WANAWAKE BARANI AFRIKA WAKUTANA TANZANIA KUJADILI AMANI YA BARA LA AFRIKA

November 03, 2017
Aliyekuwa katibu Mkuu wa Mkutano wa Beijing , Getrude Mongela akizungumza wakati wa mkutano wa Wajibu wa Mwanamke katika masuala ya Amani na kutatua Matatizo Barani Afrika uliofanyika jijini Dar es Salaam jana.
Muasisi wa Mkutano wa Wanawake juu ya Amani na kutatua matatizo Barani Afrika, Dkt. Basirat Nahibi akizungumza juu ya suala la wanawake wa bara la Afrika kukutana kujadili na kuandaa upatanishi juu ya mgogoro wa kisiasa unaondelea nchini Kenya.
Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko Kutoka Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Balozi Amina Salum Ali akizungumza katika mkutano huo kwa niaba ya Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu
Muuandaaji wa mkutano huo kwa hapa Tanzania , Khadija akimkabidhi kitabu Aliyekuwa katibu Mkuu wa Mkutano wa Beijing , Getrude Mongela
Mwanahabari Mwanamke mkongwe nchini Radhia Mwawanga akichangia hoja katika mkutano wa Wajibu wa Mwanamke katika masuala ya Amani na kutatua Matatizo Barani Afrika uliofanyika jijini Dar es Salaam jana.
Mjumbe wa mkutano huo Madam Fanta Dissa Berthe akichangia jambo mkutano wa Wajibu wa Mwanamke katika masuala ya Amani na kutatua Matatizo Barani Afrika uliofanyika jijini Dar es Salaam jana
Mhariri wa jarida la mkutano wa Wajibu wa Mwanamke katika masuala ya Amani na kutatua Matatizo Barani afrika, Fatma Othman Moma akizungumza wakati wa mkutano huo uliofanyika jijini Dar es Salaam jana.
Baadhi ya Viongozi Wanawake walioshiriki Baadhi ya Viongozi Wanawake walioshiriki mkutano wa Wajibu wa Mwanamke katika masuala ya Amani na kutatua Matatizo Barani Afrika uliofanyika jijini Dar es Salaam jana, wakifuatilia kwa makini,mada mbalimbali zilizokuwa zikitolewa katika mkutano huo.
Baadhi ya Viongozi Wanawake walioshiriki mkutano wa Wajibu wa Mwanamke katika masuala ya Amani na kutatua Matatizo Barani afrika uliofanyika jijini Dar es Salaam jana wakisikiliza mada zilizokuwa zikijadiliwa katika mkutano huo.
Picha ya Pamoja ya Baadhi ya Viongozi Wanawake walioshiriki mkutano wa Wajibu wa Mwanamke katika masuala ya Amani na kutatua Matatizo Barani Afrika.

WANAWAKE BARANI AFRIKA WAKUTANA TANZANIA KUJADILI AMANI YA BARA LA AFRIKA

November 03, 2017
Aliyekuwa katibu Mkuu wa Mkutano wa Beijing , Getrude Mongela akizungumza wakati wa mkutano wa Wajibu wa Mwanamke katika masuala ya Amani na kutatua Matatizo Barani Afrika uliofanyika jijini Dar es Salaam jana.
Muasisi wa Mkutano wa Wanawake juu ya Amani na kutatua matatizo Barani Afrika, Dkt. Basirat Nahibi akizungumza juu ya suala la wanawake wa bara la Afrika kukutana kujadili na kuandaa upatanishi juu ya mgogoro wa kisiasa unaondelea nchini Kenya.
Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko Kutoka Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Balozi Amina Salum Ali akizungumza katika mkutano huo kwa niaba ya Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu
Muuandaaji wa mkutano huo kwa hapa Tanzania , Khadija akimkabidhi kitabu Aliyekuwa katibu Mkuu wa Mkutano wa Beijing , Getrude Mongela
Mwanahabari Mwanamke mkongwe nchini Radhia Mwawanga akichangia hoja katika mkutano wa Wajibu wa Mwanamke katika masuala ya Amani na kutatua Matatizo Barani Afrika uliofanyika jijini Dar es Salaam jana.
Mjumbe wa mkutano huo Madam Fanta Dissa Berthe akichangia jambo mkutano wa Wajibu wa Mwanamke katika masuala ya Amani na kutatua Matatizo Barani Afrika uliofanyika jijini Dar es Salaam jana
Mhariri wa jarida la mkutano wa Wajibu wa Mwanamke katika masuala ya Amani na kutatua Matatizo Barani afrika, Fatma Othman Moma akizungumza wakati wa mkutano huo uliofanyika jijini Dar es Salaam jana.
Baadhi ya Viongozi Wanawake walioshiriki Baadhi ya Viongozi Wanawake walioshiriki mkutano wa Wajibu wa Mwanamke katika masuala ya Amani na kutatua Matatizo Barani Afrika uliofanyika jijini Dar es Salaam jana, wakifuatilia kwa makini,mada mbalimbali zilizokuwa zikitolewa katika mkutano huo.
Baadhi ya Viongozi Wanawake walioshiriki mkutano wa Wajibu wa Mwanamke katika masuala ya Amani na kutatua Matatizo Barani afrika uliofanyika jijini Dar es Salaam jana wakisikiliza mada zilizokuwa zikijadiliwa katika mkutano huo.
Picha ya Pamoja ya Baadhi ya Viongozi Wanawake walioshiriki mkutano wa Wajibu wa Mwanamke katika masuala ya Amani na kutatua Matatizo Barani Afrika.

BOT YAWAJENGEA UWEZO WA KUTAMBUA NOTI BANDIA WATU WENYE ULEMAVU WA KUTOSIKIA WILAYANI CHATO

November 03, 2017
Bw,Patrick Fata ambaye ni Mhelimishaji kutoka BOT akielekeza na kutoa elimu namna ambavyo unaweza kutambua Noti bandia. 
Meza kuu ikiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Chato Shaaban Ntarembe. 
Maafisa wa BOT wakifuatilia maelezo ya Meneja Msaidizi wa Idara ya Uhusiano wa BOT, Vicky Msina wakati alipokuwa akielezea juu ya elimu ambayo wanaitoa kwa viziwi. 
Meneja Msaidizi wa Idara ya Uhusiano wa BOT, Vicky Msina akielezea malengo ya kutoa elimu ya kuwawezesha viziwi kutambua alama za usalama zilizopo kwenye noti ili kuzitofautisha na noti bandia pindi wanapokuwa katika shughuli zao za utafutaji. 
Mwenyekiti wa Kituo cha Sanaa na Utamaduni kwa Viziwi Tanzania (Kisuvita), Habibu Mrope akizungumza changamoto ambazo wamekuwa wakikutana nazo watu ambao ni walemavu hususani wakati wanapokuwa wanakwenda kwenye huduma za kibenki. 
Bw,Patrick Fata ambaye ni Mhelimishaji kutoka BOT,akisisitiza swala la alama za fedha ambazo zinakuwepo kwenye noti. 
Kifaa ambacho kinatumika kuangalizia noti bandia na ile ambayo ni ya harari. 
Noti ambazo zinakuwa zimeharibiwa zikiwa kwenye mafungu fungu lenye rangi nyekundi ni elfu kumi na yenye rangi ya blue ni elfu tano. 
 
 
NA JOEL MADUKA,CHATO.

Benki kuu ya Tanzania (BOT)imekutana na kundi la watu wenye ulemavu wa kutokusikia na wale ambao hawaoni Wilayani Chato lengo likiwa ni kuwapatia na elimu ya utambuzi wa Noti bandia Wilayani humo.

Akizungumza kwenye semina ambayo imefanyika kwenye ukumbi wa KKKT Wilayani Humo,Meneja msaidizi wa idara ya uhusiano wa BOT, Vicky Msina alisema elimu wanayoitoa imelenga kuwawezesha viziwi kutambua alama za usalama zilizopo katika noti ili kuzitofautisha na noti bandia wanapokuwa katika shughuli zao kwani mtu yeyote akikutwa na noti bandia ni kosa la jinai, hivyo wanawapa mafunzo ili wasikumbwe na kadhia hiyo.

“Ni muda sasa walituomba kuwapa mafunzo na hii ni kutokana na wengi wao kutokujua noti bandia wamekuwa wakijikuta wanabambikiwa na pia wanapo kwenda benki kupeleka fedha zao wahudumu huwadharau na wakati mwingine kwa wale wanao kwenda kuchukua fedha hupatiwa noti chafu jambo ambalo lilitusukuma kuwaelimisha juu ya hatua za kufuata ilikupatiwa haki zao za msingi kwenye huduma hizo,”alisema Msima.

Mwenyekiti wa Kituo cha Sanaa na Utamaduni kwa Viziwi Tanzania (Kisuvita), Habibu Mrope alisema kuna tatizo kubwa la kutotambua noti bandia kwa Walemavu hali ambayo imechangia kuwarudisha nyuma kwani wanapokutwa na noti hizo huchukuliwa hatua za kisheria.

Hata hivyo kutokana na tatizo hilo Mkuu wa wilaya ya Chato Shaaban Ntarambe aliwaahidi watu ambao wanamatatizo ya kutokusikia kufunguliwa kwa shule ambayo itawasaidia kujifunza lugha za alama kwania ya kuboresha mawasiliano kwenye jamii.

“Idadi ya wilaya yetu kuna Viziwi 347 ambapo ni sawa na asilimia 90 ya watu wenye ulemavu wa kusikia hawajui lugha za nyakati upekee idadi hii ni kubwa sana ni lazima Serikali ifanye jitihada za kuwa kwamua watu hawa ambapo kwa kushirikisha wadau mbali mbali, nitahakikisha ujenzi wa shule hiyo unaanza mara moja,”alisisitiza Tarambe

DC SHINYANGA AKUTANA NA WAKULIMA WA PAMBA SHINYANGA VIJIJINI KUHAMASISHA KILIMO CHA KISASA

November 03, 2017
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro leo Ijumaa Novemba 3,2017 amewatembelea wakulima wa zao la pamba katika kijiji cha Sayu kata ya Pandagichiza halmashauri ya wilaya ya Shinyanga kwa ajili ya kuwahamasisha kulima zao hilo kwa njia za kitaalamu/kisasa ili kilimo hicho kiwe na tija kwa ajili ya kujikomboa kiuchumi.

Tigo yatoa zawadi kwa washindi wa nunua simu na ushinde na kuahidi makubwa siku zijazo

November 03, 2017
Meneja Mawasiliano wa Tigo, Woinde Shisael (kushoto) akikabidhi zawadi ya pikipiki kwa Yakobo Lucas ambaye alikuwa mojawapo wa washindi wa zawadi za pikipiki na televisheni za LED katika promosheni iliyokwisha ya 'Tigo Nunua Simu na Ushinde'. Jumla ya pikipiki 20 na TV 20 zilitolewa katika promosheni hiyo.


Meneja Mawasiliano wa Tigo, Woinde Shisael (kushoto) akikabidhi zawadi ya televisheni ya LED kwa Farida Rajab  ambaye alikuwa mojawapo wa washindi wa zawadi za pikipiki na televisheni za LED katika promosheni iliyokwisha ya 'Tigo Nunua Simu na Ushinde'. Jumla ya pikipiki 20 na TV 20 zilitolewa katika promosheni hiyo.

Meneja Mawasiliano wa Tigo, Woinde Shisael (kushoto) akikabidhi zawadi ya televisheni ya LED kwa Salum Yahawa  ambaye alikuwa mojawapo wa washindi wa zawadi za pikipiki na televisheni za LED katika promosheni iliyokwisha ya 'Tigo Nunua Simu na Ushinde'. Jumla ya pikipiki 20 na TV 20 zilitolewa katika promosheni hiyo.

Mohammed Dewji apongeza jitihada za Rais Magufuli kufufua viwanda

November 03, 2017
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Mohammed Enterprises (MeTL Group), Mohammed Dewji amepongeza uamuzi wa Rais wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli kuifanya Tanzania kuwa nchi ya viwanda kwa kufufua viwanda ambavyo vilikuwa havifanyi kazi.
Dewji ametoa pongezi hizo wakati akizungumza katika mkutano wa siku mbili wa Global Business Forum 2017 (GBF) kuhusu Viwanda kwa Nchi za Afrika uliofanyika Dubai, Falme za Kiarabu (UAE).
Mfanyabiashara huyo ambaye anamiliki viwanda 41 alisema uamuzi aliochukua Rais Magufuli ni mzuri hasa katika kipindi hiki ambacho Tanzania inaelekea katika uchumi wa kati.

Dewji alisema kampuni yake ya MeTL Group itaendelea kushirikiana na serikali na katika kipindi cha miaka kadhaa ijayo amejipanga kuhakikisha anatoa ajira kwa Watanzania 100,000 jambo ambalo litasaidia kukuza uchumi wa nchi na kwa wananchi..
 “Nianze kwa kumpongeza Mhe. Rais John Pombe Magufuli kwa shabaha yake ya viwanda, ni nzuri sababu kuna ongezeko la thamani lakini pia watu wanaweza kupata ajira na pia hizi biashara zitalipa kodi ambazo zitaisaidia serikali kuwekeza kwenye mambo ya afya na maji na huduma za jamii. Mimi shabaha yangu kwenye miaka saba au nane ijayo MeTL Group tunataka tuajiri watu 100,000,” alisema Dewji.
Dewji ambaye kwa mujibu wa jarida la Forbes ni tajiri namba moja nchini aliongeza kuwa utendaji wa Rais Magufuli ni wa kasi hivyo anategemea kuwa katika kipindi cha miaka michache ijayo uchumi wa Tanzania utakuwa umekuwa  sana.
“Mimi naona kwa kasi ya Mhe. Rais kwenye miaka miwili au mitatu ijayo tutakuwa tumefika mbali sana, uchumi wetu kwasasa ni asilimia sita au saba lakini kama tukitaka kuondoa umaskini lazima nchi yetu ukuaji wa uchumi uanze kukua kwa zaidi ya asimilia 10, mimi nina muamini sana Mhe. Rais na shabaha yake kwahiyo Mungu atutangulie na sisi tupo nyuma yake tutafika hivi karibuni,” alisema Dewji.
Pia Dewji alizungumzia umuhimu wa mkutano wa GBF ambao umekutanisha watu kutoka mataifa mbalimbali ya Afrika wakiwepo viongozi wa serikali za nchi za Afrika na wawekezaji alisema ni nafasi ya kipekee kwani pamoja na kujadili viwanda pia amepata nafasi ya kuwaelezea washiriki wa mkutano fursa za uwekezaji zilizopo hapa nchini.
“Umuhimu ni mkubwa sana nakuja hapa kama MO lakini pia nawakilisha nchi yangu Tanzania, nimeitangaza nchi yangu ili watu waje na wawekeze, nimewaeleza mazingira yetu ya uwekezaji ni mazuri, tuna malighafi na tunahitaji viwanda angalau watu wetu wa Tanzania wapate ajira na serikali ipate kodi,” aliongeza Dewji.

TOT PLUS WAJIFUA KUIPUA NYIMBO TATU MPYA UKIWEMO WA KUMUUNGA MKONO JPM KATIKA VITA YA KUTETEA RASILIMALI ZA NCHI

November 03, 2017
Mkurugenzi wa TOT Gasper Tumaini
NA BASHIR NKOROMO
Kundi la Tanzania One Theatre (TOT Plus), limo kambini Wanamuziki wake wakijifua vikali katika mazoezi ya nyimbo tatu ambazo kundi hilo litaziipua hivi karibuni.

Akizungumza wakati wa mazoezi ya nyimbo hizo, Mkurugezi wa TOT Plus inayomilikiwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM), Gasper Tumaini amezitaja nyimbo hizo kuwa ni 'Tumuunge mkono JPM',  'Amani ya Tanzania' na Hongera awamu ya tano'.

Tumaini amsema, wimbo wa 'Tumuunge mkono JPM' ni wa kuwahamasisha Watanzania popote walipo kumuunga mkono Rais Dk John Magufuli katika vita ya uchumi anayoongoza kwa kuhakikisha inaziba mianya inayotishia upotevu au matumizi mabaya ya rasilimali za nchi.

"Kama unavyoona Rais tayari ameshaamua kwa dhati kupigana katika vita ya kubana mianya inayotishia upotevu au matumizi mabaya yanayofanya na baadhi ya watu kutumia rasilimali za nchi vibaya kwa kujinufaisha wao huku taifa likiendelea kuwa masikini

Hii siyo vita ndogo, ni kubwa sana inayohitaji ujasiri na ari kubwa ya kujituma, hivyo ni lazima Watanzania wote tumuunge mkono ili asiyumbishwe na waliokuwa wanajinufaisha na rasilimali hizi", alisema Tumaini wakati wa mazoezi ya nyimbo hizo kwenye ukumbi wa Ofisi ya CCM Mwinjuma, Mwananyamala, Dar es Salaam.

Amesema, wimbo wa 'Amani ya Tanzania' kunahimiza Watanzania ndani na nje ya Nchi kuhakikisha pia wanaienzi amani ya nchi kwa kuunga mkono juhudi za kuiimanrisha zinazofanywa na viongozi wakiongozwa na misingi imara iliyowekwa na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere na pia Rais wa Kwanza wa Zanzibar  Hayati Sheikh Abeid Amani Karume.

Akizungumzia wimbo wa tatu wa 'Hongera awamu ya Tano', Tumaini amesema, wimbo huo ni wa pongezi kwa Mwenyekiti wa CCM, Rais Dk. John Magufuli kwa kutimiza kwa vitendo ahadi zilizotolewa na CCM wakati wa kampeni za kuomba ridhaa ya wananchi katika uchaguzi mkuu uliopita.

"Tumeona ni vizuri kutunga wimbo huu wa kumpongeza kwa sababu utekelezaji wa ilani na ahadi alizokuwa akizitoa kwenye kampeni unaonekana wazi japokuwa sasa ni miaka miwili tu tangu tumchague, kwa kweli Rais Dk. Magufuli amechapa kazi hivyo inastahili kumpongeza", alisema tumaini.

Amesema, nyimbo hizo ambazo ni kwaya tayari zimeshakamilika na sasa wanamuziki wanazifanyia mazoezi ya mwisho mwisho  kabla ya kuzirekodi ili zianze kusikika katika maeneo mbalimbali na hasa pale kundi hilo litakapokuwa likitumbuiza.

Mmiliki wa theNkoromoBlog aliyefika kwenye mazoezi ya kundi hilo, alishuhudia wanamuziki wote wakiwajibika kila mmoja katika eneo lake, huku baadhi yao wakitokwa jasho kuliko hata wanapokuwa wakitumbuiza jukwaani katika maonyesho maalum.
 Mwanamuziki nguli Juma Abdallah 'Jerry' akikipapasa kinanda kwa mkoni mmoja kuonyesha umahiri wake, Kundi la TOT Plus lilipokuwa katika mazoezi ya nyimbo tatu, leo katika ukumbi wa CCM Mwinjuma, Mwananyamala Dar es Salaam
 Waimbaji Neca Twalib aliyechukua nafasi iliyoachwa na aliyekuwa mwimbaji nguli na Mkurugenzi wa TOT Plus Marehemu Kampteni John Komba, akiimba na mwenzake Corobian Mkinga wakati wa mazoezi hayo
 Patrick Thomas akizicharaza tumba wakati wa mazoezi hayo
 Mkurugenzi wa TOT Plus Gasper Tumaini (mwenye suti) akizungumza na baadhi ya wadau waliofika kushuhudia mazoezi hayo
 Jerry akikicharaza kinanda kwa madaha wakati wa mazoezi hayo
 Waimbaji Rosemary William, Sharifa Mohammed na Mwasiti Suleimani wakiimba wakati wa mazoezi hayo
 Mwimbaji nguli Hadija Kopa na wenzake wakiimba wakati wa mazoezi hayo
 Tumaini akiwa na wadau wakati wakifuatilia mazoezi hayo. Kulia ni Jerry
 Waimbaji wa TOT Plus wakiwa kwenye mazoezi hayo
 Waimbaji wa TOT Plus wakiwa kwenye mazoezi ya wimbo wa 'Amani ya Tanzania'
MPINA: “WAFUGAJI TEMBEENI KIFUA MBELE WAZIRI MNAYE”

MPINA: “WAFUGAJI TEMBEENI KIFUA MBELE WAZIRI MNAYE”

November 03, 2017
DSC_0001
Waziri Mpina na baadhi ya viongozi wa wilaya ya Bukoba wakielekea katika zoezi la upigaji chapa ng’ombe katika kata ya katerero kijijini Kyerwa leo.
DSC_0006
Katika picha ikionekana sehemu ya ng’ombe aliyepigwa chapa katika kata ya Katerero kijijini Kyerwa leo.
IMG_20171102_152455
 Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe Luhaga Mpina, Mkuu wa Wialaya ya Biharamulo Bi. Saada Malunde baada ya zoezi la kukagua uvamizi wa mifugo katika sehemu ya pori la Bugiri Biharamuro, wengine katika picha ni askari wanyamapori wa pori hilo.
IMG_20171102_155907
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe Luhaga Mpina, Mkuu wa Wialaya ya Biharamulo Bi Saada Malunde wakizungumza  baada ya zoezi la kukagua uvamizi wa mifugo katika sehemu ya pori la Bugiri Biharamuro.
………………………………………………………………………….
NA; MWANDISHI MAALUM – KATERERO
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhanga Mpina  amewataka wafugaji nchini kutembea kifua mbele kwa kumpata yeye kama Waziri mwenye dhamana ya Mifugo, Mpina ameyasema hayo leo aliposhiriki katika zoezi la kupiga chapa Mifugo  katika Kijiji cha Kyelwa kilichopo katika kata ya Katerero halimashauri ya wilaya Bukoba mkoani Kagera,  na kuwataka viongozi kuzingatia maadili wakati wa utekelezaji wa zoezi hilo ili kuepuka hujuma na ubaguzi kwa wafugaji.
Waziri Mpina alipofika katika kata ya  Katerero aliwakuta wafugaji wamejitokeza kwa wingi kuunga mkono zoezi la uwekaji alama katika mifugo yao na kushiriki zoezi hilo kwa kuonyesha msisitizo.
Mara Baada ya kushiriki zoezi hilo, Waziri Mpina aliwataka wafugaji  hao kuendelea kujitokeza kwa wingi na kuleta mifugo yao kupigwa chapa na kusema kuwa zoezi hilo ni la manufaa na faida kwa wafugaji kwani litaweza kuwasiadia kuhepuka maambukizi ya magonjwa ya wanyama kwa mifugo yao kuto kuchanganyikana na mifugo mingine sambamba na kusaidia upotevu wa mifugo.

MESSAGE FROM DG OF UNESCO, ON THE OCCASION OF THE INTERNATIONAL DAY TO END IMPUNITY FOR CRIMES AGAINST JOURNALISTS, 2 NOVEMBER 2017

November 03, 2017
Justice is a cornerstone of a free society. It dissuades those who threaten freedom of expression and emboldens those who stand to defend it. This is why injustice against journalists is so costly for all societies.
From 2006 to 2016, no less than 930 journalists were killed. In 2016 alone, we saw the loss of 102 journalists in the line of duty.
What makes these figures even more unbearable is that, in more than nine out of ten cases, the perpetrators are never brought to justice.
This concerns mostly local journalists -- 93% of journalists killed in the last 11 years were local journalists covering local stories. This concerns also the threats faced by female journalists, including the alarming rise of online harassment.
We must ensure justice is done for every journalist killed. This is essential for their memory -- it is vital to strengthen the rule of law and good governance, and take forward the 2030 Agenda for Sustainable Development, specifically Sustainable Development Goal 16 on peace, justice and strong institutions.
Journalists perform unique functions in taking forward our fundamental freedoms and bolstering the strength of our societies -- they must be defended through concerted action by Governments, supported by the United Nations, working with all relevant actors, from international regional organizations, judiciaries and media to private companies, academia and civil society.
This partnership for action was embodied in UNESCO’s recent Multi-Stakeholder Consultation, held in Geneva to strengthen implementation of the UN Plan of Action on the Safety of Journalists and the Issue of Impunity. We must draw on this spirit to support Member States in enhancing the safety of journalists and eliminating impunity through stronger mechanisms.
On this day, UNESCO calls for the world to stand together to bolster the safety of journalists and ensure justice is