*MOTO WATEKETEZA SOKO LA BIDHAA ZA UTAMADUNI LIJULIKANALO KAMA MT.MERU CURIOS & CRAFTS MARKET JIJINI ARUSHA.
Baadhi
ya bidhaa zilizoteketea kwa moto katika SOKO la bidhaa za utamaduni
lijulikanalo kwa jina la MT.MERU CURIOS& CRAFTS MARKET usiku wa
kuamkia leo.
Wakazi wa Jiji la Arusha wakiangalia namna moto ulivoathiri soko hilo.
Bango la Soko hilo.
Wengine wakiangalia kama watabahatika kuokoa chochote.
Wengine wakiokota mabaki ya mabati yaliyoungua.
Sehemu
ya Wafanyabiashara wa SOKO la bidhaa za utamaduni lijulikanalo kwa jina
la MT.MERU CURIOS & CRAFTS MARKET wakiwa wameduwaa bila kujua la
kufanya mara baada ya Soko hilo kuteketea kwa moto usiku wa kuamkia leo
na kuunguza bidhaa zote za wafanya biashara zililopo katika soko hilo
Mkuu
wa Mkoa wa Arusha,Magesa Mulongo ameagiza uchunguzi wa kina kufanyika
kufuatia soko la wafanyabiashara wa Vinyago na bidhaa mbalimbali za
kitalii la Maasai Market kuteketea kwa moto.
Mulongo
ambaye alifatana na kamati ya Ulinzi na Usalama alishangaa kuona maduka
hayo ambayo yapo jirani na Kikosi cha Zima Moto kushindwa kuzima moto
na kusababisha hasara kwa wananchi.
"Sitakubali
kuona uzembe unaendelea katika mkoa wetu,lazima watu wawajibishwe kwa
uzembe hasa Kikosi cha kuzima moto ambao mko karibu na Ofisi za Chama
Cha mapinduzi wilaya yalipo maduka haya"amesema Mulongo
Chanzo
cha moto bado hakijaweza kufahamika huku maduka hayo yapatayo 188, huku
yakiwa hayajaunganishwa na Umeme kwa lengo la kuepusha hatari ya moto
kwani bidhaa nyingi ni vinyago vinavyotengenezwa kwa mbao.
Habari picha kwa hisani ya Othmani michuzi blog
KIKAO CHA KAMATI YA USHAURI MKOA WA MANYARA CHAFANYIKA MJINI BABATI
Baadhi
ya wajumbe wa kikao cha ushauri cha Mkoa wa Manyara, (RCC) wakifuatilia
kikao hicho kilichofanyika jana mjini Babati na kuongozwa na Mkuu wa
mkoa huo Elaston Mbwilo.
Ofisa
elimu wa Mkoa wa Manyara, Ibrahim Mbang'o na baadhi ya wajumbe
wakifuatilia jambo kwenye kikao cha ushauri cha mkoa huo (RCC)
kilichofanyika jana mjini Babati.
Mkuu
wa Wilaya ya Hanang' Mkoani Manyara, Christina Mndeme (kulia) na Mkuu
wa Wilaya ya Mbulu, Anatory Choya, wakiwa kwenye kikao cha kamati ya
ushauri ya mkoa huo (RCC) kilichofanyika jana mjini Babati
Rais Dk.Shein akutana na Uongozi wa Chama cha wapatholojia Tanzania.
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein
akizungumza na ujumbe wa Chama cha Wapatholojia wa Tanzania walipofika
Ikulu Mjini Zanzibar kwa ajili ya Kujitambulisha kwa Rais leo (wa pili
kulia) Mwenyekiti wa Chama hicho Dk. Charles Massambu,[Picha na
Ikulu.]Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali
Mohamed Shein akizungumza na ujumbe wa Chama cha Wapatholojia wa
Tanzania walipofika Ikulu Mjini Zanzibar kwa ajili ya Kujitambulisha
kwa Rais leo (wa pili kulia) Mwenyekiti wa Chama hicho Dk. Charles
Massambu,[Picha na Ikulu.]
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed
Shein akizungumza na ujumbe wa Chama cha Wapatholojia wa Tanzania
walipofika Ikulu Mjini Zanzibar kwa ajili ya Kujitambulisha kwa Rais
leo (wa pili kulia) Mwenyekiti wa Chama hicho Dk. Charles
Massambu,[Picha na Ikulu.]
WAZIRI MKUU NA MATUKIO BUNGENI DODOMA LEO
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda
akizungumza na Wabunge wa Viti Maalum, Amina Makilagi (kulia) na Mary
Chatanda kwenye jengo la Utawala la Bunge mjini Dodoma Novemba 18, 2014.
(picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri
wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Dkt. Mary Nagu akiwasilisha Muswada wa
Marekebisho ya Sheria ya Ubia Baina ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi
wa mwaka 2014, bungeni mjini Dodoma Novemba 18, 2014. (Picha na Ofisi ya
Waziri Mkuu)
TATIZO LA MSONGAMANO WA MAGARI DAR KUTATULIWA
Waziri wa Ujenzi Dkt. John
Magufuli(kulia),akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es
Salaam kuhusu ujenzi wa daraja lenye urefu wa kilometa 7.5 litakaloanzia
eneo la Aghakani na kuishia Coco beach, ujenzi huo unaotarajiwa kuanza
mapema mwakani na unafadhiliwa na Serikali ya watu wa Korea Kusini
,lengo ni kupunguza msongamano wa magari katika daraja la
Serender,kushoto ni Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi Dkt. Juma Iyombe.
(Picha Lorietha Laurence –Maelezo)
………………………………………………………………………………………..
Na Beatrice Lyimo -Maelezo
Zaidi ya Bilioni 110 zinatarajia
kutumika katika ujenzi wa daraja lenye urefu wa kilometa 7.5 ili
kupunguza msongamano wa magari jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na waandishi wa
habari leo jijini Dar es Salaam Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli
alisema daraja hilo litaanzia eneo la Aghakani na kuishia Coco beach.
Waziri Dkt. Magufuli alisema
daraja hilo litakalojengwa kwa msaada wa Serikali ya Korea Kusini
litakuwa na njia nne na barabara mbili za huduma kwa kila upande lenye
uwezo wa kupitisha magari elfu 61 kwa siku .
“Serikali ya Korea Kusini
imemaliza mradi wa ujenzi wa daraja la Kikwete pamoja na barabara ya
Malagalasi Mkoani Kigoma na sasa tumewaomba waendelee kutoa msaada kwa
ajili ya ujenzi wa barabara mkoani Dar es Salaama ili kupunguza
msongamano wa magari”, alisema Dkt. Magufuli.
Kwa upande wake Mtendaji Mkuu
kutoka TANROADS Mhandisi Patrick Mfugale amebainisha kuwa wataalamu
kutoka Korea Kusini wameshafanya Upembuzi yakinifu uliomalizika hivi
karibuni, hivyo ujenzi wa daraja hilo unatarajiwa kuanza mwanzoni mwa
mwaka ujao.
Aliongeza kuwa daraja hilo
litakalofahamika kwa jina la New Salender Bridge litaunganishwa na
barabara ya Ally Hassan Mwinyi kutokea Aghakani na kwa upande mwingine
litaunganishwa na barabara ya Chole iliyopo Masaki.
Serikali imeweka mikakati mingi
ya kupunguza msongamano wa foleni za magari kwa kuanzisha ujenzi mbadala
wa barabara za juu unaotarajiwa kujengwa maeneo ya TAZARA,Mbagala rangi
tatu hadi gerezani, kuanzishwa kwa kivuko cha Dar es Salaam hadi
Bagamoyo.
Pia utafanyika utanuzi wa
barabara nyingine za Dar es salaam kwenda Morogoro kupitia Chalinze na
ile ya Morocco hadi Mwenge na Bagamoyo hadi Msata.
KATIBU MKUU WA CCM NDUGU ABDULRAHMAN KINANA AMALIZA ZIARA YAKE JIMBO LA MTAMA
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipokelewa na Bernard Membe
Mbunge wa jimbo la Mtama na Mjumbe wa Halmashauri kuu ya taifa wakati
alipowasili katika Kiwalala Kituo cha Ufugaji cha Masister cha Narunyu
ambapo ameshiriki kazi ya kukamua maziwa akiwa katika ziara yake ya
kikazi ya mikoa ya Lindi na Mtwara akikagua utekelezaji wa Ilani ya
Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010 inayotekelezwa na serikali lakini pia
kuhimiza uhai wa Chama cha Mapinduzi CCM, Katibu mkuu Kinana katika
ziara hiyo anaongozana na Nape Nnauye Katibu wa NEC Siasa,Itikadi na
Uenezi.(PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-MTAMA -LINDI)Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki
kazi ya kukamua maziwa katika kituo cha uugaji cha Masister cha Narunyu
Mtama mkoani Lindi wakati alipotembelea kituo hicho.Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na baadhi ya Masister mara baada ya kuwasili katika kituo hicho katika jimbo la Mtama mkoani Lindi.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki ujenzi wa tanki la maji katika mradi wa maji unaojengwa katika kata ya Nyangamara jimbo la Mtama.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akionyesha
kitabu kinachoelezea shughuli mbalimbali zilizotekelezwa na Mbunge wa
jimbo la Mtama Mh. Bernard Membe alipotembelea ofisi ya mbunge huyo.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki
katika shughuli za kubangua korosho wakati alipotembelea kikundi cha
akina mama cha kubangua korosho katika kata ya Nyegendi jimbo la Mtama.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki
kazi ya kuchambua korosho kwa mashine katika kata ya Nyegendi wakati
alipokitembelea kikundi cha kubangua korosho kinachoendeshwa na akina
mama.
Baadhi ya wajumbe wa mkutano mkuu wa jimbo la Mtama wakiwa katika kikao cha ndani wakizungumza na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana .
Mbunge wa jimbo la Mtama na Mjumbe wa Halmashauri kuu ya Maifa Mh. Bernard Membe akizungumza na wajumbe wa mkutano huo huku Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisikilizia wa pili kutoka kushoto ni Nape Nnauye Katibu wa NEC Siasa, Itikadi na Uenezi.
Nape Nnauye Katibu wa NEC Siasa, Itikadi na Uenezi.
kushoto na Mbunge wa jimbo la Nchinga Mh. Said Mtanda wakicheza ngoma
za asili ya kabila la Kimakonde wakati wa mkutano wa hadhara wa CCM
uliofanyika katika kata ya Chiuta jimbo la Mtama mkoani Lindi
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia umati wa wananchi
katika mkutano wa hadhara uliofanyika kata ya Chiuta leo.
Nape
Nnauye Katibu wa NEC Siasa, Itikadi na Uenezi akimsikiliza Mbunge wa
jimbo la Mtama Mh. Bernard Membe wakati wa mkutano huo.
Mbunge wa jimbo la Mtama Mh. Bernard Membe akizungumza na wananchi wa jimbo lake katika kata ya Chiuta leo.
MWANAMUME MMOJA AUAWA NA KISHA MWILI WAKE KUTUPWA MTONI
TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA KWA VYOMBO VYA HABARI
“PRESS RELEASE” TAREHE 18.11.2014.
- MWANAMUME MMOJA AUAWA NA KISHA MWILI WAKE KUTUPWA MTONI NA WATU WASIOFAHAMIKA WILAYANI KYELA.
MWANAMUME MMOJA ALIYETAMBULIKA KWA
JINA LA HENRY AMBAKISYE (60) MKAZI WA KIJIJI CHA KANDETE ALIKUTWA
AMEUAWA NA KISHA MWILI WAKE KUTUPWA MAJINI KATIKA MTO KANDETE NA WATU
WAWILI AMBAO BADO HAWAJAFAHAMIKA MAJINA WALA MAKAZI YAO.
MWILI WA MAREHEMU ULIKUTWA KATIKA
MTO HUO MNAMO TAREHE 17.11.2014 MAJIRA YA SAA 11:00 ASUBUHI HUKO KATIKA
KIJIJI CHA KANDETE, KATA YA KAJUNJUMELE, TARAFA YA UNYAKYUSA, WILAYA YA
KYELA, MKOA WA MBEYA.
AWALI MNAMO TAREHE 15.11.2014
MAJIRA YA SAA 23:00 USIKU WAKATI MAREHEMU ANATOKA NGOMANI AKIWA NA
MWANAMKE MMOJA AITWAYE KISA KIMA (48) MKAZI WA KAPWILI ALIVAMIWA NA
KISHA KUSHAMBULIWA NA WATU HAO. AIDHA MWANAMKE HUYO BAADA YA KUONA HALI
HIYO ALIKIMBIA NA KUTOWEKA ENEO LA TUKIO.
MWILI WA MAREHEMU ULIKUTWA NA
MAJERAHA YA KUPIGWA NA KITU KIZITO KICHWANI UTOSINI. CHANZO CHA MAUAJI
HAYO NI UGOMVI WA KUGOMBEA MWANAMKE. KISA KIMA ANASHIKILIWA NA JESHI LA
POLISI MKOA WA MBEYA KWA MAHOJIANO ZAIDI KUHUSIANA NA TUKIO HILO. AIDHA
JUHUDI ZA KUWATAFUTA WALIOHUSIKA KATIKA TUKIO HILI ZINAENDELEA.
Imesainiwa na:
[BARAKAEL N. MASAKI – ACP]
KAIMU KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.
IGP MANGU AONGEZA ASKARI KITETO
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini,IGP
Ernest Mangu akimsikiliza Diwani wa Kata ya Matui Wilayani Kiteto
Bw.Athuman Kidawa wakati alipofanya ziara wilayani humo kufuatia kuwepo
kwa migogoro ya ardhi baina ya wakulima na wafugaji iliyosababisha
kutokea mapigano yaliyosababisha kutokea kwa vifo.kushoto ni Afisa
tarafa wa Matui Bw.Eliakimu Ndelekwa.(Picha na Frank Geofray-Jeshi la
Polisi)
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini,IGP
Ernest Mangu akizungumza na wananchi wa Kata ya Matui Wilayani Kiteto
wakati alipofanya ziara wilayani humo kufuatia kuwepo kwa migogoro ya
ardhi baina ya wakulima na wafugaji iliyosababisha kutokea mapigano
yaliyosababisha kutokea kwa vifo. (Picha na Frank Geofray-Jeshi la
Polisi)
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini,IGP
Ernest Mangu akizungumza na Mtendaji wa Kijiji cha Chekanao, Kata ya
Kiperesa , Wilayani Kiteto Bw.Omar Ndee (kulia) wakati alipofanya ziara
wilayani humo kufuatia kuwepo kwa migogoro ya ardhi baina ya wakulima na
wafugaji iliyosababisha kutokea mapigano yaliyosababisha kutokea
kwa vifo.Katikati ni Kamanda wa Polisi Mkoa wa Manyara, Deusdedit
Nsimike pamoja na Mwenyekiti wa Kijiji hicho Bw.Japhet Chafu (Picha na
Frank Geofray-Jeshi la Polisi)
Na Frank Geofray-Jeshi la Polisi, Kiteto.
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini
IGP Ernest Mangu ameahidi kuongeza idadi ya Askari katika kijiji cha
Chekanao, kata ya Kiperesa wilayani Kiteto Mkoani Manyara kufuatia
wananchi katika kijiji hicho kujitolea nyumba kwa ajili ya kuishi Askari
kwa lengo la kuimarisha usalama katika maeneo yao kufuatia kuwepo kwa
migogoro ya ardhi inayosababisha kutokea kwa mauaji.
IGP Mangu aliyasema hayo jana
wakati alipokuwa katika ziara Wilayani Kiteto ya kujionea uharibifu
uliojitokeza pamoja na kutafuta ufumbuzi wa migogoro hiyo iliyopelekea
kutokea kwa vifo vya wakulima na wafugaji hivi karibuni katika wilaya
hiyo ambapo watu kadhaa wanashikiliwa na Jeshi la Polisi kutokana na
vurugu hizo.
Alisema kufuatia kuwepo kwa
umbali mrefu wa kituo cha Polisi na kijiji hicho atahakikisha askari wa
kudumu wanakuwepo ili kushirikiana na wananchi katika kuwabaini wahalifu
wanaofanya vurugu na kuendeleza migogoro hiyo ambapo wananchi nao
waliahidi kujenga kituo cha Polisi.
Kwa upande wake Mtendaji wa
Kijiji cha Chekanao Bw.Omar Ndee alisema wamekuwa wakipata shida
kutokana na umbali mrefu wa kituo cha Polisi jambo ambalo limekuwa
likifanya kuongezeka kwa vitendo vya uhalifu vinavyochangiwa na migogoro
ya ardhi katika wilaya ya Kiteto.
Naye Mwenyekiti wa Kijiji hicho
Japhet Chafu alilishukuru Jeshi la Polisi kwa kuimarisha usalama
kijijini hapo tangu kutokea kwa mauji ya wakulima na wafungaji ambapo
alibainisha kuwa bila kuwepo wao hali ingekuwa mbaya zaidi kutokana na
kutokuwepo na muafaka baina ya wakulima na wafugaji.
“IGP hawa askari wako
wasingekuwepo hapa usingekuta mtu lakini tunawashukuru sana hawa askari
kwa kuwa hivi sasa hali ya usalama imerejea na hata shambani tumeanza
kwenda” Alisema Bw.Chafu.
IGP Ernest Mangu alitumia ziara
hiyo kuzungumza na Mkuu wa Wilaya ya Kiteto, kamati ya ulinzi na usalama
ya wilaya, Wakaguzi wa Tarafa pamoja na Askari Kata ili kutafuta
ufumbuzi wa migogoro hiyo na kuimarisha hali ya ulinzi na usalama.
Subscribe to:
Posts (Atom)