Simba Imeshinda katika mchezo wake wa Pili wa Mazoezi dhidi ya Timu ya Black Sailor kwa mabao 4–0

July 31, 2015


Kikosi cha Timu ya Black Sailor iliopanda daraja mwaka huu kucheza Ligi Kuu ya Zanzibar kwa Msimu wa mwakac 2015/2016, ilikubali kupigo cha mabao 4–0 dhidi ya timu ya Simba katika mchezo wa kirafiki uliofanyika usiku huu katika uwanja wa amaan Zanzibar. 
Kikosi cha Simba kilichotoa kipigo kwa Timu ya Black Sailor uwanja wa Amani usiku huu Simba ikiwa Zanzibar kwa michezo ya kirafiki kuimarisha Kikosi chake kujiandaa na Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania. 
       Jopo la Makocha wa timu ya Simba wakifuatilia mchezo huo wa kirafiki na timu ya Black Sailor.
Mchezaji wa timu ya Simba akikokota mpira akijiandaa kumpita beki wa timu ya Black Sailor, wakati wa mchezo wao wa kirafiki uliofanyika uwanja wa amaan timu ya Simba imeshinda 4–0.

Mchezaji wa timu ya Black Sailor akiwapita wachezaji wa timu ya Simba katika mchezo wa kirafiki.
                    Mshambuliaji wa timu ya Simba akimpita beki wa timu ya Black Sailor.
Mchezaji wa timu ya Simba Abdi Banda akiifungia timu yake bao la kwanza kwa kichwa katika mchezo huo wa kirafiki uliofanyika uwanja wa Amaan timu ya Simba imeshinda bao 4–0
Wachezaji wa Simba wakishangilia bao lao la kwanza lililofungwa na mchezaji Abdi Banda kwa kichwa baada ya kupigwa krosi na Khamis Kiiza, mwenye jezi namba 5
Mshambuliaji wa timu ya Simba akimpita beki wa timu ya Black Sailor wakati wa mchezo wao wa kirafiki.
              Mshambuliaji wa timu ya Simba Khamis Kiiza akimpita beki wa timu ya Black Sailor
Mshambuliaji wa timu ya Simba na Black Sailor wakiwania mpira wakati wa mchezo wao wa kirafiki uliofanyika uwanja wa Amaan Zanzibar timu ya Simba imeshinda 4–0 mchezo uliofanyika usiku huu.
Mshambuliaji wa timu ya Simba akizuiya mpira huku mabeki wa timu ya Black Sailor wakijiandaa kumzuiya.
       Kipa wa timu ya Black Sailor akidaga mpira ikiwa moja ya ulio gplini kwa timu ya Black Sailor
Mshambuliaji wa timu ya Simba akiruka kiunzi cha beki wa timu ya Black Sailor wakati wa mchezo wao wa kirafiki uliofanyika uwanja wa Amaan Timu ya Simba imeshinda 4–0
Goli la pili la timu ya Simba lililofungwa na mshambuliaji Ibrahim Hashim katika kipindi cha kwanza cha mchezo huo wa kirafiki uliofanyika uwanja wa amaan timu ya Simba imeshunda 4–0
                           Beki wa Timu ya Black Sailor akiokoa mpira galini kwake
Mchezaji wa Simba akiwa juu akipiga kichwa golini kwa timu ya Black Sailor.
Beki wa timu ya Black Sailor akioko mpira golini kwake wakati wa mchezo wa kirafiki uliofanyika katika uwanja wa Amaan Timu ya Simba imeshinda 4–0.
Picha na OthmanMapara.Blog. Zanzinews.com 

BALOZI DR MAHIGA DAWA SI KUHAMA CCM ASEMA YEYE NI MKOMBOZI WA CCM IRINGA MJINI.

July 31, 2015

Balozi Dr Mahiga -Iringa mjini.

Na matukiodaimaBlog
ALIYEKUWA balozi wa kudumu  wa umoja  wa mataifa (UN) na mgombea urais katika mchakato  wa ndani ya chama cha mapinduzi (CCM) balozi Dr Augustono Mahiga anayeomba kuteuliwa kuwa mgombea ubunge jimbo la Iringa mjini kupitia CCM amewashangaa makada  maarufu wa chama  hicho  walioshindwa katika mchakato wa ndani ya chama kwa nafasi ya urais kuhama chama hicho kuwa hao hawakuwa na mapenzi ya kuwatumikia  watanzania na kuwa watazunguka kote ila chama makini ni CCM pekee na kuwataka wana CCM jimbo la Iringa mjini kumpa nafasi yeye ili kuondoa masalia ya Chadema .

Balozi Dr Mahiga  alisema kuwa wana CCM hao  walioanza kuhama chama  kwa kukosa nafasi ya urais hawakuwa na mapenzi mema na CCM bali  walikuwa wawametanguliza  maslahi yao mbele na  kuacha kuangalia maslahi ya Taifa na chama hivyo ni vema watanzania  kuwatazama kwa jicho la tatu na ikiwezekana kuwachunguza japo kwa miaka 5 bila kuwachagua kuwa  viongozi  wao.

Alisema kuwa kama  suala ni uongozi kwa ajili ya  kuwatumikia  wananchi na chama kulikuwa hakuna  sababu ya kuhama chama ama kuanza kutukana chama kwa sasa ila wangeweza  kushuka chini na  kugombea nafasi za chini ukiwemo udiwani ama ubunge kama ambavyo  yeye alivyoshuka na kugombea ubunge ili kuwatumikia watanzania kwa ngazi ya ubunge.

"Kila nafasi ndani ya chama ina maana  kubwa katika kutumikia  watu hivyo kuhama chama si jambo jema na upande wa vyama lazima kuwa makini na wanachama wanaohama vyama kwa sasa ili  kupata nafasi za uongozi iwapo  watakosa nafasi hizo  bila shaka  watachukua hatua ya  kuvuruga nguvu ya vyama  hivyo ama kuhama vyama "

Balozi Dr Mahiga  aliyasema hayo  wakati akizungumza na waandishi wa habari mjini Iringa kuhusiana na mchakato mzima wa kumpata mgombea Urais wa CCM Dr  John Magufuli na mchakato wa kura  za maoni  katika ngazi ya udiwani na ubunge katika  jimbo la Iringa mjini ambako  ni mmoja kati ya  wana CCM 14  wanaoomba kuteuliwa kuwa wagombea wa ubunge .


Alisema akiwa kati ya  wana CCM 41 waliojitokeza  kuchukua fomu ya Urais hana kinyongo na uteuzi wa mgombea  Urais wa CCM Dr Magufuli kwani ni mtu  makini na safi ambae  viatu  vya Rais wa awamu ya nne Dr Jakaya Kikwete ataweza  kuvimudu  vema kutokana na kutokuwa  mtu wa kulipisha  kisasi na hana  makuu na mtu  zaidi ya  kulitumikia Taifa  .

Hivyo alisema iwapo wana CCM  jimbo la Iringa mji watamchagua yeye  kuwa mgombea ubunge  jimbo  hilo wawe imani  ya  kulikomboa jimbo hilo asubuhi  saa 12 kutoka kwa  Chadema  chini ya aliyekuwa mbunge  wa jimbo hilo mchungaji Peter Msigwa kwani alisema  si kweli kama Chadema Iringa mjini wananguvu kubwa kuliko  ya CCM na ukitazama idadi ya wenyeviti wa mitaa ambao CCM inao wenyeviti  104  huwezi linganisha na  wale 64 wa  Chadema kabla ya wenyeviti wake 13 kuvuliwa nafasi zao  na mahakama.

Alisema dawa ya ushindi  wa kishindo kwa CCM Iringa mjini ni moja pekee  kuvunja makundi na kuwa kundi moja la ushindi baada ya zoezi la kura za maoni kumalizika .
Dc Mwamoto  kulia akiwa na mbunge wa Kalenga Godfrey Mgimwa ,mwamoto ni mgombea ubunge Kililo
Mkuu wa wilaya  ya Kaliuwa mkoani Tabora Bw  Venance Mwamoto ambae anawania kuteuliwa kuwa mgombea ubunge  jimbo la Kilolo mkoani Iringa amesema kuwa tishio la  kutaka kuuwawa kwake  majuzi baada ya  kufyatuliwa risasi katika gari lake  wakati akitoka katika kampeni  kata ya  Ilula bado haimtishi  katika safari yake ya  kuwatumikia  wananchi  wa jimbo la Kilolo linaloongozwa na Prof. Peter Msolla .

Kwani alisema moja kati ya ahadi yake  kubwa kwa wananchi wa Kilolo ni  kuona amawatumikia kwa kasi zaidi na kumaliza kero ya maji katika mji  wa Ilula na changamoto nyingine ambazo hazijapatiwa ufumbuzi kwa kipindi kilichopita na mbunge  aliyekuwepo .

Mwamoto  alisema kuwa kazi nzuri  aliyoifanya kwa nafasi ya  ukuu  wa wilaya  kwa kipindi  kifupi ambacho  Rais Dr Jakaya kikwete alipomteua kwa  kuwa mkuu  wa wilaya ya  Kibonde na Kaliuwa ni wazi ni  kipimo tosha na heshima kubwa ya wananchi  wa Kilolo kujivunia na  wategemee makubwa zaidi  iwapo  watamchagua kuwa mbunge  wao kwa  sasa .
                                             waziri Lukuvi - Isimani

Mbunge  wa  jimbo la Isimani Bw  Wiliam Lukuvi amewaomba wananchi  wa jimbo  hilo hasa  wanachama wa CCM kuendelea  kujenga imani kwake na kuwa ndani ya CCM kuna Demokrasi  na kila mwanachama ana sifa ya  kugombea nafasi  yoyote ndani ya  chama japo  kipimo  cha kuchaguliwa bado kipo  kwa wananchi  wenyewe ambao  wanaweza kumpima kwa kazi alizofanya badala ya kushawishiwa kwa manenio bila vitendo.

Lukuvi ambae ni waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi amesema kama  si wana Isimani kuonyesha ushirikiano  wao kwake na hata  kumchagua katika nafasi hiyo ya  ubunge basi heshima ambayo  ambayo  wana Iringa wameipata  kupitia  wizara yake leo  isingekuwepo .

Alisema suala la migogoro  ya ardhi  amepata  kulishughulikia kwa umaniki mkubwa na kuwa sulaa  hilo pia  lilikuwa ni kero kubwa hata kwa wananchi wake wa jimbo la Isimani ila kwa sasa kwa kiasi  limeanza kupungua na kuwa iwapo wataonyesha imani yao tena  wategemee kuona maendeleo makubwa zaidi katika jimbo hilo na kutaka baadhi ya kazi kubwa ambazo zimefanyika kuwa ni pamoja na barabara ya lami ya Iringa- Dodoma, umeme  vijini , ujenzi wa shule pamoja na ujenzi wa nyumba bora  kwa kupata bati za ruzuku .

"Tumekuwa pamoja  muda  wote katika maendeleo  na matatizo  hivyo lazima  kila  safari ina  wasindikizaji  wake na siku  zote penye maendeleo ndipo panapopendwa na wengi  ila bado kwa tathimini yetu Ismani ya  leo  sio ya jana . nimekomesha ulanguzi wa mazao kama mpunga ,alizeti  kwa kufunga mashine"
                   Godfrey Mgimwa -Kalenga

Mbunge wa jimbo la Kalenga  Godfrey Mgimwa anayeomba kuteuliwa tena kuwa mgombea wa CCM nafasi ya ubunge  amewashukuru wananchi  wa kalenga kwa kuonyesha ushirikiano kwake na kuwa hadi  sasa amepata  kutekeleza ahadi zake kwa wananchi kwa asilimia 99 na kuwa zipo changamoto mbali mbali ambazo  watampa tena nafasi ya ubunge atakwenda  kuzifanyia kazi .

Mgimwa ambae  amepata  kuongoza jimbo hilo kwa mwaka mmoja pekee akichukua nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo Dr Wiliam Mgimwa aliyefariki duni mwaka jana mwanzioni ,alisema zilikuwepo ahadi mbali mbali ambazo ziliachwa na mbunge aliyepita na tayari zote amezikamilisha kwa kipindi cha mwaka mmoja na kubwa anajivunia kuanzisha vikundi vya Vicoba  zaidi ya 60 ,ujenzi wa barabara , maji  vijiji ,umeme na uchangiaji wa ujenzi wa zahanati ,shule  na maabara na kuwa zaidi ya Tsh milioni 100 amepata  kutumia kwa kuchangia miradi ya maendeleo jimboni.

CHAGUA AMANI RAI KATIKA KURA ZA MAONI SINGIDA MJINI

July 31, 2015
Chagua Amani Rai Jimbo la Singida Mjini.
-- ---- Cathbert Angelo Kajuna, Founder and Mananging Director Kajunason Blog, P.O Box 6482, Dar es Salaam. Tel: +255 787 999 774 Alt: +255 765 253 445 www.kajunason.blogspot.com "Everything is Possible Through Peace & Stability''

KIDOTI :VIJANA WA JIJI LA ARUSHA CHANGAMKIENI FURSA ZA KIJASIRIAMALI

July 31, 2015

 Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Kidoti Jokate Mwegelo  (kidoti) akiwa na mabalozi wake aliwapata ndani ya mkoa wa Arusha tayari kwa kwenda mtaani kutangaza bidhaa zake zake za kidoti zilizoingia jijini Arusha kwa mara ya kwanza 

 warembo wa Kidoti wakiwa wako katika pozi wameshikilia baadhi ya bidhaa za Kidoti 
 mmoja wa mabalozi wa kidoti  aliyejulikana kwa jina la Anolia Agustino akiwa anaongea na waandishi wa habari

 Meneja masoko wa kampuni ya kidoti Peter Kasija akiwa anaongea na waandishi wa habari ndani ya viwanja vya triple A hii leo wakati walivyokuja jijini Arusha kutangaza bidhaa za kampuni yao
 mabalozi wa kidoti   wakiwa kazini
 baadhi ya bidhaa zinazosambazwa nakidoti jijini Arusha
 hizi ndizo ndala za kidoti
 mawigi ya kidoti ndio haya
Na Woinde Shizza 
wa libeneke la kaskazini blog

Wito umetolewa kwa vijana ndani ya jiji la Arusha kujitokeza katika
kuchangamkia fursa za kijasiriamali zinazojitokeza ili kuweza
kuwaepushia vijana na matendo maovu yanayoweza kuwafanya ndani ya
jamii kukosaa thamani.
Wito huo umetolewa na Joketi Mwigelwa (kidoti) wakati akichagua vijana
wajasiriamali ndani ya jiji la Arusha katika ukumbi wa triple A jijini
hapa ambapo anatarajia kuwapata wajasiriamali vijana ambao
hatawaingiza katika fursa ya wajasiriamali kwa kupitia kampuni yake ya
kidoti.

Alisema  kuwa amevutiwa  kuja kuwekeza ndani ya jiji la Arusha  katika
nyanza za ujasiriamali kwa kuwa anaelewa kuwa vijana wa jiji la Arusha
hususa ni wasichana wana muitikio mkubwa katika swala zima la
ujasiriamali na maendeleo binafsi.



Aidha alibainisha kuwa katika  mchakato huo wanatarajia kupata
wajasiriamali wapatao 13 ambapo tofauti na kujiingizia kipato cha
ujasiriamali pia watakuwa mabalozi wa kutangaza bidhaa zilizo chini ya
kampuni ya kidoti.
“ndugu mwandishi unavyowaona hawa wote hapa ni vijana kutoka mkoa
mzima wa arusha na mikoa ya jirani tunawafanyia usaili na kupata
vijana ambao wanakithi vigezo vya kuingia katika ujasiriamali ,utakao
wapelekea wao kufanya kazi na kampuni ya kidoti pamoja na kujiajiri
binafsi” alisema kidoti

Pamoja na hayo alisema kuwa kampuni hiyo kwa mwaka huu imeamua
makusudi kusogeza huduma za  ikiwemo bidhaa zake katika mikoa ya nje
ya jiji la Dar Es Salaam ili kuwapa furusa watu wa mikoani ambao
walikuwa hawazipati huduma za kidoti.

Kwa upande wa mmoja wa washiriki waliojitokeza katika mchujo huo
Anolia Agustino  alimpomgeza kidoti kwa hatuqa aliofikia ya kuwaajiri
vijana haswa wasiochana kwani   ,jambo hili litawasaidia wanasichana
wengi kupata ajira pamoja na kujiajiri binafsi.

Aidha alisema kuwa  mbali na kupata ajira pia kampuni hii itawasidia
kujifunza ujasiriamali pamoja na kujiajiri binafsi kwani ,bidhaa za
kidoti ni za bei na fuuu na unaweza kuanza kujiajiri kwa kutumia mtaji
mdogo.
Kwa upande wa mshiriki mungine ambaye teari alikuwa amenufaika na
kampuni ya kidoti aliyejitaja kwa jina la Anjela Mushi alisema kuwa
kampuni hii imemsaidia sana kwani alikuwa anakaa nyumbani bila kazi
lakini alivyoona kwenye mtandao wa kijamii aliamua kujitafuta
mawasiliano na kuanza  na mtaji mdogo na kwasasa ivi mtaji wake
umekuwa.

“mimi nilianza kuona bidhaa za kidoti katika mitandao ya kijamii kama
intagramu  nikaamua kutafuta mawasilano kwakeli nilipata na nilikuwa
na mtaji mdogo kwani nilianza na mtaji wa shilingi laki moja na sasa
na shilingi laki nne na biashara yangu nilianza mwezi wa tano na sasa
ni mwezi wa saba  kwa hadi sasa nina mienzi mitatu nashukuru mungu
mtaji wangu umekuwa”alisema Anjela.
Alimalizia kw akumpongeza kidoti na kumsihi aendelee kuwasaidia
wasichana kwani hivi sasa kumekuwa na changamoto ya ajira kwani ajira
imekuwa ni ngumu.

GLOBAL EDUCATION LINK INAKUKARIBISHA KATIKA MAONYESHO YA VYUO VIKUU - ARUSHA

July 31, 2015
GARI LA KUBEBEA MAJENEZA LA KIPEKEE LAINGIA NCHINI

GARI LA KUBEBEA MAJENEZA LA KIPEKEE LAINGIA NCHINI

July 31, 2015
IMG_0469
Pichani juu na chini ni muonekano wa Gari maalum la kukodisha kwa ajili ya shughuli za kubebea majeneza katika misiba limeingia nchini.
Kwa wanaohitaji kukodi kwa shughuli za misiba wanaweza kuwasiliana kupitia barua pepe kiwiaadavidson@hotmail.com au simu namba +255 715 213213, +255 713 616606 na +255 784616606
IMG_0459 IMG_0481
Muonekano wa ndani sehemu maalum linapowekwa jeneza.
IMG_0477
MSIMU MPYA WA KANDANDA NDANI YA DSTV KUTIMUA VUMBI WIKI IJAYO.

MSIMU MPYA WA KANDANDA NDANI YA DSTV KUTIMUA VUMBI WIKI IJAYO.

July 31, 2015
IMG_0388
Meneja Uhusiano wa Kampuni ya Multichoice Tanzania, Barbara Kambogi, akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa utambulisho wa msimu mpya wa kandanda kwa wateja wa DStv jana jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Afisa Masoko wa Multichoice Tanzania, Furaha Samalu na kulia ni Meneja Mwendeshaji wa Multichoice Tanzania, Ronald Baraka Shelukindo.(Picha zote na Zainul Mzige wa modewjiblog).
IMG_0397
Meneja Uendeshaji wa Multichoice Tanzania, Ronald Baraka Shelukindo, akijibu maswali ya waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusiana na huduma za DStv. Kushoto ni Meneja Uhusiano wa Kampuni ya Multichoice Tanzania, Barbara Kambogi.
IMG_0422
Afisa Masoko wa Multichoice Tanzania, Furaha Samalu, akielezea huduma za kuunganishwa kwa wateja wapya wa DStv, ambapo ving'amuzi pamoja na dishi vinapatikana kwa gharama nafuu kabisa ya Sh.99,000/- kwa mawakala wote wa DStv nchini.
IMG_0443
Meneja Uhusiano wa Kampuni ya Multichoice Tanzania, Barbara Kambogi (wa pili kushoto) akikabidhi zawadi ya begi kwa mwandishi wa habari, Joseph Michael baada ya kuchezesha droo kwa waandishi waliohudhuria mkutano huo. Wanaoshuhudia kushoto ni Afisa Masoko wa Multichoice Tanzania, Furaha Samalu na kulia ni Meneja Uendeshaji wa Multichoice Tanzania, Ronald Baraka Shelukindo.
IMG_0454
Furaha Samalu na Barbara Kambogi wakikabidhi zawadi ya begi Super Sport kwa mpiga picha wa ITV, Abdallah Kaniki aliyeibuka mshindi katika droo iliyochezeshwa na Multichoice Tanzania wakati wa mkutano na waandishi wa habari. Kulia Meneja Uendeshaji wa Multichoice Tanzania, Ronald Baraka Shelukindo.
IMG_0458
Meneja Uhusiano wa Kampuni ya Multichoice Tanzania, Barbara Kambogi akikabidhi zawadi ya T-shirts kwa mwandishi wa habari wa gazeti la Mwananchi, Imani Makongoro.
IMG_0419
Baadhi ya waandishi wa habari waliohudhuria mkutano huo uliofanyika jijini Dar es Salaam.
Na Andrew Chale, modewjiblog
Msimu mpya wa Soka 2015/16, unatarajia kuanza rasmi Jumapili ijayo kwa kushuhudia ligi mbalimbali Duniani zikichezwa na kurushwa moja kwa moja kupitia SuperSport ambayo imejipanga kukuletea burudani kabambe kwa mashabiki wa soka barani Afrika.
Meneja uendeshaji wa Multichoice Tanzania , Ronald Baraka Shelukindo mapema jana akizungumza na vyombo vya habari amebainisha kuwa, Wateja wa DStv wakae tayari msimu huu kwenye Ulimwengu wa Mabingwa ambapo timu mbalimbali zimejiimalisha katika kuakikisha zinatwaa ubingwa.
“Ligi ya mwaka zitakuwa za kasi na kuvutia kwa kila timu. Barcelona wanajiandaa kutawala dunia kwa mara nyingine, huku Manchester United wanahitaji kurudisha kiti chao cha Ubingwa Uingereza. Jose Mourinho analenga kuhakikisha Chelsea inabaki juu, wakati huo huo , Hispania inajiandaa kuhakikisha wanashinda kwa mara ya tatu kombe la Euro 2016.” Ameeleza Baraka Shelukindo.
Ameogeza kuwa, Watazamaji wa SuperSport watakuwa na nafasi ya kipekee kushuhudia mechi kwenye ubora wa HD, ikiwa ni pamoja na michuano ya Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) , Ligi ya Hispania (La Liga) , Ligi ya Mabingwa wa Ulaya(UEFA) na Ligi ndogo ya Ulaya ( Europa) ,mechi za FIFA za kirafiki za kimataifa na Klabu Bingwa ya Dunia , Kombe la Ujerumani , Kombe la Mfalme Hispania (Copa Del Rey) , Kombe la FA na zaidi.
Kwa upande wake, Meneja Uhusiano wa Multichoice Tanzania, Barbara Kambogi anaeleza kuwa, Katika msimu huu , Ulimwengu wa Mabingwa itakuwa ikionyesha mechi zaidi ya 900 za kimataifa. Wateja wa DStv Compact Plus wataweza kufurahia baadhi ya mechi zaidi ya 450 ‘live’, huku Wateja wa DStv Premium watazawadiwa mechi zote ‘Live’ zitakazorushwa katika chaneli zote za SuperSport .
“Kuanzia msimu huu na kuendelea, vituko vyote vya Ligi Kuu ya Uingereza vitakuwa vikiletwa kwenu kupitia SuperSport 5 ( SS5 ) inayopatikana kwenye kifurushi cha Premium. SS5 sasa itakuwa ni nyumba ya soka la Afrika kwa ligi kuu ya Uingereza huku ikijumuisha mechi 3 ‘Live’ kila Jumamosi na Jumapili. Kuambatana na mechi kutakuwa na vipindi maalum vya soka kama PLTV Kick Off, Match Day Live, Fan Zone, Saturday/Sunday Review, Football Today, Classic Matches, Netbusters na Mech za Wiki” Amebainisha Barbara Kambogi.
Moto wa La Liga utawashwa ndani ya SuperSport 3 ( SS3 ). Chaneli hii itakuwa inakuletea mechi hadi tatu za ligi ya Hispania ‘ Live’ kwa siku ya Jumamosi na Jumapili . Wateja wa DStv Premium na Compact Plus watapata nafasi ya kuangalia mechi za michuano ya Kombe la mashindano Uingereza ndani ya SS3 sambamba na mechi za Jumamosi mchana za Ligi kuu ya Uingereza , mbadala wa mechi inayorushwa ndani ya SS5, pamoja na Ratiba zote za Jumatatu usiku na vipindi vya mahojiano vya studio.
Pamoja na Mechi za ‘Live’ ndani ya SS3 , itakuwa inakuonyesha vipindi muhimu vya shoo za magazeti , yanayojiri ndani ya La Liga, pamoja na vipindi maalum vya ligi za soka . Makombe yote ya mpira wa miguu, Mabingwa wa Ulaya na Ligi ya Europa, Kombe la FA , Kombe la Mfalme Hispania (Copa Del Rey), Kombe la Ujerumani , Euro 2016 na mechi za kirafiki za kimataifa zitaendelea kutapatikana kwenye SS3 .
Kwa habari zaidi za michezo na ratiba za mechi kwenye SS5 na SS3, tafadhali tembelea www.supersport.com