RC MAKONDA ATOA MAELEKEZO 17 KWA WATENDAJI WA SEKTA YA ARDHI NA UJENZI

RC MAKONDA ATOA MAELEKEZO 17 KWA WATENDAJI WA SEKTA YA ARDHI NA UJENZI

May 18, 2017
INDEC
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mheshimiwa Paul C. Makonda Leo Mei 18, 2017 akizungumza Na Watendaji wa Sekta ya Ardhi Na Ujenzi wanaohudumu katika Manispaa za Ubungo, Kigamboni, Kinondoni, Temeke, Ilala Na Halmashauri ya Jiji la Dar es salaam ametoa maelekezo 17 ya kuzingatia katika utendaji wao.
*1.*Watendaji wa Sekta ya Ardhi Na Ujenzi  Kushughulikia migogoro ya ardhi Na Ujenzi ili wananchi wasipeleke malalamiko yao ngazi za juu.
*2.*Watendaji wa Sekta ya Ardhi Na Ujenzi Wameagizwa kutoa vibali vya Ujenzi ndani ya mwezi mmoja Na zoezi hilo lianze Mwezi wa sita mwaka huu 2017. Mwanzoni mwa mwezi wa Saba kuzinduliwa teknolojia ambayo wananchi watapata taarifa zao za Ardhi kwenye mtandao Jambo ambalo litafanya Dar es salaam kuwa kiganjani mwa wananchi.
*3.*Wakuu wa Idara katika Sekta ya Ardhi Na Ujenzi  kuhakikisha wanatoa taarifa kuhusu Mipango ya Idara kwenye vyombo vya habari kwa kuwatumia maafisa habari kwani tayari wana mahusiano Na waandishi mbalimbali katika vyombo vyombo vya habari.
*4.*Wakuu wa Idara ya Ardhi Na Ujenzi kutoa TAARIFA ya maeneo yote ya wazi yaliyotolewa Hati, Na kujitokeza haraka kwa wote waliotoa Hati za maeneo ya wazi kama wapo.
*5.*Wakuu wa Idara ya Ardhi Na Ujenzi kusimamia haraka upimaji wa maeneo yote ya Umma kama kama vile Shule, Hospitali, Na Masoko kama alivyoagiza Waziri wa TAMISEMI sambamba Na kutoa Mikakati wa Upimaji.
*6.*Wakuu wa Idara ya Ardhi Na Ujenzi kuhakikisha ufanisi Na bidii ya utendaji inaongezeka hususani mikakati ya kuhusisha wapimaji binafsi wanaotambulika kwani Mji ukipimwa vyema Madiwani watafurahi lakini pia itakuwa njia rahisi ya kuepuka migogoro ya Ardhi.
KATIBU MKUU WA CCM NDUGU ABDULRAHMAN KINANA AHUDHURIA MKUTANO WA VYMA VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA NCHINI ANGOLA

KATIBU MKUU WA CCM NDUGU ABDULRAHMAN KINANA AHUDHURIA MKUTANO WA VYMA VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA NCHINI ANGOLA

May 18, 2017
ango
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) Ndugu Abdrahamani Kinana yuko nchini Angola akiongoza ujumbe wa CCM katika kikao cha Makatibu Wakuu wa Vyama vya ukombozi wa kusini mwa Afrika( Front Line State parties).Pia Ndugu Katibu Mkuu ameongoza Majadiliano na vyama Rafiki vilivyoshiriki Mkutano huo kikiwemo Chama Cha Kikomunisti Cha watu wa China .Ujumbe wa CCM umejumuisha katibu wa Itikadi,Siasa na Uenezi( Ndg.Humphrey Polepole) Katibu wa Siasa na Uhusiano wa kimataifa(Ndg.Ngemela Lubinga) na watendaji wa Jumuiya za Chama Cha Mapinduzi (CCM). Vyama Rafiki Vimepongeza CCM MPYA NA MWENENDO WAKE.
angol

MATUKIO KATIKA PICHA: YALIYOJIRI KATIKA KIKAO CHA 28, MKUTANO WA SABA BUNGE LA 11 MJINI DODOMA LEO MAY 18, 2017.

May 18, 2017

 Naibu Spika  wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dk.Tulia Ackson  akiongoza    kikao cha Ishirini na nane cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 18, 2017.
8950-Mhagama na Makamba
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Bunge,Kazi,Vijana,Ajira na Watu wenye Ulemavu Mhe.Jenista Mhagama akizungumza jambo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano Mhe.January Makamba   katika kikao cha Ishirini na nane cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 18, 2017.
8987-Mhe.Kijaji
 Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe.Dk.Ashatu Kijaji akifafanua jambo katika  kikao cha Ishirini na nane cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 18, 2017.
8994-Mhe.Makamba
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano Mhe.January Makamba akijibu maswali mbalimbali ya wabunge katika  kikao cha Ishirini na nane cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 18, 2017.
9004-Naibu Waziri wa Habari
Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Anastazia Wambura akijibu maswali mbalimbali ya wabunge katika  kikao cha Ishirini na nane cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 18, 2017.
9090-Mhe.Manyanya
Naibu Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia Mhe.Eng.Stella Manyanya akijibu maswali mbalimbali ya wabunge katika  kikao cha Ishirini na nane cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 18, 2017.
9046-Mhe.Mwakyembe
Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Dk Harrison Mwakyembe akijibu maswali mbalimbali ya wabunge katika  kikao cha Ishirini na nane cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 18, 2017.
9110-Waziri Mwakyembe na Naibu Waziri
Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Dk Harrison Mwakyembe akizungumza jambo na Naibu wake Mhe.Anastazia Wambura  katika  kikao cha Ishirini na nane cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 18, 2017.
9234-Mhe.Kigwangala
 Naibu Waziri wa Afya ,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto akijibu maswali mbalimbali ya wabunge katika  kikao cha Ishirini na nane cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 18, 2017.

Picha Zote na Daudi Manongi- Dodoma MAELEZO, DODOMA

MABASI YANAYOBEBA WANAFUNZI MKOANI SINGIDA YAKAGULIWA.

May 18, 2017

Askari wa usalama barabarani mkoani Singida, E.8763. Sgt. Benes Lucas akikagua mabasi yanayotumika kusafirisha wanafunzi mjini hapa jana.
Baadhi ya mabasi kati ya 20 yanayotumika kusafirisha wanafunzi Mkoani Singida yakifanyiwa ugazi na askari usalama barabarani kwa lengo la kujiridhisha ubora wake.
RTO Mkoa wa Singida Mrakibu wa polisi Peter Raphael Majira akitoa taarifa ya zoezi la ukaguzi wa mabasi yanayotumika kusafirisha wanafunzi kwa lengo la kukagua ubora na pia kuwakumbusha madereva na wamiliki wa mabasi hayo juu ya sheria za usalama barabarani.

MAELEZO YA PICHA.

…………………..

Jeshi la polisi kitengo cha usalama barabarani Mkoa wa Singida limeanzisha zoezi kambambe la kukagua mabasi yanayotumika kusafirisha wanafunzi huku likisisitiza kuwa zoezi hilo kuwa endelevu.

Akizungumza kwa niaba ya kamanda wa jeshi la polisi Mkoa wa Singida, RTO Mrakibu wa Polisi Peter Raphael Majira, amesema zoezi hilo lililoanza jana litaendelea kwenye wilaya zote za mkoa wa Singida.

Amesema lengo ni kuhakikisha mabasi hayo yanakidhi mahitaji yote ya sheria za usalama barabani, wakati wote yanapokuwa barabarani.

Amesema pia wanatoa elimu na wanawakumbusha madereva na wamiliki wa mabasi hayo, juu ya wajibu wao na umuhimu wa kuzingatia kwa umakini mkubwa sheria za usalama barabarani. 


Aidha RTO Peter amesema wanawakumbusha madereva kujenga utamaduni wa kuwa na tahadhari zaidi na kitendo hicho kitapunguza kwa kiwango kikubwa ajali za barabarani.

Pia ametumia fursa hiyo kuwataka wenye watoto wanaotumia mabasi hayo wahakikishe mtoto anakaa kwenye kiti chake na si kuchangia kiti.

“Mzazi/mlezi usikubali kabisa mwanao achangie kiti, umelipitia kiti kwa nini achangie na wanafunzi mwingine. Na ninyi wamiliki wa mabasi haya kama kuna hafla wanafunzi wanakwenda kuhudhuria iwapo wamejaa (yaani kila mwanafunzi ana kiti chake), peleka hao waliopata viti halafu urudie wengine” amesisitiza mrakibu Peter.

Kwa upande wao madereva hao wamelipongeza jeshi la polisi mkoa wa Singida kwa kuendesha ukaguzi huo na kuwakumbusha juu ya sheria za usalama barabarani.

Mmoja wa madereva wa mabasi ya wanafunzi Mkoani Singida Pyuza Gyumi amesema kwenye mafunzo hayo ya muda mfupi wameagizwa kwamba ni marufuku wanafunzi kuchangia kiti kimoja kwa madai ni ukiukwaji mkubwa wa sheria za usalama barabarani.

“Tumekumbushwa kwamba wakati tukiwa barabarani tuwe makini wakati wote wa kuendesha na tuwe na utulivu wa hali ya juu. Pia tumekumbushwa kuwa makini wakati tunavusha kwa miguu wanafunzi ng’ambo yingine ya barabara. Kwa ujumla binadamu anatakiwa mara kwa mara akumbushwe wajibu wake hii itasaidia kufanya kazi zetu kwa ufanisi”, amesema.

Aidha amesema jeshi la polisi kuwakutanisha na waajiri wao itasaidia kupunguza kero mbalimbali zinazowakabili kati yao na waajiri wao.

“Kuna wakati tunashindwa kuelewana na matajiri wetu wakati wanapotulazimisha kutenda mambo ambayo ni nje ya sheria za usalama barabarani. Baada ya mafunzo haya ya muda mfupi waajiri wenye tabia hizo watabadilika na kutuunga mkono uzingatiaji wa sheria za usalama barabarani”, amesema Gyumi.

Ben Paul Ndani Ya Miss Ustawi Ijumaa

May 18, 2017
Mwanamuziki nyota wa kizazi kipya nchini, Ben Paul atatumbuiza katika mashindano ya kumsaka mrembo wa Chuo cha Ustawi wa Jamii (Miss Ustawi) yaliyopangwa kufanyika Ijumaa (Mei 19) kwenye ukumbi wa King Solomon uliopo Namanga jijini.

Mratibu wa mashindano hayo, Catherine Boniface alisema kuwa Paul ambaye anatamba na wimbo wa Moyo Machine, Phone na nyinginezo nyingi, pia atatambulisha wimbo wake mpya aliomshirikisha mwanamuziki nyota nchini, Darasa.

Mashindano hayo yamedhaminiwa na kinywaji cha Windhoek, yatashirikisha jumla ya warembo 12 ambao walikaa kambini kwa muda wa wiki mbili wakijifua chini ya mwalimu wao, Clara Michael na matron, Catherine Boniface.

Warembo ambao wamepitishwa na kamati ya mashindano hayo ni Fatma Kivea, Elice Mwakajila, Melody Thomas, Diana Mwaibula, Hapifania Shedoekulu, Careen Kileo. Wengine ni Angelina Michael, Ruth Deogratius, Consolator Samwel, Loyce Jeck na Elizabeth Julius.

Washindi watatu wa mashindano hayo watapata nafasi ya kushindana katika shindano la warembo wa elimu ya juu (Miss Higher Learning Institution) ambapo warembo watatu wa kwanza watafuzu katika mashindano ya Miss Tanzania mwaka huu.

Mratibu wa mashindano hayo, Catherine Boniface alisema kuwa warembo watapanda jukwaani wakiwa wanashindania vazi la ubunifu, ufukweni na usiku na warembo watano watakaopita katika mchujo wa kwanza watajibu maswali.

“Morali ya warembo ipo juu, kila mmoja ni mshindi, lengo letu ni kushinda taji la vyuo vya elimu ya juu na kutwaa taji la Miss Tanzania kwa mara ya kwanza katika historia ya mashindano ya urembo nchini,” alisema Catherine.

Msemaji wa kampuni ya Mabibo Beer inayodhamini shindano hilo, Andrea Missama amesema kuwa wameamua kudhamini shindano hilo kama sehemu ya kampuni yao kukuza vipaji na kazi za jamii.

Missama amesema kuwa warembo wengi wamejitokeza kushindania taji hilo ambalo mshindi wake atakiwakilisha chuo hicho katika mashindano ya urembo ya vyuo vya elimu ya juu.

Rais wa Chuo cha Ustawi wa Jamii, Yohana Mabena akizungumza wakati wa  kuwatambulisha warembo wao kwa wadhamini wakuu, kampuni ya Mabibo Beer. Kulia ni msemaji wa kampuni ya Mabibo Beer, Andrea Missama na kushoto kwa Mabena ni Waziri wa Michezo wa Ustawi, Ashura Jingu. Nyuma ni warembo wa miss Ustawi 2017. 
Mwanamuziki wa muziki wa kizazi kipya nchini, Ben Paul akizungumza akizungumza wakati wa kutambulishwa kuwa msanii wa kutumbuiza katika mashindano Miss Ustawi 2017 yaliyopangwa kufanyika Ijumaa (Mei 19) kwenye ukumbi wa King Solomon uliopo Namanga, jijini.

Miss Ustawi anayemaliza muda wake Evelyn Andrew akizungumza wakati wa utambulisho wa warembo hao kwa wadhamini wakuu. Evelyn anavua taji hilo, Ijumaa (Mei 19) wakati wa mashindano ya kumsaka mrembo wa chuo hicho kwenye ukumbi wa King Solomon uliopo Namanga.


Warembo wakiwa katika picha ya pamoja na Miss Ustawi anayemaliza muda wake, Evelyn Andrew. Warembo hao watapambana Ijumaa (Mei 19) wakati wa mashindano ya kumsaka mrembo wa chuo hicho kwenye ukumbi wa King Solomon uliopo Namanga.

TGNP YASEMA BAJETI YA ELIMU YA MWAKA 2017/2018 HAIJATOA KIPAUMBELE KWA MTOTO WA KIKE

May 18, 2017
 Ofisa wa Mtandao wa Kijinsia Tanzania (TGNP), Veronica Magayane akitoa mada wakati wa  mkutano wa uchambuzi wa bajeti ya wizara hiyo kwa mlengo wa kijinsia uliofanyika jijini Dar es Salaam jana.

TADB YABISHA HODI VISIWANI ZANZIBAR

May 18, 2017

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo anaeshughulikia Kilimo na Maliasili Bibi  Maryam Juma Abdullah (aliyesimama) akiwakaribisha ugeni kutoka Benki ya Maendeleo ya Kilimo ya Tanzania (TADB). 
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo anaeshughulikia Kilimo na Maliasili Bibi  Maryam Juma Abdullah (aliyesimama kulia) akizungumza wakati wa ugeni kutoka Benki ya Maendeleo ya Kilimo ya Tanzania (TADB) ulipotembelea Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi. Ugeni huo upo visiwani Zanzibar kuangalia maeneo ya uwekezaji visiwani humo. 
Wanaomsikiliza ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo, Bw. Francis Assenga (kushoto) na wajumbe wa Bodi ya TADB, Bw. Hussein Mbululo (wapili kushoto) na Bibi Rehema Twalib ambaye ni Mkuu wa Msafara huo (wapili kulia). 
Mjumbe wa Bodi ya TADB, Bibi Rehema Twalib ambaye ni Mkuu wa Msafara huo (aliyesimama) akizungumza wakati walipotembelea Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi Zanzibar. 
Mkuu wa Msafara wa TADB, Bibi Rehema Twalib (katikati) ambaye pia ni Mjumbe wa Bodi wa Benki hiyo akihimiza jambo wakati wa ziara hiyo. Kushoto ni Mjumbe wa TADB, Bw. Hussein Mbululo na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo anaeshughulikia Kilimo na Maliasili Bibi Maryam Juma Abdullah (kulia). 
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo, Bw. Francis Assenga (aliyesimama) akieleza dhima ya Benki ya Kilimo katika kusaidia juhudi za Serikali katika kuinua ukuaji wa uchumi na kupunguza umaskini Tanzania. 
Mkurugenzi wa Mikopo na Biashara wa TADB, Bw. Augustino Chacha (kushoto) akizungumzia fursa za mikopo inayotolewa na Benki hiyo wakati walipotembelea viongozi na wajumbe wa Bodi ya TADB walipotembelea Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi Zanzibar. 
Mkurugenzi wa Mipango wa Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi Zanzibar, Sera na Utafiti, Bw. Sheha Idrissa Hamdan (aliyesimama kushoto) akizungumza wakati Ugeni wa Benki ya Kilimo ulipotembelea wizarani hapo.  
Meneja wa Mikopo wa TADB, Bw. Samuel Mshote (kulia) akizungumza wakati wa kikao hicho.


Benki ya Maendeleo ya Kilimo ya Tanzania (TADB) imeanza kuchangamkia fursa za uwekezaji katika sekta ya kilimo na mifugo visiwani Zanzibar kwa kuanza mchakato wa kutoa mikopo kwa wakulima na wakazi wa visiwa hivyo wanaojishughulisha katika uchakataji wa mazao ya kilimo visiwani humo.

Akizungumza wakati wa walipotembelea Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi, visiwani humo Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo, Bw. Francis Assenga alisema kuwa TADB ikiwa chombo cha Muungano ina wajibu kusaidia juhudi za Serikali katika kuinua ukuaji wa uchumi na kupunguza umaskini nchini Tanzania hasa katika kuchagiza mapinduzi na maendeleo katika Sekta ya Kilimo, ambayo inaajiri zaidi ya asilimia 75 ya watu wenye uwezo wa kufanya kazi nchini na pia kutoa kiasi cha zaidi ya asilimia 65 cha mali ghafi kwa ajili ya viwanda vya nchi.

“Uanzishwaji wa TADB unatokana na Serikali kutambua umuhimu wa uwekezaji wenye tija kwenye maeneo yote ya sekta ya Kilimo na kuleta mapinduzi ya dhati ya Kilimo ili kuwezesha upatikanaji wa mikopo na mitaji ya riba nafuu ikiwa ni pamoja na kuhamasisha mabenki na taasisi zingine za fedha nchini kutoa mikopo zaidi kwenye sekta ya Kilimo,” amesema.

Bw. Assenga amesema Zanzibar ina utajiri mkubwa kwenye uzalishaji wa viungo ‘spices’ ambayo ni mojawapo wa minyororo ya thamani ya mwanzo inayopatiwa mikopo kwa ajili ya uongezaji wa thamani mazao mbalimbali na Benki ya Kilimo.

Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo anaeshughulikia Kilimo na Maliasili Bibi Maryam Juma Abdullah ameishukuru Benki hiyo kwa kuiangalia Zanzibar kuwa sehemu ya kimkakati na kutaka kuanza mikopo visiwani humo.

TFDA YAWATOA HOFU WANYWAJI WA NOVIDA YA COCA COLA KWANZA KWAMBA NI SALAMA

May 18, 2017

JUMIA TRAVEL YAJIDHATITI KUFANYA MAPINDUZI YA USAFIRI BARANI AFRIKA

May 18, 2017
Na Jumia Travel Tanzania

Kampuni inayoongoza kwa kutoa huduma za hoteli kwa njia ya mtandao ndani na nje ya bara la Afrika, Jumia Travel imedhamiria kukomboa jitihada za masuala ya usafiri kupitia kampeni yake mpya itakayojulikana kwa ‘DemocratizeTravel.’