Mgombea Mwenza CCM Avunja Ngome ya ACT Tanga, Avuna Wanachama 272 wa Upinzani

September 21, 2015
Baadhi ya wana CCM na wananchi wakiwa wamefurika katika Viwanja wa Jitegemee Mjini Muheza ambapo mgombea mwenza nafasi ya urais CCM, Bi. Samia Suluhu Hassan alifanya mkutano wa kampeni leo. 
Baadhi ya wana CCM na wananchi wakiwa wamefurika katika Viwanja wa Jitegemee Mjini Muheza ambapo mgombea mwenza nafasi ya urais CCM, Bi. Samia Suluhu Hassan alifanya mkutano wa kampeni leo. 
Mgombea mwenza wa urais kupitia CCM, Bi. Samia Suluhu Hassan akihutubia umati wa wanaCCM na wananchi waliojitokeza kwenye mkutano wake wa kampeni uliofanyika viwanja vya Usagara Tanga Mjini leo. Idadi kubwa ya wananchi walihudhuria mkutano huo hadi wengine kuzimia kutokana na msongamano.

Baadhi ya wana CCM na wananchi wakiwa wamefurika katika Viwanja wa Jitegemee Mjini Muheza ambapo mgombea mwenza nafasi ya urais CCM, Bi. Samia Suluhu Hassan alifanya mkutano wa kampeni leo. 
Mjumbe wa Kamati ya Kampeni za CCM Kitaifa, Bi. Ummy Mwalimu akizungumza na wananchi kwenye moja ya mikutano ya kampeni za CCM timu ya mgombea mweza iliyofanyika mkoani Tanga leo.
Baadhi ya vijana wakiwa wamepanda juu ya gari ili kumsikiliza mgombea mwenza wa CCM, Bi. Samia Suluhu Hassan katika Jimbo la Mkinga.
Mgombea mwenza wa CCM, Bi. Samia Suluhu Hassan akiwa amesimamishwa na wananchi njiani alipokuwa akielekea katika Jimbo la Mkinga kufanya mkutano wa kampeni.
Mgombea mwenza wa CCM, Bi. Samia Suluhu Hassan akiwa amesimamishwa na wananchi njiani alipokuwa akielekea katika Jimbo la Mkinga kufanya mkutano wa kampeni.
Sehemu ya wanaCCM na wananchi ikiwa imemsimamisha barabarani mgombea mwenza wa CCM, Bi. Samia Suluhu kumsikiliza alipokuwa njiani kuelekea kwenye mikutano mikubwa ya kampeni. 


MGOMBEA mwenza wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Bi. Samia Suluhu Hassan amevunja ngome ya chama cha ACT Wazalendo Mkoani Tanga pamoja na kuvuna wanachama 272 kutoka vyama mbalimbali vya upinzani baada ya wanachama wa vyama hivyo kujiunga rasmi na CCM.

Bi. Samia Suluhu ambaye ni mgombea mwenza wa Dk. John Pombe Magufuli amefanikiwa kuvunja ngome za wapinzani leo mjini Tanga katika mikutano yake ya kampeni baada ya wagombea udiwani watano wa ACT Wazalendo kujiunga na CCM pamoja na wanachama wengine 235 toka Tanga mjini kujiunga na CCM kwenye mkutano mkubwa wa kampeni uliofanyika kwenye Uwanja wa Usagara mkoani Tanga.

Akihutubia katika mkutano mkubwa wa kampeni kunadi ilani ya CCM Tanga mjini uwanja wa Usagara, Bi. Samia Suluhu aliwapokea wagombea udiwani watano kutoka ACT Wazalendo, wakiwemo Wilson Elia (wa Kata ya Duga), Gasper Maboko (Kata ya Nguvumali), Charles Luanda (Maweni) na Marry Scoty (Kata ya Tanga Sisi) pamoja na Sada Mbwambo (viti maalum).

Mbali na madiwani hao kukihama chama cha ACT, wanachama 235 kutoka ACT, CUF na Chadema walijiunga na CCM kwenye mkutano huo wa Tanga mjini huku wengine 37 wakijiunga na CCM katika mkutano mwingine ulofanyika Jimbo la Muheza hivyo kutimiza wanachama 272 wapya kujiunga katika mikutano ya siku hiyo.

Akizungumza na wanaCCM na wananchi waliojitokeza mkutano wa Tanga Mjini, Bi. Suluhu aliwaomba kuichagua CCM kurudi madarakani ili kuendeleza maendeleo iliyofikia katika maeneo mbalimbali, ikiwemo huduma za kijamii na miundombinu hasa ya barabara. Alisema wapinzani hawafai kupewa madaraka kwa kuwa hawajajipanga kimfumo kwani hata viongozi wanaogombea wamekimbia vyama vyao na wanachotaka ni maslahi yao zaidi.

Alisema kwa mkoa wa Tanga Serikali ya CCM imepanga kuyakagua mashamba makubwa yaliotwaliwa na wawekezaji na kutelekezwa kisha kuyarejesha kwa wananchi ili waweze kuyatumia kwa uzalishaji, ikiwa ni pamoja na kupanua bandari ya mkoa huo kuchochea maendeleo.

Aidha aliongeza kuwa wakulima wa zao la korosho hawana budi kuongeza uzalishaji na kutokata tamaa kwani tayari Serikali inafanya mazungumzo na Serikali ya Norway kwa ajili ya ujenzi wa kiwanda cha kubangua korosho mkoani hapo ili kuongeza thamani ya zao hilo. Alisema lengo la Serikali ni kuhakikisha asilimia 40 ya vijana wanapata ajira kwenye viwanda vitakavyo jengwa maeneo anuai ya nchi.

Bi. Samia alifanya mikutano minne mikubwa katika majimbo ya Mkinga, Pangani, Mheza na Tanga Mjini na mikutano midogo midongo sita alioifanya njiani akisimamishwa na wananchi wakitaka kumsikia alipokuwa akipita. Hata hivyo katika mkutano wake wa Tanga Mjini baadhi ya wananchi walizidiwa kutokana na msongamano na idadi kubwa ya watu na kuzimia kabla ya kupewa huduma ya kwanza.

Gari ya Bi. Samia Suluhu ikitoka kwenye kivuko cha Mv. Pangani II mara baada ya kuvushwa, mgombea huyo mwenza wa urais CCM alikuwa akitoka kwenye mkutano wa hadhara JImbo la Pambani leo.
Kutoka kushoto ni mgombea ubunge Jimbo la Pangani, Jumaa Hamid Aweso, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Pangani, Hamis Mnegero na Mgombea mwenza wa CCM, Bi. Samia Suluhu Hassan wakizungumza jambo.
Aliyekuwa mbunge wa Jimbo la Nkenge, Asumpta Mshama akizungumza na wanaCCM na wananchi kwenye mikutano ya hadhara leo katika baadhi ya Majimbo ya Mkoa wa Tanga.
Moja ya ahadi za CCM msimu wa Rais Jakaya Kikwete ikiendelea na ujenzi wa gati Wilayani Pangani ikiendelea na ujenzi
Bi. Samia Suluhu akishuka ndani ya kivuko mara baada ya mkutano wa kampeni uliofanyika Kijiji cha Mwera Jimbo la Pangani.
Bi. Samia Suluhu akihutubia mkutano wa kampeni Muheza.

Baadhi ya wanachama wapya waliojiunga na CCM wakiwa katika msitari mara baada ya kurejesha fomu.
Sehemu ya wanaCCM na wananchi ikiwa imemsimamisha barabarani mgombea mwenza wa CCM, Bi. Samia Suluhu kumsikiliza alipokuwa njiani kuelekea kwenye mikutano mikubwa ya kampeni. 

Sehemu ya wanaCCM na wananchi ikiwa imemsimamisha barabarani mgombea mwenza wa CCM, Bi. Samia Suluhu kumsikiliza alipokuwa njiani kuelekea kwenye mikutano mikubwa ya kampeni. 
Bi. Samia Suluhu akiwa na mgombea ubunge wa Jimbo la Tanga Mjini Omary Nundu(kulia).

Mmoja wa wananchi wakipewa huduma ya kwanza mara baada ya kuzimia kutokana na msongamano katika mkutano wa kampeni kwa  mbaya.
Mkutano wa kampeni wa mgombea mwenza Tanga Mjini leo.

Mgombea Ubunge wa CCM, Jimbo la Bumbuli, January Makamba akizungumza na wanaCCM na wananchi katika mkutano wa kampeni.
Aliyekuwa mbunge wa Jimbo la Nkenge, Asumpta Mshama akizungumza na wanaCCM na wananchi kwenye mikutano ya hadhara leo katika baadhi ya Majimbo ya Mkoa wa Tanga.

Mkutano wa kampeni wa mgombea mwenza Tanga Mjini leo.



*Imeandaliwa/www.thehabari.com  Joachim Mushi
ETOILE KUPELEKWA KAMATI YA NIDHAMU YA FIFA

ETOILE KUPELEKWA KAMATI YA NIDHAMU YA FIFA

September 21, 2015

Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani (FIFA) limefungua kesi kwenye Kamati ya Nidhamu ya FIFA dhidi ya klabu ya Etoile Sportive du Saleh ya Tunisa kutokana na klabu hiyo kushindwa kuilipa klabu ya Simba SC ya Tanzania pesa za mauzo ya mchezaji Emmanuel Okwi.
Kwa mujibu wa barua ya FIFA kwa Shirikisho la Mpira wa Miguu la Tunisia (FTF) na nakala yake kwenda TFF, klabu hiyo inashitakiwa  kwa kuvunja kanuni kwa mujibu wa ibara ya 64 ya kanuni za nidhamu za FIFA (Fifa Disciplinary Code).
Kwa kuzingatia hilo, agenda hii itakuwa kwenye kikao kijacho cha kamati ya nidhamu.
Etoile Sportive du Sahel wametakiwa kulipa mara moja kiasi cha dola za kimarekani laki 3 na riba ya asilimia 2% kwa kila mwaka kama ilivyoelekezwa na maamuzi ya Jaji mmoja wa Kamati ya Nidhamu za Wachezaji mnamo tarehe 20 Novemba 2014.
Tangu wakati huo Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limekua likiwasiliana na Shirikisho la Mpira wa Miguu la Tunisia (FTF) na FIFA kwa niaba ya klabu ya Simba amabye ni mwanachama wa TFF.
Ikiwa klabu hiyo ya Tunisia itafanya malipo kwa klabu ya Simba na kupelekea ushahidi wa malipo kwa FIFA basi suala hilo litafutwa.
Aidha klabu hiyo iko kwenye hatari ya kushushwa daraja au kupokwa alama  kwenye ligi (League Point) iwapo haitalishughulikia suala hilo mara moja.
Mawakala na Wadau wa Maahindano ya urembo ya Miss Tanzania wanaotaka kuomba Uwakala watakiwa kutuma maombi

Mawakala na Wadau wa Maahindano ya urembo ya Miss Tanzania wanaotaka kuomba Uwakala watakiwa kutuma maombi

September 21, 2015

Kamati ya Miimages (5)ss Tanzania inapenda kuwatangazia wadau wote wanaotaka kuandaa Mashindano ya urembo ya Miss Tanzania kwa mwaka 2016 kutuma maombi yao ya uwakala kuanzia sasa hadi tarehe 30 Novemba 2015 ndio mwisho wa kupokea maombi ha yo.
Mashindano yatakayo fanyika ni ya mikoa tu, hakutakuwa na mashindano katika ngazi ya wilaya wala Kanda.
Sifa za kuwa Wakala wa Miss Tanzania ni pamoja na
1)      Uwe na Kampuni iliyosajiliwa na Mamlaka husika ya Serikali. 2)      Uwe na mtaji wa kutosha. 3)      Uwe na uwezo wa kuandaa shindano katika ufanisi mkubwa. 4)      Uwe mstari wa mbele katika kukuza sanaa za utamaduni nchini.
Wakala atakaye pitishwa na Kamati ya Miss Tanzania atapaswa kujisajili Baraza la Sanaa la Taifa.(BASATA) kabla hajapewa kibali cha kuandaa shindano.
Wilaya za Mkoa wa D’salaam, Ilala, Kinodoni na Temeke zitapewa hadhi ya Kimkoa, ikiwa ni pamoja na Mkoa wa Elimu ya Juu.
Ada ya Uwakala ni shilingi milioni moja.
Ada ya Uwakala italipwa kwa Kamati ya Miss Tanzania baada ya maombi kukubaliwa na kupitishwa.
Maombi yatumwe kwa barue pepe   misstanzania2015@yahoo.com
Kwa mawasiliano na ufafanuzi zaidi piga namba zifuatazo:-
0673 521037  Katibu wa Kamati 0754 337043 Msemaji wa Kamati 0755 019288 Sekretariet.
Imetolewa na:
JUMA PINTO. MWENYEKITI KAMATI YA  MISS TANZANIA.
Mikataba ya madini, gesi, mafuta kupitiwa na timu ya wataalam kabla ya kusainiwa.

Mikataba ya madini, gesi, mafuta kupitiwa na timu ya wataalam kabla ya kusainiwa.

September 21, 2015

01
Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene (kulia) akifungua  warsha kuhusu Dira ya Madini Afrika  iliyokutanisha wataalam kutoka   taasisi za serikali nchini lengo likiwa ni kuwapa uelewa juu  ya sekta ya madini na usimamizi wa mikataba. Katikati ni Kamishna Msaidizi wa Nishati Jadidifu na Mbadala Mhandisi Edward Ishengoma. Kushoto ni mtaalam kutoka  Kitengo cha  Nishati na Mabadiliko ya Tabia Nchi, Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Abbas Kitogo.
03
Washiriki  wa warsha kuhusu Dira ya Madini Afrika wakifuatilia kwa makini  hotuba ya ufunguzi iliyokuwa inatolewa na Waziri wa Nishati na Madini, George  Simbachawene (hayupo pichani)
04
Waziri wa Nishati na Madini, George  Simbachawene (wa tatu kutoka kushoto; waliokaa mbele) akiwa katika picha ya pamoja  na washiriki wa mafunzo kuhusu  Dira ya Madini Afrika iliyofanyika mjini Morogoro tarehe 21 Septemba, 2015.
…………………………………
Na Greyson Mwase, Morogoro
Ili kuhakikisha kuwa wananchi wa Tanzania wananufaika na rasilimali za madini mbalimbali pamoja na gesi iliyogunduliwa kwa wingi hivi karibuni, Serikali imeanza kutoa mafunzo kwa wataalam kutoka taasisi za serikali watakaohusika na upitiaji wa mikataba yote ya shughuli za utafutaji na uchimbaji wa madini, gesi na mafuta kabla ya kusainiwa. Hayo yalisemwa na Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene katika uzinduzi wa warsha kuhusu dira mpya ya madini Afrika iliyofanyika mjini Morogoro. Warsha hiyo ya siku tatu iliyoandaliwa na Wizara ya Nishati na Madini ilikutanisha wataalam kutoka taasisi za serikali ikiwa ni pamoja na Ofisi ya Makamu wa Rais, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Ofisi ya Waziri Mkuu, Wizara ya Fedha, Ofisi ya Rais- Tume ya Mipango, Mamlaka ya Mapato Nchini (TRA) na Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii (ESRF) Pia ilikutanisha wataalam kutoka Wizara ya Nishati na Madini pamoja na taasisi zake kama vile Wakala wa Ukaguzi wa Madini Nchini (TMAA), Shirika la Madini la Taifa (STAMICO), Shirika la Uendelezaji Nishati ya Jotoardhi Tanzania (TGDC), Mpango wa Kuongeza Uwazi na Uwajibikaji katika Tasnia ya Uziduaji Nchini (TEITI), Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) na Chuo cha Madini Dodoma (MRI). Simbachawene alisema uundaji wa timu ya wataalam mbalimbali kwa ajili ya kupitia mikataba ya madini, gesi na mafuta ni moja ya makubaliano katika utekelezaji wa Dira ya Madini ya Africa (Mining Vision for Africa) iliyoasisiwa na wakuu wa nchi zenye madini katika mkutano wake uliofanyika mwaka 2009.
Alisema kuwa katika kuhakikisha kuwa sekta ya madini inachangia katika ukuaji wa uchumi wa nchi za Afrika zinazozalisha madini wakuu wa nchi walikubaliana kuanzishwa kwa Dira ya Madini itakayowezesha sekta ya madini katika nchi wanachama kuboreshwa na kuwa na mchango mkubwa katika ukuaji wa uchumi wa nchi Alisema kuwa katika utekelezaji wa Dira ya Madini ya Afrika, nchi ya Tanzania imeanza kutoa mafunzo kwa wataalam mbalimbali katika taasisi za Serikali katika upitiaji wa mikataba hususan ya utafiti na uchimbaji wa rasilimali za madini, gesi na mafuta. Alisisitiza kuwa mara baada ya wataalam hao kupata mafunzo wataweza kupitia mikataba mbalimbali kabla ya kusainiwa. “Ieleweke kwamba suala la mikataba litakuwa si kati ya watu wawili bali wataalam watashirikishwa kwa kupitia mikataba hiyo na kutoa mapendekezo yao kabla ya mikataba kusainiwa na Waziri ambaye ni msimamizi wa sekta husika,” alisisitiza Simbachawene. Akielezea ushirikishwaji wa wananchi katika usimamizi wa sekta za madini, gesi na mafuta, Simbachawene alisema kuwa Serikali imehakikisha kuwa mikataba yote inalenga kuwanufaisha wananchi kwa kushirikishwa katika utoaji wa huduma katika sekta husika. Akitolea mfano wa sekta ya gesi nchini, alisema fursa za utoaji wa huduma zipo nyingi na kuwataka wananchi kuchangamkia fursa hizo Hata hiyo alieleza kuwa Serikali ina mkakati wa kutoa mafunzo kwa wanachi kuhusu uzalishaji wa bidhaa bora ili ziendane na soko la kimataifa. “ Tunataka ifike mahali makampuni yanayofanya shughuli za utafiti na uchimbaji wa madini, gesi na mafuta yanunue huduma na bidhaa kwa wananchi wa Tanzania badala ya kuagiza kutoka nje ya nchi,” alisisitza Simbachawene. Naye mtaalam kutoka Kitengo cha Nishati na Mabadiliko ya Tabia Nchi, Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Abbas Kitogo alisema kuwa shirika la UNDP limekuwa likishirikiana na Serikali katika utoaji wa mafunzo kuhusu sekta mbalimbali ikiwa ni pamoja na usimamizi wa mikataba Alisema sekta nyeti kama za madini, gesi na mafuta zisiposimamiwa kikamilifu zinaweza kuibua migogoro badala ya kuleta maendeleo. Alisisitiza kuwa kupitia mafunzo hayo wataalam kutoka taasisi za serikali wataweza kupitia mikataba mbalimbali ya utafiti na uchimbaji wa madini, gesi na mafuta na kuishauri serikali kabla ya kusainiwa ili kutumika rasmi.
DR. JOHN POMBE MAGUFULI AITEKA MANISPAA YA BUKOBA

DR. JOHN POMBE MAGUFULI AITEKA MANISPAA YA BUKOBA

September 21, 2015

1
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli akihutubia katika mkutano wa kampeni uliofanyika kwenye viwanja vya Gymkana mjini Bukoba leo akiomba kura za ndiyo kwa wananchi wa mkoa huo kumpigia kura za ndiyo kuwa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzaniaifikapo Oktoba 25 mwaka huu ili aweze kuwatumikia watanzania.
Mgombea urais huyo Dk. John Pombe Magufuli amesema mara atakapochaguliwa na watanzania na kuunda baraza lake la mawaziri , Kazi ya kwanza ya waziri wake wa kilimo ni kuhakikisha anatatua tatizo la bei ya zao la kahawa ambapo ameahidi kuwa serikali yake itapunguza kodi mbalimbali zaidi ya 27 zinazotozwa kwa wakulima wakati wa uuzaji wa zao la kahawa ili kuipandisha bei ya zao hilo na kuwafaidisha wakulima ambao ndiyo wanaoteseka katika kilimo cha zao hilo.(PICHA NA JOHN BUKUKU -FULLSHANGWE-BUKOBA)
2
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli akimnadi mbunge na madiwani wa jimbo la Bukoba mjini hawapo mpichani wakati wa mkutano huo wa kampeni mjini Bukoba.
3
Mgombea Ubunge wa jimbo la Bukoba mjini Mh. Balozi Khamis Kagasheki akimuombea kura Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli na kujipigia debe yeye mwenyewe.
4
Mwanamuziki Diamond Platnumz na kundi lake wakitumbuiza katika mkutano huo wa kampeni uliofanyika kwenye viwanja vya Gymkana mjini Bukoba.
5
Mwanamuziki Diamond Platnumz akitumbuiza katika mkutano huo wa kampeni uliofanyika kwenye viwanja vya Gymkana mjini Bukoba.
6
Mgombea udiwani kata ya Chanji mjini Sumbawanga akimpigia debe Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli.
7
Mgombea ubunge kupitia vijana mkoa wa Kagera Halima Bulembo akizungumza katika mkutano huo.
8
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli akiwa amekaa na Mgombea ubunge wa jimbo la Bukoba mjini Mh. Balozi Khamis Kagasheki.
????????????????????????????????????
Mgombea Ubunge wa jimbo la Muleba Kaskazini Mh. Charles Mwijage akizungumza katika mkutano huo na kuwapigia debe wabunge wa viti maalum mkoa wa Kagera kulia ni Halima Bulembo na kushoto ni Oliver Semguruka.
14
Kada wa CCM Amon Mpanju akimpigia debe Dk John Pombe Magufuli katika mkutano wa kampeni uliofanyika kata ya Maruku Bukoba Vijijini.
13
Mmoja wa wananchi akiwa amejikinga na jua kwa bango lenye picha ya Dr. John Pombe Magufuli katika mkutano wa kampeni uliofanyika kata ya Maruku Bukoba vijijini.
12
Wasanii Mh. Temba kulia na Chege wakikamua jukwaani.
11
Wananchi wakiwa wamejitokeza kwa wingi katika mkutano huo uliofanyika viwanja vya Gymkana Bukoba mjini.
10
Msanii Fid Q akiwapa mistari wananchi wa Bukoba mjini.
15
Baba na Mwana! Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya CCM Ndugu Abdallah Bulembo akizungumza jambo na mwanaye Halima Bulembo ambaye ni Mgombea Ubunge viti maalum vijana Mkoa wa Kagera.
16
Jasson Samson Rweikiza mgombea ubunge Bukoba vijijini akiomba kura kwa wananchi katika mkutano wa kampeni uliofanyika kata ya Maruku Bukoba vijijini.
17
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli akizungu za na mgombea ubunge wa jimbo la Bukoba vijijini Jasson Samson Rweikiza.
18 
Hapa ni CCM tu!
19
Hapa ni Kijani Tu mjini Biharamulo.
24
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli akiwasalimia wananchi katika kata ya Nshamba Muleba Kusini wakati akiwa njiani kuelekea Kamachumu mkoani Kagera.
 22
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli akiteta jambo na Mgombea ubunge jimbo la Muleba Kaskazini Mh. Charles Mwijage na Mwenyekiti wa Wazazi CCM Taifa Abdallah Bulembo mjini Kamachumu.
21
Mgombea ubunge jimbo la Muleba Kaskazini Mh. Charles Mwijage akiwahutubia wananchi wa Kamachumu katika mkutano wa kampeni uliofanyika jimbo la Muleba Kaskazini.
20
Watu wa Muleba na rangi ya kijani Kamachumu.
26
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli akimfariji Jojia Osward mke wa Marehemu Osward Lwakabwa aliyekuwa mgombea udiwani kata ya Muleba aliyefariki kwa ajali jana mjini Muleba
27
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli akimfariji kaka wa marehemu Osward Lwakabwa Mzee Elias Lwakabwa wakati alipohani msiba wa mwana CCM huyo aliyefaiki kwa ajali jana.
28
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli akizungumza na watoto wa Marehemu Osward Lwakabwa aliyefariki kwa ajali ya pikipiki kulia ni Fratenus Osward na Adelitus Osward.
29
CCM hoyee kijana akiwa ameshika mabango ya picha yenye picha za Dk. John Magufuli.
????????????????????????????????????
Diamond Platnumz na kundi lake wakitumbuiza mjini Bukoba wakati wa mkutano wa kampeni za CCM mjini Bukoba.
????????????????????????????????????
Diamond Platnumz akifanya vitu vyake.
????????????????????????????????????
Nyomi ya Bukoba hiyo.
????????????????????????????????????
????????????????????????????????????
Yamoto Bandi kama kawa jukwaani.