SERIKALI MKOANI MBEYA KUWACHUKULIA HATUA KALI ZA KISHERIA ASKARI POLISI WANAOTUHUMIWA KWA WIZI WA DHAHABU CHUNY

March 03, 2017
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Makalla akizungumza na wachimbaji wadogo wadogo katika mgodi wa dhabau wa Itumbi kata ya Matundasi Wilayani Chunya Mkoani Mbeya Februry 2 mwaka huu.

Filamu ya Maisha ni Siasa yawekwa mtandaoni kuwapa uhuru watazamaji

March 03, 2017
Filamu ya Maisha ni Siasa ni sinema ya kitanzania inayoonyesha pilikapilika za wanasiasa katika chaguzi za Afrika. Imechezwa na Paul Mashauri, Loue Kifanya, Violet Mushi, Bahati Chando, Lilian Mwasha, Godwin Gondwe, Hudson Kamoga na wengine wengi. Imeandikwa na Paul Mashauri na Jacqueline Mgumia na kuandaliwa na Kileleni Productions kwa ushirikiano na Mashauri Studios na the 7th Elements. Waweza kuangalia filamu yote hapa chini.

WADAU WA MUZIKI WA INJILI KUKUTANA JUMAMOSI UKUMBI WA CHUO CHA USTAWI WA JAMII JIJINI DAR ES SALAAM

March 03, 2017
 Mtaalamu wa Sheria kutoka Jeshi la Polisi Dk. Mkaguzi wa Polisi Ezekiel Kyogo, akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Hoteli ya Lamada jijini Dar es Salaam leo wakati akifafanua kuhusu sheria ya haki miliki ya kazi za wasanii wa muziki.
 Rais wa Tanzania Music Foundation (TMF) Dk. Donald Kassanga  akifafanua mambo kadhaa katika mkutano huo ikiwa ni pamoja na TMF, kuunga mkono jitihada za serikali za kupambana na dawa za kulevya.
Mwimbaji wa nyimbo za injili, Faraja Ntaboba akizungumza katika mkutano huo.


Dotto Mwaibale na Christina Mseja

WADAU wa muziki wa injili wanatarajia kukutana kesho kutwa Machi 4 mwaka huu kwenye Kongamano la Wasanii wa muziki huo litakalofanyika katika Ukumbi wa Chuo cha Ustawi wa Jamii Kijitonyama jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam leo, Mtaalamu wa Sheria kutoka Jeshi la Polisi Dk. Mkaguzi wa Polisi Ezekiel Kyogo, alisema  kongamano hilo lina dhumuni kubwa katika kujenga  uelewa kwa wasanii wa muziki  juu ya kazi zao, hususani changamoto na suluhu za kazi za Sanaa.

Kyogo alisema kazi za Sanaa ni mali na zimekosa ulinzi na hakuna jitihada zozote zinazoendelea katika kusaidia wasanii hao.Wasanii wamekosa ubunifu na watu wamekata tamaa na kujiingiza katika wimbi la dawa za kulevya. Kuwepo kwa  mapungufu ya adhabu haipunguzi uhalifu kwani wasimamizi wa sheria wanatakiwa kuwa na uwezo zaidi katika  sheria hizo.

“Lazima kuwe na sheria ya makosa ya wizi za kazi za wasanii kwani itasaidia kupunguza wizi na itaongeza kipato na ajira, kwa kuwa muziki ni mali ya jamii na ni afya na tiba”, alisema Kyogo.

Rais wa Tanzania Music Foundation (TMF) Dk. Donald Kissanga aliongeza kuwa lengo kubwa kongamano ni kuhakikisha serikali inatengeneza mazingira bora  katika tasnia nzima ya muziki jambo litakalosaidia kuongeza pato la taifa.

“Watu  wamekuwa wakiiba kazi za wasanii na kama TMF tunalaaani na kuomba serikali kupitia vyombo vya dola kuziba mianya hiyo" alisema Kissanga.

Katika hatua nyingine Kissanga alisema TMF kinaungana na Serikali katika mapambano ya dawa za kulevya nchini kwani waathirika ni pamoja na wanamuziki na wasanii kwa ujumla.

Mwimbaji wa nyimbo za injili, Faraja Ntaboba, alisema kuwa wasanii wamekuwa wakiibiwa sana kazi zao wakati wanatumia nguvu kubwa kwa kuziandaa.

"Tuna amini endapo Serikali ikisimamia vizuri kwa kushirikiana na  TMF  wataweza kulipa kodi sawa sawa na kuendesha kazi  vizuri" alisema Ntaboba.

HATIMAYE JOHN BARNES AWASILI JIJINI DAR

HATIMAYE JOHN BARNES AWASILI JIJINI DAR

March 03, 2017
Akiwa nchini Barnes atafanya mafunzo kwa timu ya taifa ya vijana chini ya miaka 15 Serengeti Boys pamoja kuhudhuria fainali za mashindano ya Standard Chartered road to Anfield ambayo ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 100 ya benki hiyo yatakayofanyika Jumamosi Machi 4. Bingwa wa Mashindano hayo atapata nafasi ya kwenda nchini Liverpool Uingereza.Timu zilizoingia fainali za mashindano hayo ya kikanda ni Azania Group ya Tanzania, Capital FM ya Kenya na Cocacola ya Uganda.
Mchezaji nguli wa kimataifa wa Timu Liverpool, John Barnes (wa pili kushoto) akiwasili Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere- VIP Terminal I na kupokelewa na wenyeji wake ambao ni Mkuu wa Idara ya Fedha wa Benki ya Standard Chartered, Abdulrahaman Said (wa pili kulia), Mkuu wa Mahusiano na Masoko wa benki hiyo, Juanita Mramba (kulia) pamoja na Afisa Habari wa TFF, Alfred Lucas (kushoto).
Mchezaji nguli wa kimataifa wa Timu Liverpool, John Barnes (wa pili kulia) akiwa kwenye picha ya pamoja na wenyeji wake Mkuu wa Idara ya Fedha wa Benki ya Standard Chartered, Abdulrahaman Said (kulia), Mkuu wa Mahusiano na Masoko wa benki hiyo, Juanita Mramba (wa tatu kulia) pamoja na Afisa Habari wa TFF, Alfred Lucas (kushoto) mara baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere- VIP Terminal II leo jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Idara ya Fedha wa Benki ya Standard Chartered, Abdulrahaman Said akizungumza na waandishi wa habari kuhusu ujio wa Mchezaji nguli wa kimataifa wa Timu Liverpool, John Barnes kwenye uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere leo jijini Dar es Salaam.
Mchezaji nguli wa kimataifa wa Timu Liverpool, John Barnes akionyesha jezi ya Timu ya Taifa kwa waandishi wa habari aliyokabidhiwa na Afisa Habari wa TFF, Alfred Lucas mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere leo jijini Dar es Salaam.
Mchezaji nguli wa kimataifa wa Timu Liverpool, John Barnes (katikati) akiongozana na wenyeji wake Mkuu wa Idara ya Fedha wa Benki ya Standard Chartered, Abdulrahaman Said (kulia), Mkuu wa Mahusiano na Masoko wa benki hiyo, Juanita Mramba (kushoto) mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere leo jijini Dar es Salaam.
Mchezaji nguli wa kimataifa wa Timu Liverpool, John Barnes (wa pili kulia) akizungumza jambo na Meneja wa Hoteli ya Hyatt Regency Dar es Salaam-The Kilimanjaro, Timothy Mlay alipowasili kwenye hoteli hiyo jioni hii jijini Dar es Salaam.
Mchezaji nguli wa kimataifa wa Timu Liverpool, John Barnes akisalimiana na mmoja wa mashabiki wa timu ya Liverpool Benjamin Kasenyenda mara baada ya kuwasili kwenye wa Hoteli ya Hyatt Regency Dar es Salaam-The Kilimanjaro.