February 16, 2014

KILIMANJARO MARATHON YATANGAZA NJIA MPYA

Waandaaji wa mbio za Kilimanjaro Marathon wametangaza njia mpya zitakazotumika kwa mbio za mwaka huu ikiwa ni hatua nyingine muhimu katika mafanikio ya mbio hizo ambazo sasa zinaingia mwaka wa 12 tangu kuanzishwa. Njia mpya zimelenga kuboresha mwendo wa washiriki barabarani na kuwafanya wafurahie zaidi mbio hizo zilizopangwa kufanyika tarehe 2 Machi, 2014 mjini Moshi.

Akitangaza njia hizo mpya jana, John Addison, Mkurugenzi wa Wild Frontiers, waandaaji wa mbio hizo alisema alisema: Tumeanzisha njia mpya ili kuzuia msongamano wa watu wakati wa mbio kutokana na kuongezeka idadi ya washiriki kila mwaka. Washiriki wa mbio ndefu za marathon ya km 42, nusu marathon km 21, mbio ya walemavu na mbio ya kujifurahisha ya Vodacom 5km Fun Run sasa hawatapishana tena barabarani bali kila njia itatiririka katika muelekeo mmoja.

“Pia kutokana na mabadiliko haya washiriki watakuwa wameepuka kilomita 3 za mwinuko mkali kuelekea Chuo cha Mweka ambapo awali ndio palikuwa mahali pa kugeuzia washiriki wa mbio za full marathon na nusu marathon. Mbio ya walemavu za Gapco ambazo zitakuwa na makundi mawili tu mwaka huu ya kiti cha magurudumu (wheelchair) na baisikeli ya mikono (handcycle) imefupishwa kutoka nusu marathon na kuwa kilomita 10 ili kutoa fursa kwa watu wengi zaidi kushiriki na njia sasa itapita eneo tambarare na lenye kivuli.
Mkurugenzi wa Wild Frontiers ambao ni waandaaji wakuu wa Kilimanjaro Marathon, John Addison(kulia) Akizungumza na Meneja wa Kilimanjaro Premium Lager, George Kavishe.
Mbio ndefu za Kilimanjaro Premium Lager 42km Marathon zitaanza saa 12.30 asubuhi kutokea uwanja wa Chuo Kikuu cha Ushirika na Biashara (MUCCoBS) na kuelekea barabara iendayo Dar es salaam kwa kilomita kumi na kurudia geti la ushirika halafu zitaenda kilomita 8 kuelekea hospitali ya KCMC na kukata kushoto hadi Barabara ya Lema (Lema Road). Wanariadha watatelemka na Lema Road wakitelemka kupitia shule ya ISM halafu watamalizia na kipande tambarare cha Barabara ya Kilimanjaro na kipande cha mita chache za barabara ya Sokoine kuelekea uwanjani. 
Mkurugenzui wa Executive Solution ambao ndio waratibu wa mbio za Kilimanjaro Marathon, Aggrey Mareale (katikati) katika moja ya matukio ya uzinduzi wa mbio hizo.
Mbio za Nusu Marathon zitaanza saa moja kamili asubuhi kutokea MUCCoBS na kupandisha kaskazini kuelekea hospitali ya KCMC kwa kilomita 8 ambazo ni sawa na ongezeko la mwinuko wa futi 250 kutoka usawa wa bahari. Halafu mbio hizo pia zitapita njia ya Lema Road na kurudi uwanjani.

Addison alisema kuwa mbio za full marathon na nusu marathon zinapita kwenye maeneo mbalimbali yenye vivutio na mandhari nzuri ya mji wa Moshi na sehemu zenye mandhari ya mashamba ya kahawa na migomba jambo ambalo pia litawavutia wananchi wengi kujitokeza kuwashangilia wanariadha.

“Njia zote zitakuwa na vituo vya maji vya kutosha ili kuwafanya wanariadha wafurahie mbio bila kushikwa na kiu muda wote wa mbio. Vilevile, njia nzima itakuwa na madaktari na wauguzi wa kutoa huduma ya kwanza pamoja na magari ya kutosha ya wagonjwa huku mamlaka husika zikidhibiti usalama wa wanariadha barabarani. Madaktari wengine na wauguzi wataukuwa uwanjani ambapo kutakuwa na zahanati ya dharula kwa ajili ya huduma ya kwanza na kuchua misuli.
Mbio ya walemavu ya Gapco Disabled 10km Marathon itaanzia uwanja wa MUCCoBS na kufata barabara ya Kilimanjaro halafu mpaka Lema Road na kugeuza.

Addison alisema mbio za kujifurahisha za Vodacom 5km Fun Run zitaanzia kwenye mzunguko wa YMCA upande wa barabara ya Arusha na zitaenda hadi kwenye mnara wa saa halafu kupita Boma Road  kuelekea mzunguko (roundabout) wa barabara ya Arusha na mzunguko wa YMCA tena na watapita Uru Road na kuingia uwanjani kupitia geti la mashariki.

Executive Solutions ni waratibu wa mbio za Kilimanjaro Marathon 2014 wakishirikiana na Riadha Tanzania, Chama cha Riadha Kilimanjaro na Kilimanjaro Marathon Club huku zikidhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager (wadhamini wakuu), Vodacom Tanzania, GAPCO, Simba Cement, and KK Security among others, Keys Hotel, TPC Sugar, TanzaniteOne, CMC Automobiles Ltd, RwandAir, FNB Tanzania, UNFPA na Kilimanjaro Water.

Mwisho.

NB: Ramani zinapatikana kwenye tovuti ya www.kilimanjaromarathon.com
February 16, 2014

RAIS KIKWETE AZINDUA SERA YA MTANDAO WA VIKUNDI VYA MAADILI NA UCHUMI TZ (MVIMAUTA)

 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na vijana baada  ya kuzindua Sera ya Mtandao wa Vikundi vya Maadili na Uchumi Tanzania (MVIMAUTA)  iliyoasisiwa na   Askofu Mkuu Sylvester Gamanywa, Mwangalizi Mkuu wa Kitaifa, wa WAPO Mission  International  na Mwasisi wa Maono ya Harakati za Maadili kwa Kizazi Kipya katika ukumbi wa BCIC Mbezi Beach jijini Dar es salaam  Jumamosi, Februari 15, 2014
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akinyanyua juu kitabu baada ya kuzindua Sera ya Mtandao wa Vikundi vya Maadili na Uchumi Tanzania (MVIMAUTA)  akiwa na mwasisi wake  Askofu Mkuu Sylvester Gamanywa, Mwangalizi Mkuu wa Kitaifa, wa WAPO Mission  International  na Mwasisi wa Maono ya Harakati za Maadili kwa Kizazi Kipya katika ukumbi wa BCIC Mbezi Beach jijini Dar es salaam  Jumamosi, Februari 15, 2014
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia wakati wa  kuzindua Sera ya Mtandao wa Vikundi vya Maadili na Uchumi Tanzania (MVIMAUTA)  iliyoasisiwa na   Askofu Mkuu Sylvester Gamanywa, Mwangalizi Mkuu wa Kitaifa, wa WAPO Mission  International  na Mwasisi wa Maono ya Harakati za Maadili kwa Kizazi Kipya katika ukumbi wa BCIC Mbezi Beach jijini Dar es salaam  Jumamosi, Februari 15, 2014.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na msanii wa vichekesho ambaye  pia ni mhubiri  na mwimbaji wa nyimbo za injili Emmanuel Mgaya maarufu kama Masanja Mkandamizaji  baada ya kuzindua Sera ya Mtandao wa Vikundi vya Maadili na Uchumi Tanzania (MVIMAUTA)  akiwa na mwasisi wake  Askofu Mkuu Sylvester Gamanywa, Mwangalizi Mkuu wa Kitaifa, wa WAPO Mission  International  na Mwasisi wa Maono ya Harakati za Maadili kwa Kizazi Kipya katika ukumbi wa BCIC Mbezi Beach jijini Dar es salaam  Jumamosi jana. Picha na IKULU
February 16, 2014

*KIKAO CHA KAMATI KUU YA CCM DODOMA, BERNARD MEMBE AHOJIWA


 Mwenyekiti wa CCM Taifa, Jakaya Kikwete, akiongoza Kikao cha kamati Kuu mjini Dodoma leo mchana.
 Baadhi ya wjumbe wa NEC, wakiwa ndani ya ukumbi wa CCM katika Kikao cha Kamati kuu.
 Baadhi ya wjumbe wa NEC, wakiwa ndani ya ukumbi wa CCM katika Kikao cha Kamati kuu.
 Baadhi ya wjumbe wa NEC, wakiwa ndani ya ukumbi wa CCM katika Kikao cha Kamati kuu.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, ambaye pia ni mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM (NEC) Bernard Membe akizungumza na waandishi wa habari nje ya Ukumbi CCM Makao Makuu Dodoma baada ya kuhojiwa na Kamati Ndogo ya Maadili ambapo alisema Kamati ya Maadili imeuliza masuala mazito na magumu yanayohusiana na uvunjaji wa maadili ya uongozi wa chama na kuongeza kuwa na bado wapo wengi watakao hojiwa.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, ambaye pia ni mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM (NEC) Bernard Membe akizungumza na waandishi wa habari nje ya Ukumbi CCM Makao Makuu Dodoma.

 Kikundi cha uhamasishaji cha vijana wa CCM, kikitoa burudani kwa nyimbo zake za kwaya na kuwapagawisha baadhi ya Wabunge.
 Mbunge, faida, akiserebuka na miondoko ya kwaya.....
 Baadhi ya waandishi wa habari wakiwajibika kuandika stori baada ya kuzungumza na Bernard Membe...nje ya Ukumbi wa CCM.
Baadhi ya waandishi wa habari wakiwajibika kuandika stori baada ya kuzungumza na Bernard Membe...nje ya Ukumbi wa CCM.