWANDISHI WETU
VURUGU na kampeni chafu zinazofanywa na baadhi ya makada wa CCM wanaojipanga kuwania ubunge katika jimbo la Tarime, zimechukua sura mpya.

Hatua hiyo imetokana na mbunge wa jimbo hilo Nyambari Nyangwine (pichani), kuweka bayana kuwa atawasilisha malalamiko kwa uongozi wa CCM ngazi ya wilaya, mkoa na taifa.