WAREMBO WANAOWANIA SHINDANO YA MISS TANGA 2016 USIPIME SASA KUFANYIKA IJUMAA MJINI TANGA

July 27, 2016

 Warembo wanaowania Taji la Mrembo wa Mkoa wa Tanga (Miss Tanga 2016) wakiwa kwenye pozi katika hotel ya Tanga Beach Resort kutakapofanyika shindano hilo Jumamosi wiki hii

Warembo hao wakiwa kwenye picha ya pozi



Warembo wanaowania Taji la Urembo Mkoa wa Tanga(Miss Tanga 2016) ambalo linaandaliwa na Kituo cha Radio cha TK FM cha Mjini Tanga kwa kushirikiana na Hotel ya Tanga Beach Resort wakiwa kwenye picha ya mapozi


Mratibu wa Shindano ya Miss Tanga 2016,Mboni Muya akizungumza na waandishi wa Habari leo kuhusiana na maandalizi ya kuelekea shindano hilo


Baadhi ya Warembo wakimsikiliza Mdau wa Tasnia ya Urembo hapa nchini Sinza,Beny Kisaka alipokuwa akizungumza nao mara baada ya kuitembelea kambi ya warembo hao wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Five Brothers Nassoro Makau

Warembo hao wakimsikiliza Mratibu wa Shindano ya Miss Sinza 2016 ambaye aliitembelea kambi hiyo leo

 Mdau wa Tasnia ya Urembo hapa nchini,Benny Kisaka akitoa nasaha kwa warembo wanaotarajiwa kushiriki kinyang'anyiro cha kumtafuta Mlimbwende wa Mkoa wa Tanga (Miss Tanga 2016 )itakayofanyika Ijumaa kesho  kwenye Ukumbi wa Hotel ya Tanga Beach Resort.
 Mdau wa Tasnia ya Urembo hapa nchini,Benny Kisaka akisisitiza jambo wakati akizungumza na warembo wanaotarajiwa kushiriki shindano la kumtafuta Mlimbwende wa Mkoa wa Tanga Ijumaa

WAZIRI SIMBACHAWENE ATEMBELEA RUVUMA NA KUKAGUA MAJENGO YA SHULE.

July 27, 2016

 Waziri wa Nchi Ofisi ya Raid TAMISEMI George Simbachawene akikagua jengo la darasa la while ya msingi Luegu wilaya ya Namtumbo baada ya kupata maafa mwaka uliopita.Waziri ametoa agizo kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo kutoa fedha  shilingi milioni 10 kwa ajili ya Ujenzi wa vyoo vya kudumu vya wanafunzi ndani ya mwezi mmoja.
 Wanafunzi wa kidato cha Tano shule ya sekondari Nasuli wilaya ya Namtumbo wakimsikiliza Waziri Simbachawene alipotembelea shule ambayo imeanzisha madarasa ya kidato cha tano mwaka huu.Jumla ya wanafunzi 90 wasichana wameanza masomo hadi  sasa.
 Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Dkt.Binilith Mahenge akimpongeza  Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais,TAMISEMI George Simbachawene alipomaliza kukagua ujenzi wa barabara  ya lami ya FFU-Matogoro yenye urefu wa kilometa 3.2 kwenye Manispaa ya Songea.
 Jengo la makao makuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Songea lililokamilika kujengwa ambalo leo  limekaguliwa na Waziri Simbachawene kwenye kijiji cha Lundusi,Peramiho.Waziri Simbachawene ameagiza ifikiapo tarehe 05 Agosti 2016 watumishi wote wa Halmashauri ya wilaya ya Songea wahamie na kuendelea na kazi baada ya kukamilika ujenzi wake.
Wananchi wa kijiji cha Lundusi Peramiho wakiwa kwenye mkutano wa hadhara uliohutubiwa na Waziri wa Nchi Ofisi  ya Rais  TAMISEMI George Simbachawene(hayupo pichani) wakati wa ziara yake  Mkoani Ruvuma leo
JAJI MKUU ATEMBELEA JENGO LA MAHAKAMA YA RUSHWA NA UHUJUMU UCHUMI LEO

JAJI MKUU ATEMBELEA JENGO LA MAHAKAMA YA RUSHWA NA UHUJUMU UCHUMI LEO

July 27, 2016

CHAN1 
Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Mheshimiwa Mohamed Chande Othman (Katikati) akimsikiliza Mhandisi wa Mahakama ya Tanzania, Khamadi Kitunzi akimuelezea jambo alipotembelea jengo litakalotumika kuanzisha Mahakama Kuu Divisheni ya Rushwa na Uhujumu Uchumi lililoko kwenye Shule ya Sheria (Law School) Sinza jijini Dar es salaam. Kulia ni Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu Mheshimiwa Ferdinand Wambali. 
CHAN2 
Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Mheshimiwa Mohamed Chande Othman (Katikati) akimuelezea jambo Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Hussein Kattanga alipotembelea  jengo litakalotumika kuanzisha Mahakama Kuu Divisheni ya Rushwa na Uhujumu Uchumi lililoko kwenye Shule ya Sheria (Law School) Sinza jijini Dar es salaam. Kushoto ni Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu Mheshimiwa Ferdinand Wambali. 
CHAN3 
Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Mheshimiwa Mohamed Chande Othman (Katikati) akimuelezea jambo Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Hussein Kattanga alipotembelea  jengo litakalotumika kuanzisha Mahakama Kuu Divisheni ya Rushwa na Uhujumu Uchumi lililoko kwenye Shule ya Sheria (Law School) Sinza jijini Dar es salaam. Kushoto ni Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu Mheshimiwa Ferdinand Wambali. 
CHAN4 
Hili ni jengo litakalotumika kuanzisha Mahakama Kuu Divisheni ya Rushwa na Uhujumu Uchumi lililopo kwenye Shule ya Sheria (Law School) Sinza jijini Dar es salaam.

VIJANA WAMETAKIWA KUJIUNGA KWENYE VIKUNDI VYA UJASILIAMALI NAKUACHA KUTUMIA MUDA WAO KUCHEZA BAO.

July 27, 2016

 Mbunge wa jimbo la Mkuranga, Abdallah Ulega akizungumza na wananchi wa kijiji cha Kibunguchana,kata ya mkamba ikiwa ni sehemu ya utaratibu ambao ameuweka wa kwenda kushukuru,na kuhimiza utekelezaji wa miradi ya maendeleo leo katiaka kijiji cha kibunguchana  mkoani Pwani.
 Mwenyekiti wa Serikali ya kijiji cha Kibunguchana, Ahamad Mbonde  akizungumza maneno yaufunguzi kabla ya kumkaribisha mbunge wa jimbo hilo Abdallah Ulega kuzungumza na wananchi hao leo mkoani Pwani.
 Mbunge ulega wajimbo la Mkuranga akihesabu fedha.
 Mbunge  wa Mkuranga Abdallah Ulega akikabidhi fedha taslimu shilingi laki tatu kwa  Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji Kibunguchana,  Ahamad Mbonde  kwa ajili ya kuazisha msingi wa ujenzi wa shule ya msingi kijijini hapo ambapo pia alifanya harambee ndogo iliyowashirikisha baadhi ya viongozi wa halmashauri hiyo akiwa Mwenyekiti wa halmashauri, Juma abed ambaye alichangia mifuko kumi yacementi na diwani wa kata hiyo Hassan Dunda alichangia pia mifuko kumi ya  cementi leo mkoani Pwani.
Wananchi wa kijiji cha Lupondo,kata ya mkamba wakimsikiliza kwa makini mbunge wao Abdallah ulega katika mkutano wake wakuwashuruku wananchi hao kwa kumchagua kuwa mbunge wa jimbo hilo huku akihaidi kutoawaangusha nakwamba atakuwa karibu na watu wake. Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya Jamii.

Na Mwandishi wetu.
MBUNGE  wa Jimbo la Mkuranga  Abdallah Ulega amewataka vijana wa Wilaya hiyo kujiunga katika vikundi vya vikoba  vinavyoazishwa kwenye maeneo yao  na kwamba wastarajie kuwa ahadi ya rais ya kutoa sh. Milioni50 kila kijijihaitaenda kwa mtu mmoja mmoja bali kwa kukaa katika makundi.

Amesema kuwa kama wananchi wanataka fedha hizo ziwafikie lazima wakae kwenye vikundi na si vinginevyo ,huku akisisitiza akina baba nao kuacha kutumia muda wao mwingi kucheza bao badala yake wajiunge katika vikundi.

Ulega ametoa wito huo  jimbo humo wakati akizungumza na wanachama wa kikundi cha Vikoba cha Tuamke kilichopo katika kijiji cha Lupondo kata ya mkamba.

Alisema kuwa hakuna namna kwani maendeleo yanakuja Kwa kukaa katika vikundi mbalimbali na hata fedha za rais zitaelekezwa katika vikundi hivyo,hivyo kazima watanzania wachangamkie fursa hiyo.

"Binafsi Leo nawachangia sh.laki tatu kwani mmeonesha dhamira ya dhati kupitia risala yenu ambayo mmesoma mbele yangu nami nahaidi nitakuwa pamoja nami kamwe si tawaacha."alisema Ulega.

Aidha alisema kuwa yeye kama mbunge kuna mipango mingi ambayo anayo Kwa ajili ya watu wake ikiwa pamoja na kuleta watu wenye makampuni ya Pikipiki ili kuja katika wilaya hiyo na kukopesha vijana Pikipiki hizo na baadae kulipa kidogokidogo Kwa muda wa miezi 11.

Alisema kuwa lazima vijana,akina baba na akina mama Kwa pamoja wakubali kutengeneza vikundi vya vikoba kwani fursa nyingi zinapitia katika vikoba na si Kwa mtu mmoja mmoja.

Aidha Ulega akiwa katika ziara ya kijiji cha Lupondo alipata fursa ya kufungua jengo la Tuamke Vikoba ambapo pia alitembelea Zahanati ya Kijiji hicho nakuhaidi kutatua tatizo la miundombinu ya Maji.

Alisema kuwa anatambua kuwa Zahanati hiyo inachangamoto kubwa ya Maji hivyo atahakaikisha anasimamia ujenzi wa kisima pamoja na kuona Zahanati hiyo inapata umeme wa Tanesco Kwa ajili ya kurahisisha utoaji huduma.

"Nitajitahidi kadri ya uwezo wangu wote kuleta umeme hapa na kama ule wa tanesco utachelewa basi nitahakikisha naleta solar hapa."alisema Ulega.

Pia mbunge huyo alisema kuwa wananchi watambue kuwa yupo Kwa ajili yao na kwamba watakuwa pamoja katika kipindi chonde cha uongozi wake ikiwa pamoja na kuhakikisha anasukuma huduma jwa wananchi wake.

Naye Diwani wa Kata Dundani ,Hassan Dunda aliwaeleza wananchi hao kuwa uchaguzi umekwisha kilichobaki ni Kazi  huku akisisitiza kuwa watu kukaa katika makundi Kwa ajili kupata mikopo.

Ulega mbali na kufanya ziara katika kijiji cha Kupondo pia alitembelea vijiji vingine mbalimbali ndani ya Kata ya Mkamba ,ambapo pia anaendelea na ziara hizo za kutoa shukrani na kukagua miradi ya maendeleo.

BENDI 10 MAARUFU ZA MUZIKI WA DANSI KUWASHA MOTO JUMAMOSI VIWANJA VYA LEADERS NI KATIKA TAMASHA KUBWA LA MUZIKI WA DANSI

July 27, 2016

 Mwanamuzi wa mziki wa dansi, Ali Choki akiwaongoza wenzake kutoa burudani mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda walipofika ofisini kwake leo, kuzungumzia Tamasha la muziki huo litakalofanyika Jumamosi  Viwanja vya Leaders ambalo litashirikisha bendi 10 maarufu za hapa nchini.
 Baadhi wa wadau wa muziki wa dansi na wanahabari wakiwa kwenye mkutano huo.
 wanahabari wakichukua taarifa hiyo.
 Mdau wa muziki wa dansi, Asha Baraka akizungumza katika mkutano huo kuhusu tamasha hilo la kukata na shoka ambalo alijawahi kufanyika hapa nchini.
 Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaa, Paul Makonda akizungumza na wanamuziki hao kuhusu tamasha hilo la muziki wa dansi nchini.
 Mkutano ukiendelea.
RC Makonda akiwa katika picha ya pamoja na wanamuziki wa dansi baada ya kuzungumza nao ofisi kwake.

(Imeandaliwa na mtandao wa www. habari za jamii.com-simu namba 0712-727062)

HAPPY BORN DAY MWANANZENGO ELIZABETH BONIVENTURE KUTOKA 102.5 LAKE FM MWANZA.

July 27, 2016

Julai 27 miaka kadhaa iliyopita, ilikuwa siku ya kuzaliwa kwa Elizabeth Boniventure (kushoto) ambae ni miongoni mwa timu ya Wananzengo wa 102.5 Lake Fm Mwanza #RahaYaRockCity #RedioYaWananzengo.

Kama ilivyo ada, uongozi wa Lake Fm umemuandalia tafrija fupi, mitaa ya ofisini, Liberty Jijini Mwanza, ambapo Wananzengo wenzake wamejumuika pamoja kufurahia siku yake ya kuzaliwa kama picha zinavyoonekana.
BMG inakutakia Maisha Mema Mwananzengo Elizabeth Boniventure.

Kampuni ya Tigo yakabidhi vifaa vya michezo kwa chama cha mpira wa miguu wilaya iringa vijijini

July 27, 2016
Katibu wa chama cha mpira mkoani iringa (IRFA) Ramadhani Mahano akiwa na Meneja wa kampuni ya Tigo kanda  ya Kusini DAVIS KISAMO na kulia ni katibu wa chama cha mpira iringa vijijini JUMA LALIKA wakati wa makabidhiano ya vifaa vya michezo kwa chama cha mpira wa miguu wilaya iringa vijiji kwa ajili ya mashindano ya ligi  daraja la pili, Tigo  ndio wadhamini wa mashindano hayo.


Meneja wa kampuni ya Tigo kanda  ya Kusini DAVIS KISAMO na katibu wa chama cha mpira iringa vijijini JUMA LALIKA wakiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wachezaji wa timu shiriki



katibu wa chama cha mpira iringa vijijini JUMA LALIKA akimshuru meneja wa kampuni ya Tigo kanda  ya Kusini, DAVIS KISAMO mara baada ya kukabidhiwa vifaa vya michezo kutoka kampuni ya tigo wakati wa makabidhiano ya vifaa vya michezo kwa chama cha mpira wa miguu wilaya iringa vijiji kwa ajili ya mashindano ya ligi  daraja la pili, Tigo  ndio wadhamini wa mashindano hayo.

Meneja wa kampuni ya Tigo kanda  ya Kusini, DAVIS KISAMO akizungumza na baadhi ya viongozi wa timu shiriki zinazoshiri ligi ya wilaya ya iringa vijijini.
Meneja wa kampuni ya Tigo kanda  ya Kusini DAVIS KISAMO akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuwakabidhi vifaa vya michezo kwa viongozi wa chama cha mpira wa miguu iringa vijijini
photo Krantz Mwantepele Founder & CEO , KONCEPT Phone: +255-712579102 /+255-767392840 Email: krantzcharles@gmail.com Blog: www.mwanaharakatimzalendo.blogspot.com