MAADHIMISHO YA SIKU YA KASA DUNIA YAFANYIKA LEO PANGANI WAANZIMISHA KIWILAYA,STORI KAMILI SOON

June 16, 2015









BERNARD MEMBE ATUA TANGA KUTAFUTA WADHAMINI KUANZA SAFARI YA IKULU

June 16, 2015


 Waziri wa Mambo ya nchi za nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernad Membe ambae pia ni Mbunge wa jimbo la Mtama, akisalimiana na wanachama wa CCM, Mkoa wa Tanga waliojitokeza makao makuu ya chama hicho kumdhamini katika fomu zake za kuomba ridhaa ya kugomea urais .


 Waziri wa Mambo ya nchi za nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe ambae pia ni Mbunge wa jimbo la Mtama, akiwahutubia wanachama wa CCM Mkoa wa Tanga waliojitokeza makao makuu ya chama hicho kumdhamini katika fomu zake za kuomba ridhaa ya kugombea urais.


MAHAFALI YA TATU YA SHULE YA AWALI YA CHEKECHEA YA OJAYS KIDDIES ZONE YAFANYIKA LEO JIJINI DAR

June 16, 2015
 Wahitimu wa shule ya Chekechea ya Ojays Kiddies Zone wakiwa kwenye picha ya pamoja
 Mkurugenzi wa Shule ya Chekechea ya Ojays Kiddies Zone, Bi Usia Nkoma Ledama akizungumza jambo wakati wa mahafali ya tatu ya shule hiyo
 Mwalimu Debby Ndulla(wa kwanza kushoto) akiwatambulisha walimu wa Shule ya Chekechea ya Ojays Kiddies Zone ambao ni Mwalimu Tatu(wa pili kutoka kushoto) akifuatiwa na Mwalimu Revina(katikati), Mwalimu Doroth(wa pili kutoka kulia) pamoja na Mwalimu Aika(kulia)
 Mwalimu Debby Ndulla(wa kwanza kushoto) akiwatambulisha wadada wanaowalea watoto wadogo wa shule ya Chekechea ya Ojays Kiddies Zone
 Mwalimu Debby Ndulla(kushoto) akimtambulisha Kaka Tobi mbele ya wazazi pamoja na walezi wa watoto waliofika kwenye mahafari ya Tatu ya shule ya Chekechea ya Ojays Kiddies Zone
 Kaka Tobi akiwapungia mikono wazazi pamoja na walezi wa watoto(hawapo pichani)
 
 Wanafunzi wa dalasa la Lantana katika shule ya Chekechea ya Ojays Kiddies Zone wakitoa burudani wakati wa mahafari ya tatu ya shule hiyo yaliyofanyika leo
 Wanafunzi wa dalasa la Lilies katika shule ya Chekechea ya Ojays Kiddies Zone wakitoa burudani wakati wa mahafari ya tatu ya shule hiyo yaliyofanyika leo
 Wanafunzi wa dalasa la Lavender katika shule ya Chekechea ya Ojays Kiddies Zone wakitoa burudani wakati wa mahafari ya tatu ya shule hiyo yaliyofanyika leo
 Bwana na Bibi Seyvunde wakizungumzia maendeleo ya mtoto wao ambaye alikuwa ni mmoja wa wahitimu leo.

Mkurugenzi wa Shule ya Chekechea ya Ojays Kiddies Zone, Bi Usia Nkoma Ledama(kulia) akiwa kwenye picha ya pamoja na Mtangazaji wa kipindi cha Power Breakfast Gerald Hando(katikati) pamoja na Mwalimu Debby Ndulla(kushoto) 
 
 Baadhi ya wazazi pamoja na walezi waliofika katika mahafari ya watoto wao wakifuatilia yanayoendelea.
Picha hizi chini ni wakati wa kukabidhiwa vyeti kwa wanafunzi hao waliohitimu leo
 















 Wazazi pamoja na walezi wakichukua matukio
UN KUSAFISHA KILIMANJARO

UN KUSAFISHA KILIMANJARO

June 16, 2015
FullSizeRender_1
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Leonidas Gama akimkaribisha Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini Bw. Alvaro Rodriguez alipomtembelea kwa ajili ya mazungumzo.
Mratibu wa mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini Tanzania Bw. Alvaro Rodriguez, alikutana na Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Bw. Leonidas Gama na kufanya naye mazungumzo.
Miongoni mwa mambo waliyojadili ni maandalizi ya shughuli na matukio kuadhimisha miaka 70 ya Umoja wa Mataifa (UN@70 ).
DSC_0046
Katika mazungumzo yao walikubaliana kufanya shughuli ya upandaji miti kuzunguka Mlima Kilimanjaro na kusafisha sehemu ya mji kabla ya Siku ya Umoja wa Mataifa.
Mkuu wa mkoa alikubaliana na wazo hilo na kusema shughuli hiyo inafaa kufanyika katikati ya mwezi wa Agosti.
FullSizeRender_3
Wawili hao wakipiga picha ya pamoja.
FullSizeRender_4
Wakiagana.

MAPOKEZI YA MH. LOWASSA MJINI BUKOBA

June 16, 2015

Sehemu ya Wakazi wa mji wa Bukoba Mkoani Kagera wakiwa nje ya Uwanja wa Ndege wa Bukoba, wakimsubiri kumlaki Mtangaza nia ya Urais kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Mh. Edward Lowassa, tayari kwa kupokea fomu ya wanaCCM wa kumdhamini.
 Wadau wa CCM wakijadiliana jambo.
 Ndege iliyombeba Mh. Edward Lowassa ikiwasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Bukoba, Mkoani Kagera.
 Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya Urais kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Mh. Edward Lowassa akisalimiana na Mwenyekiti Mstaafu wa CCM Mkoa wa Kagera, Mzee Pius Ngeze wakati alipowasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Bukoba, Mkoani Kagera leo Juni 15, 2015.
PICHA ZOTE NA OTHMAN MICHUZI.
 Mh. Lowassa katika tabasamu.
  Umati wa wanaCCM pamoja na wananchi wa Mji wa Bukoba mkoani Kagera ukiwa umemzunguka Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya Urais kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Mh. Edward Lowassa, wakati alipowasili kwenye ofisi za CCM Mkoa wa Kagera, leo Juni 15, 2015.
 Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya Urais kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Mh. Edward Lowassa akimsikiliza Katibu wa UWT wilaya ya Bukoba Vijijini, Agness Bashemu alipokuwa akitoa taarifa fupi ya namna ya kumkabidhi fomu hizo. Kulia ni Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Bukoba Mjini, Yussuf Ngaiza.
 Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Rukwa, Hypolitus Matete akiwasalimia wanaCCM pamoja na wananchi wa Mji wa Bukoba mkoani Kagera leo Juni 15, 2015.
 Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kigoba, Dkt. Aman Kaborou akiwasalimia wanaCCM pamoja na wananchi wa Mji wa Bukoba mkoani Kagera leo Juni 15, 2015. Kushoto ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga, Hamis Mngeja.
 Mjumbe wa Mkutano Mkuu (NEC) Bukoba, Nazir Karamagi akuzungumza machache mbele ya wanaCCM pamoja na wananchi wa Mji wa Bukoba mkoani Kagera leo Juni 15, 2015. 
 Mwenyekiti Mstaafu wa CCM Mkoa wa Kagera, Mzee Pius Ngeze akizungumza mbele ya umati wa wanaCCM pamoja na wananchi wa Mji wa Bukoba mkoani Kagera leo Juni 15, 2015, na kutangaza kwamba yeye pia ni mmoja ya wana Safari ya Matumaini.
 Shangwe kila kona.
 Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya Urais kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Mh. Edward Lowassa akipongezwa na Bibi huyu (ambaye jina lake halikuweza patikana kwa haraka) mara baada ya kupokea fomu za wanaCCM zaidi ya 6000 waliomdhamini ili apate ridhaa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kuwania Urais wa Tanzania, kwenye Uchachuzi Mkuu, Unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25, 2015.  
Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya Urais kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Mh. Edward Lowassa akipokea fomu kutoka kwa Katibu wa CCM Wilaya ya Bukoba mjini, Acheni Mwinshehe, zenye majina ya wanaCCM wa Mkoa wa Kagera waliomdhani ili apate ridhaa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kuwania Urais wa Tanzania, kwenye Uchachuzi Mkuu, Unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25, 2015. 
 Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya Urais kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Mh. Edward Lowassa akizungumza na umati wa wanaCCM pamoja na wananchi wa Mji wa Bukoba mkoani Kagera leo Juni 15, 2015, Wakati akitoa shukrani zake kwa kumdhamini ili apate ridhaa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kuwania Urais wa Tanzania, kwenye Uchachuzi Mkuu, Unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25, 2015. Zaidi ya wanaCCM 6000 wamdhamini mkoani Kagera.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya Urais kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Mh. Edward Lowassa akiwaaga wanaCCM pamoja na wananchi wa Mji wa Bukoba mkoani Kagera leo Juni 15, 2015, mara baada ya kupokea fomu za wanaCCM zaidi ya 6000 waliomdhamini ili apate ridhaa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kuwania Urais wa Tanzania, kwenye Uchachuzi Mkuu, Unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25, 2015.