SHEREHE ZA KUFUNGA MAFUNZO YA AWALI YA JESHI LA MAGEREZA KOZI NA. 27 CHUO CHA MAGEREZA KIWIRA ZAFANI, JIJINI MBEYA

May 29, 2015

Wahitimu wa Mafunzo ya Awali ya Uaskari Magereza wakipita kwa mwendo wa haraka mbele ya Mgeni rasmi, Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Bw. Mbarak Abdulwakil(hayupo pichani) leo Mei 29, 2015 katika Chuo cha Magereza, Kiwira Kilichopo Mkoani Mbeya.
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Bw. Mbarak Abdulwakil akikagua Gwaride Maalum lililoandaliwa na Wahitimu wa Mafunzo ya Awali ya Uaskari Magereza leo Mei 29, 2015 Chuo cha Magereza Kiwira, Mbeya.
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Bw. Mbarak Abdulwakil akipokea Salaam ya heshima akiwa jukwaan kabla ya kukagua Gwaride Maalum katika sherehe za kufunga Mafunzo ya Uaskari Magereza, Kiwira Mbeya(kushoto) ni Kamishna Jenerali wa Magereza, John Casmir Minja(kulia) ni Mkuu wa Chuo cha Magereza Kiwira, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Stanford Ntirundura.
Gadi ya Askari wa Kike ambao ni Wahitimu wa Kozi ya Awali ya Uaskari Magereza wakila Kiapo cha Utii kwa Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama ambaye ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mbele ya Mgeni rasmi, Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi(hayupo pichani) katika sherehe za ufungaji Mafunzo hayo.
Katibu Mkuu akikabidhi zawadi kwa Mhitimu wa Kozi Na. 27 ya Uaskari Magereza ambaye amefanya vizuri katika Somo la Gwaride na Ukakamavu Askari Mhitimu, Ezra Kapesa leo katika sherehe za kufunga Mafunzo hayo Mkoani Mbeya(wa pili kushoto) ni Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja(kulia) akimuongoza Mgeni rasmi, Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil(katikati) kuelekea kwenye Ukumbi wa Mihadhara kwa ajili ya kufunga rasmi Mafunzo ya Awali ya Uaskari Magereza leo Mei 29, 2015(kushoto) ni Mkuu wa Chuo cha Magereza Kiwira, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Stanford Ntirundura.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Nchini, John Casmir Minja akitoa maelezo mafupi kabla ya kumkaribisha Mgeni rasmi, Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi aweze kutoka hotuba ya kufunga rasmi Mafunzo ya Uaskari Magereza katika Chuo cha Magereza Kiwira, Mkoani Mbeya(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).
MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AZUNGUMZA NA WATANZANIA WANAOISHI NCHINI NIGERIA

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AZUNGUMZA NA WATANZANIA WANAOISHI NCHINI NIGERIA

May 29, 2015


NI1
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Watanzania wanaoishi Nchini Nigeria katika Ofisi ya Ubalozi wa Tanzania mjini Abuja Nigeria leo May 29,2015.
NI2
Baadhi ya Watanzania wanaoishi Nchini Nigeria wakimsikiliza Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, alipokua akizungumza nao leo May 29,2015  katika Ofisi ya Ubalozi wa Tanzania mjini Abuja Nigeria leo May 30,2015.
NI3
Balozi wa Tanzania Nchini Nigeria Mhe. Danniel Ole Njolai akimkabidhi zawadi ya saa iliyotolewa na Watanzania wanaoishi Nchini Nigeria Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, baada ya kuzungumza na Watanzania hao katika Ofisi ya Ubalozi wa Tanzania mjini Abuja Nigeria leo May 29,2015.
NI4
NI5
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, katikati akiwa katika picha ya pamoja na Watanzania wanaoishi Nchini Nigeria Baada ya kuzungumza nao katika Ofisi ya Ubalozi wa Tanzania mjini Abuja Nigeria leo May 29,2015. (Picha na OMR)
NI6
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, katikati akiwa katika picha ya pamoja na Watanzania wanaoishi Nchini Nigeria Baada ya kuzungumza nao katika Ofisi ya Ubalozi wa Tanzania mjini Abuja Nigeria leo May 29,2015. (Picha na OMR)

MWENGE WA UHURU WAKIMBIZWA WILAYA YA KINONDONI MKUU WA WILAYA ATANGAZA AJIRA YA PAPO KWA PAPO

May 29, 2015

 
 Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda akiwa ameubeba mwenge wa Uhuru baada ya kukabidhiwa na Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Raymond Mushi.
 Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Raymond Mushi (kushoto), akimkabidhi Mwenge wa Uhuru Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda baada ya kumaliza mbio zake wilayani humo Dar es Salaam leo leo asubuhi. Mwenge huo ulianza mbio zake Wilaya ya Ilala na kuzindua miradi mbalimbali.
 Kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa mwaka 2015, Juma Khatibu Chum (kulia), akisalimia na Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Yusuf Mwenda.
 Viongozi mbalimbali wa Wilaya ya Kinondoni wakiwa wamejipanga foleni wakisubiri kuupokea mwenge wa Uhuru kabla ya kuanza mbio zake wilayani humo.
 Wakimbiza mwenge kitaifa.
 Mwenge wa Uhuru ukikimbizwa (kushoto) ni Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda.
  Kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa mwaka 2015, Juma Khatibu Chum akivuta pazia kuashiria uwekaji wa jiwe la msingi ya mradi wa maji Mburahati Barafu na Kisiwani uliofadhiliwa na Jumuia ya Ulaya, Serikali ya Ubelgiji na Serikali ya Tanzania  wakati wa ukimbizaji wa mwenge huo Wilaya ya Kinondoni humo.
  Kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa mwaka 2015, Juma Khatibu Chum akivuta pazia kuashiria uwekaji wa jiwe la msingi ya baabara tatu katika Shule ya Sekondari ya Makulumla. Kulia ni Mkuu wa Shule hiyo, Beatrice Mhina.
 Mwanafunzi Noel Mwita wa Shule ya Sekondari ya Makulumla, akiekeza namna ya kuchanganya madawa wakati kiongozi huyo wa mwenge, Juma Chum (wa nne kushoto), alipoweka jiwe la msingi za maabara katika shule hiyo. Kutoka kushoto ni Mkuu wa shule hiyo, Beatrice Mhina, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Camilius Wambura na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda
 Vijana wa hamasa wa wilaya ya Kinondoni wakitoa burudani mbalimbali wakati wa kuupokea mwenge huo ukitokea wilaya ya Ilala.
  Vijana wa hamasa wa wilaya ya Kinondoni wakitoa burudani mbalimbali wakati wa kuupokea mwenge huo ukitokea wilaya ya Ilala.
 Wananchi wa Mburahati wakiupokea mwenge huo wakati wa uzinduzi wa mradi wa maji katika eneo hilo.
 Vijana wa hamasa wakipamba hafla hiyo kwa kuonesha matukio mbalimbali.
 Mwanamuziki Rehema Chalamila ‘Ray C’ akitoa ushuhuda wa jinsi alivyoacha matumzizi ya dawa ya kulevya mbe ya Kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa mwaka 2015, Juma Khatibu Chum (hayupo pichani), wakati wa uzinduzi wa kituo cha vijana walioathiriwa na dawa hizo katika Hospitali ya Mwananyamala.
 Kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa mwaka 2015, Juma Khatibu Chum, akimkabidhi Amina Mshana chandarua kwa ajili ya kujikinga na ugonjwa wa malaria.
Wakimbiza mwenge wa Uhuru kitaifa,  Delina Simfukwe (kushoto) na Bakia Abdallah wakiteta jambo na mwanamuziki RehemaChalamila ‘Ray C baada ya kutoa ushuhuda kuhusu matumizi ya dawa za kulevya.
…………………………………………………………………………………………….
Na Dotto Mwaibale
MKUU wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda ametoa ajira ya moja kwa moja kwa kijana Yusuf Mzitto mtaalamu wa masuala ya kompyuta ambaye alikuwa ameathiriwa na matumizi ya dawa za kulevya  wa wilaya hiyo.
Makonda alitoa ajira kwa kijana huyo mbele ya kiongozi wa mbio za mwenge wa Uhuru mwaka huu. Juma Khatibu Mchum wakati wa uzinduzi wa kituo cha vijana walioathiriwa na matumizi ya dawa za kulevya kilichozinduliwa na kiongozi huyo wa mbio za mwenge katika Hospitali ya Mwananyamala Dar es Salaam leo asubuhi.
“Kijana huyu mwenye elimu ya juu ya masuala ya kompyuta alikuwa ameathiriwa na matumizi ya dawa za kulevya hivyo baada ya kuacha kutumia dawa hizo tumempa ajira katika ofisi yangu ili aweze kufanyakazi badala ya ujuzi wake kupotea bure” alisema Makonda.
Makonda alisema kuwa katika kuwawezesha vijana walioathiriwa na dawa hizo wamepatana na viongozi wa manispaa hiyo kuwa kila kampuni inayofanya shughuli za kijamii katika wilaya hiyo ili iweze kupata tenda ya kufanya kazi yoyote ni lazima itoe mchanganuo  kwanza wa utoaji wa nafasi ya ajira kwa vijana wa wilaya hiyo.
Alisema wamechukua hatua hiyo ili kutoa fursa ya ajira kwa vijana waliohamua kuachana na matumzi ya dawa za kulevya ambao hawana kazi hivyo kupitia  kakampuni hizo ziweze kuwasaidia vijana hao baada ya kupatiwa tenda na manispaa hiyo.
Alisema ili kuunga jitihada za Rais Jakaya Kikwete za kupambana na uingizaji wa dawa za kulevya ameanzisha mpango wa kukutana mara moja kila mwezi na vijana walioathiriwa na dawa hizo ili kubadilishana mawazo badala ya kuwatenga.
Makonda alisema vijana hao wengi wao ni wataalamu wa masula mbalimbali akimtolea mfano kijana aliyepewa ajira katika ofisi yake ambaye atawasaidia katika mambo mengine.
Akizungumzia mbio za mwenge katika wilaya yake kwa mwaka huu alisema umezindua na kuweka mawe ya msingi kwenye miradi saba yenye jumla ya sh.5,079,153,972 ambapo kati ya fedha hizo sh.14,802,200 ni fedha kutoka serikali kuu, sh.2,672,992 kutoka katika Halmshauri ya Manispaa ya Kinondoni, sh.913,800,780 ni mchango wa wahisani na sh.1,477,978,000 ni michango ya wananchi.
Alitaja miradi hiyo kuwa ni pamoja na mradi wa maji, ujenzi wa barabara, ujenzi wa baabara, ujenzi wa shule za Sekondari, ujenzi wa jengo la wazazi, ujenzi wa ofisi ya Kata na ujenzi wa nyumba ya walimu.
Alisema mwenge huo ulipata fursa ya kukagua miradi endelevu wa ugawaji wa vyandarua, mradi wa wanawake wajasiriamali, mradi wa vijana wajasiriamali watunzaji wa mazingira na mradi wa huduma za ukimwi.
Kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa Juma Khatibu Chum aliwataka watanzania wote bila ya kujali itikadi za vyama vyao kudumisha amani na utulivu wa nchi hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu wa mwezi Oktoba.
Alisema amani ya nchi tusipo kuwa makini inaweza kuharibiwa kwa siku moja wakati imetafutwa kwa miaka mingi na aliwata vijana kuacha kutumia dawa za kulevya na kujikinga ma malaria ambayo yame kuwa yakiua watu wengi kuliko ukimwi. (Imeandaliwa na mtandao wa www.habari za jamii.com)

NEC YAKAMILISHA MAANDALIZI UBORESHWAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA KWA MIKOA 4

May 29, 2015
Maandalizi ugawaji wa mashine kwa ajili ya kuandikisha wanchi katika daftari la wapiga kura kwa Kanda ya 5 Tano kati ya Sita yamekamilika leo Mei 29, 2015 zaidi ya Biometric Voter Registration (BVR) zipatazo 1492 zinaanza kusambazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Kuanzia mapema Alfajiri Kanda ya Tano ni Mikoa ya Mara, Arusha, Manyara na Kilimanjaro.

SERIKALI YATANGAZA KUTENGA BAJETI ZAIDI KWENYE TAFITI ZA AFYA.

May 29, 2015


 Naibu wa Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi stadi, Mh. Anne Kilango  akisisitiza jambo  mbele ya  Madaktari na wanafunzi wa udaktari kutoka Chuo Kikuu Cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) waliohudhuria Mkutano Mkuu wa tatu wa sayansi ya afya ulioandaliwa na chuo hicho  jijini Dar es Salaam jana. Kwenye mkutano huo wa siku mbili huku ukilenga  kujadili masuala ya tafiti kwenye sayansi ya afya, Mh. Kilango alimuwakilisha Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dr Mohamed Gharib Billal.
 Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Anna Kilango (kulia) akijadiliana jambo na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) Prof.Ephata Kaaya, mara baada ya ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa tatu wa sayansi ya afya ulioandaliwa na chuo hicho  jijini Dar es Salaam jana.
Baadhi ya wanasayansi, Madaktari na wanafunzi wa udaktari kutoka  Chuo Kikuu Cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) wakifuatilia kwa umakini Mkutano Mkuu wa tatu wa sayansi ya afya ulioandaliwa na chuo hicho  jijini Dar es Salaam jana

Naibu wa Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi stadi, Mh. Anne Kilango  amebainisha kuwa bajeti ya wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2015/16 imeongeza fungu zaidi kwenye masuala ya utafiti hususani ule wa sayansi ya afya.

Mh. Kilango alitoa kauli jijini Dar es Salaam jana wakati akifungua  Mkutano Mkuu wa tatu wa sayansi ya afya ulioandaliwa na Chuo Kikuu Cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) na kuhudhuliwa na mamia ya Madaktari na wanafunzi wa udaktari kutoka chuo hicho.

“ Ili taifa liweze kufanya vizuri kwenye sekta yoyote ile ni lazima tuwekeze zaidi kwenye masuala ya tafiti. Kwa kulitambua hilo napenda kuwataarifu kuwa hata kwenye bajeti yetu ya mwaka huu wa fedha tunatenga kiasi kikubwa cha rasilimali fedha kwa ajili ya kuwezesha tafiti hizi zikiwemo hizi za masuala ya afya,’’ alisema Mh. Kilango ambaye alimuwakilisha Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dr Mohamed Gharib Billal.

Kwa upande wake Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) Prof.Ephata Kaaya alisema kuwa kwa sasa taifa linahitaji zaidi tafiti za kiafya hususani kwenye magonjwa yasiyo ya kuambukiza ikiwemo kisukari, shinikizo la damu na saratani.

“ Ni dhahiri kuwa kwa sasa magonjwa haya yasiyo ya kuambukiza yamekuwa ni tishio kwa taifa. Kama wataalamu wa masuala ya afya tunaona kuja tija zaidi tukiwekeza katika tafiti zinazohusu pia magonjwa haya,’’ alibainisha.

Mkutano huo wa siku mbili unatarajiwa kuhitimishwa leo ambapo zaidi ya tafiti 100 kuhusu maswala ya afya zitawasilishwa.

MKUU WA MKOA WA DODOMA MHE. CHIKU GALLAWA AMUAPISHA MKUU MPYA WA WILAYA YA MPWAPWA MHE. ANTH0NY MAVUNDE

May 29, 2015


Mhe. Athony Mavunde akila kiapo cha kuwa Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Chiku Gallawa (Hayupo Pichani) Mei 29,2015
Mhe. Athony Mavunde akitia saini hati ya kiapo cha kuwa Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Chiku Gallawa Mei 29, 2015
Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Mhe. Athony Mavunde (kushoto) akipongezwa na baba yake mzazi Ndg. Peter Mavunde mara baada ya kula kiapo cha kuwa Mkuu wa Wilaya Mei 29,2015
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Chiku Gallawa (Katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Mhe. Athony Mavunde (kushoto kwake) na wajumbe wa kamatiya Ulinzi na Usalama Mkoa wa Dodoma wakati wa Hafla ya kumuapisha Mkuu huyo mpya wa Wiaya ya Mpwapwa Mei 29,2015
MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AHUDHURIA KUAPISHWA RAIS WA NIGERIA LEO

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AHUDHURIA KUAPISHWA RAIS WA NIGERIA LEO

May 29, 2015

bi1
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal na Mkewe Mama Asha Bilal, wakiteremka kwenye Ndege walipowasili Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Nnamdi Azikiwe Abuja kwa ajili ya kuhudhuria sherehe ya kuapishwa Rais Mohammadu Buhari iliyofanyika leo May 29,2015 katika Uwanja wa Ego Squar mjini Abuja Nigeria.
bi2
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal na Mkewe Mama Asha Bilal, wakiwasili kwenye Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Nnamdi Azikiwe Abuja kwa ajili ya kuhudhuria sherehe ya kuapishwa Rais Mohammadu Buhari iliyofanyika leo May 29,2015 katika Uwanja wa Ego Squar mjini Abuja Nigeria.
bi3
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal akisalimiana na mtoto Ernest Nkayala alipowasili Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Nnamdi Azikiwe Abuja kwa ajili ya kuhudhuria sherehe ya kuapishwa Rais Mohammadu Buhari iliyofanyika leo May 29,2015 katika Uwanja wa Ego Squar mjini Abuja Nigeria.
bi4
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipokea shada la maua kutoka kwa Mtoto Elin Mwandobo alipowasili Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Nnamdi Azikiwe Abuja kwa ajili ya kuhudhuria sherehe ya kuapishwa Rais Mohammadu Buhari iliyofanyika leo May 29,2015 katika Uwanja wa Ego Squar mjini Abuja Nigeria.
bi5
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiangalia ngoma za kabila la Kinigeria alipowasili Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Nnamdi Azikiwe Abuja kwa ajili ya kuhudhuria sherehe ya kuapishwa Rais Mohammadu Buhari iliyofanyika leo May 29,2015 katika Uwanja wa Ego Squar mjini Abuja Nigeria.
bi6
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiangalia ngoma za kabila la Kinigeria alipowasili Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Nnamdi Azikiwe Abuja kwa ajili ya kuhudhuria sherehe ya kuapishwa Rais Mohammadu Buhari iliyofanyika leo May 29,2015 katika Uwanja wa Ego Squar mjini Abuja Nigeria.
(Picha na OMR)
PINDA AHUTUBIA SHEREHE ZA MIAKA 25 WA TAWLA

PINDA AHUTUBIA SHEREHE ZA MIAKA 25 WA TAWLA

May 29, 2015

ta1 
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na Balozi Mwanaidi Maajar baada ya kuhutubia katika sherehe za siku ya Wanasheria Wananwakde Tanzania Tawla , kwenye viwanja vya  Karimjee jijini Dar es salaam Mei 30, 2015. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
ta4
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wanachama wa Chama cha Wanasheria Wanawake Tanzania (TAWLA) baada ya kuhutubia katika sherehe za miaka 25 ya chama hicho kwenye viwanja vya  Karimjee jijini Dar es salaam Mei 30, 2015. Aliyekaa wapili kulia ni balozi wa Sweden nchini, Lennarth Hjelaker.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
ta2
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza wakati alipozindua Uandishi wa Wosia katiak sherehe za miaka 25 ya Chama cha Wanasheria Wananwake (TAWLA0 kwenye viwanja vya Karimjee jijini Dar es salaam Mei 30, 2015.Kushoto ni balozi wa Sweden nchini, Lennarth Hjelaker.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)