RAIS DKT. MAGUFULI AWEKA JIWE LA MSINGI KIWANDA CHA VIGAE CHA GOOD WILL (MKURANGA), PIA AHUTUBIA WANANCHI WA IKWIRIRI, SOMANGA NA NANGULUKULU NA MCHINGA MKONI LINDI

March 02, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza Balozi wa China hapa nchini Dkt. Lu You qing mara baada ya kuweka jiwe la Msingi katika Kiwanda kikubwa cha kutengeneza Vigae(Tiles ) cha Good Will kilichopo katika kijiji cha Mkiwa, Mkuranga mkoani Pwani. Kiwanda hicho kitakuwa na uwezo wa kuzalisha vigae laki nane kwa siku na mwekezaji ametumia zaidi ya Dola mil.50 katika uwekezaji huo.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa pamoja na Balozi wa China hapa nchini Dkt. Lu You qing   akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa Kiwanda hicho cha vigae kilichopo Mkiwa Mkuranga mkoani Pwani.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisisitiza jambo wakati akihutubia kabla ya kuweka jiwe la Msingi katika Kiwanda kikubwa cha kutengeneza Vigae(Tiles ) cha Good Will kilichopo katika kijiji cha Mkiwa, Mkuranga mkoani Pwani.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia wananchi wa Ikwiriri mkoani Pwani wakati alipokuwa akielekea mkoani Lindi na Mtwara katika ziara yake ya kikazi ya siku nne.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisikiliza maelezo kutoka kwa Mwakilishi wa Kiwanda hicho cha y Vigae cha Good Will, Huang Heng Chao  kutoka kwa Kiwandani hapo.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa anapata maelezo kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo kuhusu matumizi ya Gesi katika Kiwanda cha Vigae cha Good Will kutoka kwa Kiwandani hapo.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia wananchi wa Somanga mkoani Lindi wakati akiwa ziarani lkuelekea mikoa ya Kusini(Lindi na Mtwara).
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimsikiliza Mbunge wa Kilwa Kusini Suleiman Bungara(Bwege ) kutoka CUF katika eneo la Somanga wakati alipokuwa akielekea Nangulukulu katika ziara yake ya mikoa ya Kusini.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimsikiliza Mbunge wa Kilwa Kusini Suleiman Bungara(Bwege ) kutoka CUF katika eneo la Nangulukulu, Kilwa mkoani Lindi wakati akiwa katika ziara ya mikoa ya kusini.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia wananchi wa  Nangulukulu  mkoani Lindi.
 Waziri wa Habari Utamaduni na Michezo Nape Nnauye akifurahia hotuba iliyokuwa ikitolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli katika eneo la Nangulukulu mkoani Lindi.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Waziri wa Habari Utamaduni na Michezo Nape Nnauye mara baada ya kuhutubia wananchi wa Nangulukulu mkoani Lindi.

MALAWI YAISHAURI GIHON TANZANIA KUFUATA SHERIA

March 02, 2017
 Mkurugenzi Mtendaji wa Gihon Ministry,  Rebecca Stanford (kushoto), akiwa na  Mwanasheria wa Gihon, Monica Mhoja wakati walipokwenda ofisi ya Balozi wa Malawi nchini.
 Mwakilishi wa Balozi wa Malawi nchini, Micharl Gama (kulia), akiwa na viongozi wa Huduma ya Kiroho ya Gihon ofisi ya ubalozi huo hapa nchini. Kutoka kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Gihon Ministry,  Rebecca Stanford, Mwanasheria wa Gihon, Monica Mhoja, Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano  Gihon, Leonce Zimbandu na Ofisa Habari, Michael Malanyingi.
 Mwakilishi wa Balozi wa Malawi nchini, Micharl Gama (kulia), akiwa na viongozi wa Huduma ya Kiroho ya Gihon ofisi ya ubalozi huo hapa nchini. Kutoka kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Gihon Ministry,  Rebecca Stanford, Mwanasheria wa Gihon, Monica Mhoja, Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano  Gihon, Leonce Zimbandu


Na Mwandishi,  Wetu

OFISI ya Ubalozi wa Malawi nchini imeushauri Uongozi wa huduma ya Gihon kuwasiliana na Bodi ya usajili ya Malawi kabla ya kujaza fomu ya maombi ya usajili wa huduma hiyo.

Lengo ni kuutaka uongozi huo kufahamu sheria za usajili za nchini Malawi ili kuepuka usumbufu ambao unaweza kujitokeza iwapo fomu zitajazwa bila kuzingatia sheria na taratibu za nchi husika.

Katibu wa Balozi  wa Malawi nchini, Micharl Gama aliyasema hayo alipokuwa akizungumza na Uongozi wa Gihon jana  katika ofisi ya ubalozi huo ili kupata ufafanuzi wa namna ya kufungua huduma hiyo nchini Malawi.

Alisema ubalozi utahakikisha mawasiliano yanapatikana ili mwanasheria kutoka bodi ya usajili ya Malawi kutoa maelekezo yanayotakiwa kufuatwa kabla ya kufanya usajili wa taasisi (NGO).

“Unajua  mimi siyo mtaalamu wa masuala ya sheria, hivyo mawasiliano nitakayowapatia yatafafanua vizuri kifungu cha sheria  namba 5.05 cha Malawi,” alisema.

Alisema wajibu wa ofisi hiyo ya ubalozi ni kuwaunganisha na wenye mamlaka ili waweze kutekeleza wajibu wao wa kisheria, hivyo  hana uwezo wa tafsiri sharia ya usajili wa NGO.

Mwanasheria wa  Huduma ya Gihon, Monica Mhoja alisema kuwa huduma hiyo imeona kabla ya kujaza fomu za usajili wa huduma  hiyo ya kiroho nchini Malawi, waliamua  kuomba ushauri kutoka katika ofisi za ubalozi huo.

Alisema taratibu zipo tofauti kati ya nchi moja na nyingine, hivyo itakuwa busara kufahamu sheria za usajili kutoka nchini Malawi ili kuepuka uvunjaji wa taratibu za kisheria.

“Tunaomba kufahamu taratibu za usajili wa NGO zilizopo nchini Malawi, kwani tunahitaji kufungua huduma ili kufahamu mgawanyo wa madaraka ulivyo kabla ya huduma kuanza kisheria,” alisema.

Mkurugenzi Mtendaji wa huduma ya Gihon nchini, Rebecca Stanford alisema wamefikia uamuzi wa kushughulikia usajili nchini Malawi baada  ya watu hao kubarikiwa  huduma hiyo kiroho na kimwili.

“Tayari tumefungua tawi la huduma ya Gihon nchini  Malawi  kwa muda wa miaka miwili, hivyo kutokana na uhitaji uliopo tumeona tuisajili huduma hiyo ili itambulike rasmi,” alisema.


TAASISI YA MISA TANZANIA YAWANOA WANAHABARI KANDA YA ZIWA

March 02, 2017
Afisa Habari na Utafiti kutoka Taasisi ya Vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika (MISA) tawi la Tanzania, Gasirigwa Sengiyumva, akifananua jambo kwenye mafunzo kwa waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari Kanda ya Ziwa.

Mafunzo hayo yanayofanyika kwa siku mbili Jijini Mwanza kuanzia hii leo, yamelenga kuwajengea uelewa wanahabari juu ya Sheria Mpya ya Huduma za Habari ya mwaka 2016 na Kanuni zake za mwaka 2017 na yamewahusisha wanahabari kutoka mikoa ya Mwanza, Geita, Mara na Simiyu.

Sengiyumva amebainisha kwamba mafunzo hayo yamelenga kuwajengea uwezo wanahabari katika kutimiza vyema majukumu yao bila kukinzana na sheria za habari na hata haki kuhusu uhuru wa kujieleza pamoja na vyombo vya habari.

Washiriki wa mafunzo hayo yanayofadhiliwa na Taasisi ya Friedrick Ebert Stiftung (FES) Tanzania, wamebainisha kwamba elimu waliyoipata itawasaidia katika utendaji wa majukumu yao kwani wengi wao walikuwa wakitatizwa na sheria mpya ya huduma za habari ya mwaka 2016 na kanuni zake za mwaka 2017. 
#BMGHabari
Mmoja wa wakufunzi wa mafunzo hayo, Jesse Kwayu, akiwasilisha mada kuhusu nafasi ya vyombo vya habari kwenye michakato mbalimbali ya sheria nchini ikiwemo sheria ya huduma za habari ya mwaka 2016
Mwakilishi wa Metro Fm Mwanza, Alphonce Kapela, akichangia mada wakati wa mafunzo hayo
Mwakilishi wa gazeti Majira mkoani Mwanza, Judith Ndibalema, akichangia mada kwenye mafunzo hayo
Washiriki wamefurahishwa na mafunzo hayo yanayofadhiliwa na Taasisi ya Friedrick Ebert Stiftung (FES) Tanzania na kubainisha kwamba yatawasaidia katika utendaji wa majukumu yao kwani wengi wao walikuwa wakitatizwa na sheria mpya ya huduma za habari ya mwaka 2016 na kanuni zake za mwaka 2017.

WAZIRI MKUU KASSIM MAJARIWA KUFUNGUA MKUTANO WA TISA WA WADAU WA LAPF JIJINI ARUSHA

March 02, 2017
 Meneja Masoko la Mawasiliano wa LAPF, James Mlowe (katikati), akizungumza katika mkutano na wanahabari Dar es Salaam leo, kuhusu mkutano wa tisa wa LAPF utakaofanyika Machi 9 na 10, 2017 Ukumbi wa Mikutano ya Kimataifa wa AICC jijini Arusha. Kulia ni Meneja wa Takwimu Hadhari na Tathmini wa LAPF, Abubakar Ndwata na Ofisa Masoko na Mawasiliano wa LAPF, Rehema Mkamba.

MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA AKUTANA NA WAZIRI UMMY MWALIMU NA KUFANYA NAE MAZUNGUMZO

March 02, 2017
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu pamoja na Katibu Mkuu Wizara ya Afya Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi. Sihaba
Nkinga ofisini kwake, Ikulu jijini  Dares Salaam.
(Picha kwa Hisani ya Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,  Jinsia,  Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu (kushoto)  na Katibu Mkuu Wizara ya Afya Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi. Sihaba Nkinga (kulia) ofisini kwake, Jijini  Dar es Salaam.
(Picha kwa Hisani ya Ofisi ya Makamu wa Rais)
SSRA YAZINDUA MFUMO MPYA WA KURAHISISHA MAWASILIANO

SSRA YAZINDUA MFUMO MPYA WA KURAHISISHA MAWASILIANO

March 02, 2017
kib1
Mkuu wa Kitengo cha Mahusiano na Uhamasishaji cha Mamlaka ya Udhibiti na Usimamizi wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (Kulia), Sarah Msika akiwaelekeza waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu mfumo wa kupokea malalamiko kwa njia ya TEHAMA wakati wa mkutano na waandishi hao uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.Kutoka kushoto ni Afisa TEHAMA wa Mamlaka hiyo, Ernest Masaka pamoja na Afisa Mwandamizi wa TEHAMA wa Mamlaka hiyo, David Ngh’ambi.
kib2 kib3
Afisa Mwandamizi wa TEHAMA wa Mamlaka ya Udhibiti na Usimamizi wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), David Ngh’ambi akielezea jinsi ya kutuma malalamiko kwa njia ya simu wakati wa mkutano na waandishi wa habari uliofanyika leo jijini Dar es Salaam,kushoto ni Afisa TEHAMA wa Mamlaka hiyo, Ernest Masaka na kulia ni   Mkuu wa Kitengo cha Mahusiano na Uhamasishaji cha Mamlaka ya Udhibiti na Usimamizi wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (Kulia), Sarah Msika.
……………………………………………………………………….
Na. Georgina Misama – MAELEZO
 
Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA) imeanzisha mfumo wa TEHAMA utakaowawezesha wanachama kutuma na kufuatilia malalamiko yao moja kwa moja kwa mamlaka hiyo.
 
Akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mkuu wa Kitengo Cha Mahusiano na Uhamasishaji kutoka mamlaka hiyo Sarah Kibonde alisema Mfumo huo utaiwezesha SSRA kupokea na kushughulikia malalamiko ya wanachama moja kwa moja.
 
“Mfumo huu unapatikana katika simu za mkononi (mobile app), unapatikana kwa watumiaji wa simu za mkononi zinazotumia mfumo wa android na unatambuliwa kwa jina la SSRA” alisema Sarah.
 
Akitoa maelezo ya namna ya kutumia mfumo huo, Afisa TEHAMA wa SSRA Bw.Ernest Masaka alisema mara baada ya mwanachama kuingiza taarifa zake ambazo ni majina matatu, anwani ya posta, namba ya simu, pamoja na namba ya uanachama na makazi, mfumo utampa namba ya kumbukumbu ya lalamiko husika.
 
Aidha, taarifa hizi husaidia kumtambua muhusika na Mamlaka kufanya mawasiliano na mwanachama mwenye malalamiko pamoja na kushughulikia malalamiko husika moja kwa moja.
 
“Mfumo huu umeweka utaratibu wa mlalamikaji kufuatilia  hatua za utatuzi wa malalamiko yake kwa kumbukumbu za mlalamikaji” alisema Bw.Masaka.
 
Akizungumzia faida zinazopatikana kwa wanachama kutumia mfumo huo Bw.Masaka alisema ni pamoja uwekaji mzuri wa kumbukumbu kwa Mamlaka,kutoa mrejesho wa idadi na hatua za utekelezaji pamoja na mwanachama kupata mrejesho kwa haraka bila kujali mahali alipo ambayo itasaidia kupunguza ghara za fedha na muda.
 
Mamlaka inatoa wito kwa wanachama na wananchi wote kwa ujumla kutumia mfumo huu kwasababu unarahisisha mawasiliano kati ya mlalamikaji na Mamlaka.

ZIARA YA NAIBU WAZIRI WA MAZINGIRA MPINA RUFIJI

March 02, 2017
 Naibu Waziri Mpina akiwaasa wasimamizi wa mradi wa upandaji na utunzaji mikoko katika delta ya kaskazini Rufiji hawapo pichani wamueleze ukweli kuhusu matumizi ya fedha na hali halisiya mradi kabla ya kwenda kukagua upandaji, utunzaji wa mikoko na uharibifu wa mazingira.
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina na ujumbe wake wakiwa katika Boat, wakielekea katika ukaguzi wa upandaji na utunzaji wa Mikoko, pamoja na uharibifu wa Mazingira katika Delta ya Rufiji Kaskazini.
 Naibu Waziri Mpina  (kaikati) na Ujumbe wake katika picha wakitembea kukagua mikoko iliyopandwa katika Delta ya Kaskazini Rufiji.
Naibu Waziri Mpina akiwaasa wasimamizi wa mradi wa upandaji na utunzaji mikoko katika delta ya kaskazini Rufiji hawapo pichani wamueleze ukweli kuhusu matumizi ya fedha na hali halisiya mradi kabla ya kwenda kukagua upandaji, utunzaji wa mikoko na uharibifu wa mazingira.

“KAIMU RC TANGA AGIZA WILAYA ZA MKOA HUO KUUNDA MAJUKWAA YA WANAWAKE”

March 02, 2017
Mmmoja wa Wajasiriamali kushoto akimuonyesha Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Tangaa,Mhandisi Mwanasha Tumbo ambaye pia ni Mkuu wa wilaya ya Muheza akiangalia moja kati ya bidhaa wanazozalisha wakati wa kongamano la wanawake wajasiriamali mkoani Tanga lililofanyika kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga hivi karibuni.

 Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Mhandisi Mwanasha Tumbo kushoto aliyevaa hijabu ambaye pia ni Mkuu wa wilaya ya Muheza akipata maelekezo kutoka kwa mmoja wa wanawake wajasiriamali wakati alipofungua jukwaa la wanawake mkoani Tanga hivi karibuni.


Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Mhandisi Mwanasha Tumbo ambaye pia ni Mkuu wa wilaya ya Muheza kulia akipata maelekezo kutoka kwa mmoja wa wanawake wajasiriamali wakati alipofungua jukwaa la wanawake mkoani Tanga hivi karibuni.
Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Mhandisi Mwanasha Tumbo ambaye pia ni Mkuu wa wilaya ya Muheza kulia akipata maelekezo kutoka kwa mmoja wa wanawake wajasiriamali wakati alipofungua jukwaa la wanawake mkoani Tanga hivi karibuni.



MH. MWAKYEMBE ASHUHUDIA MV. RUVUMA IKIINGIZWA ZIWA NYASA KWA MAJARIBIO

MH. MWAKYEMBE ASHUHUDIA MV. RUVUMA IKIINGIZWA ZIWA NYASA KWA MAJARIBIO

March 02, 2017
unnamed
Mhe. Dkt Harrison Mwakyembe, Waziri wa Mambo ya Katiba na Sheria na Mbunge wa Kyela , ameshudia zoezi la kuingizwa majini kwa Meli mpya ya pili ya mizigo iitwayo MV Ruvuma kwenye bandari ya Itungi, Wilayani Kyela. 
Tukio hilo la kuiingiza Meli hiyo making limefanyika Machi Mosi . Meli hiyo yenye uwezo wa kubeba mzigo zaidi ya tani 1000 inaungana na Meli nyingine mpya MV Njombe yenye uwezo wa kubeba zaidi ya tani 1000 ambayo iliingizwa majini siku tano zilizopita. Meli zote mbili zipo kwenye hatua ya mwisho ya utengenezaji na majaribio kabla hazijaanza rasmi kubeba mizigo kwenye ziwa Nyasa. 
Tayari wateja mbalimbali wamejitokeza kutaka mizigo yao ianze kubebwa yakiwemo makampuni yanayojishughulisha na biashara ya makaa ya mawe.