WAZIRI MKUU WA ZAMANI WA TAIFA LA ISRAEL ATEMBELEA SERENGETI NA NGORONGORO

April 15, 2017
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani akisalimiana na Waziri Mkuu wa zamani wa taifa la Israel,Ehud Barak walipokutana katika eneo la Olduvai Gorge katika Hifadhi ya Taifa ya Ngorongoro akiwa njiani kuelekea katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti (katikati) ni Meneja Mawasiliano wa Shirika la Hifadhi za Taifa(TANAPA) Pascal Shelutete.
Waziri Mkuu wa zamani wa Taifa la Israel,Ehud Barak (kushoto) akimueleza jambo Naibu Waziri wa Malisili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani baada ya kukutana katika eneo la Makumbusho ya kale la Olduvai Gorge ndani ya Hifadhi ya Ngorongoro akiwa njiani kuelekea Hifadhi ya Taifa ya Serengeti (kushoto) ni Meneja Mawasiliano wa TANAPA,Pascal Shelutete.
Mhandisi Ramo Makani akimueleza jambo Waziri Mkuu wa zamani wa Taifa la Israel ,Ehud Barak baada ya kukutana katika Hifadhi ya Taifa ya Ngorongoro akiwa njiani kuelekea Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.
Naibu Waziri wa Malisili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani (katikati) akimongoza Waziri Mkuu wa zamani wa Taifa la Israel ,Ehud Barak (kushoto) kutembelea eneo la Olduvai Gorge .kulia ni Meneja Mawasiliano wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Pascal Shelutete.
Waziri Mkuu wa zamani wa taifa la Israel ,Ehud Barak akitia saini katika kitabu cha wageni huku Naibu Waziri wa Malisili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani akishuhudia mara baada ya kufika eneo la Olduvai Gorge akiwa njiani kuelekea Hifadhi ya Taifa ya Serengeti kushudia tendo la wanyama aina ya Nyumbu wahamao kwa makundi.
Mhandisi Ramo Makani akimueleza jambo Ehud Barak.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani akieleza mambo ambayo amepata kuongea na Waziri Mkuu wa Israel baada ya kukutana nae katika ene la Olduvai Gorge.
Naibu Waziri wa Malisili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani akiwa katika picha ya pamoja na Watalii wa ndani baada ya kukutana nao katika eneo la Olduvai Gorge.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

WATAKAORUHUSU WATOTO KUZAGAA MITAANI SIKU KUU YA PASAKAKUKIONA-RPC TANGA”

April 15, 2017
IKIWA imebakia siku moja kabla ya sikukuu ya Pasaka, Jeshi la Polisi Mkoani Tanga limesema halitasita kuwachukulia hatua kali za kisheria wazazi na walezi ambao watawaacha watoto wao wakizagaa mitaa siku hiyo bila kuwepo kwa uangalizi.

Sambamba na hilo wamepiga marufuku pia wazazi na walezi kuacha watoto wao wadogo kuzagaa hovyo bila usimamizi mzuri kwani jambo hilo ni kosa kisheria.

Onyesho hilo limetolewa na Kamanda wa Polisi Mkoani
Tanga,Benedict Wakulyamba (Pichani kushoto ) wakati akitoa taarifa ya hali ya usalama katika mkoa wa Tanga kwa kipindi cha Mwezi Machi mwaka huu kwa waandishi wa habari.

Alisema kuwa kumekuwa na tabia kwa wazazi kuacha kuweka uangalizi mzuri kwa watoto wao hasa nyakati za sikukuu na kuwaacha wakizagaa mitaani jambo ambalo ni hatari kwao kwani wanaweza kukumbana athari mbalimbali.

Alisema uzembe huo unatumiwa na watu waovu kufanya vitendo vya uhalifu vikiwemo wizi, uvunjaji na kupotea kwa watoto pamoja na kuwataka wananchi kuwa kuwa makini na mali zao.
 
“Kama unavyojua sikukuu hii huambatana na shamra shamra kwenye nyumba za ibada na mitaa hivyo nipende kuchukua nafasi hii kuwakumbusha wakazi wa Tanga tusheherekee sikuu hii kwa amani na usalama”Alisema

Licha ya hivyo lakini pia Jeshi hilo limepiga marufuku mtu yeyote kulipua au kusababisha milipuko ya aina yoyote ile ikiwemo kulipua baruti, fataki au eksozi za magari.

Aidha alisema ni kosa kisheria kumiliki au kufanya kiti chochote
kinachoweza kusababisha milipuko au ajali ya moto kwa mujibu wa kifungu cha 13 cha sheria ya milipuko (sura ya 45 Re 2002) ambapo sheria hiyo inatoa adhabu ya faini ya shilingi milioni tano au kifungocha miaka mitano au vyote kwa pamoja.

RAIS DKT MAGUFULI AWEKA JIWE LA MSINGI LA UJENZI WA NYUMBA ZA MAKAZI MAGOMENI KOTA JIJINI DAR ES SALAAM LEO

April 15, 2017

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia wananchi wakati wa sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi kuashiria kuanza rasmi ujenzi wa nyumba za makazi eneo la Magomeni Kota jijini Dar es salaam leo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akikata utepe na viongozi wengine na muwakilishi wa wananchi kuashiria kuanza rasmi ujenzi wa nyumba za makazi eneo la Magomeni Kota jijini Dar es salaam leo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na viongozi wengine na muwakilishi wa wananchi wakishangilia baada ya kukata utepe kuashiria kuanza rasmi ujenzi wa nyumba za makazi eneo la Magomeni Kota jijini Dar es salaam leo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na muwakilishi wa wananchi wakifunua pazia kuashiria uwekaji wa jiwe la msingi kuanza rasmi ujenzi wa nyumba za makazi eneo la Magomeni Kota jijini Dar es salaam leo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na viongozi wengine akikagua eneo la ujenzi wa nyumba za makazi baada ya kuweka jiwe la msingi eneo la Magomeni Kota jijini Dar es salaam leo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na akipata maelezo kutoka kwa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo (TBA) Arch. Elius Mwakalinga wakati akikagua eneo la ujenzi wa nyumba za makazi baada ya kuweka jiwe la msingi eneo la Magomeni Kota jijini Dar es salaam leo. Wengine ni Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliani, Profesa Makame Mbarawa.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipongezwa kwa furaha na wasanii mbalimbali wa filamu na wananchi wakati akikagua eneo la ujenzi wa nyumba za makazi baada ya kuweka jiwe la msingi eneo la Magomeni Kota jijini Dar es salaam leo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipiga tumba wakati bendi ya Msondo Ngoma ikitumbuiza wananchi wakati wa sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi kuashiria kuanza rasmi ujenzi wa nyumba za makazi eneo la Magomeni Kota jijini Dar es salaam leo.

MIILI YA ASKARI NANE WALIOUAWA NA MAJAMBAZI MKOANI PWANI YAAGWA RASMI,WAZIRI MWIGULU ATANGAZA KIAMA KWA WATUHUMIWA

April 15, 2017
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchini, Mwigulu Nchemba, akitoa heshima za mwisho Dar es Salaam leo mbele ya majeneza yenye miili ya askari nane waliouawa na majambazi Kibiti wilayani Mkuranga mkoani Pwani juzi jioni.Kulia kwake ni Naibu Waziri wa wizara hiyo, Masauni.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchini, Mwigulu Nchemba, akitoa pole kwa wafiwa.
Ndugu,jamaa na marafiki wa wafiwa wakiwa katika shughuli hiyo ya kuaga miili ya wapendwa wao.
Maofisa wa Uhamiaji wakiwa kwenye shughuli hiyo.
Wananchi wakiwa katika shughuli hiyo ya uagaji wa miili hiyo.
Maofisa wa Polisi wakishiriki kuaga miili ya wenzao hao.
Foleni ya kuaga miili hiyo.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchini, Mwigulu Nchemba (kulia), akiteta jambo na Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Ernest Mangu wakati wa kuaga miili hiyo.

RAIS DKT MAGUFULI AZINDUA MAJENGO YA HOSTELI ZA WANAFUNZI WA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM LEO

April 15, 2017
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akilakiwa na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam Profesa Rwekaza Mukandala wakati akiwasili kuzindua majengo mapya ya mabweni ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam eneo la Mlimani jijini Dar es salaam. Kiushoto ni Mama Janeth Magufuli na kulia ni Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) Arch. Elius Mwakalinga. Mabweni hayo yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 3840, yamejengwa chini ya muda wa mwaka mmoja na yamegharimu shilingi bilioni 10.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongozana na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam Profesa Rwekaza Mukandala wakati akiwasili kuzindua majengo mapya ya mabweni ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam eneo la Mlimani jijini Dar es salaam.Mabweni hayo yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 3840, yamejengwa chini ya muda wa mwaka mmoja na yamegharimu shilingi bilioni 10.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipokea zawadi ya mchoro toka kwa Rais wa Wanafunzi wakati wa sherehe za kuzindua majengo mapya ya mabweni ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam eneo la Mlimani jijini Dar es salaam. . Mabweni hayo yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 3840, yamejengwa chini ya muda wa mwaka mmoja na yamegharimu shilingi bilioni 10.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia wakati wa sherehe za kuzindua majengo mapya ya mabweni ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam eneo la Mlimani jijini Dar es salaam. Kulia ni Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) Arch. Elius Mwakalinga. Mabweni hayo yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 3840, yamejengwa chini ya muda wa mwaka mmoja na yamegharimu shilingi bilioni 10.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipongezwa na na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam Profesa Rwekaza Mukandala wakati akielekea kuzindua majengo mapya ya mabweni ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam eneo la Mlimani jijini Dar es salaam. Mabweni hayo yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 3840, yamejengwa chini ya muda wa mwaka mmoja na yamegharimu shilingi bilioni 10.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisaidiana na viongozi wengine akizindua majengo mapya ya mabweni ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam eneo la Mlimani jijini Dar es salaam. Kulia ni Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) Arch. Elius Mwakalinga. Mabweni hayo yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 3840, yamejengwa chini ya muda wa mwaka mmoja na yamegharimu shilingi bilioni 10.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipata maelezo toka kwa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) Arch. Elius Mwakalinga wakati akizindua majengo mapya ya mabweni ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam eneo la Mlimani jijini Dar es salaam. Mabweni hayo yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 3840, yamejengwa chini ya muda wa mwaka mmoja na yamegharimu shilingi bilioni 10.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipongezwa na Waziri Mkuu Mstaafu Jaji Joseph Sinde Warioba baada ya kuzindua majengo mapya ya mabweni ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam eneo la Mlimani jijini Dar es salaam. Kulia ni Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam Profesa Rwekaza Mukandala Mabweni hayo yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 3840, yamejengwa chini ya muda wa mwaka mmoja na yamegharimu shilingi bilioni 10.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akikagua baadhi ya mabweni baada ya kuzindua majengo mapya ya mabweni ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam eneo la Mlimani jijini Dar es salaam. Mabweni hayo yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 3840, yamejengwa chini ya muda wa mwaka mmoja na yamegharimu shilingi bilioni 10.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia jambo na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam Profesa Rwekaza Mukandala (kushoto) na Mkuu wa Idara ya Sanaa za Ubunifu wa Chuo hicho Dkt. Kedmon Mapana baada ya kuzindua majengo mapya ya mabweni ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam eneo la Mlimani jijini Dar es salaam. Mabweni hayo yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 3840, yamejengwa chini ya muda wa mwaka mmoja na yamegharimu shilingi bilioni 10. PICHA NA IKULU

DUKA LA KISASA LA GSM MALL LAUNGUA MOTO DAR

April 15, 2017
 Magari ya Zimamoto na Uokoaji yakiwa nje ya Duka kubwa la GSM Mall tayari kuzima moto uliokuwa unaunguza duka hilo katika Barabara ya Nyerere eneo la Mtava, Dar es Salaam. Chanzo cha moto huo hakikuweza kujulikana mara moja. PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG
 Mmoja wa majeruhi wa ajali hiyo akiwahishwa hospitali.
 Pilikapilika katika lango kuu la kuingilia duka hilo

 Mmoja wa majeruhi akitolewa kwenda kwenye gari ili awahishwe hospitali kwa matibabu
Wananchi wakishuhudia ajali hiyo ya moto


Na Richard Mwaikenda 

DUKA kubwa la GSM Mall ililopo Barabara ya Nyerere eneo la Mtava, Dar es Salaam, linateketea kwa moto hivi sasa.

Kwa mujibu wa mashuhuda ni kwamba duka hilo lilianza kuungua majira ya 8;30,Hadi sasa chanzo cha moto huo hakijaweza julikana. 

Magari ya zimamoto na uokoaji yamejazana eneo hilo kunusuru mali na maisha ya watu waliokuwemo kwenye jengo hilo lenye ghorofa nne.

Watu wengi wakiwemo wafanyakazi wa duka hilo walionekana kutoka mkuku kuokoa maisha yao. Baadhi yao walitolewa wakiwa mahututi na kukimbizwa hospitali kwa kutumia magari ya polisi.

Duka hilo kubwa la kisasa lenye maduka yenye aina mbalimbali za bidhaa ni moja kati ya maduka makubwa yaliyopo jijini Dar es Salaam.

Waokoaji waliokuwepo wamepata wakati mgumu kuzima moto kutokana na ndani ya jengo hilo kuwa na giza nene lililotawaliwa na wingu la moshi uliosababishwa na moto huo.

Wamejitahidi kupata mwanga kwa kuwasha taa za magari karibu na lango kuu la kuingilia ndani lakini ilishindikana.

Kampuni ya TTCL Yatoa Msaada wa Pasaka kwa Yatima

Kampuni ya TTCL Yatoa Msaada wa Pasaka kwa Yatima

April 15, 2017
Meneja Uhusiano wa TTCL, Nicodemas Mushi (wa pili kulia) akimkabidhi Mama Mlezi Mkuu wa Kituo cha Valentino Children Home, Lucy Lipenga sehemu ya msaada wa vyakula na vinywaji vilivyotolewa na TTCL kwa ajili ya siku kuu ya Pasaka kwa watoto. Meneja Uhusiano wa TTCL, Nicodemas Mushi (kulia) akimkabidhi mbuzi Mratibu wa Kituo cha Watoto Wetu Kimara Suka, Musa Mgenzi (kulia) ikiwa ni sehemu ya msaada wa vyakula na vinywaji vilivyotolewa na TTCL kwa ajili ya siku kuu ya Pasaka kwa watoto. Meneja Uhusiano wa TTCL, Nicodemas Mushi (kulia) akiwakabidhi baadhi ya watoto wa Kituo cha Watoto Wetu Kimara Suka kiroba cha sukari ikiwa ni sehemu ya msaada wa vyakula na vinywaji vilivyotolewa na TTCL kwa ajili ya siku kuu ya Pasaka kwa watoto hao.

 KAMPUNI ya Simu Tanzania (TTCL) imetoa msaada wa vyakula mbalimbali na vinywaji katika vituo vya watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu kwa ajili ya kusherekea Siku Kuu ya Pasaka. Msaada huo wenye thamani ya shilingi milioni nne umetolewa leo Makao Makuu ya TTCL jijini Dar es Salaam ikiwa ni utaratibu wa kampuni hiyo kurejesha sehemu ya faida kwa jamii hasa inayoitaji msaada. Miongoni mwa vyakula vilivyotolewa ni pamoja na Unga wa sembe, mchele, sukari, chumvi, mafuta ya kula, maji, soda na mbuzi wawili kwa ajili ya watoto kufurahiya siku kuu hiyo. Akizungumza mara baada ya kukabidhi bidhaa hizo, Meneja Uhusiano wa TTCL, Nicodemas Mushi alisema vituo vilivyonufaika na msaada huo ni Kituo cha Watoto wetu cha Kimara Suka na Valentino Children Home cha Buza vyote vya jijini Dar es Salaam.   Viongozi wa Kituo cha Watoto Wetu Kimara Suka na Valentino Children Home cha Buza wakiwa pamoja na Meneja Uhusiano wa TTCL, Nicodemas Mushi katika picha ya pamoja huku wakipokea sehemu ya msaada uliyotolewa na TTCL kwa ajili ya siku kuu ya Pasaka. Meneja Uhusiano wa TTCL, Nicodemas Mushi (wa tatu kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watoto wa kituo cha Watoto Wetu Kimara Suka mara baada ya kuwakabidhi sehemu ya msaada wa vyakula na vinywaji vilivyotolewa na TTCL kwa ajili ya siku kuu ya Pasaka kwa watoto. Meneja Uhusiano wa TTCL, Nicodemas Mushi akiwa na Mama Mlezi Mkuu wa Kituo cha Valentino Children Home, Sista Lucy Lipenga katika picha ya pamoja na baadhi ya watoto wa kituo hicho walipopokea sehemu ya msaada wao. Meneja Uhusiano wa TTCL, Nicodemas Mushi (kulia) akigonganisha kinywaji na baadhi ya watoto wa Kituo cha Valentino Children Home cha Buza mara baada ya kupokea sehemu ya msaada uliotolewa na TTCL kwa ajili ya siku kuu ya Pasaka. Meneja Uhusiano wa TTCL, Nicodemas Mushi (kulia) akiwagawia vinywaji baadhi ya watoto wa Kituo cha Valentino Children Home cha Buza mara baada ya kupokea sehemu ya msaada uliotolewa na TTCL kwa ajili ya siku kuu ya Pasaka. Meneja Uhusiano wa TTCL, Nicodemas Mushi (katikati) akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kukabidhi msaada wa vyakula na vinywaji vilivyotolewa na TTCL kwa ajili ya siku kuu ya Pasaka kwa watoto wa vituo vya Watoto Wetu Kimara Suka na Valentino Children Home.[/caption] Akizungumza na wanahabari mara baada ya kukabidhi msaada huo kwa niaba ya Kaimu Ofisa Mtendaji wa TTCL, Waziri Kindamba, Mushi alisema huo ni utaratibu wa kawaida wa kampuni hiyo kusaidia vikundi mbalimbali vinavyoitaji msaada hasa kipindi hiki cha sikuu kuu. Alisema TTCL imekuwa ikirejesha sehemu ya faida yake kwa jamii kwa kusaidia makundi mbalimbali ili kuendeleza mahusiano mazuri na wateja wake.  Sehemu ya msaada wa vyakula na vinywaji vilivyotolewa na TTCL kwa ajili ya siku kuu ya Pasaka kwa watoto.