SERIKALI IMETOA ZAIDI YA BILIONI 3 UKARABATI VYUO VYA SITA VYA WATOTO WENYE ULEMAVU

May 21, 2022
Naibu Waziri toka Ofisi ya Waziri Mkuu, Patrobas Katambi akizungumza jambo Mwenyekiti  wa Watu Wenye ulemavu  toka Korogwe Vijijini Shaban Shekihiyo wakati wa ghafla ya ufunguzi wa chuo cha walemvu
Naibu Waziri toka Ofisi ya Waziri Mkuu, Patrobas Katambi akizungumza jambo Mwenyekiti  wa Watu Wenye ulemavu  toka Korogwe Vijijini Shaban Shekihiyo wakati wa ghafla ya ufunguzi wa chuo cha walemvu
Naibu Waziri toka Ofisi ya Waziri Mkuu, Patrobas Katambi kulia akicheza mziki na wanafunzi walemavu toka kituo cha YDCP kwenye ghafla ya ufunguzi wa Chuo cha walemavu


NA OSCAR ASSENGA,TANGA
 
SERIKALI ya awamu ya Sita inaoongozwa na Rais Samia Suluhu imetenga zaidi ya Shs bil 3 kwa ajili ya ukarabati wa vyuo Sita vya watoto wenye ulemavu nchini


Kauli hiyo imetolewa Jijini Tanga  na Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu kazi,vijana,ajira na wenye ulemavu Patrobas Katambi wakati wa ufunguzi wa Chuo cha Ufundi na marekebisho kwa watu wenye ulemavu

Katambi alisema Serikali inatambua umuhimu wa kundi hilo na ilitoa maelekezo ya kufanyiwa ukarabati wa vyuo hivyo ili kutoa fursa kwa jamii hiyo kupata elimu itakayowasaidia kujifunza ufundi utakao wanufaisha katika maisha yao.


Aidha aliitaja mikoa ambayo ina vyuo hivyo ni pamoja na Daresalaam,Tanga,Tabora,Mtwara,Singida na Mwanza ambapo alisema kuwa kama vyuo hivyo vitatumika vizuri idadi kubwa ya watoto walemavu inaweza kujitegemea na kuingia katika ajira kwa maslahi ya maisha yao na familia zinazowazunguka.
 
Katambi aliongeza kuwa Mh:Rais Samia Suluhu ameziagiza Wizara zote zihakikishe zinatoa ajira kwa asilimia 3 kwa kundi hilo la walemavu ili kuwaondolea dhana ya kuwa wategemezi na watu wasioweza kujiajiri ama kuajiriwa.


"Lazima haki ya elimu,afya na ajira zitekelezwe kwa mujibu wa sheria za Nchi yetu,unafikiri bila ya kuliwezesha kundi hili kielimu na ufundi,utawaajiri wapi,nazima tuwaandae na tunaweza kupata watumishi bora"Alisema Katambi.


Hata hivyo amemuagiza Katibu Tawala Mkoa kuhakikisha wanapata eneo kubwa kwa ajili ya ujenzi wa chuo hicho ambapo kitakuwa na uwezo wa kupokea wanafunzi walemavu toka Kanda nzima ya Kaskazini.


Kwa upande wa katibu Tawala Mkoa Tanga Pili Mnyema alisema wapo walemavu elfu tatu ambapo Mkoa inawatambua na Serikali imeweka mazingira rafiki ili kuweza kuwawezesha.


Mnyema alisema kwa mwaka huu wa fedha tayari  Halmashauri imetoa Shs Mil 121 ambayo ni asilimia 2 ya Shs Mil 600 kwa ajili ya kuwawezesha walemavu.
 
Nae Mkuu wa Chuo hicho Joharia Msuya alisema changamoto ya chuo ni pamoja na kuwa na walimu 3 wa kuajiriwa jambo ambalo linazorotesha ufanisi wa majukumu ya kila siku.


Msuya alisema mbali ya walimu na wafanyakazi wasiokuwa walimu pia eneo la chuo hicho ni dogo ungilinganisha na idadi ya wanafunzi inayotakiwq kuhudumiwa ambapo wanatoka mikoa 3.

Mwisho.

HALIMA KOPWE MISS TANZANIA , RAIS SAMIA KUJENGA UKUMBI WA KIMATAIFA JIJINI DAR

May 21, 2022



Na John Mapepele

Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Mhe, Mohamed Mchengerwa amesema Serikali ya Mhe. Rais Samia imedhamiria kuinua kuinua kiwango cha mashindano ya urembo nchini  ikiwa ni pamoja na kujenga ukumbi wa kimataifa  katika jiji la Dar es Salaam.


Akizungumza usiku wa kuamkia leo Mei 21, 2022 kwenye kilele cha mashindano ya kumtafuta  Miss Tanzania 2022 ambapo Halima Kopwe toka Mtwara ametwaa taji hilo, Mhe . Mchengerwa amesema ukumbi huo  licha ya kufanyiwa kazi mbalimbali za Sanaa na burudani pia utatumika kwenye mashindano ya kimataifa ikiwa ni pamoja na shindano la Miss Tanzania.

 "Ukumbi huo unatarajiwa kuongoza kwa ubora na ukubwa barani Afrika ambapo utachukua takribani watu elfu ishirini" amesisitiza Mhe. Mchengerwa

Aidha, amesema Serikali ya Awamu ya Sita itaendelea kuwashika mkono washindi wote na kufafanua kuwa washiriki wote walioshiriki shindano hili hadi kufika fainali ni washindi.

Amewapongeza waandaji wa shindano hilo kwa uratibu mzuri  ambapo ameongeza kuwa washiriki  wamefanya kazi nzuri ya ubunifu na Sanaa.

Pia amesema Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo ndiyo Wizara pekee inayowapa furaha na faraja watanzania wengi.

Pia Mhe. Mchengerwa amesema Filamu ya Royal Tour imesaidia kufungua milango na kuitangaza Tanzania  duniani na kuwataka wasanii kutumia fursa hiyo kutengeneza ajira na vipato.

Miss Tanzania kwa mwaka huu; Halima Kopwe amejishindia gari  dogo aina ya Benzi lenye thamani ya shilingi milioni 30 na  fedha taslimu shilingi milioni kumi.


Shindano hilo limefanyika jijini Dar es Salaam kwenye Ukumbi wa Mlimani City na kuhudhuriwa na mamia ya washabiki wa urembo.