Benki ya CRDB yamtangaza mshindi wa tano wa Toyota Crown katika kampeni ya Benki ni Simbanking

December 13, 2023

Dar es Salaam. Tarehe 13 Disemba 2023:  Benki ya CRDB imemkabidhi Rehema Cletus Lupapa, mkazi wa Gongo la Mboto jijini Dar es Salaam gari jipya aina ya Toyota Crown baada ya kuibuka mshindi katika awamu ya tano ya kampeni ya Benki ni Simbanking.

Akieleza namna anavyoitumia huduma za SimBanking, Rehema amesema amekuwa mteja wa Benki ya CRDB kwa miaka mingi na huduma hiyo imekuwa ikimrahisishia kufanya miamala mbalimbali kwa urahisi na kwa wakati.

Akizungumza katika hafla ya kukabidhi zawadi kwa mshindi huyo iliyofanyika katika Tawi la Benki ya CRDB Kijitonyama, Dar es salaam, Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa Benki ya CRDB, Godfrey Rutasingwa, amesema mshindi huyo alipatikana katika droo ya tano ya kampeni hiyo iliyofanyika Disemba 4, 2023 kwenye Makao Makuu ya Wasafi, jijini Dar es salaam.
Rutasingwa, alibainisha kuwa katika kusaidia jitihada za Serikali za kuchochea uchumi wa kidijitali nchini, kampeni ya “Benki Ni SimBanking” imekuwa ikihamasisha wateja kufanya miamala kidijitali kupitia SimBanking na kuachana na matumizi ya pesa taslimu.

Akielezea kampeni hiyo, Rutasingwa alisema “Benki Ni SimBanking” ni kampeni iliyoendeshwa kwa muda wa miezi 10, ambapo kila siku wateja wamekuwa wakijishindia zawadi, huku pia kukiwa na zawadi za mwezi, miezi miwili, na zawadi kubwa ya Toyota Vanguard ambayo itatolewa mwishoni wa kampeni.

“Hadi kufikia sasa tayari tumeshatoa zawadi mbalimbali ikiwamo pesa taslimu, simu janja, na laptop kwa washindi. Hivyo niwasihi wateja na wale wasio wateja waendelee kufanya miamala kupitia SimBanking ili kujijengea mazoea ya kutumia huduma kidigitali,” alisema Rutasingwa huku akiwakaribisha wale ambao sio wateja wa Benki ya CRDB kufungua akaunti ili waunganishwe na SimBanking.
Akizungumza baada ya kukabidhiwa gari mshindi wa shindano hilo, Rehema Lupapa aliishukuru Benki ya CRDB kwa zawadi hiyo ya gari huku akibainisha siri ya ushindi ni kujenga utamaduni wa kutumia SimBanking kufanya miamala yake yote ya kifedha.

“Ninafurahia sana kufanya miamala kupitia SimBanking iliyoboreshwa, imekuwa rahisi na nafuu sana kutumia. Sasa hivi miamala yangu yote nakamilisha kupitia SimBanking, iwe kufanya malipo kupitia CRDB Lipa Namba, kutuma pesa, kulipia bima, kulipia kodi na kutoa fedha kwa CRDB Wakala/ ATMs na Tawini bila ya kadi,” alibainisha Rehema.
Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa Benki ya CRDB, Godfrey Rutasingwa (wapili kushoto) akikabidhi funguo ya gari jipya aina ya Toyota Crown kwa Rehema Cletus Lupapa (katikati) ambaye ni mshindi katika awamu ya tano ya kampeni ya Benki ni Simbanking, katika hafla fupi iliyofanyika kwenye Tawi la Benki ya CRDB Kijitonyama, Dar es salaam, Disemba 13, 2023. Wengine pichani ni Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi Benki ya CRDB, Stephen Adili (kushoto), Meneja wa Benki ya CRDB Kanda ya Mashariki, Badru Idd (wapili kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi Huduma za Kidigitali, Mangile Kibanda. 
 Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa Benki ya CRDB, Godfrey Rutasingwa akizungumza wakati wa hafla fupi ya kukabidhi gari jipya aina ya Toyota Crown kwa mshindi wa awamu ya tano ya kampeni ya Benki ni Simbanking, iliyofanyika kwenye Tawi la Benki ya CRDB Kijitonyama, Dar es salaam, Disemba 13, 2023. 
 Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi Benki ya CRDB, Stephen Adili akizungumza wakati wa hafla fupi ya kukabidhi gari jipya aina ya Toyota Crown kwa mshindi wa awamu ya tano ya kampeni ya Benki ni Simbanking, iliyofanyika kwenye Tawi la Benki ya CRDB Kijitonyama, Dar es salaam, Disemba 13, 2023. 
Meneja wa Benki ya CRDB Kanda ya Mashariki, Badru Idd akizungumza wakati wa hafla fupi ya kukabidhi gari jipya aina ya Toyota Crown kwa mshindi wa awamu ya tano ya kampeni ya Benki ni Simbanking, iliyofanyika kwenye Tawi la Benki ya CRDB Kijitonyama, Dar es salaam, Disemba 13, 2023.






MAKAMU WA KWANZA WA RAIS ZANZIBAR AWAFAGILIA BAKIZA NA BAKITA KWA KUENEZA KISWAHILI DUNIANI

December 13, 2023



MAKAMU wa Rais Zanzibar, Othman Masoud Othman akikagua vitabu pamoja na kazi za sanaa za ufundi nje ya ukumbi wa Sheikh Idrisa Abdulwakil

MAKAMU wa Kwanza wa Rais Zanzibar, Othman Masoud Othman akihutubia katika Kongamano la Kimataifa la Saba la BAKIZA katika ukumbi wa Sheikh Idrisa Abdulwakil- Kikwajuni , Unguja


KATIBU Mtendaji wa BAKIZA, Dk. Mwanahija Ali Juma




WAZIRI wa Habari, Vijana Utamaduni na Michezo Zanzibar, Mh. Tabia Maulid Mwita


****


NA. ELISANTE KINDULU, UNGUJA


MAKAMU wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mh. Othman Masoud Othman ameyapongeza mabaraza ya kiswahili kwa kueneza vema kiswahili ndani na nje ya nchi.


Mh. Othman alitoa pongezi hizo alipokuwa akifunga kongamano la Saba la kimataifa la baraza la kiswahili Zanzibar (BAKIZA) lililofanyika katika ukumbi wa Sheikh Idrisa Abdulwakil, akimwakilisha Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi, mwanzoni mwa wiki hii Kikwajuni- Unguja.


"Napenda nitumie fursa hii kuzipongeza BAKIZA na BAKITA kwa kueneza kiswahili kitaifa na kimataifa ikiwa pamoja na kufundisha lugha hiyo kwa wageni ndani na nje ya nchi".


Amesema kiswahili kimekuwa na watumiaji wengi duniani ambapo takribani watu milioni 200 wanaitumia lugha hiyo, hivyo amewaasa wataalamu wa lugha hiyo kuendelea kuitumia katika nyanja mbalimbali ikiwemo kuandika vitabu na kuvisambaza.


Aidha Makamu huyo wa Kwanza wa Rais amewataka watumiaji wa lugha hiyo ikiwa pamoja na wanazuoni kuendelea kujifunza zaidi utaalamu katika lugha hiyo ili kuepuka mapungufu katika kuandika na kuzungumza.


" Hata kisu kikali lazima kinolewe. Mimi niliwahi kuwa mwalimu wa kiswahili kabla ya kuingia katika tasinia ya sheria. Lakini hadi leo bado mwanafunzi wa Kiswahili. Hivyo sote kwa pamoja licha ya kukieneza kiswahili lakini bado tunahitajika kujifunza zaidi.


Akimkaribisha mgeni rasmi kuzungumza, Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bi. Tabia Maulid Mwita alitoa wito kuwa vijana wanaotumika katika sanaa za maonyesho kwenye dhifa mbalimbali waendelezwe ili
kusasisha vipaji vyao.


Mapema akitoa taarifa za baraza hilo, Katibu Mtendaji wa BAKIZA Dk. Mwanahija Ali Juma alisema kongamano hilo limehudhuriwa na washiriki kutoka nchi za Sweden, India, Korea kusini, Uganda, Kenya, Komoro, Tanzania bara na Tanzania Visiwani.


Jumla ya maazimo 11 yaliwasishwa na washiriki wa kongamano ikiwemo wanaotafsiri tamthilia mbalimbali watafsiri kwa uhalisia wake ili kuepuka upotoshaji katika matumizi ya lugha.

WAZIRI MWIGULU AZINDUA OFISI ZA TADB KANDA YA KASKAZINI

December 13, 2023

 -Kuhudumia mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Tanga na Manyara



Na Mwandishi Wetu

Waziri wa Fedha, Mhe Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba leo amezindua Ofisi ya Kanda ya Kaskazini ya Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) ikiwa ni sehemu ya mkakati wa benki hiyo kupanua wigo wa upatikanaji wa huduma za kifedha na mikopo yenye masharti nafuu kwa wakulima na wafugaji wa mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Tanga na Manyara.

Akizungumza katika uzinduzi huo, Waziri Nchemba aliishukuru TADB kwa kazi nzuri inayoendelea kufanya katika kuinua sekta ya kilimo, mifugo na uvuvi nchini, pamoja na sekta ya fedha kwa ujumla.


“Serikali kwa kutambua umuhimu wa sekta hii, imeendelea kutoa kipaumbele kwenye sekta ya kilimo ili kuinua Pato la Taifa na la mtu mmoja mmoja, kuimarisha usalama wa chakula, kuongeza ajira, kuchukua hatua za kuhakikisha pembejeo za kilimo zinapatikana kwa wakati na kwa gharama nafuu, pamoja na kubainisha fursa za masoko za mazao hayo zilizoko ndani na nje ya nchi yetu,” alisema.

Aliongeza kuwa ofisi hiyo ya Kanda ya Kaskazini ya TADB itakwenda kuimarisha huduma za kifedha kwenye Mikoa ya Kaskazini na kurahisisha upatikanaji wa mikopo kwa wakulima, wavuvi na wafugaji, kufungua fursa na kuendeleza zaidi ukuaji wa biashara katika mnyororo wa thamani katika mikoa yote minne ya Arusha, Kilimanjaro, Manyara na Tanga. Mikoa hiyo inasifika kwa kuzalisha mazao muhimu kwa uchumi wa nchi, kama vile kahawa, mahindi, ngano, na sekta zingine kama utengenezaji wa mbolea, ufugaji wa ng’ombe wa nyama na maziwa, ufugaji wa samaki na kuku wa nyama na mayai, kilimo cha maua, mboga mboga na matunda .

“Naihakikishia Bodi na Menejimenti ya TADB kuhusu utekelezaji wa agizo nililotoa wakati wa Bunge la Bajeti, ambapo nilitangaza kwamba Serikali itaiongezea Benki ya TADB na TIB jumla ya mtaji wa Shilingi Bilioni 235.9 kwa lengo la kupanua wigo wa mikopo kwa sekta binafsi kwa ajili ya miradi ya kukuza sekta za uzalishaji na kuongeza thamani.


Pia serikali itatekeleza programu ya kuwezesha mtaji usiopungua Shilingi Trilioni 1 kwa miaka mitano hadi kumi kwa benki kama TADB ili ziweze kufanya shughuli ya utoaji wa mikopo kwa ufanisi zaidi, na wakulima wazidi kupata mitaji ya kujiendeleza,” Waziri alisema.

Aliwasisitizia Wananchi wa mikoa hiyo kuchangamkia fursa ya uwepo wa Ofisi hiyo ya Kanda kupata uelewa zaidi wa utaratibu wa kupata mikopo, kufanya matumizi sahihi ya mikopo na kulipa kwa wakati, na pia kuishauri Menejimenti ya Benki na watumishi wake kuweka masharti nafuu ya mikopo, kuwatembelea wanufaika katika miradi yao na kutoa elimu ili kusimamia kikamilifu mikopo husika kwa wakulima, wavuvi na wafugaji.

Akizungumza katika uzinduzi huo, Mkurugenzi Mtendaji wa TADB Bw Frank Nyabundege alielezea kuwa ufunguzi wa ofisi hiyo ni mwendelezo wa mafanikio ya benki ya TADB kutimiza malengo yake kutoa mikopo ya masharti nafuu, kwa viwango vya riba za chini na kutoa muda mrefu zaidi wa marejesho kwa wakulima wadogo, wa-kati na wakubwa katika mnyororo mzima wa thamani wa sekta ya kilimo, ili kuwezesha upatikanaji wa mitaji ya kuleta mapinduzi katika sekta ya kilimo, ufugaji na uvuvi.

“Hadi kufikia Novemba mwaka huu mizania yetu ya mikopo imeendelea kukukua na kufikia kiasi cha Shilingi Bilioni 600.7 mwezi Novemba, 2023. Ofisi hii ya Kanda ya Kaskazini inaenda kupunguza adha kwa kufikisha huduma za benki karibu zaidi na wateja wake waliokuwa wanahudumiwa na ofisi ya Dodoma, ambapo hadi kufikia Novemba 2023, TADB imekwisha wezesha wakulima na wafugaji wa kanda ya Kaskazini kwa kutoa mikopo yenye thamani ya Shilingi bilioni 18.3 kwa Mkoa wa Tanga, Shilingi bilioni 7.9 Mkoa wa Arusha, Shilingi bilioni 3.2 Mkoa wa Kilimanjaro na Shilingi bilioni 3.1 kwa mkoa wa Manyara.

Mikopo hii imewezesha upatikanaji wa pembejeo na viwatilifu, mbegu bora za mifugo, ukuzaji viumbe hai kwenye maji na uvuvi.”

Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuchochea maendeleo ya nchi kupitia kilimo na kuiongezea TADB mtaji wake kufika Shilingi Bilioni 268, pamoja na juhudi nyingine za kuongeza mitaji na mikopo ya masharti nafuu kwa wakulima, wafugaji na wavuvi nchini.Tunathamini juhudi mbalimbali za serikali kuhakikisha benki yetu inafanya kazi kwa mafanikio ya malengo yaliyokusudiwa,” alisema.

TADB sasa ina ofisi saba mbazo ni Kanda ya Ziwa yenye ofisi Mwanza - na kuhudumia mikoa ya Kagera, Mara, Shinyanga, Geita na Simiyu; Kanda ya Nyanda za Juu Kusini yenye ofisi Mbeya - na kuhudumia mikoa ya Songwe, Iringa, Njombe na Rukwa.

Kanda ya Mashariki yenye ofisi Dar es salaam na kuhudumia mikoa ya Pwani na Morogoro; Kanda ya Magharibi yenye ofisi Tabora na kuhudumia mikoa ya Katavi na Kigoma; Kanda ya Kati yenye ofisi Dodoma na kuhudumia mkoa wa Singida; Kanda ya Kusini yenye ofisi Mtwara na kuhudumia mikoa ya Lindi na Ruvuma; na sasa Kanda ya Kaskazini yenye ofisi Arusha na kuhudumia Mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Tanga na Manyara.

“Aidha, tumeshapata ofisi ndogo Zanzibar tukiwa tunasubiri vibali kutoka Benki Kuu ya Tanzania kwa ajili ya kufungua ofisi kubwa na ya kisasa Zanzibar,” Bw Nyabundege alielezea.

Serikali iliamua kuanzisha Benki ya TADB mwaka 2015 kwa malengo makubwa mawili; Ambayo ni: kuchangia utoshelevu na usalama wa chakula nchini; pamoja na kuchagiza mapinduzi ya kilimo toka kilimo cha kujikimu kwenda kilimo cha kibiashara.



Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Nchemba akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa ofisi za kanda ya Kaskazini za Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) jijini Arusha Arusha. Ofisi hiyo ya kanda itahudumia mikoa ya Arusha, Manyara, Kilimanjaro na Tanga.





Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Nchemba (wa kwanza kulia) akizundua rasmi ofisi ya kanda ya Kaskazini ya Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) itakayohudumia mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Manyara na Tanga. Wanaoshuhudia wa kwanza kushoto ni mmbunge wa Arusha mjini Mrisho Gambo akifuatiwa na mwenyekiti wa bodi ya TADB Ishmael Kasekwa.


Mwenyekiti wa bodi ya Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) Ishmael Kasekwa (kati kati) Akimtambulisha mkurugenzi mtendaji wa Benki hiyo Frank Nyabundege (kulia) kwa Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Nchemba (kushoto) muda mfupi kabla ya uzinduzi wa ofisi za kanda ya Kaskazini za benki hiyo uliofanyika jijini Arusha














Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Nchemba (kati kati) akisalimiana na wafanyakazi wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) muda mfupi kabla ya kuzindua rasmi tawi la benki hiyo kanda ya Kaskazini jijini Arusha. Ofishi hiyo ya kanda itahudumia mikoa ya Arusha, Manyara, Kilimanjaro na Tanga.


Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Nchemba akisalimiana na kufurahia jambo na Meneja Masoko na mwasiliano wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) Amani Nkurlu (kulia) muda mfupi kabla ya kuzindua rasmi tawi la benki hiyo kanda ya Kaskazini jijini Arusha. Ofisi hiyo ya kanda itahudumia mikoa ya Arusha, Manyara, Kilimanjaro na Tanga.
RAIS WA ZANZIBAR MHE.DK.HUSSEIN MWINYI AWASILI NCHINI AKITOKEA NCHINI QATAR ALISHIRIKI JUKWAA LA DOHA (DOHA FORUM)

RAIS WA ZANZIBAR MHE.DK.HUSSEIN MWINYI AWASILI NCHINI AKITOKEA NCHINI QATAR ALISHIRIKI JUKWAA LA DOHA (DOHA FORUM)

December 13, 2023









RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe Hemed Suleiman Abdulla,Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja Mhe. Idrisa Kitwana Mustafa na Mstahiki Meya wa Jiji la Zanzibar Mhe Mahmoud Muhammed Mussa, alipowasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar akitokea Nchini Qatar,baada ya kumalizika kwa Jukwaa la Doha (Doha Forum) lililofanyika Jijini Doha, alimuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan.



RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwa na Mkewe Mama Mariam Mwinyi wakisalimiana na Wazee wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar alipowasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar akitokea Nchini Qatar,baada ya kumalizika kwa Jukwaa la Doha (Doha Forum) lililofanyika Jijini Doha, alimuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan.(Picha na Ikulu)

PROFESA NDALICHAKO AIPONGEZA GGML

December 13, 2023

  

Makamu Rais wa AngloGold Ashanti -GGML anayeshughulikia miradi endelevu na masuala ya ubia/ ushirika (Afrika), Simon Shayo akizungumza katika hafla ya kukabidhi tuzo kwa muajiri bora wa mwaka 2023 - zilizoandaliwa na Chama cha Waajiri Tanzania (ATE) hivi karibuni jijini Dar es salaam. Shayo alisema GGML ambayo ilikuwa mmoja wa wafadhili wa hafla hiyo, zaidi ya asilimia 80 ya menejimenti ya kampuni hiyo inaongozwa na Watanzania hivyo kuwa mgodi kinara unaoajiri Watanzania wengi tofauti na kampuni nyingine za sekta ya madini.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Profesa Joyce Ndalichako akimpatia cheti cha shukrani Meneja Mwandamizi wa Rasilimali Watu kutoka GGML, Charles Masubi baada ya kampuni hiyo kuwa mmoja wa wadhamini wakuu wa hafla ya kukabidhi tuzo kwa muajiri bora wa mwaka 2023 - tuzo ziliandaliwa na Chama cha Waajiri Tanzania (ATE). Kulia ni Meneja Uhusiano na Mawasiliano, Stephen Mhando akifuatiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa ATE, Suzanne Ndomba-Doran na wa kwanza kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya ATE, Bwana Oscar Mgaya.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Profesa Joyce Ndalichako akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi na menejimenti ya GGML katika hafla hiyo ya ugawaji wa tuzo za muajiri bora kwa mwaka 2023.
Baadhi ya wafanyakazi wa GGML wakifurahia cheti cha shukrani walichokabidhiwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Profesa Joyce Ndalichako katika hafla hiyo ya kukabidhi tuzo kwa mwajiri bora kwa mwaka 2023.

CCM YATOA SALAMU KWA VIONGOZI VIJANA WANAWAKE KUTOKA NCHI 16 ZA AFRIKA

December 13, 2023

 

Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndugu Anamringi Macha akizungumza wakati wa kutoa salaam za CCM, Jumanne, Disemba 12, 2023, kwa viongozi vijana wanawake kutoka nchi 16 za Afrika wanaohudhuria Mkutano wa Mwaka wa Asasi ya Kiraia ya Young Women of Africa (YWOA), wanaotoka katika vyama tawala katika nchi hizo. 
 
Mkutano huo unaoendelea katika Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere, iliyoko Kibaha, mkoani Pwani, unafanyika sambamba na mafunzo na mijadala ya masuala anuai yanayowahusu wanawake na uongozi katika nyanja mbalimbali kwenye jamii za Afrika na dunia kwa ujumla na kuweka maazimio yatayakochangia mstakabali wa jamii zilizo bora zaidi kwa kila mmoja.







MKURUGENZI WA PANGANI AJITAFAKARI KWA KUSHINDWA KUSIMAMIA MIRADI

December 13, 2023

 NAIBU Waziri Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mhe. Deogratius Ndejembi amemtaka Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Pangani, Isaya Mbenje na watendaji walio chini yake kujitafakari juu ya mwenendo wa utendaji kazi wao kutokana na kushindwa kusimamia miradi inayotekelezwa kwenye halmashauri hiyo.


Mhe Ndejembi ametoa kauli hiyo leo alipotembelea miradi ya elimu ya msingi na sekondari inayotekelezwa kwenye halmashauri hiyo ikiwa ni maandalizi ya kupokea wanafunzi wa mwaka mpya wa masomo 2024

Katika ziara yake, Mhe Ndejembi ameonesha kutoridhishwa na maendeleo ya ujenzi wa Shule ya Sekondari Pangani Halisi iliyogharimu kiasi cha Sh. Bilioni Moja, Shule ya Sekondari Masiaka inayojengwa kupitia mradi wa SEQUIP inayogharimu Sh. Milioni 585 na Shule ya Msingi Bushiri iliyogharimu Sh. Milioni 440 ikijengwa kupitia mradi wa BOOST.

Amesema Shule ya Pangani Halisi ilipaswa iwe imeshakamilika lakini mpaka sasa ujenzi huo haujakamilika huku halmashauri ikiwa imeishiwa fedha ikilinganishwa Shule ya Masiaka ambayo imepata sh. Milioni 580 majengo yake yapo kwenye hatua kubwa na inaendelea na ujenzi.

“Ofisi ya Rais-TAMISEMI chini ya Waziri Mhe Omary Mchengerwa hatutomchekea yeyote anayechezea fedha za umma, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Pangani na wasaidizi wako mjitafakari kwa sababu hawamsaidii kazi Mhe. Rais Dkt Samia Suluhu Hassan katika ngazi ya huku chini kuna tatizo la usimamizi wa miradi na kutojali fedha zinazoletwa kutekeleza miradi hii. Sasa kwa TAMISEMI hii hatuwezi kuja tukakuta usimamizi mbovu wa miradi tukashindwa kuchukua hatua,”amesema.