WAZIRI MKUU AREJEA DODOMA LEO KUENDELEA NA BUNGE MAALUM LA KATIBA

April 23, 2014
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda  akisalimiana na viongozi wa mkoa   baada ya kuwasili kwenye  uwanja wa ndege wa Dodoma   kwa ajili ya kikao cha Bunge Maalum la Katiba akitoka Dar es Salaam, Aprili 23, 2014. Kulia ni Mkuu wa Mkoa huo, Dk. Rehema Nchimba (Picha na Ofisi  ya Waziri Mkuu)

BASI LA URIO LAPATA AJALI 31 WAJERUHIWA

April 23, 2014

 picha ya chini na juu ni baadhi ya majeruhi walikuwa kwenye  basi hilo aina ya Urio lililopata ajali leo jioni katika eneo la Kia wilayani Hai  mkoani Kilimanjaro


 wananchi wawakiwa wanashuhudia ajali hiyo iliotokea leo jioni katika eneo la kia ambapo inasemekana watu zaidi ya 31 wamejeruliwa

 Basi aina ya Urio yenye namba za usajili T 137 BCX inayofanya safari zake moshi kuelekea  leguruki mkoani  Arusha leo limepinduka katika eneo la kia na kujeruhi watu zaidi ya 31

kwa mujibu wa mashuhuda waliokuwepo katika eneo la tukio walisema kuwa dereva huyo alikuwa anajaribu kukwepa pikipiki iliyokuwa imejichomeka barabarani

"dereva huyu alikuwa anajaribu kukwepa pikipiki ndipo gari ikamshinda na kuama barabara ndipo ilipo anguka gafla  na kubiringita mara tatu apa yenyewe unavyoiyona tumeigeza ilikuwa kichwa chini matairi juu"alisema mmoja wapo wa shuhuda ambaye akutaka kutaja jina

mpaka kamera ya libeneke la kaskazini inaondoka eneo la tukio watu 31 walikuwa wamekwishwa pelekwa katika hospitali ya wilaya ya hai kwa ajili ya matibabu wakiwemo wanafunzi wa shule ya leguruki ambao walikuwa wanarejea shuleni mara baada ya kumaliza likizo yao ya sikukuu ya pasaka 

kwa habari zaidi libeneke itaendelea kukujuza nini kinachoendelea.

MZEE MSUYA AJITOA KATIKA SIASA; JK AMPONGEZA

April 23, 2014
Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete akiwa viongozi wengine wakuu wa serikali chama cha Mapinduzi CCM, akiwemo Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Abdulrahman Kinana (kushoto) katika hafla ya kumuaga aliyekuwa Waziri mkuu wa Tanzania mara mbili katika awamu mbili tofauti, Mzee Cleopa David Msuya (wa kwanza kulia kwa Rais) ambaye amestaafu rasmi siasa baada ya kuitumikia kwa zaidi ya miaka 33.
 Katibu wa CCM, wilaya ya Mwanga, akisoma historia fupi ya Mzee Msuya kabla na baada ya kujiunga na siasa
Baadhi ya Wananchi waliohudhuria hafla hiyo iliyofanyika katika Ofisi za CCM wilaya ya Mwanga leo
Mjumbe wa Halmashauri kuu wa CCM wilaya ya Mwanga, Joseph Thadayo akitoa salamu za marafiki na wasomi waishio nje ya Mwanga, ikiwemo salamu za Mwanasiasa maarufu na mdhamini wa CCM, Mzee Peter Kisumo ambaye aliwahi kufanya kazi pamoja na mzee Msuya katika Siasa.
Mzee Msuya akitoa pongezi zake kabla ya kuaga rasmi.


Kundi la wazee wa kimila wakiongozwa na Mzee Kasim Msemo wakimkaribisha Mzee Msuya kijijini
 Mzee Msuya akiwa amekaa kwenye kiti cha jadi kama ishara ya kurudi rasmi kijijini baada kutangaza kustaafu siasa
 Rais Kikwete akizungumza na wananchi katika hafla ya kumuaga Mzee Msuya katika ulingo wa siasa, uliofanyika leo katika ofisi za CCM wilaya ya Mwanga.
 Mamia ya Wananchi waliokusanyika kushuhudia hafla hiyo

RAIS JAKAYA KIKWETE AFANYA ZIARA MKOANI KILIMANJARO.

April 23, 2014

Rais Kikwete akiwasili ikulu mjini Moshi akipokelewa na mwenyeji wake mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Leonidas Gama pamoja na mkuu wa wilaya ya Moshi Ibrahim Msengi.
Viongozi mbalimbali wa chama na serikali wakijiandaa kumpokea rais Kikwete alipowasili mjini Moshi.
Rais Kikwete akisalimiana na baadhi ya viongozi pamoja na wananchi waliofika ikulu ya Moshi.
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Leonidas Gama akizungumza mara baada ya rais kuwasili ikulu mjini Moshi kwa ajili ya ziara wilayani Mwanga .
Baadhi ya wanannchi wakiwemo makada wa chama cha mapinduzi wakiwa Ikulu ya Moshi kungojea rais Jakaya Kikwete.
Waziri wa maji Prof Jumanne Maghembe akiteta jambo na Niabu Meya wa manispaa ya Moshi Dk Mmbando ikulu ya mjini Moshi.
Baadhi ya wageni mbalimbali wakiwemo viongozi wa chama na serikali.
 Na Dixon Busagaga wa globu ya jamii kanda ya kaskazini.


Jumuiya ya Kiislamu yaungana na maaskofu kumtetea Warioba

Jumuiya ya Kiislamu yaungana na maaskofu kumtetea Warioba

April 23, 2014

Msemaji wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu nchini, Rajab Katimba akizungumza na waandishi wa habari jana, kuhusu mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na mchakato wa Katiba. Kulia ni Wajumbe, Shaban Ibrahim na Suleiman Abdallah.  Picha na Rafael Lubava 
Dar es Salaam. Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania imeungana na maaskofu mbalimbali kuwataka wajumbe wa Bunge la Katiba kuheshimu Rasimu ya Katiba iliyowasilishwa kwa mujibu wa sheria na Tume ya Mabadiliko ya Katiba.

Pia, taasisi hiyo imemtaka Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi kujiuzulu nafasi zake zote za uongozi kutokana na kauli waliyodai ya kichochezi, aliyoitoa katika Kanisa la Methodist, Jimbo la Dodoma kuwa ukipitishwa muundo wa serikali tatu, jeshi litachukua nchi kwa sababu itashindwa kuwalipa mishahara.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Msemaji wa Jumuiya na Taasisi hizo, Sheikh Rajab Katimba alilaani kauli kuhusu jeshi na kuwa makanisa yote yatafungwa na nchi itakosa amani kutokana na kupitisha muundo huo wa serikali.

Sheikh Katimba alisema Rasimu ya Katiba iliyowasilishwa bungeni na aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba imetokana na utafiti na uchambuzi wa maoni ya wananchi wa Tanzania Bara na Visiwani ili kuboresha Muungano kutatua kero zilizodumu kwa miaka 50 sasa.

Msimamo

Jumuiya hiyo iliweka wazi msimamo wake wa kutaka serikali tatu na kutaka maoni ya makundi mbalimbali ndani ya Bunge la Katiba kuheshimiwa.

Mjumbe wa Jumuiya hiyo, Sheikh Ramadhan Sanze pia alisema si ustaarabu kwa kundi moja kuhodhi mchakato kwa masilahi binafsi.

Alisema kukosoa maoni ya waasisi wa Taifa si dhambi kwa sababu wao hawakuwa Mungu kwamba hawakosei, badala yake alipendekeza watu waachwe wazungumze kwa utashi wa matakwa yao juu ya kile kilichowasilishwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba.

“Nchi hii haithamini mchango wa wataalamu, tumeona Tume ilivyofanya kazi nzuri, leo hii wanatukanwa hadharani, nawashangaa sana viongozi wa nchi hii,” alisema.

Sheikh Sanze alisema miiko na misingi waliyoiweka waasisi wa Taifa inavunjwa na viongozi wenyewe ambao leo wanasema waasisi wanatukanwa kwa kuwa wamependekeza serikali tatu badala ya mbili walizounda waasisi.

“Kulikuwa na utaratibu wa kubadilishana awamu za uongozi katika Serikali ya Muungano, awamu hii rais akitoka Tanzania Bara, ijayo atatoka Zanzibar; hii ndiyo misingi waliyoiweka waasisi, mbona leo haifuatwi? Huu ni unafiki...” alifafanua Sheikh Sanze.

Jumuiya hiyo imewataka wananchi wote kuendelea na mshikamano katika kutengeneza Katiba Mpya yenye maridhiano na itakayoondoa kero zilizodumu kwa zaidi ya miaka 50.
chanzo:Mwananchi

MUZIKI KIMATAIFA : MWANAMUZIKI TOKA UGANDA DKT. JOSE CHAMELONE APAGAWISHA MASHABIKI NDANI YA LONDON, UINGEREZA

April 23, 2014


Dkt. Jose Chameleone akiwapagawisha wabongo na wazungu wa London, UK 

Jestina George wa Jestina-george.com akiwa bize na simu yake katiak show ya Jose Chameleone

Jestina George wa kwanza kulia akipata picha na marafiki zake katika show ya Chameleone jijini London


MWANDISHI ANUSURIKA, MTOTO MCHANGA AOKOLEWA

April 23, 2014

 Mgambo aliyetaka kumtwisha Nyundo mtoto Anna Yohana, akimbeba mtoto akiwa na hofu kuwa amemdhuru vibaya....
 Mtoto Anna Yohana aliyenusurika kuuawa kwa nyundo na Mgambo wa Jiji la Mbeya, akiwa amebebwa na msamaria mwema, baada ya mwandishi Gordon Kalulunga, kusogea na kuwapiga picha Mgambo wakashituka na kuanza kumshambulia kisha oparesheni ikaahirishwa.
 Baada ya kujinasua na kupigana na mgambo zaidi ya saba, nikipiga simu kwa baadhi ya waandishi wa habari huku Tape recorder ikiwa imeporwa.
 
 
*Ni kichanga cha miezi minne kilichofunikwa kwenye salfeti sokoni.
*Wauza magazeti nao wahaha meza zao kuvunjwa usiku wa manane.
 
Na,Christopher Nyenyembe, Mbeya
 
MWANDISHI wa Habari wa Gazeti hili (Tanzania Daima) mkoa wa Mbeya, Gordon Kalulunga, ameambulia kipigo kutoka kwa mgambo wa jiji alipokuwa kazini akipiga picha kwenye ‘operesheni vunja vunja’ sehemu ambayo mtoto mchanga wa miezi minne alikuwa amelazwa na mama yake mzazi kwenye salfeti  sokoni eneo la Kabwe Mwanjelwa.
 
Tukio hilo lilitokea wakati wa sherehe za pasaka(jumatatu ya pasaka) baada ya uongozi wa jiji la Mbeya kwa kutumia mgambo wake walipoamua kuendesha operesheni ya kuwaondoa wafanyabiashara waliopanga bidhaa zao kando kando ya barabara kuu ya Tanzania- Zambia katika eneo maarufu la Mwanjelwa.
 
Mwandishi Kalulunga alikutwa na mkasa wa kupigwa na mgambo zaidi ya saba na kusababisha purukshani kubwa mara alipofanikiwa kupiga picha zilizowahusu mgambo hao waliokuwa wakivunja vibanda na kuwatimua wafanyabiashara ndogo ndogo waliopigwa marufuku kupanga bidhaa zao kwenye maeneo yasiyoruhusiwa kwa lengo la kuweka usafi wa jiji hilo.
 
“Nilikuwa natimiza wajibu wangu wa kazi kama mwandishi wa habari,alitokea mwanamke  mmoja aliyekuwa amevaa gauni refu la rangi ya njano na kunikaba shati,ndipo mgambo wa jiji walipokuja na kuanza kunipiga,ilibidi kamera yangu nimkabidhi polisi mmoja lakini nimepoteza redio yangu ya kurekodia”alisema Kalulunga.
 
Alisema baada ya tukio hilo kutokea ilibidi akatoe taarifa kwenye kituo kidogo cha polisi Mwanjelwa na kupewa fomu ya kwenda kutibiwa (PF 3) ambako ilibidi apatiwe matibabu na aliporudi polisi Mwanjelwa alitakiwa na mkuu wa kituo hicho akatoe maelezo yake kituo kikuu cha polisi mjini kwa OC –CID au mkuu wa polisi wilaya (OCD).
 
Kitendo cha Mwandishi huyo kushambuliwa akiwa kazini kulisababisha habari za haraka zisagae jijini humo na kisha kumfikia Kamanda wa Polisi mkoa huo,Ahmed Msangi aliyeongea moja kwa moja na Kalulunga ili aweze kufahamu aina ya uvunjifu wa amani uliojitokeza wakati wa operesheni vunja vunja iliyokuwa akifanywa na mgambo hao ambao imechangia pia kuvunjwa vibanda vya kuuzia magazeti tangu zoezi hilo lilipoanza.
 
“Namshukuru sana mkuu wa polisi wilaya ya Mbeya,Richard Mchomvu ametumia busara kubwa sana kunikutanisha na kiongozi wa operesheni hiyo kutoka idara ya afya aliyejulikana kwa jina la Odas na mkuu wa mgambo pamoja na bosi wangu kazini,jiji wamekiri kunifanyia kitendo hicho eti walikuwa hawafahamu kama mimi ni mwandishi” alisema Kalulunga.
 
Kufuatia tukio hilo lililotulizwa na Mchomvu aliushauri uongozi wa jiji hilo kushirikiana na vyombo vya habari katika majukumu yake kwa kuwa  wananchi wanapaswa kuelimishwa zaidi kila jambo linapofanyika na kusisitiza kuwa usafi wa jiji ni muhimu hivyo kila upande una jukumu lake hivyo hawana sababu yoyote ya kuonyeshana ubabe.
 
“Nikiwa mkuu wa polisi wa wilaya sipendi kuona haki za binadamu zikivunjwa kienyeji,uhai wa kila mtu ni muhimu zaidi,tumieni vyombo vya usalama kuweka mambo yenu vizuri,waandishi nao wana jukumu kubwa la kuwasaidieni watumieni,angalieni sasa mmepoteza kifaa chake cha kazi,naomba suala hili mlimalize kwa ustaarabu hata Mkurugenzi anapaswa kujua” alisema Mchomvu.
 
Kufuatia tukio hilo na mtoto mchanga aliyenusurika kupigwa nyundo wakati mgambo hao wakiendelea kubomoa vibanda,operesheni hiyo ilisitishwa mara moja katika eneo hilo baada ya mama mzazi wa mtoto huyo alipofanikiwa kutimua mbio na kumuacha mwanae aliyeangukia kwenye mikono ya wasamaria.
 
Wakati hali hiyo ikitokea,wauzaji wa magazeti jijini humo wamelalamikia zoezi hilo ambalo limewasababishia  hasara kubwa baada ya meza zao kuvunjwa usiku wa manane wakati uongozi wa jiji hilo unafahamu fika aina ya meza zilizoruhusiwa kuwepo kwa ajili ya kuuzia magazeti na haijulikani mahali zilipotupwa.
 
Jiji la Mbeya limekubali kulipa kifaa kilichoibwa/kupotea katika tafrani hiyo.

WAKULIMA NA WAFANYABIASHARA ZAIDI YA 500 KANDA YA KASKAZINI KUKUTANISHWA NA TAASISI ZA FEDHA

April 23, 2014


Mkurugenzi wa Tanzania Horticulture Association(TAHA) bi,Jackline Mkindi akizungumza na vyombo vya habari ambao hawapo pichani juu ya maonesho ya kilimo ambao yanatarijiwa kufanyika siku ya Aprili 25 na 26 katika viwanja vya AVRDC vilivyopo eneo la Tengeru wilayani arumeru mkoani arushakilia kwake ni Mratibu wa Agri-Hub Tanzania bw,Tom ole sikar. 
Na Ashura Mohamed-Arusha
WAKULIMA  na wafanyabiashara za kilimo zaidi ya 500 kanda ya kaskazini mwa Tanzania wanatarajiwa kukutanishwa na taasisi za kifedha 48 ili kuweza kuongeza ufahamu na uelewa juu ya huduma mbalimbali za nkifedha zitolewazo na mabenki,taasisi ndogo ndogo za kifedha,mashirika ya bima,taasisi za elimu na mashirika yasiyo ya kiserikali.

Akizungumza na vyombo vya habari  afisa mtendaji mkuu wa TAHA bi.Jackline Mkindi alisema kuwa wakulima wadogo wadogo wamekukwa wakikabiliwa na changamoto kubwa ya ya upatikanaji wa huduma za kifedha hususani kwa wadau wa sekta ya kilimo.

Katika kutatua changamoto hiyo ya mitaji Agri-Hub Tanzania ikishirikiana na TAHA mashirika,asasi  mbalimbali kwa umoja wao wamethamiria kuwaunganisha wadau wa kilimobiashara na watoa huduma za kifedha moja kwa moja ili pande zote mbili ziweze kukuelewana na juu mahitaji yao na hatimaye watoa huduma za kifedha waweze kubuni huduma bora zaidi za kuimarisha utoaji huduma zao kwa wadau wa kilimo.

Mkindi alisem kuwa maonesho hayo yatakwenda sambamba na uwasilishwaji wawa mada mbalimbali ikiwemo uaandaaji bora wa wa mpango biashara (business plans),umuhimu wa wa soko la hisa katika kuhakikisha upatikanaji wa mitaji  ya muda mrefu na matumizi bora ya mikopo katika biashara hususani za kilimo.

Naye mtaribu kutoka kampuni ya Agri-Hub Tanzania bw,Tom Ole Sikar,alisisitiza kuwa maonesho hayo yanalenga kuwawezesha wakulima wajasiriamali pamoja na wamiliki wa biashara za kilimo kama wachuuzi,wauzaji wa pembejeo na wasindikaji kutambua fursa mbalimbali za mitaji na usalama wa kifedha(Financial security) zilizopo kwa biashara za kilimo.
Aidha sikar alisema kuwa wadau hao wataweza kuunganishwa na taasisi muhimu za  fedha ikiwa ni pamoja na kushiriki katika mawasilisho na majadilino juu ya fursa za sekta binafsi katika kilimo pamoja na wataalamu wa mambo ya fedha na watoa huduma za maendeleo ya biashara kupitia semina zitakazotolewa sambamba na maonesho hayo.

‘’maonesho hayo yatawawezesha wadau kutambua njia za kuboresha biashara na utoaji wa huduma kwa walengwa ikiwa ni pamoja na kujifunza kutoka kwa wafanyabiashra wengine wa kilimo waliofanikiwa kutembelea maonesho “alisema bw,Sakar

Maonesho hayo yanatarajiwa kufanyika katika viwanja vya Taasisi ya AVRDC(The World Vegetable Centre) kuanzia tarehe 25  na 26 april kuanzia majira ya saa tatu aubuhi mpaka saa kumi na moja jioni.

MCHEZAJI WA ZAMANI WA MAJIMAJI YA SONGEA, MTAWA KAPARATA AIBUKA MSHINDI WA SHINDANO LA TANZANIA MOVIE TALENTS MKOANI MBEYA

April 23, 2014

Na Josephat Lukaza wa Proin Promotions Limited - Mbeya
Shindano la Tanzania Movie Talents Kwa kanda ya Nyanda ya Juu Kusini, Mkoani Mbeya limefikia Tamati hapo jana kwa washindi watatu kutoka kanda hii ya nyanda ya juu Kusini Kupatikana na Kutangazwa na Majaji watatu.
Washindi waliotangazwa na Jaji Mkuu wa Shindano hilo, Roy Sarungi kwa kushirikiana na Majaji wawili Single Mtambalike na Yvonne Chery ni Steven Mapunda, Issalito Issaya na Mtawa Kaparata "BABU"
 
Mmoja kati ya washindi watatu waliopatikana Jana na Kutangazwa na Jaji Mkuu wa Shindano hilo Roy Sarungi ni mchezaji wa zamani wa timu ya mpira wa Miguu ya Majimaji ya Songea, Bw Mtawa Kaparata.
Mtawa Kaparata aliibuka mshindi kwa kuweza kuonyesha kipaji chake cha kuigiza achilia mbali uwezo wa mpira aliokuwa nao kipindi hiko.
Kwa upande wake mmoja wa washindi wa Shindano la Tanzania Movie Talents ambae pia alikuwa mchezaji wa zamani wa Majimaji ya Songea , Bwa Mtawa Kaparata alithibitisha kuwa 'Tanzania Movie Talents imepokelewa vizuri na watanzania wa Mkoa wa Mbeya  kwani  ameona usaili ulivyokuwa mgumu kutokana na vipaji vilivyoonyeshwa na vijana wengi waliojitokeza na kuona ongezeko la washiriki waliojitokeza kwaajili ya usaili wa kushiriki katika Shindano hili kubwa na la kwanza Afrika Mashariki na Kati. 
Hii nikutokana na ukweli kwamba washiriki wote wanaofika kwaajili ya Usaili hawatozwi kiasi chochote cha pesa kutoka timu ya Tanzania Movie Talents na pia kufurahishwa na uamuzi wa Majaji wa Timu ya Tanzania Movie Talents,  niwazi kabisa kuwa kutotozwa kwa kiasi chochote cha pesa kwa washiriki kumekuwa ni kivutio kikubwa kabisa hivyo kuongeza idadi ya washiriki katika kila Kanda tunayoenda"alisema Mtawa Kaparata Mkazi wa Mkoa wa Mbeya, Eneo la Soko Matola.
Shindano hili kwa kanda ya nyanda Ya juu kusini limehitimishwa rasmi jana kwa washindi watatu kupatikana na hatimaye shindano hili litahamia Kanda ya Kusini na Usaili utafanyika Mkoani Mtwara 
Shindano hili limelenga kuinua na kukuza vipaji vya kuigiza Tanzania na hatimaye kuendeleza vipaji hivi vya kuigiza Tanzania.
Usaili wa Shindano hili ni bure kabisa na fomu hupatikana eneo la usaili.

*MALINZI AWAPONGEZA SUKER, LEKJAA

April 23, 2014

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi amewapongeza marais Davor Suker na Fouzi Lekjaa kwa kuchaguliwa tena hivi karibuni kuongoza mashirikisho ya mpira wa miguu katika nchi zao. 

Suker amechaguliwa tena kuwa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu la Croatia (CFF) wakati Lekjaa amechaguliwa kuwa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu la Morocco (FRFM).
Katika salamu zake za pongezi, Rais Malinzi amesema ushindi waliopata ni uthibitisho kuwa familia ya mpira wa miguu katika nchi zao ina imani kubwa kwao katika kuendeleza mchezo huo ndani na nje ya nchi hizo.

Rais Malinzi amesema Lekjaa na Suker wana uwezo wa kuendeleza kazi nzuri ambayo tayari imefanyika, lakini vilevile kuja na mawazo mapya ambayo yatakuwa changamoto kwa ustawi wa mchezo huo nchini Morocco na Croatia kwa ujumla.

BURUNDI YAWASILI KUIKABILI TAIFA STARS JUMAMOSI

April 23, 2014


Timu ya Taifa ya Burundi (Intamba M Rugamba) inatarajiwa kuwasili nchini kesho (Aprili 24 mwaka huu) saa 12 jioni kwa ndege ya Kenya Airways tayari kwa mechi dhidi ya Taifa Stars itakayochezwa Jumamosi (Aprili 26 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Intamba Mu Rugamba itakuwa na msafara wa watu 28 wakiwemo wachezaji, benchi la ufundi na viongozi, na itafikia hoteli ya Accomondia. Mechi hiyo itachezwa kuanzia saa 10 jioni.
Nayo Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager ipo kambini kwenye hoteli ya Kunduchi Beach ikijiandaa kwa mechi hiyo itakayochezeshwa na waamuzi kutoka Kenya.
Viingilio katika mechi hiyo vitakuwa sh. 5,000 kwa viti vya rangi ya chungwa, bluu na kijani. Kwa VIP A kiingilio kitakuwa sh. 20,000 wakati VIP B na C ni sh. 10,000. Mechi hiyo ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 50 ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

ANGALIA PICHA 12 ZA UTENGENEZWAJI WA VIDEO YA WIMBO WA MIAKA 50 YA MUUNGANO, IMEHUSISHA WASANII WAKALI NA WANAOKIMBIZA BONGO

April 23, 2014