KOROGWE WATEKELEZA AGIZO LA RAS KWA ASILIMIA 65.

September 26, 2014
Mkuu wa Wilaya ya Korogwe Mrisho Gambo leo ameungana na viongozi mbalimbali wa Kata katika kushiriki katika ujenzi wa maabara katika moja ya sekondari za 'Kata' zilizopo Wilayani kwake. Pichani ni DC huyo kushoto waliobeba matofali na kusaidia katika ujenzi huo.
MKUU wa Wilaya ya Korogwe mkoani Tanga, Mrisho Gambo, amesema wilaya yake imetekeleza agizo la Rais la ujenzi wa maabara kwa asilimia 65.
Gambo aliyasema hayo hivi karibuni katika ya kutembelea ujenzi wa vyumba vya maabara unaoendelea katika kata mbalimbali wilayani hapa na kueleza kuwa wilaya hiyo ipo kwenye hatua nzuri ya makusanyo ya michango ya wananchi ambapo Novemba mwaka huu tatizo la maabara litakuwa limepatiwa ufumbuzi.
Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya hiyo, Lucas Mweri, alisema mtendaji atakayeshindwa kusimamia kazi hiyo atakatwa mshahara wake, ili aone umuhimu wa na unyeti wa jambo hilo kwa maslahi ya kizazi cha sasa na kijacho.
Diwani wa kata ya Mazinde, Abdalah Mangare, alisema wananchi wameona umuhimu wa ujenzi wa vyumba vya maabara na kukubali kuchangia.
  Chanzo Tanzania Daima

MKUTANO WA WANAHISA WA TBL WAFANA.

September 26, 2014

 Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Waziri Mkuu Mstaafu, Bw. Cleopa Msuya akifafanua jambo, wakati akizungumza na wana hisa wa kampuni hiyo, wakati wa Mkutano Mkuu wa mwaka, uliofanyika Dar es Salaam jana. Kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa TBL, Bw. Roberto Jarrin na Kampuni wa Kampuni hiyo, Bw. Huruma Ntahema.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Waziri Mkuu Mstaafu, Bw. Cleopa Msuya akifafanua jambo, alipozungumza na wana hisa wa kampuni hiyo, wakati wa Mkutano Mkuu wa mwaka, uliofanyika Dar es Salaam jana. Kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa TBL, Bw. Roberto Jarrin. (Na Mpigapicha Wetu)
Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Bw. Roberto Jarrin (kulia), akitata jambo na Maofisa wa shirika hilo, Mkurugenzi wa Afrika Mashariki, Bw. Mario Van Gelden (kushoto) na Mkurugenzi wa Rasilimari watu, Bw. David Magese, wakati wa Mkutano Mkuu wa mwaka wa wana hisa, uliofanyika Dar es Salaam
 Mkurugenzi akibadilishana mawazo na baadhi ya wanahisa wa TBL
Msuya akibadilishana mawazo na viongozi wa TBL WAKATI WA MKUTANO HUO