Mashindano haya yatakuwa mazuri sana

March 20, 2013
 
MBUNGE wa Jimbo la Korogwe Vijijini,Steven Ngonyani "Maji Marefu"akizungumza wakati wa ufunguzi wa Ligi ya Gambo Cup mwishoni mwa wiki wilayani Korogwe.
TIMU 43 KUSHIRIKI UMISETA NGAZI YA WILAYA YA TANGA.

TIMU 43 KUSHIRIKI UMISETA NGAZI YA WILAYA YA TANGA.

March 20, 2013
Na Mwandishi Wetu,Tanga.
JUMLA ya timu 43 zinatarajiwa kushiriki mashindano ya Umoja wa michezo shule za Sekondari nchini (Umiseta) ngazi wilaya ya Tanga ambayo yanatarajiwa kuanza Machi 22 mwaka huu.
 
Mratibu wa Mashindano hayo, Damiani Mabena aliiambia blogi hii kuwa mashindano hayo yatachezwa viwanja saba ambavyo zimeteuliwa na kamati ya inayoratibu mashindano hayo.
Mabena alisema vituo vitakavyochezewa ni shule za sekondari Popatlaly, Usagara, Galanosi,Rosimini, Kiomoni, Tanga Ufundi pamoja na kituo maalumu kilichopo Ndaoya na Marungu
 
Aliitaja michezo ambayo itashindaniwa katika mashindano hayo msimu huu kuwa ni mchezo wa mpira wa miguu,mchezo wa mpira wa wavu,mchezo wa riadhaa,mchezo wa kikapu,mchezo wa mpira wa mikono,mpira wa meza na mpira wa pete.
Mratibu huyo alizitaka shule ambazo zimethibitisha kushiriki kuwa ni Pande,Kirare,Pongwe, Marungu,Mwapachu, Chumbageni, Mnyanjani,Mikanjuni,Kihere,Toledo,Macechu,Nguvumali,Old Tanga, Haki, Besha, Japani,Eckernforde Girls, Rosmini, Horten, Chongoleani, Mabokweni, Tongoni,Maweni,Maawal na Arafah.
Alizitaja shule nyingine kuwa ni Eckernforde, Popatlaly, Usagara, An –Noor,Al-Kheir,St.Christina,Tanga Ufundi, Kiomoni,Sahare, Jumuiya, Mkwakwani, Galanosi, Eckernforde Cambridge, Ndaoya, Coastal, Elohim, Msambweni na Don Bosco.
 Mabena alizitaka timu za shule zinazotarajiwa kushiriki mashindano hayo zianze maandalizi mapema ili kuweza kuleta msisimuko zaidi wakati wa mashindano hayo.
 
Mwisho.
KIKOSI CHA MOROCCO KUTUA NCHINI IJUMAA

KIKOSI CHA MOROCCO KUTUA NCHINI IJUMAA

March 20, 2013
Na Boniface Wambura,Dar es Salaam.
 
Timu ya Taifa ya Morocco (Lions of the Atlas) inatarajiwa kuwasili nchini keshokutwa Ijumaa kwa ndege ya Emirates tayari kwa mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia dhidi ya Tanzania (Taifa Stars) itakayochezwa Jumapili katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Msafara wa timu hiyo yenye watu 58 wakiwemo maofisa 19 na waandishi wa habari 12 utawasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) saa 8.55 mchana na utafikia hoteli ya Kilimanjaro Hyatt Regency.

Siku hiyo Morocco inatarajia kufanya mazoezi jioni kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, na Jumamosi itafanya mazoezi yake ya mwisho kwenye Uwanja wa Taifa kwa ajili ya mechi hiyo itakayochezwa saa 9 kamili alasiri.

Wachezaji walioko kwenye kikosi hicho chini ya Kocha Rachid Taoussi ni Nadir Lamyaghri, Anas Zniti, Yassine Bounou, Younnes Bellakhadar, Abdellatif Noussair, Abderrahim Achchakir, Zoheir Feddal, Younnes Hammal, Zakarya Bergdich na Abdeljalil Jbira.

Issam El Adou, Kamel Chafni, Salaheddine Saidi, Mohamed Ali Bamaamar, Abdelaziz Barrada, Salaheddine Aqqal, Abdessamad El Moubarky, Nordin Amrabat, Chahir Belghazouani, Abdelilah Hafidi, Youssef Kaddioui, Brahim El Bahri, Hamza Abourazzouk na Youssef El Arabi.

Wakati huo huo, tiketi kwa ajili ya mechi hiyo zitaanza kuuzwa keshokutwa katika vituo vya Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa, Sokoni Kariakoo, mgahawa wa Steers ulioko mtaa wa Ohio/Samora, Oilcom Ubungo, Kituo cha Mafuta Buguruni, Uwanja wa Taifa na Dar Live Mbagala.

Milango siku ya mechi kwa ajili ya watazamaji itafunguliwa saa 6 kamili mchana.

Mwisho.