MANISPAA YA ILALA JIJINI DAR ES SALAAM YAOMBWA KULINUSURU DARAJA ZISISOMBWE NA MAFURIKO

April 26, 2017


Wakazi wa Gongolamboto wakipita katika  daraja ambalo kingo zake zimesombwa na mafuriko barabara ya kuelekea Machinjio ya Pugu Kajiungeni Dar es Salaam leo.Jitihada za makusudi zisipochukuliwa daraja hilo litasombwa  na maji.

Mshindi wa Milioni 10 Ukonga apokea chake

April 26, 2017
Ofisa wa benki ya NMB Makao Makuu jijini Dar es Salaam kushoto, akimkabidhi moja ya karatasi muhimu baada ya kufanikiwa kumfungulia akaunti mshindi wa Biko, Ijue Nguvu ya Buku, Nicholaus Mlasu aliyeibuka na ushindi wa Bahati Nasibu ya Biko mwishoni mwa wiki. Makabidhiano ya fedha za ushindi huo yalifanyika jijini Dar es Salaam jana. Kulia ni Meneja Masoko wa Biko, Goodhope Heaven. Picha zote na Mpiga picha Wetu.

Milioni 10 za Biko ‘Nguvu ya Buku’ zamfikia Nicholaus Mlasu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
ZAWADI ya juu ya Sh Milioni 10 inayotolewa na Bahati Nasibu ya Biko, Ijue Nguvu ya Buku imetolewa jana na kukabidhiwa mshindi Nicholaus Mlasu, mkazi wa Ukonga Mombasa, Manispaa ya Ilala, huku akipokea fedha zake Makao Makuu ya Benki ya NMB, jijini Dar es Salaam jana.

Fedha za mshindi huyo ziliingizwa moja kwa moja kwenye akaunti yake iliyofunguliwa kwenye benki hiyo kwa ajili ya kijana huyo kujipanga vizuri kabla ya kuanza kuzitumia fedha hizo kwa maendeleo yake.
Meneja Masoko wa Biko Tanzania waendeshaji wa Bahati Nasibu kwa njia ya ujumbe wa maneno kwenye simu za mikononi, Goodhope Heaven kulia akizungumza jambo wakati wa kumfungulia akaunti mshindi wao wa Sh Milioni 10 na kumkabidhi fedha hizo jana Makao Makuu ya benki ya NMB, jijini Dar es Salaam. Katikati ni mshindi huyo Nicholaus Mlasu akifuatiwa na Ofisa wa NMB Makao Makuu.

Akizungumza katika makabidhiano hayo yaliyofanyika jana jijini Dar es Salaam, Meneja Masoko wa Biko Tanzania, Goodhope Heaven, alisema kwamba mbali na kutoa fedha hizo kila mwisho wa wiki, pia wanaendelea kutoa pesa za papo kwa hapo ambapo ongezeko la washiriki ni kubwa.

Alisema wale wanaoshinda papo hapo fedha kuanzia Sh 5000, 10,000, 20,000, 50,000, 100,000, 500,000 na Sh Milioni moja hupokea kwenye simu zao wanazotumia ambazo ni Tigo Pesa, Mpesa na Airtel Money, ikiwa ni baada ya kuingia kwenye kipengele cha lipa bili, kuingiza namba ya kampuni 505050 na kuingiza namba ya kumbukumbu 2456.

EfG YAPONGEZWA KUFUNGUA KLABU ZA KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA SOKO LA ILALA BOMA JIJINI DAR ES SALAAM

April 26, 2017
 Mfanyabiashara wa nguo za mitumba ya kike katika Soko la Ilala Boma jijini Dar es Salaam, Daud Omary (kushoto), akitoa maelezo Dar es Salaa jana ya vitendo vya ukatili wa kijinsia wanavyofanyiwa na baadhi ya askari polisi wa Kituo cha Pangani kwa Mwezeshaji wa kisheria katika soko hilo (kulia) kutoka Shirika la Equality for Growth (EfG), wakati wa uhamsishaji wa kufungua klabu za mabadiliko ya kupinga ukatili wa kijinsia masokoni unaofanywa na Shirika hilo kwa kusimamiwa na Kituo cha Msaada wa Kisheria kwa Wanawake Tanzania (WLAC) kupitia kampeni ya miezi miwili ya  Tunaweza. Katikati ni mfanyabiashara Seleman Adam.