Nchi 19 zashiriki Tamasha la Kimataifa la Lugha na Utamaduni nchini
Waziri wa Habari, Vijana,
Utamaduni na Michezo Mhe. Dkt. Fenella Mukangara akiwahutubia washiriki
wa Tamasha la Kimatafa la Lugha na Utamaduni lililoandaliwa na
Kilimanjaro Dialogue Institute na kufanyika katika Ukumbi wa Mwalimu
Nyerere jana Jijini Dar es Salaam na kuhusisha washiriki kutoka nchi 19
wakiwa na lengo la kuhamasisha matumizi ya lugha ya kiswahili.
Rais wa Kilimanjaro Dialogue
Institute Bw. Ali Akkiz akizungumza na washiriki wa Tamasha la Kimataifa
la Lugha na Utamaduni jana katika Ukumbi wa Mwalimu Nyerere Jijini Dar
es Salaam.
Waziri wa Habari, Vijana,
Utamaduni na Michezo Mhe. Dkt. Fenella Mukangara akipokea zawadi kutoka
kwa Rais wa Kilimanjaro Dialogue Institute Bw. Ali Akkiz wakati wa
Tamasha la Kimataifa la Lugha na Utamaduni jana katika Ukumbi wa Mwalimu
Nyerere Jijini Dar es Salaam.
Naibu katibu Mkuu Wizara ya
Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel kushoto
akifurahia maonyesho mbalimbali yaliyokua yakionyeshwa na vijana wakati
wa Tamasha la Kimatafa la Lugha na Utamaduni jana jijini Dar es Salaam.
Kulia ni Rais wa Kilimanjaro Dialogue Institute Bw. Ali Akkiz na wapili
kulia ni Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mhe. Dkt.
Fenella Mukangara.
Washiriki kutoka nchi 19
wakifuatilia kwa makini matukio yaliyokua yakiendelea katika Tamasha la
Kimatafa la Lugha na Utamaduni lililoandaliwa na Kilimanjaro Dialogue
Institute na kufanyika katika Ukumbi wa Mwalimu Nyerere jana jijini Dar
es Salaam.
Wanafunzi kutoka shule za Feza
wakiburudisha wakati wa Tamasha la Kimatafa la Lugha na Utamaduni
lililoandaliwa na Kilimanjaro Dialogue Institute na kufanyika katika
Ukumbi wa Mwalimu Nyerere jana jijini Dar es Salaam na kuhusisha
washiriki kutoka nchi 19 wakiwa na lengo la kuhamasisha matumizi ya
lugha ya kiswahili.
…………………………….
Na Lorietha Laurence na May-Zuhura Simba -Maelezo
Waziri wa Habari, Vijana,
Utamaduni na Michezo Mhe. Dkt. Fenella Mukangara ameeleza kuwa lugha ina
mchango mkubwa katika maendeleo ya jamii ikiwa itakuzwa sambamba na
maendelao ya teknolojia.
Kauli hiyo ameitoa jana jijini Dar es Salaam wakati wa Tamasha
la Kimataifa la Lugha na Utamaduni na kufafanua kuwa tamasha hilo
limeonyesha kukua kwa lugha ya Kiswahili ambao ni utambulisho wa nchi
yetu tangu kupatikana kwa uhuru.
“Mkusanyiko wa leo umeanzisha safari ndefu ya kukuza lugha yetu
ya Taifa toka ngazi za chini hadi za kimataifa, hivyo Tanzania
imefarijika kuwa mwenyeji wa shughuli hii muhimu “alisema Mhe. Dkt.
Mukangara.
Aliongeza kuwa kwa upande wa serikali ya Tanzania imechukua
hatua mbalimbali ya kukiendeleza Kiswahili kwa kukifanya kuwa lugha ya
kufundishia kuanzi shule ya Msingi hadi Elimu ya Juu.
Dkt. Mukangara ametoa wito kwa vijana kujifunza Kiswahili na
kuitumia lugha hiyo kuweza kujipatia ajira kwa kutangaza utumiaji wa
bidhaa za lugha na utamaduni ambazo zina thamani kubwa kiuchumi.
“Lugha ni sawa na kiwanda ikitumiwa vizuri italeta ajira kwa
jamii husika na kutumika kama lugha ya kufundisha wageni mbalimbali
wanaokuja nchini na hata nchi za nje kwa kuipa hadhi ya kuzungumzwa
sehemu mbalimbali” alisema Mhe. Dkt. Mukangara
Kwa Upande wa muandaaji wa tamasha hilo ambaye ni Rais wa Asasi
za Kilimanjaro Dialogue Institute, Bw. Ali Akkiz amesema kuwa kupitia
tamasha hilo wameweza kutangaza vivutio mbalimbali vya kiutamaduni vya
jijini Dar es salaam na Zanzibar.
“Kwa kweli watoto wamefurahi kushiriki katika tamasha hili kwa
kuweza kutembelea sehemu zenye vivutio vya utamaduni pamoja na historia
najua wataondoka na taswira nzuri ya kutokuisahau nchi ya Tanzania”
alisema Bw. Akkiz
Tamasha la Kimataifa la Lugha na Utamaduni ni la kumi 13
kufanyika ambalo limeshirikisha vijana wenye umri kati ya miaka 12 hadi
18 kutoka katika nchi 19 na nchi ya Tanzania kuwa mwenyeji wa tukio hili
kwa mara ya kwanza.
MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL ATEMBELEA ENEO LA BUGURUNI KWA MNYAMANI LILILOATHIRIKA NA MAFURIKO
Makamu wa rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanznaia, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimsikiliza
mkandalasi wa ujenzi wa mtaro wa kupitishia maji machafu wakati
alipotembelea eneo la Buguruni kwa Mnyamani leo Machi 23, 2015 kwa ajili
ya kukagua maeneo yaliyoathirika kutokana na mafuriko ya mvua
zinazoendele kunyesha jijini Dar es Salaam.
Picha na OMR
Makamu wa Rais wa jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipata maelezo juu ya
hatua zilizokwishachukuliwa na Serikali, kutoka kwa Mkuu wa wilaya ya
Ilala, Raymond Mushi, wakati Makamu alipotembelea eneo la Buguruni Kwa
Mnyamani lililoathirika na mafuriko yaliyotokana na mvua zinazoendelea
kunyesha jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiondoka eneo hilo
baada ya kujionea athari zilizotokana na mafuriko hayo kwa wakati wa
Buguruni kwa Mnyamani jijini Dar es Salaam, leo machi 23,
KILELE CHA MAADHIMISHO YA WIKI YA MAJI MKOA WA DODOMA
Mkuu
wa Wilaya ya Mpwapwa Dkt. Jasmine Tiisekwa aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa
wa Dodoma, akikata utepe kama ishara ya kuweka jiwe la msingi la mradi
wa maji wa kijiji cha Mseta wilayani Kongwa wakati wa kilele cha
maadhiisho ya wiki ya maji Mkoa wa Dodoma Machi 22, 2015.
Mkuu
wa Wilaya ya Mpwapwa Dkt. Jasmine Tiisekwa aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa
wa Dodoma, akiweka jiwe la msingi la mradi wa maji wa kijiji cha Mseta
wilayani Kongwa wakati wa kilele cha maadhiisho ya wiki ya maji Mkoa wa
Dodoma Machi 22, 2015.
Mkuu
wa Wilaya ya Mpwapwa Dkt. Jasmine Tiisekwa aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa
wa Dodoma, akifungua bomba la maji kama moja ya zoezi lililofanyika
wakati wa kuweka jiwe la msingi la mradi wa maji wa kijiji cha Mseta
wilayani Kongwa wakati wa kilele cha maadhiisho ya wiki ya maji Mkoa wa
Dodoma Machi 22, 2015.
Mkuu
wa Wilaya ya Mpwapwa Dkt. Jasmine Tiisekwa aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa
wa Dodoma, akinawa mikono yake kwa maji safi na salama wakati wa
kiongozi huyo akiweka jiwe la msingi la mradi wa maji wa kijiji cha
Mseta wilayani Kongwa wakati wa kilele cha maadhiisho ya wiki ya maji
Mkoa wa Dodoma Machi 22, 2015.
Mkuu
wa Wilaya ya Mpwapwa Dkt. Jasmine Tiisekwa aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa
wa Dodoma, akimtwisha ndoo ya maji bi. Asha Omary wa kijiji cha Mseta
Wilayani Kongwa mara baada ya kiongozi huyo kuweka jiwe la msingi la
mradi wa maji ulioanza kuhudumia wananchi kijijini hapo mapema jana
(Machi 22,2015) wakati wa kilele cha maadhiisho ya wiki ya maji Mkoa wa
Dodoma.
Mkuu
wa Wilaya ya Mpwapwa Dkt. Jasmine Tiisekwa aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa
wa Dodoma, akiwasilisha hotuba yake ya kuhitimisha maadhimisho ya wiki
ya maji Mkoani Dodoma yaliyofanyika Kijiji cha Mseta Wilayani Kongwa
MACHI 22, 2015.
Baadhi
ya Wakazi wa Kijiji cha Mseta Wilayani Kongwa wakiserebuka ngoma za
asili wakati wa sherehe za kilele cha wiki ya maji Mkoa wa Dodoma
zilizofanyika kijijini hapo Machi 22,2015.ICF na TIC Kuongeza Uwekezaji Nchini
Rais
mtaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (awamu ya tatu) na Mwenyekiti
Mwenza wa ICF,Mh. Benjamin Mkapa akikaribishwa na Waziri wa nchi Ofisi
ya Waziri Mkuu - Uwekezaji na Uwezeshaji,Mh. Ing. Christopher Chiza
wakati alipowasili kwenye Ofisi za Kituo cha Uwekezaji nchini (TIC) leo
Machi 23.Picha zote na Othman Michuzi.
Rais
mtaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (awamu ya tatu) na Mwenyekiti
Mwenza wa ICF,Mh. Benjamin Mkapa akisalimiana na Mwenyekiti wa Bodi ya
Wakurugenzi ya Kituo cha Uwekezaji nchini (TIC),Prof. Lucian Msambichaka
wakati alipowasili kwenye Ofisi za Kituo cha Uwekezaji nchini (TIC) leo
Machi 23.Kushoto ni Waziri wa nchi Ofisi ya Waziri Mkuu - Uwekezaji na
Uwezeshaji,Mh. Ing. Christopher Chiza.
Rais
mtaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (awamu ya tatu) na Mwenyekiti
Mwenza wa ICF,Mh. Benjamin Mkapa akiwasalimia baadhi ya Wafanyakazi wa
Kituo cha Uwekezaji nchini (TIC) waliojitokeza kumpokea wakati
alipowasili.
Rais
mtaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (awamu ya tatu) na Mwenyekiti
Mwenza wa ICF,Mh. Benjamin Mkapa (wa pili kushoto) akizungumza jambo na
Waziri wa nchi Ofisi ya Waziri Mkuu - Uwekezaji na Uwezeshaji,Mh. Ing.
Christopher Chiza pamoja na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Kituo
cha Uwekezaji nchini (TIC),Prof. Lucian Msambichaka.Kulia ni Mkurugenzi
Mkuu wa Kituo cha Uwekezaji nchini (TIC),Juliet Kairuki.
Waziri Membe awaasa waimbaji wa nyimbo za injili nchini kuwa chachu ya amani na uadilifu nchini
Sehemu ya Wachungaji walioudhuria uzinduzi wa albamu hiyo. |
MFUKO WA TAIFA WA BIMA YA AFYA (NHIF) MKOA WA TANGA WAHAMASISHA MPANGO WA MIKOPO YA VIFAA TIBA KWA WATOA HUDUMA LEO
MENEJA WA MFUKO WA TAIFA WA BIMA YA AFYA MKOA WA TANGA(NHIF) ALLY MWAKABABU AKIZUNGUMZA WAKATI WA KIKAO HICHO LEO |
KAIMU KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA,MONICA KINALA AKIZUNGUMZA KATIKA KIKAO HICHO LEO |
KAIMU MGANGA MKUU WA HALMASHAURI YA JIJI LA TANGA,DR.JESTINA MSUMARI AKIULIZA SWALI KATIKA KIKAO HICHO |
DR.SANA KUTOKA MFUKO WA TAIFA WA BIMA YA AFYA MKOA WA TANGA(NHIF) AKIFUATILIA HOTUBA YA RC MAGALULA LEO |
MGANGA MFAWIZI WA HOSPITALI YA MKOA WA TANGA BOMBO,DR KARIA AKIFUATILIA KIKAO HICHO LEO |
WASHIRIKI WAKIFUATILIA KIKAO HICHO |
Dkt. Bilal afunga Maadhimisho ya Wiki ya Maji Kitaifa mjini Musoma.
Makamu wa Rais wa Serikali ya
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohamed Gharib Bilal akishuka
kwenye ndege baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Musoma
Makamu wa Rais wa Serikali ya
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohamed Gharib Bilal, akiambatana
na wenyeji wake baada ya kuwasili mjini Musoma.
Makamu wa Rais, Dkt. Bilal, akisalimiana na Katibu Mkuu wa CCM mkoa wa Mara Adam Ngalawa baada ya kuwasili mjini Musoma.
Makamu wa Rais, Dkt. Bilal, akisikiliza wimbo wa Tanzania uliokuwa unaimbwa na wanafunzi wa Shule ya Sekondari Kisangula.
Mkurugenzi Mtendaji ya Mamlaka ya
Majisafi na Usafi wa Mazingira Musoma, (MUWASA) Mhandisi Said Gantala,
akimuonesha Makamu wa Rais, Dkt. Bilal (katikati), ramani ya Mradi wa
Ujenzi wa Uboreshaji wa Hudumu ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mjini
Musoma. Kushoto ni Waziri wa Maji, Prof. Jumanne Maghembe.
Waziri wa Maji, Prof. Jumanne Maghembe, akimkaribisha Makamu wa Rais, Dkt. Bilal kuzungumza na wananchi kwenye eneo la mradi.
Makamu wa Rais, Dkt. Bilal,
akizungumza na wananchi.Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Mara Kapteni Mstaafu
Aseri Msangi na kushoto ni Waziri wa Maji, Prof. Maghembe.
Makamu wa Rais, Dkt. Bilal
(katikati) akikata utepe wa Mradi wa Ujenzi wa Uboreshaji wa Hudumu ya
Majisafi na Usafi wa Mazingira Mjini Musoma.Kushoto kwake ni Balozi wa
Ufaransa nchini, Melika Berak na viongozi wengine wa chama.
Makamu wa Rais, Dkt. Bilal
akiweka jiwe la Msingi la Mradi wa Ujenzi wa Uboreshaji wa Hudumu ya
Majisafi na Usafi wa Mazingira Mjini Musoma.Kushoto ni Waziri wa Maji,
Prof. Jumanne Maghembe na katikati ni Balozi wa Ufaransa nchini Melika
Berak.
Mkurugenzi wa Idara ya Ubora wa
Maji, Nadhifa Kemikimba akimuonesha Makamu wa Rais, Dkt. Bilal
teknolojia ya kusafisha maji kwa kutumia mifupa.
Baadhi ya washiriki wa maonesho ya Wiki ya Maji Kitaifa
Makamu wa Rais, Dkt. Bilal akimpa
kikombe Mkuu wa Idara ya Rasilimali za Maji na Uhandisi wa Umwagiliaji
wa Chuo cha Maji, Eng. Pantaleo Tumbo ikiwa ni moja ya zawadi
zilizotolewa kwa washiriki wa maonesho ya maadhimisho ya wiki ya Maji.
……………………………………………………………………..
Hussein Makame-MAELEZO, Musoma
MAKAMU wa Rais wa Serikali ya
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohgamed Ghalib Bilal amesema kuwa
kila ahadi ya Serikali iliyotolewa itatimizwa ili kuhakikisha kuwa
inaacha kazi nyepesi kwa viongozi watakaokuja katika kuendeleza
maendeleo ya Tanzania.
Dkt. Bilal aliyasema hayo kwenye
kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Maji Duniani ambayo kitaifa
yamefanyika mkoani Mara yakiwa na Kaulimbiu isemayo “Maji kwa Mandeleo
Endelevu.
Katika kilele cha Maadhimisho
hayo, Dkt. Bilal aliweka jiwe la Msingi kwenye Mradi wa Ujenzi wa
Uboreshaji wa Hudumu ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mjini Musoma
ambao utagharimu Shilingi Bilioni 44 hadi kukamilika kwake.
“Tumewaahidi kupata maji na hilo
tutatekeleza.Kila ahadi ya Serikali itatimizwa swali ni muda na wakati
lakini kwa kweli hatukusudii kuwaacha njiani, mambo tuliyosema
tutayafanya ili tuwaachie watakaokuja kazi nyepesi ya kuendeleza
maendeleo ya nchi yetu” alisema Dkt. Bilal.
Mradi huo mkubwa wa maji
unatarajiwa kukamilika mwezi Aprili, 2015 ambapo Dkt. Bilal alisema
mradi huo utakapokamilika itaipatia Manispaa ya Musoma maji ya uhakika
kwa asilimia 100.
Aliongeza kuwa mafanikio ya mradi huo pia ni kuongezeka kwa
uzalishaji wa maji kutoka mita za ujazo 10,000 za sasa kwa siku, hadi
mita za ujazo 36,000 kwa siku.
Dkt. Bilal alitoa rai kwa wananchi
wa Manispaa ya Musoma na mkoa wa Mara kutunza mradi huo na miradi yote
inayoendelea kutekelezwa ili iendelee kuwasaidia wananchi na vizazi
vijavyo.
“Na juu ya haya yote, ni msisitizo
katika utunzaji endelevu wa mazingira yetu ili yaendelee kutuhifadhi.
Aidha, teknolojia za uvunaji wa maji ya mvua na ujenzi wa mabwawa ni
maeneo ambayo yatatuhakikishia kwamba tunakuwa na huduma endelevu ya
rasilimali ya maji” alisema.
Alisema Tanzania haina budi kuwa
na mikakati ya makusudi kukabiliana na changamoto hizo, jambo ambalo
Serikali imeanza kulifanyia kazi.
Alifafanua kuwa uhaba wa maji na kutopatikana kwake kwa uhakika kunaleta athari mbaya katika shughuli zote za kiuchumi.
“Majanga yanayohusiana na maji
kama vile, mafuriko na ukame kwa kiwango kikubwa ni maafa yanayojitokeza
mara nyingi katika sehemu mbalimbali duniani hivi sasa” alisema Dkt.
Bilal na kupngeza kuwa:
“Vifo, uharibifu wa mali, makazi
na miundombinu vina athari kubwa kwa maendeleo ya mtu mmoja mmoja,
kikundi, jamii na hata Taifa”
Hivyo, alitoa wito kwa wadau wote
kuunganisha nguvu pamoja katika kukabiliana na athari mbaya za
mabadiliko ya hali ya hewa kwani, mabadiliko hayo yana athari kuanzia
kwenye kupungua kwa misitu na vyanzo vya maji.
Alitaja athari nyingine kuwa ni
kupungua kwa rasilimali za maji juu na chini ya ardhi; kuathirika kwa
ubora wa maji ya kunywa; hadi kukua kwa utoaji wa gesi ya ukaa.
Hata hivyo alisema, Serikali ya Tanzania itaendeleza juhudi
za kuhakikisha inawafikishia wananchi maji safi na salama katika maeneo
ya nchi ambayo yamekosa huduma hiyo.
Aliwakumbusha wananchi kuwa wana
jukumu kubwa la kutunza vyanzo vya maji popote pale vinapopatikana na
kwamba wana kubwa kwenu wananchi ni kutoa mchango unaostahili katika
usimamizi na uendelezaji wa rasilimali za maji.
Akimkaribisha Dkt. Bilal, Waziri
wa Maji, Prof. Jumanne Maghembe alisema wizara yake itajitahidi na
kufanya kila linalowezekana ili katika kipindi kisichozidi miezi mitatu
maji yatoke mjini Musoma na wananchi wafurahie huduma hiyo.
Alisema katika kipindi cha
Maadhimisho ya Wiki ya Maji, viongozi mbalimbali walishiriki katika
kukagua miradi ya maji na kutembelea wilaya zote za Mara na kuweka mawe
ya msingi na kuzindua miradi ya maji ambayo imekamilika.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji ya Mamlaka ya Majisafi na
Usafi wa Mazingira Musoma, (MUWASA) Mhandisi Said Gantala alisema mradi
huo unajengwa na Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na Serikali ya
Ufaransa kupitia Shirika la Maendeleo la Ufaransa (AFD).
Alisema mradi huo unajumuisha ujenzi wa chanzo kipya cha maji,
chujio, mtambo wa kisasa wa kutibu maji na ujenzi wa matenki mapya
mawili yenye mita za ujazo 5,500.
Aliongeza pia kuwa, ujenzi huo utajumuisha ujenzi wa mfumo mpya wa mabomba ya usambazaji maji na ujezni wa miundombinu mingine.
“Mheshimiwa mgeni Rasmi Serikali ya Ufaransa kupitia Shirika
lake la AFD kwa kushirikiana na Benki ya Uwekezaji ya Jumuiya ya Ulaya
(EAD) wamekubali kufadhili mradi wa kuondoa majitaka katika manispaa ya
Musoma” alisema Mhandisi Gantala.
Naye Balozi wa Ufaransa nchini Melika Berak alisema kuwa
amefurahishwa na ushirikiano anaoupata kutoka Serikali ya Tanzania
katika kuhakikisha wanapunguza tatizo la maji nchini.
Katika kilele cha maadhimisho hayo ya 27 ya Wiki ya Maji
Duniani, washiriki wa maonesho katika maadhimisho hayo walipewa vyeti
vya kushiriki na zawadi za vikombe kutokana na makundi washiriki.
Subscribe to:
Posts (Atom)