Rais Kikwete Amfariji Salva Rweyemamu

Rais Kikwete Amfariji Salva Rweyemamu

May 16, 2014

D92A2854  
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akisaini kitabu cha maombolezo nyumbani kwa Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Ofisi ya Rais Ikulu Bwana Salva Rweyemamu Kinondoni jijini Dar es Salaam kufuatia kifo cha mwanaye Private Brian Salva Rweyemamu kilichotokea jana katika hospitali ya jeshi Lugalo jijini baada ya kuugua kwa muda mfupi. Marehemu Private Brian anatarajiwa kuzikwa kesho mchana(Jumamosi) katika makaburi ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.
D92A2875  
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akipa pole Bibi Isabela Salva Rweyemamu ambaye ni mama wa Marehemu Private Brian Salva Rweyemamu wakati alipokwenda kutoa pole nyumbani kwa marehemu Kinondoni jijini Dar es Salaam leo.
D92A2886  
Rais Dkt.Jakaya Mrisho kikwete akiwafariji Mkurugenzi wa Mawasiliano Ofisi ya Rais Ikulu Bwana Salva Rweyemamu na Mkewe Isabela Salva Rweyemamu ambao ni wazazi wa Marehemu Private Brian Salva Rweyemamu nyumbani kwao Kinondoni jijini Dar es Salaam leo.
D92A2905 
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na kuifariji familia ya Marehemu Private Brian Salva Rweyemamu nyumbani kwao Kinondoni jijini Dar es Salaam leo(picha na Freddy Maro)
KATIBU MKUU WA CCM TAIFA NDUGU ABDULRAHMAN KINANA AWASILI URAMBO NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

KATIBU MKUU WA CCM TAIFA NDUGU ABDULRAHMAN KINANA AWASILI URAMBO NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

May 16, 2014
1 
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akivishwa skafu mara baada ya kuwasili katika kata ya Uyumbu wilayani Urambo leo akitokea wilayani Sikonge akiwa katika ziara ya kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa na serikali, kusikiliza kero za wananchi na kuzitafutia ufumbuzi na kuimarisha chama ikiwa ni usimamizi wa ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010, Katika ziara hiyo Kinana anaongozana na Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi, Siasa na Uenezi ambapo ziara hiyo iliyoanzia mkoa wa mkoa Tabora itaendelea na ziara katika mikoa ya Singida na Manyara.(PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-URAMBO-TABORA) 2Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na Mbunge wa jimbo la Urambo na Waziri wa ushirikiano wa Afrika Mashariki Mh. Samwel Sitta wakati alipowasili katika kata ya Uyumbu. 4Wana CCM na viongozi mbalimbali wa chama cha Mapinduzi wakimpokea Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana wakati alipowasili katika kata ya Uyumbu wilayani Urambo. 9 
Mbunge wa jimbo la Urambo na Waziri wa ushirikiano wa Afrika Mashariki Mh. Samwel Sitta akimsikiliza kwa makini Mkuu wa mkoa wa Tabora Bi. Fatma Mwassa wakati wa mapokezi ya Katibu mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana. 10Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na mbunge wa jimbo la Urambo na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mh. Samwel Sitta katikati ni Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi, Siasa na Uenezi. 12 
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki ujenzi wa maabara ya shule ya sekondari ya Uyumbu pamoja na Mbunge wa Urambo na Waziri wa  Ushirikiano wa Afrika Mashariki. 13Kikundi cha ngoma za asili kikitumbuiza wakati wa mapokezi ya Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana katika kata ya Uyumbu wilayani Urambo leo. 14Mbunge wa Urambo na Waziri wa Ushirikiano wa  Afrika Mashariki Mh. Samwel Sitta akishiriki kucheza ngoma katika kijiji cha Izengamatugalo kata ya Ugara. 15Vijana wa sungusungu wakicheza ngoma yao 16Wana CCM mbalimbali wakiwa katika mkutano huo. 17 
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wananchi  katika kata ya Ugara wakati alipotembelea zahanati ya kijiji cha Izengamatugalo, kulia ni Katibu wa NEC Itikadi, Siasa na Uenezi wa  pili ni Mbunge wa Urambo na Waziri wa  Ushirikiano wa Afrika Mashariki na kushoto ni Kaimu mganga mkuu wa hospitali ya wilaya ya Urambo Dk. Heri Kagwa. 18 
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiongozwa na Kaimu Mganga mkuu wa hospitali ya wilaya Urambo Dk. Heri Kagwa wakati alipokagua zahanati ya kijiji cha Izengamatugalo. 19 
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikagua zahanati ya kijiji cha Izengamatugalo. 21 
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikagua mashine ya kukamua mafuta ya alizeti katika kata ya Itundu, Kulia Mbunge wa viti maalum Mkoa wa Tabora Mh. Magreth Simwanza Sitta. 22a 
Shamba la mahindi la umwagiliaji la kikundi cha hiari ya Moyo katika kijiji cha Urasa kata ya Kipilula 23 
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akitembelea shamba la umwagiliaji la kikundi cha Hiari ya Moyo kijiji cha Urasa kata ya Kipilula huku akiwa ameongozana na mkuu wa shamba hilo mzee Ramadhan Majala. 24 
Mbunge wa jimbo la Urambo na Waziri wa Ushirikiano wa  Afrika Mashariki Mh. Samwel Sitta akitembelea kikundi cha Hiyari ya Moyo. 25 
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akielekea kukagua kisima  cha maji kwa ajili ya kumwagilia shamba hilo. 26 
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikagua kisima cha maji kinachotumika kumwagilia shamba hilo la kikundi cha Hiari ya Moyo akiongozwa na mzee Ramadhana Majala. 27 
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiangalia mabomba madogo ya kumwagilia maji iliotandazwa katika shamba hilo. 28 
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiongozana na Mzee Ramadhan Majala kiongozi wa mradi huo.Kushoto ni Mbunge wa jimbo la Urambo na Waziri wa Ushirikiano wa  Afrika Mashariki Mh. Samwel Sitta. 29 
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipiga picha na wanakikundi wa kikundi cha Hiari ya Moto wilayani Urambo. 30 
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na wafanyakazi wa hospitali ya wilaya ya Urambo mara baada ya kuwasili hospitalini hapo. 31 
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikagua jengo jipya la wodi ya wazazi lililojengwa katika hospitali ya wilaya ya Urambo. 32 
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikagua wodi hiyo. 33 
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikagua jengo la wazazi ktika hospitali hiyo huku akiongozana na Mbunge wa jimbo la Urambo na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mh. Samwel Sitta. 34 
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiondoka mara baada ya kukagua jengo hilo. 35 
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki katika ujenzi wa ofisi ya CCM Tawi la Mabatini. kushoto anayeshirikiana naye ni Mbunge wa jimbo la Urambo na Waziri wa Afrika mashariki Mh. Samwel Sitta.

TAARIFA KUTOKA NDANI YA SHIRIKISHO LA SOKA NCHINI TFF LEO

May 16, 2014
TUPO TAYARI KUIKABILI ZIMBABWE- NOOIJ
Kocha wa Taifa Stars, Mart Nooij amesema wachezaji wake wako tayari kwa ajili ya mechi ya Kombe la Afrika dhidi ya Zimbabwe (Mighty Warriors) itakayochezwa Jumapili kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo (Mei 16 mwaka huu), Nooij amesema kabla ya kuja Tanzania alikuwa akifuatilia Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), hivyo anawafahamu wachezaji wengi.

Amesema wachezaji wanaounda kikosi chake ni wenye uzoefu na mechi za kimataifa, hivyo wapo tayari kwa ajili ya mechi hiyo, kwani wamepata mechi za kirafiki na mazoezi ya kutosha kwenye kambi iliyokuwa Tukuyu mkoani Mbeya ambapo kulikuwa na utulivu mkubwa.

Nooij amesema ujio wa washambuliaji Mbwana Samata na Thomas Ulimwengu wanaochezea timu ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (RDC) kutaongeza morali ya kikosi chake.

Samata na Ulimwengu watawasili nchini Jumamosi mchana, saa 7.30 mchana kwa ndege ya Ethiopian Airlines wakitokea Khartoum, Sudan ambapo leo (Mei 16 mwaka huu) wanacheza mechi ya Ligi ya Mabingwa dhidi ya Al Hilal ya huko.

Wachezaji waliopo kambini kwa sasa ni Deogratias Munishi, Aishi Manula, Said Moradi, Oscar Joshua, Kelvin Yondani, Erasto Nyoni, Nadir Haroub, Shomari Kapombe, Aggrey Morris, Himid Mao, Mwinyi Kazimoto, Frank Domayo, Amri Kiemba, Jonas Mkude, Haruna Chanongo, Simon Msuva, Mrisho Ngasa, Khamis Mcha, Ramadhan Singano, John Bocco, Elias maguli na Kelvin Friday.

Wakati huo huo, timu ya Zimbabwe (Mighty Warriors) inawasili kesho alfajiri (Mei 17 mwaka huu) kwa ndege ya Ethiopian Airlines ikiwa na msafara wa watu 27. Kesho saa 4 asubuhi (Mei 17 mwaka huu) Kocha wa timu hiyo atakuwa na mkutano na waandishi wa habari katika ofisi za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).

Tiketi kwa ajili ya mechi hiyo zinaanza kuuzwa kesho (Mei 17 mwaka huu) kwenye vituo vya Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa, mgahawa wa Steers uliopo Mtaa wa Ohio na Samora, OilCom Ubungo, Uwanja wa Taifa, kituo cha mafuta Buguruni na Dar Live Mbagala. Viingilio ni sh. 5,000, sh. 10,000 na sh. 20,000 tu.

…MDAU AAHIDI WACHEZAJI MIL 5/-
Mdau mmoja wa mpira wa miguu ambaye hataki jina lake litajwe ameahidi kutoa sh. milioni tano kwa wachezaji wa Taifa Stars iwapo wataifunga Zimbabwe katika mechi ya Jumapili.

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linamshukuru mdau huyo, na linatoa mwito kwa wadau wengine wajitokeze kutoa motisha kwa Taifa Stars.

Bonasi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kwa wachezaji wa Taifa Stars itatolewa kwa mujibu wa taratibu zilizopo.

TFF YAOMBOLEZA VIFO VYA WASHABIKI DR CONGO
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi amemtumia salamu za rambirambi mwenzake wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo- FECOFA, Omar Constant kutokana na vifo vya washabiki.

Washabiki 12 walipoteza maisha uwanjani wakati wa mechi ya Ligi Kuu ya nchi hiyo kati ya TP Mazembe na AS Vita iliyochezwa kwenye Uwanja wa Tata Raphael, jijini Kinshasa.

“Tumeguswa na msiba huo mzito, tunatoa salamu za rambirambi kwako (Rais wa FECOFA), familia za marehemu pamoja na wadau wote wa mpira wa miguu katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo,” imesema sehemu ya barua hiyo ya Rais Malinzi.

KOZI ZA UKOCHA LESENI A, B KUFANYIKA JUNI
Kocha a ukocha wa mpira wa miguu kwa ajili ya leseni A na B zinazotambuliwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF)  zitafanyika jijini Dar es Salaam kuanzia Juni 2 mwaka huu.

Ada kwa kozi zote ni sh. 300,000 ambapo wale watakaofanya ya A (equivalent) itaanza Julai 21-26 mwaka huu. Washiriki wa kozi hiyo ni wale wenye leseni B za ukocha za CAF.

Kwa wale watakaoshiriki kozi ya leseni B ambao ni wale wenye leseni C watakuwa na vipindi viwili. Kipindi cha kwanza ni kuanzia Juni 2-15 mwaka huu wakati cha pili kinaanza Juni 23 mwaka huu na kumalizika Juni 28 mwaka huu.

Wakufunzi wanaotambuliwa na CAF watakaoendesha kozi hiyo ni Sunday Kayuni na Salum Madadi kutoka Tanzania, na washiriki watajigharamia kwa kila kitu. Baadaye CAF watatuma Mkufunzi mwingine kwa ajili ya mitihani.

BONIFACE WAMBURA
OFISA HABARI NA MAWASILIANO
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

TBA WAANZA MIKAKATI YA KUENEZA MCHEZO WA NGUMI ZA RIDHAA MKOANI TANGA.

May 16, 2014
NA MWANDISHI WETU,TANGA.
CHAMA cha ngumi za Ridhaa Mkoa wa Tanga,(TBA)kimeanza mkakati kabambe wa kuhakikisha mchezo huo unaenea katika wilaya mbalimbali mkoani hapa kwa kuunda timu ya mkoa ambayo itashirikisha wilaya zote.

Akizungumza jana,Mwenyekiti wa Chama hicho Mkoani Tanga,Mansour Soud alisema timu hiyo itakuwa ikiuwakilisha mkoa huu kwenye mashindano mbalimbali ya mchezo huo ikiwa na matumaini ya kulitangaza vema jina la mkoa.

VIDEO MPYA YA WIMBO WA MB DOOGY "BABY UMENUNA NI BALAA

VIDEO MPYA YA WIMBO WA MB DOOGY "BABY UMENUNA NI BALAA

May 16, 2014
Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
MWIMBAJI wa muziki wa kizazi kipya, Mbwana Mohamed Mb Doggy, pichani chini, amekamilisha video ya wimbo wake mpya inayokwenda kwa jina la ‘Baby Mbona Umenuna’.
Video ya wimbo huo imetengenezwa chini ya Abby Kazi, ambaye ameikamilisha mapema wiki hii, huku akijiandaa kuisambaza katika vituo vya televisheni sanjari na kuingizwa kwenye mitandao ya kijamii.