MANGULA, NAPE WAONGOZA KONGAMANO LA MAADHIMISHO YA KUMBUKUMBU YA MWALIMU NYERERE YA VIJANA WA CCM VYUO VIKUU , LEO

October 19, 2014

Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Philip Mangula akihutubia Jumuia ya Wanafunzi wa Vyuo vya Elimu ya Juu katika Kongamano la Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere, lililoandaliwa na Vijana wa CCM wa Vyuo Vikuu, kwenye Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam, leo, Oktoba 19, 2014.
Katibu wa NEC, Irikadi na Uenezi, Nape Nnauye akimpongeza Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara), Mzee Mangula baada ya kuhutubia katika kongamano hilo. Kulia ni Katibu Mtendaji Mkuu wa CCM mkoa wa Vyuo Vikuu, Christopher Ngubiagai
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akihutubia katika Kongangamano hilo la Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere. Nape amewataka wasomi kutofumbia macho matatizo ndani ya CCM, badala yake wakati wakisifu  mema wawe mstari wa mbele kuyafichua na kuyakemea mapungufu ili chama kiende na wakati
Katibu Mtendaji Mkuu wa CCM mkoa wa Vyuo vya Elimu ya Juu, Christopher Ngubiagai akizungumza wakati wa kongamano hilo la Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere.
Mwenyekiti wa CCM tawi la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam,, Theodora Malata akizungumza mwanzoni mwa kongamano hilo
Washiriki wakisikiliza kwa makini mada mbalimbali zilizokuwa zikitolewa wakati wa kongamano
Katibu Mwenezi wa CCM mkoa wa Dar es Salaam, Juma Simba akizingumza kwenye kongamano hilo.
Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Philip Mangula na Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye wakiwa na viongozi wengine meza kuu baada ya kuwasili ukumbini.(Picha na Bashir Nkoromo)

YANGA NA SIMBA KATIKA PICHA

October 19, 2014

Kiungo wa timu ya Simba,Amri Kiemba akuchuana vikali na Mshambuliaji wa timu ya Yanga,Andrey Coutinho wakati wa mtanange wa watani wa Jadi Yanga na Simba uliochezwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam leo ikiwa ni sehemu ya muendelezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.Timu hizo zimetoka sare ya bila kufungana.PICHA ZOTE NA OTHMAN MICHUZI.
 
Mtanange ukiendelea...
Dogo akiwachambua wana Yanga...
Jaja hakuweza fua dafu...

*MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AHUDHURIA SHEREHE YA KUWEKWA WAKHFU ASKOFU MTEULE WA KANISA LA AFRICAN INLAND DAYOSISI YA MWANZA, MCHUNGAJI JOHN BUNANGO, JIJINI MWANZA

October 19, 2014

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana nabaadhi ya viongozi wa dini ya Kikristu, wakati alipowasili kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza leo, Oktoba 19, 2014, kwa ajili ya kuhudhuria sherehe za kuwekwa Wakhfu Askofu Mteule wa Kanisa la African Inland Dayosisi ya Mwanza, Mchungaji John Bunango, iliyofanyika jijini humo leo mchana.
 Maaskofu wakimwekea mikono ya Baraka Askofu mwenzao, Askofu Mteule wa Kanisa la African Inland Dayosisi ya Mwanza, Mchungaji John Bunango, wakati akiwekwa Wakhfu katika sherehe zilizofanyika kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza leo.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwahutubia waumini wa dini ya Kikristu, waliohudhuria katika Sherehe za kuwekwa Wakhfu Askofu Mteule wa Kanisa la African Inland Dayosisi ya Mwanza, Mchungaji John Bunango, zilizofanyika kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza, leo.
 Wanakwaya wakitoa burudani wakati wa sherehe hizo..
 Makamu wa Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimpongeza Askofu Mteule wa Kanisa la African Inland Dayosisi ya Mwanza, Mchungaji John Bunango, baada ya kuwekwa Wakhfu katika sherehe zilizofanyika kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza leo.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa dini ya Kikristu na wanafamilia ya Askofu  Mteule wa Kanisa la African Inland Dayosisi ya Mwanza, Mchungaji John Bunango, baada ya sherehe za kuwekwa wakhfu zilizofanyika kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza leo.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na  Askofu Mteule wa Kanisa la African Inland Dayosisi ya Mwanza, Mchungaji John Bunango, wakati akiondoka Askofu huyo kuwekwa Wakhfu katika sherehe zilizofanyika kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza leo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na  baadhi ya viongozi wa dini ya Kikristu wakati akiondoka kwenye uwanja wa CCM Kirumba, baada ya kuhudhuria sherehe za kuwekwa Wakhfu Askofu Mteule wa Kanisa la African Inland Dayosisi ya Mwanza, Mchungaji John Bunango, leo.

*MBUNGE WA KAWE HALIMA MDEE ALIPOUNGURUMA VIWANJA VYA FURAHISHA MWANZA JANA

October 19, 2014

 Mbunge wa Kawe na Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Chadema, Halima Mdee, akipeana mikono kusalimiana na wafuasi wa Chadema baada ya kumaliza kuwahutubia katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya Furahisha jijini Mwanza jana. 
 Mbunge huyo mara baada ya kumaliza kuwahutubia wafuasi wake, aliwatangazia kuanza kutoa chochote kitu ili kuchangia na kumwezesha Mbunge huyo kuweza kuendelea na ziara za mikiani ili kufanya mikutano kama huo, ambapo walijitokeza na kuchangia kila mmoja kwa alichonacho.
Salamu zikiendelea baada ya kuwahutubia.
Rais Kikwete ahitimisha Mafunzo ya Wakongo.

Rais Kikwete ahitimisha Mafunzo ya Wakongo.

October 19, 2014

DSC_1017
. Atunuku kamisheni kwa watanzani 23
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete leo ametunuku kamisheni kwa maafisa wapya wa Kitanzania 23 miongoni mwa maafisa 437 wa kundi la 53/13 – Kongo. Kundi hilo liliwajumuisha maafisa wa kitanzania wapatao 23 na wahitimu 414 kutoka Kongo.
Jumla ya wanajeshi 414 kutoka Jamuhuri ya Kidemokrasi ya Kongo leo wamehitimu mafunzo ya Uafisa katika chuo cha maafisa (TMA) Monduli baada ya kufanya kozi kwa muda wa mwaka mmoja.

Maafisa hao wanafunzi kutoka Kongo walipata mafunzo hayo pamoja na maafisa watanzania 23 waliohitimu leo na kupata kamisheni ya cheo cha luteni usu baada ya kula kuapa mbele ya Mhe. Rais Dkt Jakaya Kikwete.

Tofauti na kamisheni zingine kwani pamoja na Mhe. Rais Kikwete aliweza kutoa Kamisheni kwa maafisa wapya wapatao 23 .

Aidha, leo hii kitu ambacho ni kigeni vijana kutoka kongo walihitimu pasi kutunukiwa kamisheni kwani kulingana na taratibu maafisa wa kongo wanapaswa kupewa kamisheni na Rais na wakiwa katika ardhi yao, hivyo wahitimu hao watakapewa kamisheni nchini mwao.

Akitoa shukurani kwa Rais Kikwete wa Tanzania, Rais Joseph Kabila ambaye alishuhudia maafisa wake wakihitimu mafunzo hayo, alisema anawashukuru kwa kukubali kutoa mafunzo kwa maafisa hao.

Pia alisema anaamini atakuwa amepata makamanda wazuri watakaosaidia kuimarisha usalama nchini mwao na pia kuondoa maadui wanaohatarisha amani nchini Kongo.

Miongoni mwa viongozi waliohudhuria sherehe hizo Wazri wa Ulinzi na JKT, Mhe. Dkt Hussein Ali Mwimnyi, Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard Membe, Katibu mkuu wa Wizara ya Ulinzi na Waziri Mkuu Mstaafu na mbunge wa Monduli, Mhe. Edward Lowasa, Mkuu wa Mkoa wa Arusha Bw. Magesa Mlongo, majenerali, majenerali wastaafu, na mabalozi wa kijeshi wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini.

kwa upande wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Naibu Waziri Mkuu na waziri wa Ulinzi, Alexander Luba Ntambo, na Waziri wa Mambo ya Nje, Raymond Tshibanda N’tungamulongo, Balozi wa Kongo nchini Jean Pierre Juma Alfani, Mkurugenzi wa Idara ya Usalama Kahimbi Delphin na Mkuu wa Mafunzo, ya Kijeshi, brigedia Jenerali Aguru Mamba Maurice.