ZAIDI YA BILIONI 23 ZAOKOLEWA KWA KUONDOA WATUMISHI HEWA.
Waziri
wa Nchi Ofisi ya Rais Manejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora,
Angela Kairukiakizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam
leo kuhusiana na maadhimisho ya wiki ya utumishi wa umma ambayo
hufanyika Juni 16 -23 kila mwaka.
Na Avila Kakingo, Globu ya Jamii.
SERIKALI
ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeokoa zaidi ya shilingi bilioni 23
kwa kuondoa watumishi hewa katika mfumo malipo ya mishahara ya
serikali.
Hayo yamesemwa na Waziri
wa Nchi Ofisi ya Rais Manejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora,
Angela Kairuki jijini Dar es Salaam leo wakati akizungumza na waandishi
wa habari, amesema kuwa kiasi hicho kimepatikana mara baada ya kuanza
kwa kutafuta watumishi hewa wa serikali.
Amesema
kuwa watumishi ambao wameshaondolewa tangu Machi, 1 hadi Mai 30 ni
watumishi 12,246 ameondolewa kwenye mfumo wa malipo ya mishahara ya
Serikali kwa sababu mbalimbali ikimo kutimiza umri wa Kustaafu kwa
lazima, kufukuzwa kazi, vifo na kuhitimishwa kwa mikataba.
Aidha amesema kuwa wasingeondolewa kwenye mfumo wa mishara kwa wafanyakazi wa serikali zaidi ya shilini Bilioni 25 zingepotea.
WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AFUTARISHA WANANCHI DAR ES SALAAM
Mke
wa Waziri Mkuu, Mary Majaliwa akiwa na baadhi ya waalikwa katika
futari ilyoandaliwa na Waziri Mkuu, kwenye makazi yake jijini Dar es
salaam Juni 10, 2016. Wapili kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Temeke,
Sophia Mjema.
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na baadhi ya waalikwa waliohudhuria
futari aliyoiandaa kwenye makazi yake jiji Dar es salaam
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na baadhi ya waalikwa waliohudhuria
futari aliyoiandaa kwenye makazi yake jiji Dar es salaam
Waziri
Mkuu Kassim Majliwa akisalimiana na Bw. Seif Ali Seif katika futari
aliyoiandaa kwenye makazi yake jijini Dar es salaam
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimian na Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Raymound
Mushi katika futari aliyoiandaa kwenye makazi yake jijini Dar es
salaam Juni 10, 2016.
Mke
wa Waziri Mkuu, Mama Mary Majaliwa akisalimiana na baadhi ya waalikwa
walioshiriki katika futari iliyoandaliwa na Waziri Mkuu kwenye Makazi
yake jijini Dar es salaam Juni 10, 2016. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya
Temeke Sophia Mjema.
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na baadhi ya waalikwa waliohudhuria
futari aliyoiandaa kwenye makazi yake jiji Dar es salaam
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiongea na waalikwa waliohudhuria futari aliyoiandaa kwenye makazi yake jiji Dar es salaam
Waziri
Mkuum Kassim Majaliwa akisalimiana na Katibu Kamati ya Amani ya
Viongozi wa Dini ya mkoa wa Dar es salaam, Padri John Solomon wa Kanisa
la Anglikani (kulia) na Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Sheikh wa Mkoa wa
Dar es salaam , Alhad Mussa Salum katika Futari iliyoandaliwa na Waziri
Mkuu kwenye makazi yake jijini Dar es salaam Juni10, 2016.
Swala kabla ya kufuturu
Mke
wa Waziri Mkuu, Mama Mary Majaliwa akiwa katika picha ya pamoja na
wanawake walioshiriki katika futari aliyoiandaa Waziri Mkuu, Kassim
Majaliwa kwenye makazi ya Waziri Mkuu jijini Dar es salaam Juni 10,
2016. Kulia kwake ni Mkuu wa Wilaya ya Temeke Sophia Mjema.
Mke
wa Waziri Mkuu, Mary Majaliwa akisalimiana na Mke wa Mwenyekiti wa CCM
wa mkoa wa Dar es salaam Azalina Madabida katika futari aliyoiandaa
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kwenye Makazi yake jijini Dar es salaam
Baadhi ya waalikwa wakishiriki katika futari iliyoandaliwa na Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa kwenye makazi yake jijini Dar es salaam Juni 10,
2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
HALMASHAURI YA MBEYA YAKAMILISHA UTENGENEZAJI MADAWATI WAMKABIDHI MKUU WA MKOA WA MBEYA AYAGAWE KWA SHULE 51
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Amos Makalla akikagua madawati hayo kabla ya kuyagawa.
Mkuu wa Mkoa, Amos Makalla akigawa madawati hayo.
Halmashauri
ya Mbeya imekamilisha utengenezaji wa madawati 5,371 ikiwa ni agizo la
Rais kuhakikisha wanafunzi wote wanakaa katika madawati.
Akisema
taarifa kwa Mkuu wa mkoa wa Mbeya, Amos Makalla, mkurugenzi wa
halmashauri hiyo Upendo Sanga amesema wamekamilisha maoema utengenezaji
madawati mapema kabla ya juni 30 kwenda sambamba na agizo la Mkuu wa
mkoa halmashauri zote zikamilishe madawati tarehe 20 juni siku kumi
kabla ya tarehe ya mwisho ya mheshimiwa Rais.
Mkuu wa Mkoa amekabidhi madawati 3,746 kwa shule 51 na yaliyobaki ameagiza yaendelee kukabidhiwa kwa Shule zingine.
Amesisitiza halmashauri zote kukamilisha utengenezaji wa madawati ifikapo tarehe 20 Juni.
MASAUNI AFANYA ZIARA MKOANI GEITA, ATEMBELEA KITUO CHA POLISI KILICHOLALAMIKIWA BUNGENI
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akizungumza na mamia ya wananchi wa Kijiji cha Nyakabale, Kata ya Mgusu, mkoani Geita ambao ni majirani wa Kampuni ya Uchimbaji wa Dhahabu ya GGM mkoani humo. Wananchi hao wamelalamika kuwepo na vitendo vya ukatili dhidi yao vinavyofanywa na baadhi wa askari wa kampuni hiyo. Hata hivyo Mhandisi Masauni aliwataka Polisi mkoani humo kufanya uchunguzi wa haraka dhidi ya tuhuma hizo.
Mkazi wa Kijiji cha Nyakabale, Kata ya Mgusu, mkoani Geita, Biosi Makongoro akitoa kero yake kwa Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kushoto aliyekaa) dhidi ya Kampuni ya Uchimbaji wa Dhahabu ya GGM mkoani humo ambayo ipo jirani na kijiji hicho, kuwa askari wa kampuni hiyo wanadaiwa kuwanyanyasa wananchi hao wanapopita katika eneo la Kampuni hiyo. Hata hivyo Mhandisi Masauni aliwataka Polisi mkoani humo kufanya uchunguzi wa haraka dhidi ya tuhuma hizo.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kulia) akiwasili Kituo cha Polisi Runzewe kilichopo Kata ya Uyovu wilayani Bukombe ambacho Mbunge wa Jimbo hilo, Dotto Biteko aliuliza swali la nyongeza Bungeni hivi karibuni akisema kituo hicho kinahitaji matengenezo makubwa na kumuomba Naibu Waziri huyo kufanya ziara jimboni kwake kujionea kituo hicho. Hata hivyo, Masauni alisema Serikali yake itahakikisha kituo hicho kitakuwa katika hali nzuri.
Mkuu wa Kituo cha Polisi Runzewe kilichopo Kata ya Uyovu wilayani Bukombe, Jackson Kirahuka akimuonyesha Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kushoto aliyevaa koti) sehemu mbalimbali za kituo hicho ambacho Mbunge wa Jimbo la Bukombe, Dotto Biteko (katikati) aliuliza swali la nyongeza Bungeni hivi karibuni akisema kituo hicho kinahitaji matengenezo makubwa na kumuomba Naibu Waziri huyo kufanya ziara jimboni kwake kujionea kituo hicho. Hata hivyo, Masauni alisema Serikali yake itahakikisha kituo hicho kitakuwa katika hali nzuri. Aliyevaa Kaunda suti ni Mkuu wa Wilaya hiyo, Amani Mwenegoha.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (wa pili kushoto) akizungumza jambo na Mkuu wa Mkoa wa Geita, Meja Jenerali, Mstaafu Ezekiel Kyunga (meza kuu), Mbunge wa Jimbo la Geita Vijijini, Joseph Msukuma (kulia), na Mkuu wa Jeshi la Polisi mkoani humo, Mponjoli Mwabulambo, wakati Naibu Waziri huyo alipofanya ziara ya kikazi mkoani humo.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akimfafanulia jambo Mbunge wa Jimbo la Geita Vijijini, Joseph Msukuma (watatu kulia), na Mkuu wa Jeshi la Polisi mkoani humo, Mponjoli Mwabulambo (wapili kushoto), wakati Naibu Waziri huyo alipofanya ziara ya kikazi mkoani humo.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kulia) akitoka ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bukendo, Amani Mwenegoha (kushoto) mara baada ya kumaliza kikao cha Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya hiyo iliyopo mkoani Geita. Naibu Waziri alifanya ziara ya kikazi mkoani Geita. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
WAZIRI PROF. MBARAWA AKEMEA HUJUMA KWENYE MIUNDOMBINU YA BARABARA MKOANI SINGIDA
Waziri
wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa (wa pili
kushoto), akijadiliana jambo na Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Manyoni Bw.
Gishuli Charles (wa nne kushoto), wakati alipoanza ziara yake ya ukaguzi
wa miundombinu katika Mkoa wa Singida. Wa kwanza kushoto ni Meneja wa
Wakala wa Barabara nchini (TANROADS) Mkoa wa Dodoma Eng. Leonard
Chimagu, na wa tatu kushoto ni Meneja wa TANROADS Mkoa wa Singida Eng.
Leonard Kapongo.
Meneja
wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), Mkoa wa Singida Eng. Leonard
Kapongo akimuonesha Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano, Prof.
Makame Mbarawa uharibifu wa barabara unaotokana na ajali za barabarani
katika barabara ya Manyoni-Itigi-Chaya yenye urefu wa Kilometa 89.3
mkoani Singida.
Wananchi
wa Itigi wakimsilikiza Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano, Prof.
Makame Mbarawa, (hayupo pichani) alipotangaza kuanza kwa ujenzi wa
barabara ya Mkiwa-Itigi-Makongorosi kwa kiwango cha lami itakayoanza
kujengwa kwa kilomita 35 mkoani Singida.
Meneja
wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), Mkoa wa Singida Eng. Leonard
Kapongo (wa tano kushoto) akitoa maelezo kwa Waziri wa Ujenzi Uchukuzi
na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa (wa nne kushoto) kuhusu mradi wa
ujenzi wa mzani katika barabara ya Manyoni-Itigi-Chaya ambao ujenzi
utakamilika hivi karibuni.
Muonekano wa ujenzi wa kituo cha Mzani Itigi, kinachojengwa katika barabara ya Manyoni-Itigi-Chaya, mkoani Singida.
Waziri
wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa, akionesha moja
ya picha ya uharibifu wa alama za barabarani uliofanywa na wananchi
katika ujenzi wa barabara ya Manyoni-Itigi-Chaya yenye urefu wa Kilomita
89.3.
Waziri
wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa, akihutubia
wananchi wa Itigi mara baada ya kukagua barabara ya Manyoni-Itigi-Chaya
yenye urefu wa Kilomita 89.3 mkoani Singida, ambayo ujenzi wake kwa
kiwango cha lami umekamilika kwa asilimia 98.
Waziri
wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa, akisalimiana
na wananchi wa Itigi mara baada ya kuhutubia mkutano wa hadhara.
Katikati ni Mbunge wa Manyoni Magharibi Mhe. Omary Yahya Massare.
Muonekano
wa Barabara ya Manyoni-Itigi-Chaya yenye urefu wa Kilomita 89.3
inayojengwa na Mkandarasi SynoHydro Corporation Limited kutoka China
inayojengwa kwa gharama ya shilingi bilioni 109 mkoani Singida.
Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini,
Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.
Subscribe to:
Posts (Atom)